Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,571
Katibu wa CCM Mkoa wa DSM Ameandika barua polisi akiomba kibali cha wana CCM kuandamana kutoka Vijana mpaka Kidongo chekundu eti kulaani viongozi wa CDM kukiuka sheria halali huko Arusha.
Ijulikane kuwa CDM waliandika barua tangu jana , na ilipofikia leo majira ya saa tano asubuhi huko Arusha Paul Chagonja ambaye ni kamishna wa Operesheni za Polisi alitoa tamko la kuzuia maandamano ya CDM nchi nzima .
Jioni hii Kova , ametoa barua kwa CDM na CCM akisema eti masuala hayo yapo mahakamani na wote wameshapewa dhamana ,
Kichekesho: Katibu wa CCM mkoa wa DSM ameongea na vyombo vya habari na kushukurui jeshi la polisi kusitisha maandamao yao .
Ndio maana CDM tunalalamika kuwa polisi wanashirikiana na CCM kutuhujumu kwenye kazi yetu ya siasa.
Mwenyekiti Mbowe mpaka sasa yupo Polisi huko Arusha akihojiwa tangu asubuhi saa tano kamili.
Ijulikane kuwa CDM waliandika barua tangu jana , na ilipofikia leo majira ya saa tano asubuhi huko Arusha Paul Chagonja ambaye ni kamishna wa Operesheni za Polisi alitoa tamko la kuzuia maandamano ya CDM nchi nzima .
Jioni hii Kova , ametoa barua kwa CDM na CCM akisema eti masuala hayo yapo mahakamani na wote wameshapewa dhamana ,
Kichekesho: Katibu wa CCM mkoa wa DSM ameongea na vyombo vya habari na kushukurui jeshi la polisi kusitisha maandamao yao .
Ndio maana CDM tunalalamika kuwa polisi wanashirikiana na CCM kutuhujumu kwenye kazi yetu ya siasa.
Mwenyekiti Mbowe mpaka sasa yupo Polisi huko Arusha akihojiwa tangu asubuhi saa tano kamili.