Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Magazeti mengi leo yakiwemo Mtanzania na Majira yameripoti Waziri mwenye dhamana ya kusimamia maendeleo ya elimu hapa chini Profesa Jumanne Maghembe akinena ya kuwa sera ya elimu ya chama chake cha CCM ni kuruhusu wahitimu wa darasa la saba kuendelea kidato cha kwanza bila ya mchujo.
Hii inamaanisha ya kuwa kufanya vizuri darasani sasa siyo sera ya CCM ili mradi tu CCM wapate idadi kubwa ya wahitimu wa kidato cha nne bila ya kujali ujuzi ambao watakuwa wameupata: Quantity vs Quality..........CCM opts for quantity and trivialize quality in the process.
Vile vile Prof. Maghembe alitofautiana na viongozi wa ngazi ya juu ndani ya chama tawala pale alipodai ya kuwa elimu bure ni sera ya CCM. Hili linashangaza kwa sababu viongozi wengi wa ngazi ya juu ndani ya chama hicho wameendelea kuviponda vyama vya upinzani ya kuwa elimu bure haiwezekani na ni njozi za alinacha...........Ikumbukwe mahitaji ya miundo mbinu ya kutimiza njozi hii ya Prof. Maghembe ni kubwa maradufu na kama miaka mitano iliyopita mashule na zahanati bado zilizokusudiwa bado hazijakamilka na nyumba za waalimu ni ahadi nyingine hewa ya miaka mitano ijayo. Sijui ni lini CCM wataanza kujifunza kuacha kudharau uwezo wa watanzania katika kupambanua mambo.......
Hili linatia mashaka ya kuwa pengine Prof. Maghembe baada ya kuona upepo mkali wa matarajio ya raia kutaka elimu iwe bure basi ameamua kuigeuza sera ya chama chake bila ya ridhaa ya Kamati kuu au Halmashauri Kuu ya chama chake.
Vile vile si katika ilani ya uchaguzi ya CCM ambapo suala la elimu bure limewekwa bayana hata kidogo.
Prof. Maghembe anaonekana hana mawasiliano na uongozi wa juu ndani ya chama chake kwa sababu hakuonyesha ni elimu ipi ambayo CCM itatoa bure na kuanzia lini na itagharimu nini ukizingatia ahadi za mgombea uraisi wa CCM hadi hivi sasa zimezidi trilioni 90 na huku akidai elimu na afya havitakuwa bure.
Ni dhahiri kama elimu nayo ni bure kwa CCM basi jumla ya ahadi zake sasa zitazidi trilioni tisini ambazo hata hapo zilipo hazitekelezeki hata wapigakura wangeliamua kuipa CCM miaka mingine ishrini madarakani.......... Kwa hiyo CCM ni danganya toto.........
Hii inamaanisha ya kuwa kufanya vizuri darasani sasa siyo sera ya CCM ili mradi tu CCM wapate idadi kubwa ya wahitimu wa kidato cha nne bila ya kujali ujuzi ambao watakuwa wameupata: Quantity vs Quality..........CCM opts for quantity and trivialize quality in the process.
Vile vile Prof. Maghembe alitofautiana na viongozi wa ngazi ya juu ndani ya chama tawala pale alipodai ya kuwa elimu bure ni sera ya CCM. Hili linashangaza kwa sababu viongozi wengi wa ngazi ya juu ndani ya chama hicho wameendelea kuviponda vyama vya upinzani ya kuwa elimu bure haiwezekani na ni njozi za alinacha...........Ikumbukwe mahitaji ya miundo mbinu ya kutimiza njozi hii ya Prof. Maghembe ni kubwa maradufu na kama miaka mitano iliyopita mashule na zahanati bado zilizokusudiwa bado hazijakamilka na nyumba za waalimu ni ahadi nyingine hewa ya miaka mitano ijayo. Sijui ni lini CCM wataanza kujifunza kuacha kudharau uwezo wa watanzania katika kupambanua mambo.......
Hili linatia mashaka ya kuwa pengine Prof. Maghembe baada ya kuona upepo mkali wa matarajio ya raia kutaka elimu iwe bure basi ameamua kuigeuza sera ya chama chake bila ya ridhaa ya Kamati kuu au Halmashauri Kuu ya chama chake.
Vile vile si katika ilani ya uchaguzi ya CCM ambapo suala la elimu bure limewekwa bayana hata kidogo.
Prof. Maghembe anaonekana hana mawasiliano na uongozi wa juu ndani ya chama chake kwa sababu hakuonyesha ni elimu ipi ambayo CCM itatoa bure na kuanzia lini na itagharimu nini ukizingatia ahadi za mgombea uraisi wa CCM hadi hivi sasa zimezidi trilioni 90 na huku akidai elimu na afya havitakuwa bure.
Ni dhahiri kama elimu nayo ni bure kwa CCM basi jumla ya ahadi zake sasa zitazidi trilioni tisini ambazo hata hapo zilipo hazitekelezeki hata wapigakura wangeliamua kuipa CCM miaka mingine ishrini madarakani.......... Kwa hiyo CCM ni danganya toto.........