CCM wakomba hela Hazina, mishahara ya Septemba hamna!

Mwaka wa fedha 2011/12 taarifa ya ukusanyaji wa mapato ya serikali inaonesha ilikuwa zaidi ya asilimia 98 ya malengo yaliyokusudiwa lakini jambo la kushangaza na la kusikitisha ni kuwa hakuna wizara ama idara ya serikali iliyopata mgawo wa fedha za matumizi kwa kiwango kinachozidi asilimia 60 ya bajeti.

Kama ni mtu unaefuatilia na kutafakari ni lazima ujiulize hizo fedha zilizokusanywa zilielekezwa wapi, kwa matumizi gani na kwa idhini ya nani. Mlipaji Mkuu wa Serikali ambaye ni Katibu Mkuu Hazina anatakiwa aweke wazi/atoe ufafanuzi juu ya hilo pamoja na hizo tuhuma za CCM kujichotea kwa ajili ya kugharamia shughuli zao za chama.
 
Mimi ni mfanyakazi wa serikali kuu na mshahara unakalibia kuisha sasa hivi toka niuchukue! Jamani hizi habari bora JF waanzishe jukwaa la udaku na umbea/propaganda kuliko kutufanya watu wazima watoto.

"Kuna watu wanamiliki viwanda vya kuzalisha uongo" by JK.
si kila mfanyakazi wa serikali kuu amepata mshahara si kweli wengi wetu hatujapata acha kudanganya watu hapa
 
kukosekana mshahara ni kweli,lakini eti zimechotwa na ccm ni propaganda za chadema kujipa umaarufu tu kwa kila baya kuitupia ccm
Sasa kama unakiri, mishahara haijalipwa, lakini unakanusha hazijachotwa na CCM, sasa kama pesa hizo zilipangiwa kasma ya mishahara, sasa wewe unayesema kuwa siyo kweli, tueleze hizo pesa za mishahara ya watumishi wa serikali zimeenda wapi?! Maana nyiye mliyekunywa maji ya bendera za CCM, mna roho ngumu kweli, mabaya yoyote ya magamba, mnayakingia kifua!! Kazi kweli kweli!!
 
ukweli seriakali inatakiwa iwe makini sana mbona inatesa wafanyakazi wake hata kama hazina kunatatizo ni bora kutoa taarifa kwa wananchi maana mshahara hautoshi ifikapo tarehe 15 ya kila mwezi asilimia kubwa ya wafanya kazi wanakuwa hawana hela
 
Habari siyo ya kweli kwa sababu mshahara wangu nilichukua tangu tarehe 30 Septemba 2012
Mimi nipo serikalini, ni kweli mshahara hatujapata. Inawezekana kweli ndani ya serikali hiyo hiyo wengine watakuwa wamepata, maana itakuwa vigumu kuwanyima mishahara Jeshi la Ulinzi, Jeshi la polisi la akina Mwema, Chagonja, Kamuhanda na Shilogile na usalama wa Taifa wa akina Zoka, maana wanajua watu hao ndiyo wanaowadumisha watawala madarakani, maana bila majeshi hayo kujiegemeza upande wa magamba, CCM ingekuwa ishaondoka madarakani siku nyingi tu!!!
 
Hivi Mwanahalisi litafunguliwa lini, natumai liengeweza kutuletea hundi au TT iliyotumika kufanya malipo, akaunti husika ambako fedha zilitoka na ambako fedha zilikwenda, pia na walohusika ku-idhinisha malipo.

Ningetamani kichwa cha habari kisomeke hivi - CCM yashika hatamu hazina na kuwaacha wafanyakazi wa serikali bila mishahara. Tihi tihiiiiiiiiiiii
 
sina shaka juu ya hilo maana sio moi wala muhimbili madaktari mpaka attendants hakuna aliyelipwa.kaka yangu askari nae analalamika.wakati huo huo dogo anatakiwa kuripoti chuo mkopo hakuna.
tutafika?????????????
 
Wakumbuke kuwa kila uovu unaotendwa una malipo yake. Wajifunze kutoka tawala dhalimu zilizoanguka, wasifikiri watatawala milele. SAA YA UKOMBOZI NI SASA WATANZANIA WENZANGU TUAMKE. TUMECHOKA KUNYANYASWA NA WATU WACHACHE AMBAO TUNA UWEZO WA KUWADHIBITI.
UNANIKUMBUSHA MTKILA NA DP ya saa ya ukombozi ni sasa na magabachori, na Farao (Nyerere) na Yuda Eskarioti (Mrema lyatonga) mh ! cjui huyu mzee kafia wapi kisiasa?
 
Huu wizi wa mishahara ya wafanyakazi hauvumiliki..kuanzia kesho siendi kazini hadi mshahara uingie!!
 
si kila mfanyakazi wa serikali kuu amepata mshahara si kweli wengi wetu hatujapata acha kudanganya watu hapa


Sijasema wote waliopo serikali kuu wamepata mkuu,hebu usiwe mwepesi wa kutoa kauli kabla ya kuelewa maoni ya mwenzako!
 
Umenifanya nikumbuke wafanyakazi wa Ugiriki. Juzi waliitisha mgomo kisa waziri mkuu wao amewasilisha bajeti ya kubana matumizi.
 
Habari si ya kweli.

Watu wengne sijui mkoje!
Wafanyakazi wote walio chini ya Wizara ya afya(serikali kuu) kuanzia regional hospitals, vyuo vya afya, wanahesabu tarehe 34 leo, halafu wewe unaropoka kupitia masaburi yako!
 
Nilihisi kwamba jambo hili inawezekana limefanyika.Zile sare nilizoziona na niki-imagine ni Tanzania nzima sikuelewa.Hivi kweli watanzania tumekuwa wanyama na wapuuzi kiasi hiki.Kweli wafanyakazi wanateseka kwa ajili ya mambo ya kipuuzi namna hii and nobody cares.Kweli upendo umekwisha.Kitakachoikumba Tanzania ni kibaya sana and not in the distant future.
Kwa habari za uhakika, kutoka chanzo cha uhakika ni kwamba mkutano wa CCM Dodoma na chaguzi zinazoendelea ndani ya chama vinanendeshwa kwa mamil ya pesa zilizochotwa Hazina.

Pesa hizo ambazo nyingi zilikuwa za mishahara ya wafanyakazi wa serikali na mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini zimesababisha mpaka leo wafanyakazi kadhaa hawajapata mishahara ya Septemba, na "boom" la wanafunzi linapigwa danadana.
 
Back
Top Bottom