Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Na Mwandishi wetu.
MTAFARUKU mkubwa umezuka ndani ya kikao cha Kamati ya Maadili ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Kyela uliosababisha Polisi kuingilia kati na kumwokoa Katibu wa chama hicho wilaya, Bi. Maria Mwambanga.
Polisi walichukua hatua hiyo baada ya, Bi. Mwambanga kupokea kipigo kutoka kwa wanachama hao waliomtuhumu kuwa ni kibaraka wa baadhi ya wanasiasa huku wajumbe wengine wakitwangana makonde wao kwa wao.
Kikao hicho cha Kamati ya Maadili, kiliwaita makatibu kata wa chama hicho wa Kata za Kyela mjini, Kajunjumele, Makwale, Lusungo, Katumba Songwe, Itope na Diwani wa Kyela Mjini, Bw. Visk Mahenge wakidaiwa kuwa walimkashifu Mbunge wa Kyela, Dkt. Harrison Mwakyembe kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya
Kamati hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti, Bw. Japhet Mwakasumi na Katibu wake Bi. Mwambanga, waliwaeleza makatibu hao na diwani kuhusu kumkashifu, Dkt. Mwakyembe na kuwataka waeleze sababu za kufanya hivyo na kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu.
Kwa mujibu wa mmoja wa watuhumiwa hao, ugomvi uliibuka baada ya wao kuhoji hatua ya kuitwa peke yao bila pande zote zinazohusika kwenye mvutano huo.
Baada ya suala hilo kuzua mtafaruku mkubwa, Polisi walifika eneo hilo la ofisi ya CCM wilaya kumwokoa Katibu huyo aliyekuwa akipokea kipigo, huku wajumbe wa kikao hicho wakisambaratika kila mtu na njia yake kwa hofu ya kukamatwa na Polisi.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Bw. Japhet Mwakasumi alipotakiwa kuzungumzia sakata hilo alisema kwa muda huo akili yake ilikuwa haijatulia hadi hapo baadae.
Naye Mwandishi Grace Michael anaripoti kuwa katika kile kinachoonesha kuwa hali si shwari katika majimbo mengi ndani ya CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu mwakani, Mbunge wa Ukonga Dkt. Makongoro Mahanga ameonya dhidi ya tabia ya wana CCM kuchafuana.
Dkt. Mahanga amewataka badhi ya wanachama wenye nia ya kugombea udiwani na ubunge kuacha mara moja tabia ya kupitapita kwa wananchi na kuchafua majina ya viongozi waliopo madarakani kwa lengo la kujipatia umaarufu kisiasa.
Alidai mbali ya kuchafua majina ya vingozi pia wanakwamisha utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kuwachanganya wananchi na kupoteza mwelekeo wao wa kushirikiana na viongozi katika shughuli mbalimbalia za maendeleo.
Akifungua semina ya Jumuiya ya Wazazi katika Kata ya Ukonga, Dar es Salaam juzi, Dkt. Mahanga alisema ni vyema wanachama wa CCM, wakatumia muda huu kuweka mikakati ya namna chama hicho kitakavyoibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
"Wapo baadhi ya wana CCM ambao tayari wameanza kuwapitisha wagombea wao kwa wananchi ili kufanya kampeni za ubunge mwakani, hatukatai watu kujitokeza kugombea kwani ni haki yao kidemokrasia lakini ni lazima kanuni na taratibu za uchaguzi za CCM zifuatwe kwa maana ya muda wa kuanza kampeni hizo," alisisitiza Dkt. Mahanga.
Alisema kuwa tatizo kubwa linalofanywa na wagombea hao ni kupita kwa wananchi huku wakitoa kashfa kwa viongozi ambao bado wako madarakani nakuwataka kuacha mara moja tabia hiyo na kujikita katika kumaliza kero za wananchi zilizobaki katika kipindi hiki.
Dkt. Mahanga alisema kuwa, vitendo vya kuchafuana kwa sasa vitasababisha kukwama kwa utekelezwaji wa Ilani ya CCM, ambapo kiongozi aliyepo madarakani anatakiwa kushirikiana na wananchi wake katika utekelezaji huo.
"Kuanza kuvutana kwa sasa ni kupoteza dira kwani uchaguzi ni mwakani hivyo ni bora tukajikita kwanza kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na sio kuweka nguvu katika uchaguzi ambao muda wake bado, lakini wanaotumia jina la Mbunge kusaka udiwani hilo nalo pia ni tatizo linaloweza kunigombanisha na wanachama wangu, haya mambo tuyaache kwanza," alionya Dkt. Mahanga.
Naye Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji, Bw. Ahmad Mkude, alisema kuwa vitendo vya watu kupita kwa wananchi huku wakiharibu majina ya viongozi, si sahihi hivyo aliwataka wanajumuiya hiyo kuwa makini na watu hao.
"Hawa watatugombanisha na viongozi wetu, tunatakiwa kuwa makini zaidi na sio kusikiliza maneno ya watu bila kuangalia wamefanya nini ndani ya jamii yetu, wanatakiwa kuja kwa hoja lakini si kwa kashfa kwa kiongozi aliyepo na tukiendekeza itatugawa na madhara makubwa yatatokea ndani ya chama chetu," alisema Bw. Mkude.
MTAFARUKU mkubwa umezuka ndani ya kikao cha Kamati ya Maadili ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Kyela uliosababisha Polisi kuingilia kati na kumwokoa Katibu wa chama hicho wilaya, Bi. Maria Mwambanga.
Polisi walichukua hatua hiyo baada ya, Bi. Mwambanga kupokea kipigo kutoka kwa wanachama hao waliomtuhumu kuwa ni kibaraka wa baadhi ya wanasiasa huku wajumbe wengine wakitwangana makonde wao kwa wao.
Kikao hicho cha Kamati ya Maadili, kiliwaita makatibu kata wa chama hicho wa Kata za Kyela mjini, Kajunjumele, Makwale, Lusungo, Katumba Songwe, Itope na Diwani wa Kyela Mjini, Bw. Visk Mahenge wakidaiwa kuwa walimkashifu Mbunge wa Kyela, Dkt. Harrison Mwakyembe kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya
Kamati hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti, Bw. Japhet Mwakasumi na Katibu wake Bi. Mwambanga, waliwaeleza makatibu hao na diwani kuhusu kumkashifu, Dkt. Mwakyembe na kuwataka waeleze sababu za kufanya hivyo na kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu.
Kwa mujibu wa mmoja wa watuhumiwa hao, ugomvi uliibuka baada ya wao kuhoji hatua ya kuitwa peke yao bila pande zote zinazohusika kwenye mvutano huo.
Baada ya suala hilo kuzua mtafaruku mkubwa, Polisi walifika eneo hilo la ofisi ya CCM wilaya kumwokoa Katibu huyo aliyekuwa akipokea kipigo, huku wajumbe wa kikao hicho wakisambaratika kila mtu na njia yake kwa hofu ya kukamatwa na Polisi.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya, Bw. Japhet Mwakasumi alipotakiwa kuzungumzia sakata hilo alisema kwa muda huo akili yake ilikuwa haijatulia hadi hapo baadae.
Naye Mwandishi Grace Michael anaripoti kuwa katika kile kinachoonesha kuwa hali si shwari katika majimbo mengi ndani ya CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu mwakani, Mbunge wa Ukonga Dkt. Makongoro Mahanga ameonya dhidi ya tabia ya wana CCM kuchafuana.
Dkt. Mahanga amewataka badhi ya wanachama wenye nia ya kugombea udiwani na ubunge kuacha mara moja tabia ya kupitapita kwa wananchi na kuchafua majina ya viongozi waliopo madarakani kwa lengo la kujipatia umaarufu kisiasa.
Alidai mbali ya kuchafua majina ya vingozi pia wanakwamisha utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kuwachanganya wananchi na kupoteza mwelekeo wao wa kushirikiana na viongozi katika shughuli mbalimbalia za maendeleo.
Akifungua semina ya Jumuiya ya Wazazi katika Kata ya Ukonga, Dar es Salaam juzi, Dkt. Mahanga alisema ni vyema wanachama wa CCM, wakatumia muda huu kuweka mikakati ya namna chama hicho kitakavyoibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
"Wapo baadhi ya wana CCM ambao tayari wameanza kuwapitisha wagombea wao kwa wananchi ili kufanya kampeni za ubunge mwakani, hatukatai watu kujitokeza kugombea kwani ni haki yao kidemokrasia lakini ni lazima kanuni na taratibu za uchaguzi za CCM zifuatwe kwa maana ya muda wa kuanza kampeni hizo," alisisitiza Dkt. Mahanga.
Alisema kuwa tatizo kubwa linalofanywa na wagombea hao ni kupita kwa wananchi huku wakitoa kashfa kwa viongozi ambao bado wako madarakani nakuwataka kuacha mara moja tabia hiyo na kujikita katika kumaliza kero za wananchi zilizobaki katika kipindi hiki.
Dkt. Mahanga alisema kuwa, vitendo vya kuchafuana kwa sasa vitasababisha kukwama kwa utekelezwaji wa Ilani ya CCM, ambapo kiongozi aliyepo madarakani anatakiwa kushirikiana na wananchi wake katika utekelezaji huo.
"Kuanza kuvutana kwa sasa ni kupoteza dira kwani uchaguzi ni mwakani hivyo ni bora tukajikita kwanza kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na sio kuweka nguvu katika uchaguzi ambao muda wake bado, lakini wanaotumia jina la Mbunge kusaka udiwani hilo nalo pia ni tatizo linaloweza kunigombanisha na wanachama wangu, haya mambo tuyaache kwanza," alionya Dkt. Mahanga.
Naye Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji, Bw. Ahmad Mkude, alisema kuwa vitendo vya watu kupita kwa wananchi huku wakiharibu majina ya viongozi, si sahihi hivyo aliwataka wanajumuiya hiyo kuwa makini na watu hao.
"Hawa watatugombanisha na viongozi wetu, tunatakiwa kuwa makini zaidi na sio kusikiliza maneno ya watu bila kuangalia wamefanya nini ndani ya jamii yetu, wanatakiwa kuja kwa hoja lakini si kwa kashfa kwa kiongozi aliyepo na tukiendekeza itatugawa na madhara makubwa yatatokea ndani ya chama chetu," alisema Bw. Mkude.