CCM yahaha kuimaliza CHADEMA

Mimi nasema hivi kama CCM wamechoka na amani,utulivu na mshikamano wa nchi yetu tanzania wafanye haraka hicho kitendo cha kuwaondoa wabunge wachadema kwa azimio la bunge hiyo februari 8,2011. Nawahakikishia ccm kuwa kama hawajaona nchi inawaka moto basi ni wakti huo.ccm watajuta kwa huo upuuzi wao wanaotaka kuufanya. Wajaribu waone. Watanzania sasa hivi tumebadilika. Hatutakubali wabunge wetu waondolewa bungeni.

  1. tunachotaka ccm kwa sasa ni kuanza mchakato wa taratibu za kuunda katiba mpya ili kuondoa sheria ya kutopinga matokeo ya urais baada ya kutangazwa na tume ya uchaguzi. Sheria ambayo ni ya kidikteta! Kwanini matokeo ya ubunge na udiwani tu ndiyo yahojiwe na ya rais yasihojiwe wakati wapiga kura ni walewale????????????
  2. tunachotaka kuwe na tume huru ya uchaguzi ambayo mwenyekiti na mkurugenzi wake hawateuliwi na rais aliyeko madarakani. Hili ccm wanajua kabisa haliko sawa.
CCM lazima wajue kuwa kuna watanzania milioni 2.2 walioko nyuma ya chadema kwa hesabu zao za kuchakachua, lakini ukweli ni kwamba kama hesabu za nec za watu waliojiandikisha kupiga kura zilikuwa sahihi kwa 20 milioni na na wakajitokeza milioni 8 tu basi wajue kuna milioni 12 ambao hawakuchagua ccm lakini walikuwa tayari kuichagua chadema baali walinyimwa fursa hiyo na ccm/nec makusudi ili wasipige kura. Hawa wata-support chadema kwa vyovyote.

hayo maandamano ya watu milioni 14+ zidi ya milioni 5 wa ccm sijui kama kutakuwa na vifaru/risasi vya kuyazuia!!!
ccm tunataka mabadiliko ya katiba na si vitisho.
 
CCM taifa wamewazuia CCM dar kufanya maandamano maana CCM taifa wanajua kura halisi walizo pata chadema,wanajua utafiti halisi uliyofanywa na synovate,wanajua asilimia ngapi ya watanzania wanaisapoti chadema.Hivyo wakawahi kuwazuia hao bwana wadogo wasije wakawasha moto usiozimika.
Sasa waende mbele na mpango wa kuwafukuza wabunge wa chadema waone.
 
CCM taifa wamewazuia CCM dar kufanya maandamano maana CCM taifa wanajua kura halisi walizo pata chadema,wanajua utafiti halisi uliyofanywa na synovate,wanajua asilimia ngapi ya watanzania wanaisapoti chadema.Hivyo wakawahi kuwazuia hao bwana wadogo wasije wakawasha moto usiozimika.
Sasa waende mbele na mpango wa kuwafukuza wabunge wa chadema waone.

Je hawa synovate wamesajiliwa lini?
 
Nafikiri changamoto hii itawafanya watanzania waamke na kuisoma katiba. Maana wakisikia katiba imevunjwa nafikiri wanavuta picha kama vile msahafu wa dini umevunjwa literally. Chadema ikitolewa bungeni huenda mauzo ya katiba yatapaa.
 
Kwa hilo CCM wasithubutu, maana kitakachofata ni maafa.
Hapa ndipo unapokuja ukweli kuwa kile kitendo kiliwauma sana CCM na kimewaachia majeraha ambayo JK hatayasahau maana watu sasa badala ya kudiscuss hotuba wanadiscuss kitendo cha CHADEMA. Hapa CHADEMA walichanga karata zao vema, na kubadilisha kabisa mtazamo wa wananchi, pamoja na wengi kuponda lakini kitendo cha kutoka kimewafanya wabunge wa CHADEMA kuonekana kuwa wao si watu wa ndio mzee
 
Roho inaniuma roho, hii kazi ya mafisadi roho
CHADEMA kuhujumu roho, Roho inauma roho
Walianza ndogondogo roho, Chadema kuiuma roho
Mafisadi wamepanga roho, CHADEMA kuiua Roho

Enzi zile elfu mbili na tano roho, Mafisadi hawakuhofu roho
Chadema Bado changa roho, Tupambane nayo CUF roho
Mkakati waliweka roho, hiyo CUF kuimeza roho
Mafisadi wamepanga roho, Chadema kuiua roho

Wakaona hiyo Cuf roho kibindoni imetinga roho
Mkakati wakaweka roho Chadema kunanani roho
Japo changa Inatisha roho, Hiyo Chadema kwao mwiba roho
Mafisadi wamepanga roho Chadema kuia roho

Kwa mifano walifanya roho,vikaoni tukaona roho
Zito kabwe fukuzisha roho,ukumbini kama mwizi roho
Wakaona haitoshi roho mijadala wakazima roho
Mafisadi wamepanga roho, Chadema kuiua roho

Walianza naye Wangwe roho, mgogoro pandikiza roho
Mara kifo kimezuka roho, Wao Chadema Singizia roho!
Eti kifo chake kilipangwa roho, Chadema wahusika roho!
Mafisadi wamepanga roho, CHADEMA kuiua Roho

Mtego huo ukashidwa roho, watu wengi stukia hiyo roho
Wakaona wabadilishe gia roho,mtegoni waingize roho
Wakaaza naye Kabwe roho,Kwenye tume muingiza roho
Mafisadi wamepanga roho, CHADEMA kuiua Roho

Kwenye tuma kaingia roho,Zoto kabwe wameweza roho
Mijadala ikazuka roho,Zitto kabwe sio yule roho
Yao manenon akubali roho, Ya mageuzi ayapinga roho
Mafisadi wamepanga roho,Chadema kuiua roho

Pundepunde tukaona roho, mabadiliko taratibu roho
Zitto kabwe sio yule roho, Kauli zake za utata roho
Hazifanani nao mwazo roho, Mafisadi kufanana roho
Mafisadi wamepanga roho, Chadema kuiua roho

Dowans,EPA alipinga roho hapo, mwazo Zitto kabwe roho
Kwenye tuma ametoka roho, Zitto kabwe sio yule roho,
Mafisadi hoja zao roho, Zitto kabwe akubali roho
Mafisadi wamepanga roho, Chadema kuiua roho

Mara uenyekiti mara urais roho, Huyo ndio Zitto kabwe roho
Na mzozo ukazuka roho,Chadema tikisika roho
Zitto kabwe Freeman roho, kunanini kati yao roho
Mafisadi wamepanga roho,Chadema kuiua roho

Yamesikika maneno roho, Mafisadi walihonga roho
Zitto kabwe ahusishwa roho, Siamini macho yangu roho
Kachukua mlungula roho, Zitto kabwe naambwiwa roho
Mafisadi wamepanga roho, Chadema kuiua roho

Wenye viti makatibu roho,Chadema matatizo roho
Nje ndani ndani nje roho, Makatibu nao pia roho
Wenyeviti usiseme roho, Chadema kunanini roho
Mafisadi wamepanga roho Chadema kuiua roho

Kwamfano wa Shitambala roho, Wasiwasi wanishika roho
Kuna nini mtu huyu roho,maneno mengi yamezuka roho
Huko Mbeya kubalika roho, Mbona sasa ipo hivyi roho
Mafisadi wamepanga roho, Chadema kuiua roho

Kuna nini Tanzania roho, nchi yatu inayumba roho
Mafisadi wanania roho, Tanzania kuiuza roho
Wanachi ni vipofu roho, wananchi bado tambua roho
Mafisadi wamepanga roho, Chadema kuiua roho
 

  • Chenge abebeshwa mzigo kuwasilisha hoja binafsi
View attachment 17359

Andrew Chenge​


na Mwandishi wetu


SIKU moja baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati, kueleza mkakati wa kutaka kuwaondoa bungeni wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), chama hicho tawala sasa kinajiandaa kuleta hoja binafsi kuwaondoa wabunge wa CHADEMA, Tanzania Daima Jumapili imeelezwa.



Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata kutoka ndani ya CCM, zilisema chama hicho kimetoa maagizo kwa wanasheria wake ili waandae hoja binafsi itakayowasilishwa bungeni na mwanasheria, Andrew Chenge, kisha kupiga kura ya kutaka wabunge hao waondolewe bungeni.


“Mchezo uliopangwa kufanyika ni kama ule aliofanyiwa Zitto Kabwe alipotoa hoja ya Buzwagi. Licha ya utetezi wake mzuri, aliondoka. Safari hii kazi hii atapewa Chenge, tumepania lazima wabunge wa CHADEMA waondoke bungeni hadi hapo watakaposema wanamtambua rais,” alisema mmoja wa makada wa CCM.



Kwa mujibu wa habari hizo, mpango huo unasubiri baraka za Katibu Mkuu, Yusuf Makamba, ambaye alitarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam jana baada ya kuwa nje ya ofisi yake kikazi.


Kada huyo alipohojiwa ni kifungu gani cha Katiba au cha kanuni za Bunge kilichovunjwa, alishindwa kujibu, lakini alisisitiza kuwa chini ya mkakati huo, CCM itahakikisha inamtumia spika wake mtiifu, Anne Makinda, kuhakikisha wabunge wa CHADEMA wanashughulikiwa.


“Hakuna kitu kilichomuumiza rais kama kitendo cha wabunge wa CHADEMA kusimama na kuondoka kwa dharau. Bora wasingekuja bungeni na katika hilo chama kimedhamiria, Bunge lijalo moto utawaka,” alisema mpashaji habari huyo.


Wakati mkakati huo ukisukwa, CCM Mkoa wa Dar es Salaam, jana iliitisha mkutano na waandishi wa habari kueleza mkakati wake wa kutaka kufanya maandamano ya kulaani kitendo cha wabunge wa CHADEMA kususia hotuba ya Kikwete.


Licha ya kwamba gazeti hili halikualikwa kwenye mkutano huo, taarifa zilizotufikia baadaye zilisema kuwa uongozi wa CCM taifa uliingilia kati na kuamuru maandamano hayo yasifanyike leo hadi watakapopata maelekezo mengine.



CCM juzi ililazimika kutoa taarifa mbili tofauti, moja ikitolewa na Kaimu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Beno Malisa na nyingine ikitolewa na Chiligati, kulaani kitendo hicho na kuahidi kuchukua hatua dhidi ya wabunge wa CHADEMA.


Tamko lililotolewa na Chiligati lilieleza kuwa kitendo hicho cha CHADEMA ni cha uasi na uhaini dhidi ya demokrasia na utawala wa nchi.



Chiligati alisema CHADEMA wanapaswa kutambua kuwa zoezi la uchaguzi lilishuhudiwa na waangalizi wa ndani na nje ya nchi na wameishatoa taarifa kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki.


“Waangalizi wa uchaguzi walishatoa taarifa kwamba uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, sasa iweje CHADEMA peke yao kutotambua matokeo kama si uchochezi unaoweza kusababisha uvunjaji wa amani na kuleta vurugu nchini?” alihoji Chiligati katika taarifa hiyo.


Alisema kwa mujibu wa sheria na Katiba ya nchi, matokeo ya rais yakiwa yametangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) hayapaswi kuhojiwa na mahakama wala chombo chochote, hivyo rais yuko madarakani kwa matakwa ya Katiba hiyo.


“Sasa madai ya CHADEMA kwamba iundwe tume huru ya uchaguzi ichunguze nini?...Nia yao wanataka tuache kazi ya kushughulikia maendeleo ya wananchi ili tuingie katika mgogoro wa kikatiba utakaodumu kwa muda mrefu na kuiingiza nchi katika misuguano na mzozo wa kisiasa?” aliuliza.


Alieleza kuwa chama hicho kimeshangazwa na kitendo cha chama hicho kukubali matokeo ya ubunge na madiwani na kuacha kutambua ya urais, wakati uchaguzi ulifanyika kwa siku moja na kusimamiwa chini ya chombo kimoja kinachodaiwa kuendesha uchakachuaji.



“Tunawasihi CHADEMA waache unafiki, wasiisingizie NEC. Wanalalamikia kura za urais pekee na si za wabunge wala madiwani... kama NEC ilichakachua matokeo ya urais kwa manufaa ya CCM, ilishindwaje kufanya hivyo kwenye kura za wabunge na madiwani?” ilihoji taarifa hiyo.


Chiligati alieleza kuwa walichofanya wabunge wa CHADEMA kususia hotuba ya Rais Kikwete ni kumridhisha Dk. Willbrod Slaa ambaye hana shughuli za kufanya kutokana na kukosa urais na kushindwa kugombea ubunge.


Alisema wabunge hao wamevunja katiba kutokana na kitendo chao cha kutomtambua rais aliyewaweka madarakani kwa mujibu wa kiapo walichokula, hivyo hawastahili kuwepo ndani ya Bunge.


“Tunawashauri wajiondoe bungeni haraka, vinginevyo wajiandae kuondolewa kwa Azimio la Bunge hadi hapo watakapogundua kwamba rais yupo, na serikali ipo,” alisema.


Alieleza kushangaa kuona chama hicho kinapingana na madai yao ya kwamba ni wavumilivu wa kisiasa na wanalinda amani, hali kitendo cha kukacha hotuba ya rais ni wazi kuwa wanaandaa wafuasi wao kuweza kuleta vurugu na uvunjifu wa amani nchini.



Naye Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Benno Malisa, amelaami kitendo hicho na kusema ni ishara ya utovu wa nidhamu kwa wapiga kura waliowachagua.



Lakini CHADEMA kwa nyakati tofauti, wamesema kuwa CHADEMA haisemi haimtambui Kikwete kama Rais wa Tanzania, bali haiyatambui matokeo ya uchaguzi yaliyompa Kikwete mamlaka ya kuwa rais, wakimfananisha na marais wa nchi nyingine wanaotumia mbinu mbalimbali kuupata urais bila ridhaa ya wananchi wanaowaongoza.



Wanasisitiza kuwa Rais Kikwete amewekwa madarakani na Tume ya Uchaguzi, si wapiga kura; na kwamba hawaongelei matokeo ya kura za ubunge kwa sababu sheria inaruhusu kuhoji matokeo ya ubunge kwenye vyombo vya kisheria.



Katika majimbo ambayo CHADEMA haikuridhika na matokeo, inatarajiwa kuyapinga mahakamani. Lakini kwa kuwa sheria haziruhusu kuhoji matokeo ya urais mara Tume ya Uchaguzi ikishayatangaza, jitihada pekee zinazoweza kutumika ni za kisiasa.



Na licha ya CCM kusisitiza kwamba CHADEMA imevunja Katiba, wameshindwa kuonyesha kifungu cha Katiba kilichovunjwa, huku Mnadhimu Mkuu wa Upinzani Bungeni, Tundu Lissu, akisema hawajavunja Katiba.


Hata hivyo, uamuzi huu wa CHADEMA kususa matukio yanayomhusisha rais umemfadhaisha na kumsumbua rais mwenyewe na CCM mbele ya umma na macho ya kimataifa.



Tanzania Daima 21/11/2010



CCMinachofanya ni kutafuta huruma ya wananchi mbumbumbu wasiojua sheria ili waisapoti itakapofanya uhaini wowote, hakuna kipengele kwenye katiba au kwenye kanuni za bunge kinachoweza kuwawezesha kuwatimua chadema, otherwise wajue kuwa wananchi wameamka si kama ilivyokuwa hapo awali.
 
Wakijaribu tuu wataona chamoto. Wawaulize wenzao Arusha, kama si kutangaza matokeo yangetokea maafa. Sasa wasichokoze nyuki maana watu bado wana usongo wa kuibiwa kura waziwazi. Hiyo njia ya CHADEMA ilyo tumika ni ya kistaarabu saana. Sio vita wala maandamano. Watu wamechoka upuuzi wao, wasithubutu kuchokoza watu walio tulia na mikwara mbuzi yao.
Aluta Continua. Mapambano ya kistaarabu bila kumwaga damu bado yanaendelea. VIVA CHADEMA.
 
Tumetumia muda mwingi sana kujadili hii hoja. Sijui ni kwa nini imekuwa hivyo. CHADEMA sio wa kwanza kususia kikao cha bunge imewahi kutokea siku la nyuma kwenye bunge letu la Tanzania, lakini hakukuwa na maneno. Inabidi tuelewe kuwa ccm na CHADEMA ni vyama vyenye itikadi tofauti hivyo haviwezi kuwa na mawazo sawa kila siku na ndio maana hata bungeni wanajulikana kama wapinzani. Kama wapinzani hawaridhiki na kitu fulani wanayo haki ya kujieleza kwa namna yoyote iwayo ile mradi tu wasivunje sheria. Kwanza tutafakari sababu ya wabunge wa upinzani kufanya hivyo na kujaribu kuitatua kama ipo kama haipo wabunge wenyewe na wananchi waambiwe ukweli kwa kukanusha kile wananchodhani wamedhulumiwa. Haina maana kuanza kuleta vitisho, masimngo etc .

Kwa upande mwingine sio mbaya kujiuliza, je, kwa kususia hotuba ya raisi CHADEMA wamevunja sheria gani ya nchi????? Kama ipo tuone sheria inasema nini, kama hakuna tuache maneno tuendelee na kazi zenye tija kuliko kuongelea non issues wiki nzima.
 
wana JF,

Kumekuwepo na taarifa ambazo hazipaswi kupuuzwa na mwanamageuzi wa kweli kuwa, mbinu mbalimbali zimeandaliwa na baadhi zimeshanza kutekelezeka za baadhi ya vigogo kutoka vyama vingine na kuacha vyadhifa zao nyeti na kuhamia chadema,lakini kikubwa ni hapo baadaye kuanzia mwezi april 2013, kuna vigogo wa kutumainiwa watahama kutoka chadema na kuachia nyadhifa zao zote kama ubunge na uongozi kwenye chama.kwa kile kinachoitwa wamechoshwa na Mfumo wa kibabe ndani ya chama chao.

Imepangwa kutekelezwa kuanzia april ili pasiwepo na uchaguzi katika jimbo lililowazi kwa kuwa nusu ya muda wa kutumika utakuwa umekwisha kwa maana ya miaka miwili na nusu huwezi fanya uchaguzi tena, kwa hiyo wanachadema tusifurahie baadhi ya vigogo walioanza hamia cdm,kama baadhi tunaowaona wanatoka kwa mbwembwe katika vyama vyao kwa kile kinachoitwa kutohudumiwa na chama husika,hii imewekwa kuuaminisha umma kwamba hata chadema inapata vigogo toka vyama vingine.

Huu ni mpango mahsusi wa kijasusi unaofanywa na CCM, kuhakikisha kwamba CDM mpaka 2014 isiwepo kabisa, viongozi wangu wapendwa wa CDM ichukulieni kwa umakini mkubwa tahadhali yawezaleta madhara makubwa sana katika chama ambacho ni mbadala kwa watanzania kwa sasa. Na wabunge wa CDM na hasa wenye nyadhifa na ushawishi mkubwa chonde chonde msikisaliti chama chenu kwa kutekeleza mpango haramu wa kijasusi wa CCM.

Tathmini za kisisa zinaonye CCM badala ya kupanda kinazidi kushuka kadri tunavyoelekea uchaguzi mkuu, pamoja na kubadili uongozi na kujinadi na mitandao ya barabara nchini lakini bado wananchi wanataka mabadiriko ya uongozi.

Tujadili tahadhari kwa maslahi mapana ya nchi na chama cha CDM.
 
Tumepokea, Lakini wanatakiwa watambue wao wana FEDHA, UWT,POLICE,JWTZ,TAKUKURU lakini CHADEMA wana Mungu na siku zote mtegemea Mungu Hufanikiwa tofauti na Mtegemea SHETANI, na kama ni kweli hao wanaotaka kuhamia huko wakapate somo kwa Masumbuko Lamwai halafu wajifunze.
 
usiishi kwa wasiwasi kama Lukosi alipohama chama kisa mbowe hajampigia simu au kumtafuta akiwa UK.
kasema moja ya sababu ni kuona barabara zimejengwa sasa sijui zimejengwa na CCM au na kodi za watanzania
na kadai watz wana maisha mazuri sijui ndio wamepewa pesa na CCM ama la
Kijana ishi kwa imani,pigania nchi yako,Chadema ndio mkombozi pekee wa Watanzania
kila kukicha chadema inasonga mbele nami niko mbioni kuchukua kadi ya chadema
 
usiwe na wasiwasi mkuu,wanaotaka mabadiliko ni wananchi na sio wanasiasa.kwa hiyo kwa vyovyote vile lazima tutayafikia hayo mabadiliko tena kupitia chadema.wasaliti wote wataondoka na kutuacha
 
usiishi kwa wasiwasi kama Lukosi alipohama chama kisa mbowe hajampigia simu au kumtafuta akiwa UK.
kasema moja ya sababu ni kuona barabara zimejengwa sasa sijui zimejengwa na CCM au na kodi za watanzania
na kadai watz wana maisha mazuri sijui ndio wamepewa pesa na CCM ama la
Kijana ishi kwa imani,pigania nchi yako,Chadema ndio mkombozi pekee wa Watanzania
kila kukicha chadema inasonga mbele nami niko mbioni kuchukua kadi ya chadema

Mkuu ya Lukosi yaache tu. Huyu jamaa ametia aibu na maneno yake. Sijuhi anaishi UK ya wapi. Kama anaona Tanzania imeendelea na kuridhika hana haja ya kuendelea kupigwa na baridi arudi nyumbani tu kwa sababu vision yake ni ndogo sana. Target yake ya maendeleo ni ndogo mno na hakupaswa kuwa kiongozi.
 
Utaonaje point wakati mkisikia CHADEMA hawalali ili kuwaondoeni madarakani nyie wezi wakuu mmeiba hela mmepeleka swiss, EPA umeme shida, watu wanakufa hasa wakina mama na watoto kwa kukosa huduma muhimu wakati huo mafisadi wanamagari 20 kila mmoja wananchi wakawaida wanakosa hata ambulance moja ya kuwapeleka hosp. CCM nyie ni wauwaji naona na Mungu sasa amesharudi ngoja kwanza huko mahakama ya kimataifa wajibu najua Mungu yupo na mtalipa damu zote zilizomwajika bila aibu. Mungu njoo haraka uwaokoe hawa wakina mama na watoto wanakufa ili hali ardhi hii imejaa madini, gasi na mafuta.
sijaona point hapa
 
Back
Top Bottom