Ukizungumza na watu wa CCM, CUF, NCCF et al, wanasema CDM itabomoka maana Mbowe atalazimisha kugombea urais na chama kitagawanyika. Mimi simfahamu sana Mbowe lakini sioni kama atafanya hivyo. ningekuwa mshauri wa chadema ningesema demokrasia ipewe nafasi kubwa. Kama demokrasia isipohujumiwa, na maamuzi yote yakatokana na vikao, hakutakuwa na uwezekano wa migigoro. Dr Slaa anakubalika sana na kama Zitto na Mbowe watataka wagombee wasinyimwe. Kura za wanachama zipigwe atakayeshinda ndio apewe tiketi ya chama