MANI
Platinum Member
- Feb 22, 2010
- 7,320
- 6,376
Jamani Waungwana wezangu mimi nashindwa kuelewa matamshi ya viongozi wakuu wa CCM kuelekea uchaguzi mbona hayaendani na chama kinachotegemea sanduku la kura kupata ushindi. Mwenyekiti wao alisema hahitaji kura za wafanyakazi kwa hiyo hawezi kuwaongezea mshahara hata kama hawatampigia kura, jana makamu mwenyekiti wao amesema wale wote ambao wanaona hawakutendewa vyema kwenye mchakato wa kupitishwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi wanaweza kuondoka pamoja na wafuasi wao. Sasa kama chama kinachoingia kwenye ushindani wa kura kinaanza kuwakataa wapiga kura kwamba hakina haja nao je wenzetu wana mbinu gani nyingine wanazotumia kushinda!