CCM yadai wafadhili wao wameisusa CHADEMA na Wafadhili hao ni Consevative Party

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
CHADEMA yapigwa kombora Arumeru

CCM yadai wafadhili wao wameisusa

Pamela Mollel, Arumeru

C H A M A C h a M a p i n d u z i
(CCM) kimesema siri ya Chama
cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) kutembeza bakuli ya
michango inatokana na wafadhili
wake kukinyima fedha baada
ya Serikali kukataa shinikizo
lililotolewa na Waziri Mkuu wa
Uingereza David Cameroon, la
kutaka nchi zote rafiki na vyama
vyote vya kisiasa kukubali ndoa ya
jinsia moja.

Hayo yalisemwa na mjini hapa
jana na Mkuu wa Kampeni wa
CCM Bw. Mwigulu Nchemba, kwa
nyakati tofauti wakati akihutubia
mikutano ya kampeni ya kumnadi
mgombea wa chama hicho, Bw.
Sioi Sumari.

Bw. Nchemba aliipongeza
Serikali ya Rais Jakaya Kikwete
kwa msimamo wa kukataa shinikizo
la Uingereza la kutaka ndoa za jinsia
moja zisikubalike nchini.

"CCM na Watanzania wote
wanaunga mkono msimamo huo
na hivyo tuko tayari kukosa misaada
kuliko kukubali ndoa za jinsia
moja," alisema.

Aliwaambia wananchi kwamba
siri ya CHADEMA kutembeza
bakuli katika mikutano ya hadhara
kwa wanachama wake ili wachangie
kampeni ni kutokana na wafadhili
wa chama chao Consevative cha
Uingereza kinachoongozwa na
Waziri Mkuu David Cameroon
kukinyima fedha za misaada
kutokana na Serikali ya Rais
Kikwete kukataa kuunga mkono
suala hilo.

Alisema kuwa tangu chama
hicho kianzishwe hakijawahi hata
siku moja kutembeza bakuli na
kuwakamua wanachama na wapenzi
wake kwenye mikutano ya hadhara
baada ya Serikali kukataa masharti
ya ushoga na ndoa za jinsia moja
kama ilivyokuwa imependekezwa
na Uingereza sasa kimeibua mbinu
hiyo ya kuwakamua wanachama na
wafuasi wake.

Aliongeza kuwa katika uchaguzi
mdogo uliofanyika jimbo la Igunga,
mkoani Tabora mwaka jana, chama
hicho kilikuwa na fedha nyingi
ambazo kilipewa msaada na ndio
maana kiliweza kusumbua, lakini
safari hii wamenyimwa ndio maana
hata viongozi wao wa kitaifa
ushiriki wao kwenye kampeni
hizo za Arumeru Mashariki ni wa
kusuasua.

"Haiwezekani ghafla fedha
w a l i z o k u w a w a k i z i f a n y i a
mbwembwe kwenye uchaguzi
wa Igunga zikawa hazipo na
hapa wameshindwa kuonesha
m b w e m b w e h i z o k u m b e
wamenyimwa fedha kutoka kwa
wafadhili sasa kazi waliyobakiza
ni kuwakamua wanachama na
wafuasi wao kwa kutembeza bakuli
kwenye mikutano kama alivyofanya
Mwenyekiti wa Taifa (Bw. Freeman
Mbowe)," alisema Bw. Mwigulu.

Aliwaambia wananchi kuwa
wapinzani wameshindwa kueleza
sera na matokeo yake wanaeneza
propaganda za uongo, lugha za
matusi na chuki.

"Sisi tunaeleza ilani na sera za
kumsaidia mwananchi kuboresha
maisha sanjari na kutatua kero
zilizopo hivyo mchagueni mgombea
wa CCM ambaye sera za chama
chake ndizo zinazotekelezwa na
serikali iliyopo madarakani,"alisema


 
So hiyo inamsaidia vipi mwananchi wa kawaida
Ambaye hana maji au barabara au shule au madawati au ajira
Wao wenye chama na sera nzuri mbona wameshindwa kuiendeleza arumeru miaka yote imebaki na hoi
 
Mwingulu just take the CCM tie from your Neck you will be able to think straight...
 
CHADEMA yapigwa kombora Arumeru

CCM yadai wafadhili wao wameisusa

Pamela Mollel, Arumeru

C H A M A C h a M a p i n d u z i
(CCM) kimesema siri ya Chama
cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) kutembeza bakuli ya
michango inatokana na wafadhili
wake kukinyima fedha baada
ya Serikali kukataa shinikizo
lililotolewa na Waziri Mkuu wa
Uingereza David Cameroon, la
kutaka nchi zote rafiki na vyama
vyote vya kisiasa kukubali ndoa ya
jinsia moja.

Hayo yalisemwa na mjini hapa
jana na Mkuu wa Kampeni wa
CCM Bw. Mwigulu Nchemba, kwa
nyakati tofauti wakati akihutubia
mikutano ya kampeni ya kumnadi
mgombea wa chama hicho, Bw.
Sioi Sumari.

Bw. Nchemba aliipongeza
Serikali ya Rais Jakaya Kikwete
kwa msimamo wa kukataa shinikizo
la Uingereza la kutaka ndoa za jinsia
moja zisikubalike nchini.

"CCM na Watanzania wote
wanaunga mkono msimamo huo
na hivyo tuko tayari kukosa misaada
kuliko kukubali ndoa za jinsia
moja," alisema.

Aliwaambia wananchi kwamba
siri ya CHADEMA kutembeza
bakuli katika mikutano ya hadhara
kwa wanachama wake ili wachangie
kampeni ni kutokana na wafadhili
wa chama chao Consevative cha
Uingereza kinachoongozwa na
Waziri Mkuu David Cameroon
kukinyima fedha za misaada
kutokana na Serikali ya Rais
Kikwete kukataa kuunga mkono
suala hilo.

Alisema kuwa tangu chama
hicho kianzishwe hakijawahi hata
siku moja kutembeza bakuli na
kuwakamua wanachama na wapenzi
wake kwenye mikutano ya hadhara
baada ya Serikali kukataa masharti
ya ushoga na ndoa za jinsia moja
kama ilivyokuwa imependekezwa
na Uingereza sasa kimeibua mbinu
hiyo ya kuwakamua wanachama na
wafuasi wake.

Aliongeza kuwa katika uchaguzi
mdogo uliofanyika jimbo la Igunga,
mkoani Tabora mwaka jana, chama
hicho kilikuwa na fedha nyingi
ambazo kilipewa msaada na ndio
maana kiliweza kusumbua, lakini
safari hii wamenyimwa ndio maana
hata viongozi wao wa kitaifa
ushiriki wao kwenye kampeni
hizo za Arumeru Mashariki ni wa
kusuasua.

"Haiwezekani ghafla fedha
w a l i z o k u w a w a k i z i f a n y i a
mbwembwe kwenye uchaguzi
wa Igunga zikawa hazipo na
hapa wameshindwa kuonesha
m b w e m b w e h i z o k u m b e
wamenyimwa fedha kutoka kwa
wafadhili sasa kazi waliyobakiza
ni kuwakamua wanachama na
wafuasi wao kwa kutembeza bakuli
kwenye mikutano kama alivyofanya
Mwenyekiti wa Taifa (Bw. Freeman
Mbowe)," alisema Bw. Mwigulu.

Aliwaambia wananchi kuwa
wapinzani wameshindwa kueleza
sera na matokeo yake wanaeneza
propaganda za uongo, lugha za
matusi na chuki.

"Sisi tunaeleza ilani na sera za
kumsaidia mwananchi kuboresha
maisha sanjari na kutatua kero
zilizopo hivyo mchagueni mgombea
wa CCM ambaye sera za chama
chake ndizo zinazotekelezwa na
serikali iliyopo madarakani,"alisema



234445.jpg
Watanganyika amkeni muongo huyo! Hivi kwanini wanasiasa hawamwogopi mungu? Hapo wao walikuwa wanaomba DUDU au?
 
‘Mpeni Sioi ubunge mumfute machozi'
Send to a friend
Monday, 19 March 2012 09:23
0digg

0001sioi%20sumari.jpg
Sioi Sumari akiwa amebebwa na wafuasi wa chama chake CCM

Mwandishi Wetu, Arumeru
WANANCHI wa Jimbo la Arumeru Mashariki, wameombwa kumchagua mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM, Sioi Sumari ili kumfuta machozi yaliyotokana na kifo cha baba yake mzazi, Jeremiah Sumari ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo hilo.

Mbali na hilo wananchi hao wameelezwa kuwa kwa kufanya hivyo, watakuwa wamejipatia baraka kwa Mungu kwani watamwezesha Sioi kupata mshahara utakaomwezesha kuendesha familia aliyoachiwa na baba yake.

Mwito huo ulitolewa juzi katika Kijiji cha Migadini, Kata ya Mororoni na Mbunge wa Mtera(CCM), Livingstone Lusinde alipokuwa akimnadi mgombea huyo katika kampeni za uchaguzi mdogo zinazoendelea jimboni humo.

Lusinde alisema wananchi hao wanastahili kuwa na moyo wa huruma kwa kumchagua kwa kura nyingi ili ajipatie mshahara wa kumwezesha kumudu familia aliyoachiwa na marehemu baba yake, ikiwa ni moja ya njia ya kumfuta machozi.

"Mkimchagua Sioi mtapata baraka za Mungu kwa vile mtakuwa mmewezesha kutokea kwa mambo matatu… kwanza kura zenu zitamfuta machozi ya kufiwa na baba yake, pili mtamwezesha kupata mshahara utakaomwezesha kulea familia yake ambayo sasa haina baba," alisema Lusinde.

Pia aliwaambia wananchi hao kwamba kumchagua Sioi kuwa mbunge wa jimbo hilo ni kumfurahisha Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa huyo ndiye chaguo lake na ndiye aliyeongoza vikao vya Kamati Kuu iliyokutana mara mbili kupitisha jina lake kuwa mgombea wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Alisema katika kura hizo za maoni zilizofanyika mara mbili, zote Sioi alionekana kushinda na kuibuka kidedea.

"Njia pekee ya kumfurahisha Rais ni kumchagua Sioi kwa kuwa ni chaguo lake, hakika mtamfurahisha na Sioi ataweza kutekeleza vyema ilani ya chama," alisema Lusinde.

Kwa upande wake, Sioi alisema anayaelewa vyema matatizo yanayoikabili Kata ya Maroroni ikiwemo ukosefu wa mashamba ya uhakika, maji, barabara na zahanati hivyo akichaguliwa, atayatatua matatizo hayo mara moja.

"Nawaombeni sana mnichague kuwa mbunge wenu ili kwa pamoja tuweze kushirikiana kutatua kero hizi ambazo kimsingi zote nazifahamu vyema na nafahamu pia hatua za kuchukua ili kuhakikisha tunaondokana nazo," alisema Sioi.

Shabiki wa Chadema
Katika tukio jingine hekima na busara za Mratibu Mkuu wa kampeni za CCM, Mwigulu Nchemba zilitumika kuepusha maafa kwa mwanachama mmoja wa Chadema, aliyevalia sare za chama hicho baada ya kufika kwenye mkutano wa CCM katika Kata ya Kikatiti.

Wakati Mwigulu akihutubia mkutano huo, mwanachama huyo wa Chadema, ghafla alivamia mkutano huo na kuanza kupiga mayowe huku akitamka maneno ya "Peoples Power" (Nguvu ya umma).

Hatua hiyo iliwakera wafuasi wa CCM ambao waliamua kumtia adabu kabla ya Mwigulu kuingilia kati kuwazuia akiwataka wamwache kwani alikuwa anapaswa kufundishwa sera za CCM.

 
Duuh! Yaani nimesoma huku nimeshika kichwa mbona hawakufunga mahusiano ya kibalozi, mbona our dear leader ametoka UK juzi juzi....
 
Dah mambo mengine haya sio hata ya kuongea jukwaani
ni ya kwenye vijiwe vya kahawa na maeneo ambako wamekaa wanywa kahawa
Watu wamekuja kukusikiliza sera zako na unawaambia nini wajikomboe na umaskini wanaelezwa mambo kama haya
 
Huyu Mwigulu anaumwa? Siamini kama mtu mwenye akili timamu anaweza kusema wa level ya juu kiasi hicho. Uingereza ndio wanaongoza kwa kuchangia bajeti ya serikali (General Budget Support). Approx. theluthi moja ya National budget ya Tanzania inatoka kwa Cameroon. Infact, Uingereza inazidi (kwa misaada hapa TZ) World Bank, IMF! Leo hii Cameroon akikataa kuandika cheque, serikali ya CCM itachemsha vibaya sana. Maajabu haya!
 
Cameron akutana na JK, aisifu Tanzania

28 January 2012 09:12




Fredy Azzah
RAIS Jakaya Kikwete amekutana na Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron na kufanya mazungumzo, huku kiongozi huyo wa Uingereza akisifia Tanzania kwa kupiga hatua katika sekta ya elimu na kilimo.


Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na kusainiwa na Mwandishi wa Habari Msaidizi wa Rais, Premiere Kibanga, Cameron alimweleza Rais Kikwete kuwa Tanzania ni mfano wa kuigwa kwa kuleta mabadiliko chanya kwenye sekta za kilimo na elimu barani Afrika.


"Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron ametoa pongezi hizo kwa Rais Kikwete wakati wa mazungumzo yao jana (juzi) jioni hapa Davos, ambapo wote wawili wanahudhuria mkutano wa uchumi duniani wa kila mwaka, World Economic Forum (WEF)," inaeleza taarifa hiyo. Inasema katika mkutano huo masuala ya uchumi, ikiwamo athari zinazokabili uchumi duniani kwa sasa na jitihada mbalimbali zinazofanywa kuunusuru vitajadiliwa.


"Afrika inapitia kipindi cha mabadiliko ambayo ni chanya, Tanzania ni mfano bora wa kuigwa katika hili," taarifa hiyo ilimnukuu Cameron akimweleza Rais Kikwete walipokutana juzi jioni. Inasema katika mazungumzo yao, Rais Kikwete amemweleza Cameron kuwa kilimo ni sekta kubwa na inayotegemewa na Watanzania wengi na kwamba, Serikali inalenga kujitosheleza kwa chakula ndani na nje ya nchi.


Inasema Rais Kikwete na Cameron pia walizungumzia masuala mbalimbali yanayohusu siasa na usalama barani Afrika. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, awali juzi asubuhi, Rais Kikwete alijumuika na viongozi wengine kutoka Ethiopia, Guinea-Conackry, Kenya na Afrika Kusini kuzungumzia mabadiliko mbalimbali ya uchumi na maendeleo barani Afrika.


Taarifa hiyo inaeleza kuwa, mjadala huo uliongozwa na Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Gordon Brown, ambapo Rais Kikwete alisema bara la Afrika limepata athari mbalimbali zinazotokana na mabadiliko ya uchumi duniani. "Afrika ina mahitaji zaidi katika kutekeleza sera zinazolenga uchumi imara na kuwekeza katika sekta za elimu, utafiti, kilimo, viwanda na miundombinu," taarifa inamkariri Rais Kikwete.
 
CHADEMA yapigwa kombora Arumeru

CCM yadai wafadhili wao wameisusa

Pamela Mollel, Arumeru

C H A M A C h a M a p i n d u z i
(CCM) kimesema siri ya Chama
cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) kutembeza bakuli ya
michango inatokana na wafadhili
wake kukinyima fedha baada
ya Serikali kukataa shinikizo
lililotolewa na Waziri Mkuu wa
Uingereza David Cameroon, la
kutaka nchi zote rafiki na vyama
vyote vya kisiasa kukubali ndoa ya
jinsia moja.

Hayo yalisemwa na mjini hapa
jana na Mkuu wa Kampeni wa
CCM Bw. Mwigulu Nchemba, kwa
nyakati tofauti wakati akihutubia
mikutano ya kampeni ya kumnadi
mgombea wa chama hicho, Bw.
Sioi Sumari.

Bw. Nchemba aliipongeza
Serikali ya Rais Jakaya Kikwete
kwa msimamo wa kukataa shinikizo
la Uingereza la kutaka ndoa za jinsia
moja zisikubalike nchini.

"CCM na Watanzania wote
wanaunga mkono msimamo huo
na hivyo tuko tayari kukosa misaada
kuliko kukubali ndoa za jinsia
moja," alisema.

Aliwaambia wananchi kwamba
siri ya CHADEMA kutembeza
bakuli katika mikutano ya hadhara
kwa wanachama wake ili wachangie
kampeni ni kutokana na wafadhili
wa chama chao Consevative cha
Uingereza kinachoongozwa na
Waziri Mkuu David Cameroon
kukinyima fedha za misaada
kutokana na Serikali ya Rais
Kikwete kukataa kuunga mkono
suala hilo.

Alisema kuwa tangu chama
hicho kianzishwe hakijawahi hata
siku moja kutembeza bakuli na
kuwakamua wanachama na wapenzi
wake kwenye mikutano ya hadhara
baada ya Serikali kukataa masharti
ya ushoga na ndoa za jinsia moja
kama ilivyokuwa imependekezwa
na Uingereza sasa kimeibua mbinu
hiyo ya kuwakamua wanachama na
wafuasi wake.

Aliongeza kuwa katika uchaguzi
mdogo uliofanyika jimbo la Igunga,
mkoani Tabora mwaka jana, chama
hicho kilikuwa na fedha nyingi
ambazo kilipewa msaada na ndio
maana kiliweza kusumbua, lakini
safari hii wamenyimwa ndio maana
hata viongozi wao wa kitaifa
ushiriki wao kwenye kampeni
hizo za Arumeru Mashariki ni wa
kusuasua.

"Haiwezekani ghafla fedha
w a l i z o k u w a w a k i z i f a n y i a
mbwembwe kwenye uchaguzi
wa Igunga zikawa hazipo na
hapa wameshindwa kuonesha
m b w e m b w e h i z o k u m b e
wamenyimwa fedha kutoka kwa
wafadhili sasa kazi waliyobakiza
ni kuwakamua wanachama na
wafuasi wao kwa kutembeza bakuli
kwenye mikutano kama alivyofanya
Mwenyekiti wa Taifa (Bw. Freeman
Mbowe)," alisema Bw. Mwigulu.

Aliwaambia wananchi kuwa
wapinzani wameshindwa kueleza
sera na matokeo yake wanaeneza
propaganda za uongo, lugha za
matusi na chuki.

"Sisi tunaeleza ilani na sera za
kumsaidia mwananchi kuboresha
maisha sanjari na kutatua kero
zilizopo hivyo mchagueni mgombea
wa CCM ambaye sera za chama
chake ndizo zinazotekelezwa na
serikali iliyopo madarakani,"alisema


changiaCCM2010-2.png
Mkiambiwa hawa jamaa wameishiwa sera mnakataa, hapa wao walikuwa anataka kuchangiwa nywele wapeleke kwa mganga au fedha??? Mwigulu gonjwa ya akili, inaropoka tu hovyo kama mtu anayeharisha!!!! Hovyooooooooo!!
 
Mwigulu kapime akili...hivi kuomba watu wakuchangie ni kwasababu ya wafadhili? Kwanini Mwigulu anakuwa na mawazo ya kimaskini hivi? Mawazo yake yamekaa kitegemezi kama mtumwa vile,hii dhana ya misaada imewaathiri sana CCM.Mimi nasema,hata kama ni kweli misaada imekoma,hii dhana ya CDM kuwataka wananchi,wapenzi na wanachama wake kuchangia ni dhana inayofaa kuigwa na hata watawala wetu.Nguvu ya wananchi maskini ikiwekwa pamoja ina uwezo wa kuangusha utawala dhalimu wa CCM.
 
mbona chadema mara nyingi tu inaendesha harambee kwenye mikutano yake?. hili halijaanzia arumeru. Mwigulu ni hopless sana.
 
Huyu Mwigulu anaumwa? Siamini kama mtu mwenye akili timamu anaweza kusema wa level ya juu kiasi hicho. Uingereza ndio wanaongoza kwa kuchangia bajeti ya serikali (General Budget Support). Approx. theluthi moja ya National budget ya Tanzania inatoka kwa Cameroon. Infact, Uingereza inazidi (kwa misaada hapa TZ) World Bank, IMF! Leo hii Cameroon akikataa kuandika cheque, serikali ya CCM itachemsha vibaya sana. Maajabu haya![/QUOTMwigulu anaweza akawa amesoma lakini hakuelimika! Sijui kama alikua anaelewa kama matamshi yake ya uwongo yanaumiza uhusiano wetu na chama kinachoongoza serikali ya Uingereza muda huu na ambao ni wafadhili wakuu wa serikali yetu inayoongozwa na chama chake! Hawa watu CCM inawatoa wapi?!
 
View attachment 49837

Nadhani kuchangia fedha kwa mtandao si hoja, hoja ni kutembeza bakuli!!!!!! Akili nyingine bana yaani kweli Mwigulu anatumia masaburi kufikiri katika hoja ndogo kama hizi, je kubwa si ndiyo ataingia chaka kabisa!!!!
 
"Sisi tunaeleza ilani na sera za
kumsaidia mwananchi kuboresha
maisha sanjari na kutatua kero
zilizopo hivyo mchagueni mgombea
wa CCM ambaye sera za chama
chake ndizo zinazotekelezwa na
serikali iliyopo madarakani,"alisema


Kwa hiyo kuelezea CDM wanakotoa hela za kampeni ndo ilani na sera za kumsaidia mwananchi? Watu wengine bwana sijui wanawachukulia vipi hao wananchi wanaokuwa wanawasikiliza mikutanoni!!
 
Kumbe Chadema ndio wakombozi wa Watanzania kama Mwigulu anajuwa kuwa wako tayari kumpoteza mfadhili kwa mambo yasiyo na tija.Viva CDM.
 
Back
Top Bottom