CCM Yaanza Rafu!, Yaandaa Zengwe Kuwapiga Panga Baadhi ya Wagombea!

Wanabodi, Wazee hao wamekuja na viogezo vipya vitatu ambavyo sikuwahi kuvisikia kwenye sifa za uongozi za CCM hata mara moja!.

1. Umri- eti CCM ichague wagombea wenye umri mkubwa kama uthibitisho wa long expiriance ya uzoefu wa muda
mrefu!
.
2. Awe na shahada ya Chuo Kikuu ama ya Sheria, ama ya Uchumi kwa hoja kuwa kule kuna issues za kisheria na
issues za kiuchumi!.
3. Uzoefu wa kidplomasia.

Lengo la vigezo hivi ni kuwaengua wagombea vijana!
Pasco, Ulivyoileta thread yako inaonyesha wazi uko upande gani, vijana hawatatusaidia chochote kama hawana vigezo vinavyohitajika, na uzuri wake umevitaja. Lile bunge si bunge la kisiasa kama bunge letu la ndani la NDIYOO na kupiga meza, linahitaji mtu mwenye uwezo wa kuchambua sheria na mchumi.

Elewa kule hatuendi kushindana kisiasa vinashindana vifungu vya sheria, tunakwenda kuwaambia Kenya kuwa sheria zetu kwenye ardhi zinasema hivi, kwenye immigration zinasema hivi kama hamkubaliani navyo basi. Kwa hiyo tunahitaji mtu wenye uwezo wa kutetea hayo si kutetea tu mwenye uelewa mzuri. At least awe na ujuzi wowote wa sheria au uchumi, kama huna hivyo unakwenda kufanya nini. Tusifanye masihara kwenye hili wenzetu Kenya na Rwanda wako serious when comes to defend their countries, they mean business.

Kumbuka Nile Delta Agreement Misri walivyotupiga bao kuuvunja ni kazi, tusirudie makosa ya aina hiyo kwa kupeleka incompetent people tutastukia nchi na ardhi inauzwa.
 
Hivi from nowhere kumpeleka "a fresh graduate" kuwakilisha interest za Taifa kwenye Bunge la Afrika Mashariki tunajitendea haki kama Taifa? Mfano madhara ya ardhi kuingizwa au kutoingizwa kwenye Jumuia huyo kijana aliyetoka chuo anafahamu? Unapozungumza kuwa na sarafu moja ndani ya mataifa yanayotofautiana sana katika pato la Taifa "GDP, "skilled labour", "balance of payment", "Industries" n.k. huyo mtoto anafahamu madhara ya hayo yote kwa ukuaji wa Taifa? Iweje "Government Bonds denominated in Euro" ziuzwe Jamhuri ya Ireland na Ujermani za Ujermani zifanye vizuri lakini Ireland zisifanye vizuri wakati sarafu ni moja?


Kwa ajili ya ustawi wa Taifa ni vizuri hivyo vigezo vikazingatiwa na kama waliopitishwa hawana hivyo vigezo, zoezi zima lirudiwe. Kwa maana nyingine ilitakiwa vigezo viwekwe hadharani kabla ya waombaji kujaza fomu.

Mkuu Ndachuwa nashukuru kwa hii maneno umeweka hapa;

1. Pasco; Kwa nini uliamua kutumia maneno kama "Yaanza rafu" na "Yaandaa zengwe" badala ya "Yaweka mazingatio na vigezo vipya kwa wagombea"

Hii ingekuweka wewe (ukiwa mtoa mada not as Pasco) huru na topic hii ila kwa jinsi ilivyo ni kama umekerwa na huafiki hatua hii ambayo mimi naiona ni chanya sana na ina manufaa kwa Taifa hili kwani inatupa sasa nafasi ya kuhoji vigezo vya mwanzo vilivyotufikisha hapa na kuwa na wagombea hawa as yawezekana walioachwa ndo khaswaa tunaowahitaji

KEYS; UMRI, SHAHADA YA UCHUMI NA AU SHERIA, UZOEFU WA KIDIPLOMASIA

Kama kweli tunaipenda nchi yetu na tunataka mabadiliko then ni lazima kuangalia kila jambo with high degree of neutrality so as to obtain and maintain objectivity

UMRI; Sijaona popote walipoweka limitation ila ni zingatio kwamba tuchague watu ambao ni age relevant na kazi tunayotaka kuwapa.....cha maana ni sisi vijana kuwabana wazee kwa hoja kwamba ni vipi tofauti ya umri inaweza kuwa kigezo kama wote ni watu wazima kwa mujibu wa sheria na vigezo vingine muhimu wanavyo.........hapo hachaguliwi baba wa ubatizo jamani....ni Mbunge

SHAHADA; Wao wamependekeza hizo mbili.....kama tunaona hazifai tuweke mbadala na justification ya kila ongezeko au punguzo........sasa kama mtu specialization yake haieleweki tumpe tu kwa sababu ya ujana au uzee wake?????
Mfano; Kuna watu wamesoma political science with/ and economics hawa pia wana mawanda mapana sana kwenye issues revolving arround the stake of the union na kama ni sheria mwanasheria wa wizara ata-complement kwenye mahitaji ya kufanya hivyo......au hata mwanasheria mkuu.....chief justice etc etc...team work approach

UZOEFU WA KIDIPLOMASIA; Yaweza kuwa hoja yenye mashiko lakini ina maswali mengi pia kabla ya kupitishwa.....si tunao mabalozi kwenye nchi hizo husika???? Ofisi za kibalozi zina tija gani kwa union hii??? Attachee(s), Liaisons......is not this a high time for these people to recogn the importance of having round table chambers in their routines?????

Mystand;
1. The so called wazee nao pia ni watu na watapenda kuwa hapo walipo hata kama ni machweo ndo hulka ya wanaadamu walio/ tulio wengi ila kwa sababu mawasiliano yanawezesha kuwa na malumbano ya hoja kama hivi then tuendelee kuboresha hoja zetu kama vijana.
2. Unless we have good, sustainable and persistent pressure being echoed with clearly defined pre-requisites on the so called liberation via youths tutakuwa tunaonekana kama walalamishi na waroho wa madaraka kwa sababu hoja za hao wanaotaka kutuwakilisha (vijana) ni sooo light yaani kama ni mtihani kwa kweli watafeli wanashindwa kutuwekea plans, mission, vission za wao kama vijana as compared to Wazee wetu.....sasa hapo ujana utatusaidia nini???? Labda kama kuna kukimbia huko bungeni sawa

Hii sio rafu wala zengwe ni changamoto tu na kama kweli sisi vijana tumeazimia kuleta mabadiliko na tuanze kuwa na tabia ya kuchukulia mambo kama fursa na si kama vikwazo......na ndio moja kati ya tofauti baina ya THE CONSCIOUS REVOLUTIONARIST as compared to A MERE POLITICAL ASPIRANT
 
Wanabodi,

Nyakati za uchaguzi mjini Dodoma, ni nyakati, za harakati kubwa na pilika pilika nyingi katika mji wa Dodoma, hivyo sisi wenye interest na siasa za nyumbani, tupatapo nafasi, hupenda kupeleka pua japo kidogo mjini Dodoma japo kunusa tuu kile kinachoendelea.

Miongoni mwa pilika pilika kubwa za kisiasa mjini Dodoma kwa sasa, ni harakati za kugombea ubunge wa Afrika Mashariki ambapo vikao vya wazi na vya siri vimekuwa vikiendelea mjini hapa, huku wagombea wakijitahidi kuandaa "the winning coalition", huku wabunge ambao ndio walengwa wakijikuta katika wakati mgumu kuchagua kambi ya mgombea gani waiunge mkono!.

Mvutano mkubwa wa vuta nikuvute, shika nikushike ni miongoni mwa wagombea 9 wa CCM wanaogombea nafasi 3, hivyo ushindani ni mkubwa kuliko huku kila mmoja akiepuka kudondokea miangoni mwa wale 6 wataopigwa chini, hivyo pia kuna harakati za chini chini kila mmoja wao akifanya jitihada za kujinusuru.

Ushindani mkubwa ni kati ya wale wanaowaunga mkono vijana wa kisasa ambao wana uughwaji mkubwa na wana CCM wanaotaka mageuzi ya ukweli dhidi ya wagombea wazee ambao tayari ni spent force, watakuwa hawana jipya la kuleta zaidi ya kumendea fungu la kustaafu kwa heshima!.

Kufuatia upepo kuwavumia vizuri wagombea vijana, kuna tetesi kuwa wagombea wazee kwa kuwatumia wazee wa CCM, wamejipanga kuwaundia zengwe wagombea vijana ili kuwapiga panga la kimtindo!.

Zengwe hili linapikwa chini kwa chini ambapo kwa kuamua kuandaa vigezo vitatu vya sifa mpya za wagombea wa CCM ambavyo wata lobby kuvipeleka kwenye caucus ya CCM over the weekend ili vipitishwe hivyo kuwapiga panga wagombea vijana wenye uugwaji mkubwa wa wabunge wengi.

Zengwe hilo ambalo msingi wake mkubwa ni kupiga fitna ili kuwapiga chini wagombea vijana.

Wazee hao wamekuja na viogezo vipya vitatu ambavyo sikuwahi kuvisikia kwenye sifa za uongozi za CCM hata mara moja!.

1. Umri- eti CCM ichague wagombea wenye umri mkubwa kama uthibitisho wa long expiriance ya uzoefu wa muda
mrefu! .
2. Awe na shahada ya Chuo Kikuu ama ya Sheria, ama ya Uchumi kwa hoja kuwa kule kuna issues za kisheria na
issues za kiuchumi!.

3. Uzoefu wa kidplomasia.

Lengo la vigezo hivi ni kuwaengua wagombea vijana!

Baadhi ya wabunge wa EALA ambao ambao hawagombei tena, wamepiga kambi bungeni hapa wakiwa na wagombea wao kwapani, wengi wakiwa ni hawa wazee ambao ni spent force!.

Wakati huo huo, nimehudhuria tafrija moja mahali, usiku huu hapa Dodoma, kufumba kufumbua, kumbe ni tafrija ya kampeni ya wazee fulani wawili, ambao walituamkia wote kwa shikamoo!.

My Take.
CCM kama chama, kimekaa mkao wa kifo, watu pekee wanaoweza kukinusuru CCM na kifo cha aibu, ni hawa wagombea vijana wa kileo ambao sasa wanataka kupigwa zengwe. Kama kweli itatokea CCM ikawapiga zengwe hawa vijana, hiyo ndio itakuwa uthibitisho wa CCM ni chama mfu, hakiwahitaji vijana wa kisasa, wito wangu kwa vijana hawa ni kuwa baada ya kupingwa panga, hameni CCM, achaneni na CCM ili mjiokoe nafsi zenu kwa 2015, jiungeni na vyama vinavyo kubali nguvu ya vijana, vinginevyo down the drain, mtakwenda chini na CCM yenu!.

Asante.

Pasco.

Hii ni hoja muhimu sana kuliko kupeleka baharia...
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom