CCM waomba rasmi msaada wa dola kuwadhibiti wapinzani wao wakuu, CHADEMA

Naitaman cku ile ya ukomboz ...nayo yaja i karibuni...ndio hapo ccm watakapo kumbuka shuka while kushakucha..
 
Hebu tuwe Wakweli na kuacha Ushabiki wa Kisiasa na kuangalia Mustakbali wa nchi yetu Kama kweli tuna Uchungu nayo, Maandamano ya Chadema as Such si tatizo kubwa, si Watu wanaandamana Kisha by Rae end of The day Wanaenda kulala? Lakini kauli zinazotolewa na Viongozi wa Chadema kwenye Mikutano ya Hadhara ya kuhitimisha maandamano hayo, Kwa kweli si Njema kwa Usalama wa Nchi yetu, k.m. kauli za Freeman kule Mwanza baada Maandamano, aliwahamasisha watu Wamkatae Rais wa Nchi (Kikwete) na Wawe tayari kwa lolote. Yanini? Kule Tunisia na Misri, maandamano hayakuongozwa na Vyama vya Siasa bali Wananchi waliochoshwa na Viongozi wao waliokaa Miaka mingi na Hawakuwa na Dalili za kuondoka Madarakani, Wananchi wakiamua, hakuna nguvu za Dola zinazoweza kuwadhibiti, lakini Wawe wameamua Wenyewe kwa kuona Hali imeshindikana, Sio kwa kuchochewa na Chama Fulani cha Siasa kinachotaka kushika Madaraka kwa Kuwaingiza watu Barabarani wala Msituni, angalieni Huko Tunisia na Misri mnakopenda kutolea Mfano, hakuna Chama kilichoshika Madaraka na Wala hakuna kinachoelekea kushika, Bali Misri ni Jeshi (la Mubarak) ndilo linaongoza, na Tunisia ni Vurugu Tupu zinaendelea kwani Waandamanaji hivi Sasa wamegeuka Vibaka wanapora Ovyo maduka na Kila Biashara iliyo Mbele Yao, Hali ni mbaya mno na Hakuna Mwelekeo wowote, Kama Chadema inadai inataka Kufanya hivyo, haitafanikiwa, Watanzania tulio Wengi hatutakubali. Savimbi aliposhindwa Uchaguzi alikuwa na Madai Kama ya Slaa na Chadema na alikuwa na wafuasi Wengi katika Maeneo mengi ya Nchi yake ya Angola kuliko ilivyo Chadema kwa Tanzania (Msisahau Chadema imeshindwa hata Kusimamisha Wagombea tu katika Majimbo Takriban 50! Na imeshinda 9% ya majimbo yote, basi hata Kama ni kuibiwa Kura lakini si kwa Kiasi hicho!) alianza Kama Chadema inavyoanza sasa, akapata Support ya nchi za Magharibi na akaanzisha Mapambano ya kisawsawa ya Kuondoa utawala wa MPLA, lakini wafuasi wa MPLA walikuwa wengi Zaidi, hivyo damu ilimwagika Kisawasawa Kuliko maelezo, kwa Miaka mingi. Savimbi alipochinjwa, Amani ikapatikana Angola kwa Kiasi kikubwa, hata Wafuasi wa Savimbi wanajutia walichofanya, hivi sasa wako Pamoja wanajenga Nchi Yao, Vyama vya Siasa vipo vinaendelea na Siasa na wanaamini Wakitaka kuiondoa MPLA wataweza kufanikiwa ikibidi kwa njia za Kisiasa na Sio Kama hivi Chadema inavyotaka kufanya.
 
mbona maandamano kanda ya ziwa yameenda shwari jamani? Hawa ccm wanataka wawapangie cdm ratiba ya kuendesha mambo yao?
 
Hebu tuwe Wakweli na kuacha Ushabiki wa Kisiasa na kuangalia Mustakbali wa nchi yetu Kama kweli tuna Uchungu nayo, Maandamano ya Chadema as Such si tatizo kubwa, si Watu wanaandamana Kisha by Rae end of The day Wanaenda kulala? Lakini kauli zinazotolewa na Viongozi wa Chadema kwenye Mikutano ya Hadhara ya kuhitimisha maandamano hayo, Kwa kweli si Njema kwa Usalama wa Nchi yetu, k.m. kauli za Freeman kule Mwanza baada Maandamano, aliwahamasisha watu Wamkatae Rais wa Nchi (Kikwete) na Wawe tayari kwa lolote. Yanini? Kule Tunisia na Misri, maandamano hayakuongozwa na Vyama vya Siasa bali Wananchi waliochoshwa na Viongozi wao waliokaa Miaka mingi na Hawakuwa na Dalili za kuondoka Madarakani, Wananchi wakiamua, hakuna nguvu za Dola zinazoweza kuwadhibiti, lakini Wawe wameamua Wenyewe kwa kuona Hali imeshindikana, Sio kwa kuchochewa na Chama Fulani cha Siasa kinachotaka kushika Madaraka kwa Kuwaingiza watu Barabarani wala Msituni, angalieni Huko Tunisia na Misri mnakopenda kutolea Mfano, hakuna Chama kilichoshika Madaraka na Wala hakuna kinachoelekea kushika, Bali Misri ni Jeshi (la Mubarak) ndilo linaongoza, na Tunisia ni Vurugu Tupu zinaendelea kwani Waandamanaji hivi Sasa wamegeuka Vibaka wanapora Ovyo maduka na Kila Biashara iliyo Mbele Yao, Hali ni mbaya mno na Hakuna Mwelekeo wowote, Kama Chadema inadai inataka Kufanya hivyo, haitafanikiwa, Watanzania tulio Wengi hatutakubali. Savimbi aliposhindwa Uchaguzi alikuwa na Madai Kama ya Slaa na Chadema na alikuwa na wafuasi Wengi katika Maeneo mengi ya Nchi yake ya Angola kuliko ilivyo Chadema kwa Tanzania (Msisahau Chadema imeshindwa hata Kusimamisha Wagombea tu katika Majimbo Takriban 50! Na imeshinda 9% ya majimbo yote, basi hata Kama ni kuibiwa Kura lakini si kwa Kiasi hicho!) alianza Kama Chadema inavyoanza sasa, akapata Support ya nchi za Magharibi na akaanzisha Mapambano ya kisawsawa ya Kuondoa utawala wa MPLA, lakini wafuasi wa MPLA walikuwa wengi Zaidi, hivyo damu ilimwagika Kisawasawa Kuliko maelezo, kwa Miaka mingi. Savimbi alipochinjwa, Amani ikapatikana Angola kwa Kiasi kikubwa, hata Wafuasi wa Savimbi wanajutia walichofanya, hivi sasa wako Pamoja wanajenga Nchi Yao, Vyama vya Siasa vipo vinaendelea na Siasa na wanaamini Wakitaka kuiondoa MPLA wataweza kufanikiwa ikibidi kwa njia za Kisiasa na Sio Kama hivi Chadema inavyotaka kufanya.

Kama kawaida yenu ccm huwa mnatishia wananchi ili wahofu kwamba amani inaweza kuvurugika, kisha wananchi wakitulia mnaendelea kuwaibia mali zao kupitia dowans, meremeta, tangold, kiwira coal mines, mwananchi gold, etc. Wakati wa uchaguzi mnatumia mapato haramu kuwahonga walalahoi chumvi, tshirt za kifisadi, sh 2000/-, etc huku mkiongezea ahadi tele! Dawa yenu ni kuwabana msilale mkamaliza shamba lote peke yenu, amani itakujaje huku nyinyi mkiendelea kufaidi nchi hii peke yenu kwa gharama ya kudumisha "amani na usalama?"
 
mbona maandamano kanda ya ziwa yameenda shwari jamani? Hawa ccm wanataka wawapangie cdm ratiba ya kuendesha mambo yao?
Matamshi yatolewayo na Viongozi wa CDM baada ya Maandamano ndiyo yenye Utata, hakutakuwa na Mwisho mwema, Kwani wasiokubaliana na Matamshi hayo nao pia wapo na ni Wengi pia, Jee nao Wakiingia barabarani Hali itakuwaje?
 
Mimi nadhani CCM bado hawajajua maana halisi ya Peoples Power, wanadhani maana yake ni kuiondoa serikali iliyoko madarakani. japo uelekeo wake ni huo kutokana na maasi yanayofanywa na serikali ya ccm. Tatizo ccm wamejaa viongozi ambao hawana vision. wamezeeka akili ikachakaa.
Tutaandamana nchi nzima kuonyesha kwa katiba hii hii mbovu mpaka kieleweke.

CCM acheni kulewa madaraka tambueni kuwa sauti umma ni sauti ya mungu mjue hilo!
 
ambacho kinafanya maandamano na
mikutano ya hadhara nchi nzima.Maandamano na
mikutano hiyo,kwa mujibu wa viongozi wa CHADEMA yana malengo ya kupinga malipo ya fidia ya sh.bilioni 94 kwa kampuni ya kufua umeme ya dowans,kupinga kupanda kwa
gharama za maisha,kupinga kupanda kwa gharama za umeme,kupinga vitendo vya ufisadi,kuishinikiza serikali ya jk iweke ratiba ya mchakato utakaohakikisha uchguzi wa mwaka 2015 unafanyika chini ya katiba mpya.<br />
CCM na serikali yake hawana majibu kwa hoja hizi nzito za CHADEMA,sasa wanakimbilia kuomba msaada wa dola.Kwa CCM kujifanya ionekane inaomba msaada wa dola badala ya kuviagiza vyombo vya dola ni unafiki mkubwa wa kisiasa,CCM wanataka waonekane machoni pa watanzania kuwa&quot;hawatumii vibaya vyombo vya dola kuudhibiti upinzani,wakati inajulikana ni tabia yao kuvitumia vyombo vya dola kuwadhibiti wapinzani wao.<br />
Kitendo cha CCM kuomba msaada wa dola kuwamaliza CHADEMA kisiasa ni ishara ya kufilisika kihoja na kisiasa,CCM sasa hawana hoja wanakimbilia kutumia nguvu za dola ambazo ziko chini ya udhibiti wao. CCM kutaka waeleweke na watu kwamba wanaomba msaada wa dola ni uzandiki na hadaa kwa watanzania.<br />
Alichokiongea bwana Chiligati leo na wandishi wa habari alipokuwa anatoa tamko la kuomba msada wa dola kuidhibiti CHADEMA,hakina tofauti na kile alichokiongea bosi wake Kikwete.Kwa maana hiyo dhamira ya kuwabana CHADEMA ilishaanza kusukwa kabla hata kikwete hajaiweka hotuba yake yenye vitisho kwa CHADEMA hadharani kwa taifa.<br />
Wakati katibu mkuu wa CHADEMA DK Wilbrod Slaa akisisitiza kwamba maandamano yanafanywa na CHADEMA ni ya amani ya yenye shabaha ya kuihimiza serikali iitikie kilio cha Umma ofisi ya msajili wa vyama vya siasa chini ya bwana tendwa imeungana na CCM kuwatisha na hatimaye kuwadhofisha CHADEMA kwa kuwasingizia kwamba wanafanya &quot;UCHOCHEZI&quot; katika mikutano yao.<br />
Kudhihirisha kwamba anataka kuwafurahisha CCM au anatekeleza matakwa ya kisiasa ya CCM,Tendwa amefikia hatua ya kutamka maneno ya kukifuta CHADEMA na kuzungumzia uwezekano wa mkurugenzi wa mashita ya jinai kuwafungulia mashitaka CHADEMA.<br />
Mtiririko wote huu unaonesha jinsi serikali ilivyojipanga kuwadhibiti CHADEMA.Fikiria Mtiririko wa mambo haya;&quot;Kikwete anatoa hotuba leo ya kuwatuhumu CHADEMA bila sababu kesho wakuu wa CHADEMA wanakatwa kwa kisingizio cha uchochezi.CCM watangaza hadharani kuomba msaada wa dola na Tendwa anaingilia kati kutumia ofisi ya umma kuwasaidia CCM&quot; yote haya ni ya kupangwa.<br />
Jambo moja la faraja ni hili &quot;CHADEMA kama watetezi makini wa watanzania walishajua yote haya kabla na walitarajia yangefanywa&quot; Kwa hiyo kwa CHADEMA&quot;MWENDO ULEULE MPAPAKA KIELEWEKE&quot;[/QUOTE]<br />
<br />
Nakushangaa kwa maana ya kwamba unachokielezea hukijui.Nchi ilishakombolewa muda mrefu na hao CDM wakiwemo.Usitarajie kuna mtanzania labla mhuni ama kibaka ndie atafanya huo ukombozi unaofikiri kwa maana ya kuandamana kuipinga serikali.Mimi ningetarajia CDM wange mshukuru kikwete na chama chake kwa kuwapa uhuru wa kupiga domo la uzushi badala ya kuanza kukejeli,kumbukeni enzi ya Mkapa alivyokuwa akiwatandika Lipumba,mrema bila huruma haya yangewakuta hao ndugu zako CDM na uzushi walionao si ingekuwa balaa.Kwa ujumla Slaa anakaunafiki,si mkweli sana kwa baadhi ya mambo kama baadhi ya watu wanavyofikiri,mlopokaji kwa tamaa binafsi na anahisi ikulu iko jirani yake hivya katabia kauzushi ambako ni ngao kubwa kwake hawezi acha mpaka akumbane na mkono wa Jk.
 
Kwanini JK asiwe Supported ili amalizie Mabarabara ya Lami anayoendelea kuyajenga Nchi nzima, aboreshe Sekondari za Kata alizozijenga kwa Kuzipatia Waalimu wa kutosha, Maabara, Nyumba za walimu, Vifaa vya kufundishia nk, Adhibiti mfumuko wa Bei (ulishatokea huko nyuma ukadhibitiwa, basi na Safari hii pia udhibitiwe) akabiliane na Mgao wa umeme nk Akishindwa kufanya hivyo mpaka 2015, basi hata CCM iibe kura vipi, haitaweza kurudi Madarakani. Lakini makele ya Ufisadi uliofanyika miaka kadhaa iliyopita na Kulikuza Suala la Dowans kupita kiasi (Dowans pekee haikusababisha Mgao na wala pekee haiwezi Kuuondoa!) ni Propaganda za Mafisi wanaogombea kupewa Dhamana ya Kuuza Bucha kwa Kuona Mafisi wenzao Waliopewa Dhamana hiyo wanafaidi Kiulaini!
 
Hebu tuwe Wakweli na kuacha Ushabiki wa Kisiasa na kuangalia Mustakbali wa nchi yetu Kama kweli tuna Uchungu nayo, ....

Ndugu yangu hujakitafakari vizuri kinachoendelea, wala hujatafakari vizuri kwa nini tupo hapa tulipo
1. ishu sio kuandamana na at the end of the day watu wanaenda kulala. ishu hapa ni kwamba kwa muda mrefu sana CCM na serikali zake, hasa kuanzia Mkapa na huyu JK, wameshindwa kuonesha kwa dhati kabisa kwamba wanasimamia maslahi ya watanzania. hilo wananchi wanalijua, hata kama wewe hulijui. kilichokuwa kinakosekana ni namna ya kuwaunganisha hawa wananchi na kuwapa chombo cha kuwakilisha sauti zao. katika mfumo huu wa vyama vingi, CHADEMA imeonekana kulifanya hilo vizuri sana. na ndio maana wingi wa watu wanaofurika kuunga mkono maandamano haya unatisha watawala waliojisahau. hawa hawaandamani tu na kurudi kulala, wanatoa message kali kwa watawala.

2. Kauli za viongozi wa CHADEMA zinaweza kujibiwa comprehensively and conclusively kwa CCM na serikali yake kujizatiti na kutekeleza yale waliyoahidi. hata kama kuna matatizo ya uchumi wa dunia, mgawanyo wa kile kidogo kilichopo hapa nchini ni mbovu kiasi kwamba kila mtu anajua kwamba akina fulani ndio wanakula keki yote! kama serikali ingefanya yale yalioahidiwa na yale waliyoapa kuyafanya, walio wengi wangekuwa na mawazo kama yako na wala wasingeona haja ya kwenda katika maandamano ya CHADEMA. kufanya nini?

3. Nikueleze kile kinachotishia amani ya nchi yetu? ni ukimya wa serikali na undumila kuwili, kushindwa kutolea kauli za kueleweka kuhusu hujuma kama za Kagoda, Meremeta, nk. hivi kwa nini serikali imeshindwa kabisa kutoa kauli kuhusu wizi wa Kagoda kwa mfano? na kwa nini kuna mengi tu ya ufisadi mkubwa yanafukiwa chini ya jamvi, eti ili kulinda usalama wa taifa letu? huo usalama ni wa nani hasa? badala ya kuilaumu CHADEMA kwamba inachochea vurugu, nadhani inabidi tuwashukuru CHADEMA kwamba angalau wanaongea lugha ambayo itasaidia kulipasua jipu ili tupate dawa na kupona, badala ya kulipaka mafuta na kuliwekea barafu litulie. Wananchi wanajua sana haya ya ufisadi na yanawauma sana. ndio maana hata kauli za watu kama wewe hazitasaidia

4. CHADEMA sasa hivi haihitaji kusimamisha wagombea kila jimbo. uma wa watu wanaoiunga mkono ni tosha kabisa. kwanza kusimamisha wagombea kila jimbo inahitaji uwe na fedha nyingi sana, ambazo CHADEMA hawakuwa nazo, lakini hata ukiwa na wagombea wengi, bado CCM wako tayari kula njama ili kuiba kura na kuhujumu zoezi lote la uchaguzi. na kwa hiyo kutegemea wabunge, ambapo bunge lenyewe limechakachuliwa kwa kuhakikisha kwamba spika ni Anna Makinda, kama tulivyoona, CHADEMA hawawezi kupata haki katika mfumo huo. kilichobaki ni kwenda kwa wananchi moja kwa moja, na hilo ndilo linalofanyika.

5. Kumfananisha Slaa na watu kama Savimbi walioua watu, sio jambo la kiungwana. Savimbi hakuwa na support kubwa ya watu namna hiyo, na alikuwa na majeshi ya kupambana na majeshi ya serikali. Slaa majeshi yake ni wananchi walio wengi. nadhani hapa ungesema savimbi ni Serikali ya CCM na makuwadi wake. kufungia CHADEMA sio suluhisho. kuidhibiti pia sio suluhisho. ni sawa na kuzuia mto wa maji. utatafuta tu njia ya kutokea. tena ukidhibiti ndio kabisaa, utaharibu hata nyumba ili upate pa kutokea. moto uliowashwa na CHADEMA, Mungu atusaidie, ulete mabadiliko ambayo yatatupeleka kwenye amani ya kweli. operesheni yoyote inauma, hatuwezi kukwepa maumivu. afadhali kufa ukipambana na wezi, kuliko kuwapigia makofi wakikuibia
 
Siasa huendeshwa majukwaani kwa wanasiasa kuwaita watu na kuwaeleza yale wanayoyaamini. CCM inaona kuwa Chadema kutumia majukwaa ni kuwachonganisha CCM na wananchi! Hili ni suala ambalo halielezeki. Hivi CCM mara ngapi wanatoa kauli za kuichonganisha Chadema na wananchi tena kwa kutumia majukwaa yasiyostahili? Chukulia mfano rais wa nchi anapotumia fursa ya kikatiba aliyo nayo ya urais na kutoa hotuba za kukiponda chama cha upinzani, hapo havunji katiba? Hapo hakichonganishi chama na wananchi?

Bungeni, CCM wamekuwa wakitumia uwingi wao bungeni kutoa kauli zenye wingi wa kejeli na mipasho dhidi ya Chadema. Hata waziri mkuu aliwahi kutumia fursa aliyopewa kama kiongozi mkuu wa serikali Bungeni kukishambulia Chadema kuwa ni chama cha vurugu, haya yote washabiki wa CCM mwayaonaje? Hivi ni lini CCM itajifunza kutofautisha serikali na Chama?

Haya yote yakiendelea wapinzani wanaamua kuwaita watu kwenye mikutano ya hadhara na kuwaambia yale ambayo yamekuwa yakiandikwa kila siku na vyombo vya habari mbali mbali, leo wanaambiwa wanafanya uchochezi, wanaikosanisha serikali na wananchi, wanachochea vurugu: Msajiri wa vyama vya siasa ameshasimama kidete kutaka kuifuta chadema!!! Hilo linatia shaka juu ya uelewa wa CCM juu ya siasa za kupingana bila kupigana.

Hakuna aliyekwisha thibitisha kuwa chadema wanaongea kitu kipya ambacho hakijazungumzwa sana kwenye vyombo vya habari! Ni kipi wanachoongea kipya. Hata tukisema tupime kwa matokeo, je huko walikofanya maandamano wananchi wametoka kwenye maandamano wakaenda kushambulia ofisi za serikali au kufanya fujo za aina yoyote? Bila lolote kuthibitika katika haya, kina Tendwa wanaingia kwenye mkururu ule ule wa dola na vyombo vyake kuwa mawakala wa kuisemea CCM.

CCM yenye serikali yake inatakiwa isimame ijitetee kwa wananchi tena kwenye majukwaa ya wazi kama wanayotumia Chadema. Kushindwa kufanya hivyo ni kushindwa siasa; sasa wanataka kutumia nguvu kwa kuwa tu wao wanadhibiti dola. Hili wajue litawatokea puani. Hakuna ambacho Chadema imefanya cha kufanya hadi msajiri wa vyama vya siasa kutishia hadharani kukifungia Chama. Hili linazidi kuwafanya hawa watendaji wengi waonekane ni mawakala tu.

Hayo wanayoyasema Chadema, wakati yanaandikwa kwenye magazeti na kutangazwa kwenye redio na televisheni, mbona hizi ndulu za uchochezi hazikusikika? Tuwe wakweli, demokrasia ya vyama vingi ndo hii ndo inafanya kazi vile inatakiwa ifanye kazi. CCM wajirekebishe ama waache waendelee kutishia kutumia dola kwa gharama ya kupoteza uhalali wa kutawala kidemokrasia. Vitisho vingine hata havifai kuzungumzwa na watu wenye akili timamu. Kama ndo panic, basi CCM wamefika kubaya!
 
Chama tawala,CCM kinaonekana kufikwa na maji shingoni na sasa kinatapatapa huku na kule ili kukidhibiti chama kikuu cha upinzani-CHADEMA ambacho kinafanya maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima.Maandamano na mikutano hiyo,kwa mujibu wa viongozi wa CHADEMA yana malengo ya kupinga malipo ya fidia ya sh.bilioni 94 kwa kampuni ya kufua umeme ya dowans,kupinga kupanda kwa gharama za maisha,kupinga kupanda kwa gharama za umeme,kupinga vitendo vya ufisadi,kuishinikiza serikali ya jk iweke ratiba ya mchakato utakaohakikisha uchguzi wa mwaka 2015 unafanyika chini ya katiba mpya.
CCM na serikali yake hawana majibu kwa hoja hizi nzito za CHADEMA,sasa wanakimbilia kuomba msaada wa dola.Kwa CCM kujifanya ionekane inaomba msaada wa dola badala ya kuviagiza vyombo vya dola ni unafiki mkubwa wa kisiasa,CCM wanataka waonekane machoni pa watanzania kuwa"hawatumii vibaya vyombo vya dola kuudhibiti upinzani,wakati inajulikana ni tabia yao kuvitumia vyombo vya dola kuwadhibiti wapinzani wao.
Kitendo cha CCM kuomba msaada wa dola kuwamaliza CHADEMA kisiasa ni ishara ya kufilisika kihoja na kisiasa,CCM sasa hawana hoja wanakimbilia kutumia nguvu za dola ambazo ziko chini ya udhibiti wao. CCM kutaka waeleweke na watu kwamba wanaomba msaada wa dola ni uzandiki na hadaa kwa watanzania.
Alichokiongea bwana Chiligati leo na wandishi wa habari alipokuwa anatoa tamko la kuomba msada wa dola kuidhibiti CHADEMA,hakina tofauti na kile alichokiongea bosi wake Kikwete.Kwa maana hiyo dhamira ya kuwabana CHADEMA ilishaanza kusukwa kabla hata kikwete hajaiweka hotuba yake yenye vitisho kwa CHADEMA hadharani kwa taifa.
Wakati katibu mkuu wa CHADEMA DK Wilbrod Slaa akisisitiza kwamba maandamano yanafanywa na CHADEMA ni ya amani ya yenye shabaha ya kuihimiza serikali iitikie kilio cha Umma ofisi ya msajili wa vyama vya siasa chini ya bwana tendwa imeungana na CCM kuwatisha na hatimaye kuwadhofisha CHADEMA kwa kuwasingizia kwamba wanafanya "UCHOCHEZI" katika mikutano yao.
Kudhihirisha kwamba anataka kuwafurahisha CCM au anatekeleza matakwa ya kisiasa ya CCM,Tendwa amefikia hatua ya kutamka maneno ya kukifuta CHADEMA na kuzungumzia uwezekano wa mkurugenzi wa mashita ya jinai kuwafungulia mashitaka CHADEMA.
Mtiririko wote huu unaonesha jinsi serikali ilivyojipanga kuwadhibiti CHADEMA.Fikiria Mtiririko wa mambo haya;"Kikwete anatoa hotuba leo ya kuwatuhumu CHADEMA bila sababu kesho wakuu wa CHADEMA wanakatwa kwa kisingizio cha uchochezi.CCM watangaza hadharani kuomba msaada wa dola na Tendwa anaingilia kati kutumia ofisi ya umma kuwasaidia CCM" yote haya ni ya kupangwa.
Jambo moja la faraja ni hili "CHADEMA kama watetezi makini wa watanzania walishajua yote haya kabla na walitarajia yangefanywa" Kwa hiyo kwa CHADEMA"MWENDO ULEULE MPAPAKA KIELEWEKE"

Mimi ninadhani CCM haiwatendei wananchi haki wanapo taka kuelewa mwenendo mzima wa serikali yao na ni kitu gani kinachochangia mpaka huu umasikini umekithiri hivi. Mimi ninavyoona katika kauli aliyotoa Chiligati ya kumfananisha Dr Slaa na Savimbi kimtizamo na kifikra inarudi moja kwa moja kwa CCM kwa kuchakachua kura za wananchi na akiwa yeye ni mmoja wapo. Kwa sababu sera zao na za kibaguzi kuthamini alienacho kuliko kumjenga yule masikini, na hilo ndilo watanzania wanataka kulijua iweje kila familia wanalia umasikini, ni kwa nini. Kwa mfano watanzania waamue ya kuwa wanataka Tanzania yao wao watasema kuna demokrasia ya miaka mitano, hiyo Demokrasia ipo seriklini au ipo kwa wananchi. Ndio hicho tunacho jiuliza leo hiyo demokrasia ipo wapi? CCM itafute mbinu jinsi ya kupangua hoja siyo kukimbilia vyombo vya dola. Vyombo vya dola viachwe vifanye kazi yake kwa uhuru bila mamlaka ya mtu yeyote. Kwa sasa tunaona wanashindwa kufanya kazi yao kisheria na wanazidi kupoteza sifa kwa ajilli ya CCM. Kama serikali inataka kutoka kwenye haya matatizo ifanye kazi kama serikali iachane na mambo ya majungu ya CCM. Propaganda za CCM hazimtishii mtanzania kutafuta haki yao. Dola itaingilia endapo itaona madhara, yeyote, unafikiri CCM sasa hivi watawapeleka tena Dola puta kama kule Arusha, ile ya Arusha ilikuwa shule tosha na kama hawkujifunza wawemkini. Kama itatokea vita Tanzania ya leo italetwa na CCM sio CHADEMA JAPOKUWA SIOMBEI YAFIKIE HUKO.
 
Mindi, maelezo yako yana Ukweli kiasi fulani ila yana Lack Proportionality. K.m. Mtu akipewa dhamana ya Kusimamia kilimo cha Shamba la Mahindi, shamba ambalo Normaly linatoa Gunia 500, yeye akalisimamia likatoa Gunia 2,000, lakini wenzake aliofanya nao kazi Wakaiba gunia 20! Sasa nyie wenye Shamba mkianzisha zogo kwa Wizi huo wa Gunia 20, na kudai kuwa Msimamizi hafai, Mkakataa katakata Kutambua kuwa kuna Gunia 1,800 ambazo ni ziada ya Gunia 1,300 kulinganisha na Awali. Sasa wenye Shamba wakihamasishwa Kumlaani na kumkataa Msimamizi huyo ndipo tunasema Kunakosekana Rationality, Waswahili wanasema Hasidi Hana Sababu, Lengo la Kuu la Chama chochote cha Siasa ni Kushika Dola, CDM is no Exception, huku CDM ikijua fika kuwa CCM haiongozwi na Malaika, lazma itafanya makos ya hapa na pale, ikaamua kuPortray makosa hayo kwa Jamii kana kwamba ndio kazi Pekee iliyofanywa na CCM na hakuna zuri hata Moja lilofanyika, labda wakishika Dola wao (Malaika?) maisha Yatakuwa mazuri Ghafla! Hebu piga Total ya fedha zote Unazojua zimeliwa na Mafisadi kupitia hujuma zote ulizozisikia, Kuanzia EPA, Kagoda, Meremeta, Dowans nk (ambazo zote Zina Miaka 5 au zaidi iliyopita, linganisha na Kiasi ambacho Serikali imezipata kutoka Vyanzo mbalimbali kwa Miaka 5 iliyopita na Zikatumika kwenye miradi mbalimbali ya Maendeleo Nchi nzima, Mijini na Vijijini ambayo inaonekana Waziwazi. Kijijini kwangu hivi Sasa kumepitishwa Barabara ya Lami, tumepata Mikopo kupitia SACCOS yetu, Tumepewa fedha za TASAF tukajenga Soko zuri linaongeza mapato ya Kijiji,Tuna Kituo cha Afya cha kata Kipo kijijini kwetu, tuna Sekondari ya Kata ipo kijiji Jirani, haina Walimu wala Vifaa vya Kutosha, lakini vyote hivi miaka 5 iliyopita havikuwepo, Kwanini tusiwape waliotufanyia Yote haya Muda zaidi ili warekibishe Mapungufu yaliyopo Kama ya Sekondari na Mengineyo badala ya Kuwatimua kwa Sababu ya Wizi wa 'yale Magunia 20?'
 
Chiligati ni miongoni mwa walewale waliofilisika kisiasa,Hakuna hoja yoyote muhimu inayoweza kutolewa na bwana.Kumfananisha kamanda na mtetezi wa wanyonge,Dk slaa,Chiligati anautangazia umma wa watanzania jinsi alivyopumbazwa na kulogwa na CCM.La mhimu kwa Chiligati ni kuomba Azeeke vizuri,.
 
Mindi, maelezo yako yana Ukweli kiasi fulani ila yana Lack Proportionality. K.m. Mtu akipewa dhamana ya Kusimamia kilimo cha Shamba la Mahindi, shamba ambalo Normaly linatoa Gunia 500, yeye akalisimamia likatoa Gunia 2,000, lakini wenzake aliofanya nao kazi Wakaiba gunia 20! Sasa nyie wenye Shamba mkianzisha zogo kwa Wizi huo wa Gunia 20, na kudai kuwa Msimamizi hafai, Mkakataa katakata Kutambua kuwa kuna Gunia 1,800 ambazo ni ziada ya Gunia 1,300 kulinganisha na Awali. Sasa wenye Shamba wakihamasishwa Kumlaani na kumkataa Msimamizi huyo ndipo tunasema Kunakosekana Rationality, Waswahili wanasema Hasidi Hana Sababu, Lengo la Kuu la Chama chochote cha Siasa ni Kushika Dola, CDM is no Exception, huku CDM ikijua fika kuwa CCM haiongozwi na Malaika, lazma itafanya makos ya hapa na pale, ikaamua kuPortray makosa hayo kwa Jamii kana kwamba ndio kazi Pekee iliyofanywa na CCM na hakuna zuri hata Moja lilofanyika, labda wakishika Dola wao (Malaika?) maisha Yatakuwa mazuri Ghafla! Hebu piga Total ya fedha zote Unazojua zimeliwa na Mafisadi kupitia hujuma zote ulizozisikia, Kuanzia EPA, Kagoda, Meremeta, Dowans nk (ambazo zote Zina Miaka 5 au zaidi iliyopita, linganisha na Kiasi ambacho Serikali imezipata kutoka Vyanzo mbalimbali kwa Miaka 5 iliyopita na Zikatumika kwenye miradi mbalimbali ya Maendeleo Nchi nzima, Mijini na Vijijini ambayo inaonekana Waziwazi. Kijijini kwangu hivi Sasa kumepitishwa Barabara ya Lami, tumepata Mikopo kupitia SACCOS yetu, Tumepewa fedha za TASAF tukajenga Soko zuri linaongeza mapato ya Kijiji,Tuna Kituo cha Afya cha kata Kipo kijijini kwetu, tuna Sekondari ya Kata ipo kijiji Jirani, haina Walimu wala Vifaa vya Kutosha, lakini vyote hivi miaka 5 iliyopita havikuwepo, Kwanini tusiwape waliotufanyia Yote haya Muda zaidi ili warekibishe Mapungufu yaliyopo Kama ya Sekondari na Mengineyo badala ya Kuwatimua kwa Sababu ya Wizi wa 'yale Magunia 20?'

Hicho kijiji unachoongelea Tanzania hii hakipo na kama hali iko hivyo katika vijiji vyote sasa kwa nini CCM iogope wanaoenda kuisema kwa mambo ambayo wewe unaona ni madogo tu? Yaani msururu huo wa mikashfa ambayo imedidimiza mabilioni ya shillingi za mlipa kodi wewe unaona ni mambo madogo tu? Ikiwa hivyo ndivyo kwa nini CCM nayo isitumie majukwaa halali kuyasema hayo unayoyasema?
 
Jueni kuwa nyie CCM ndo mmeleta yote haya. Mmebeba mafisadi, mmeshindwa kusimamia sera zenu wenyewe! Hapo wenye nchi mnafikiri wafanye nini na maisha magumu mliowasababishia na hao marafiki zenu mnaowaita wawekezaji wakikwapua mali za taifa letu?
 
Mindi, maelezo yako yana Ukweli kiasi fulani ila yana Lack Proportionality. K.m. Mtu akipewa dhamana ya Kusimamia kilimo cha Shamba la Mahindi, shamba ambalo Normaly linatoa Gunia 500, yeye akalisimamia likatoa Gunia 2,000, lakini wenzake aliofanya nao kazi Wakaiba gunia 20! Sasa nyie wenye Shamba mkianzisha zogo kwa Wizi huo wa Gunia 20, na kudai kuwa Msimamizi hafai, Mkakataa katakata Kutambua kuwa kuna Gunia 1,800 ambazo ni ziada ya Gunia 1,300 kulinganisha na Awali. Sasa wenye Shamba wakihamasishwa Kumlaani na kumkataa Msimamizi huyo ndipo tunasema Kunakosekana Rationality, Waswahili wanasema Hasidi Hana Sababu, Lengo la Kuu la Chama chochote cha Siasa ni Kushika Dola, CDM is no Exception, huku CDM ikijua fika kuwa CCM haiongozwi na Malaika, lazma itafanya makos ya hapa na pale, ikaamua kuPortray makosa hayo kwa Jamii kana kwamba ndio kazi Pekee iliyofanywa na CCM na hakuna zuri hata Moja lilofanyika, labda wakishika Dola wao (Malaika?) maisha Yatakuwa mazuri Ghafla! Hebu piga Total ya fedha zote Unazojua zimeliwa na Mafisadi kupitia hujuma zote ulizozisikia, Kuanzia EPA, Kagoda, Meremeta, Dowans nk (ambazo zote Zina Miaka 5 au zaidi iliyopita, linganisha na Kiasi ambacho Serikali imezipata kutoka Vyanzo mbalimbali kwa Miaka 5 iliyopita na Zikatumika kwenye miradi mbalimbali ya Maendeleo Nchi nzima, Mijini na Vijijini ambayo inaonekana Waziwazi. Kijijini kwangu hivi Sasa kumepitishwa Barabara ya Lami, tumepata Mikopo kupitia SACCOS yetu, Tumepewa fedha za TASAF tukajenga Soko zuri linaongeza mapato ya Kijiji,Tuna Kituo cha Afya cha kata Kipo kijijini kwetu, tuna Sekondari ya Kata ipo kijiji Jirani, haina Walimu wala Vifaa vya Kutosha, lakini vyote hivi miaka 5 iliyopita havikuwepo, Kwanini tusiwape waliotufanyia Yote haya Muda zaidi ili warekibishe Mapungufu yaliyopo Kama ya Sekondari na Mengineyo badala ya Kuwatimua kwa Sababu ya Wizi wa 'yale Magunia 20?'

OK, nimekuelewa. tatizo la argument yako ni msingi wake. naelewa kwamba hakuna malaika, lakini ndugu yangu yanayotokea hapa kwetu Tanzania ni maajabu makubwa na watu wengi wa nje wanatushangaa. serikali yetu is so inefficient kiasi kwamba haiwezi kuji-sustain. hebu angalia tulikotoka. tulikuwa na viwanda vingi tu, tulikuwa na mashirika ambayo yangeweza kuendeshwa kwa njia tofauti lakini sio hivi ilivyotokea - ubinafsishwaji holela. nikupe mfano mdogo, Nyerere alijenga institutions nyingi sana: vyuo vya benki, Posta, na aliwekeza fedha zetu za walala hoi katika mashirika kama NBC, TTCL, nk. ukiangalia yalivyotupwa kwa chee, unaweza kulia machozi. haiwezekani tupoteze tulichokipata kwa taabu, eti kwa kufurahia makombo! ukitaka kujua tunachopoteza, piga hesabu ya mashirika yoote yaliyouzwa kwa wizi, halafu nambie tumepata nini. ukitaka kujua athari, angalia umaskini wetu ambao haukutakiwa kabisa kuwepo. idadi ya watanzania wanaopata elimu ya kweli leo ni asilimia ndogo sana. idadi kubwa ya watanzania wanaishi kwa chini ya dola moja kwa siku. you cannot even begin to consider your argument
 
Mkapa aliwahi kusema Sera za CCM hazitekelezeki.

Sera zao ni kwa ajili ya kuombea kura tu yaani kuwahadaa watanzania.
 
Back
Top Bottom