Elections 2010 Ccm wahofia kupoteza viti maalumu

KIDUNDULIMA

JF-Expert Member
Aug 18, 2010
966
537
Moja ya vitu vinavyo waumuza kichwa wapanga mikakati ya ushindi wa CCM ni kupoteza viti maalumu. Viti maalumu hutolewa kwa uwiano wa kura anazopata mgombea urais. Hivyo basi kama mgombea wa CCM (Kikwete) ataambulia 40% ya kura zote (hata viti maalumu atapewa hivyo hivyo) na inamaana kuwa asilimia 60% ya viti maalumu vitakwenda kwa wapinzani. Hivyo msishangae CCM wakihaha kutumia mabilioni kwa ajili ya kampeni, kubandika picha kila mtaa, kuongeza ratiba na helikopta kwa mgombea wao wa urais, kusomba watu kwa ajili ya mikutano ta kampeni, kumchafua Dr Slaa, na kutumia propaganda kuwa afya na elimu haviwezi kutolewa bure kwa kuwa pesa za kufanya hivyo hazipo. Kwa maana anguko kuu linawasubiri

Chadema tuendeleze mpambano. Hakuna kulala mpaka kieleweke
 
Moja ya vitu vinavyo waumuza kichwa wapanga mikakati ya ushindi wa CCM ni kupoteza viti maalumu. Viti maalumu hutolewa kwa uwiano wa kura anazopata mgombea urais. Hivyo basi kama mgombea wa CCM (Kikwete) ataambulia 40% ya kura zote (hata viti maalumu atapewa hivyo hivyo) na inamaana kuwa asilimia 60% ya viti maalumu vitakwenda kwa wapinzani. Hivyo msishangae CCM wakihaha kutumia mabilioni kwa ajili ya kampeni, kubandika picha kila mtaa, kuongeza ratiba na helikopta kwa mgombea wao wa urais, kusomba watu kwa ajili ya mikutano ta kampeni, kumchafua Dr Slaa, na kutumia propaganda kuwa afya na elimu haviwezi kutolewa bure kwa kuwa pesa za kufanya hivyo hazipo. Kwa maana anguko kuu linawasubiri

Chadema tuendeleze mpambano. Hakuna kulala mpaka kieleweke

Hii sio sahihi kabisa. Mchanganuo wa kupata wabunge wa viti maalumu ni kama ifuatavyo:

Kulingana na Ibara Na. 66 na 78 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 Vyama vya Siasa vitapendekeza kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi majina ya wanawake ambao Tume inaweza kuwatangaza kuwa Wabunge kama ikiridhika kwamba wana sifa zinazostahili.

Tume inatakiwa kutangaza majina ya wanawake kwa idadi isiyopungua asilimia 30 ya Wabunge wote kwa ajili ya viti maalumu kwa wanawake. Mgawanyo huo utazingatia uwiano wa kura ambazo kila chama kimepata katika uchaguzi wa Bunge. Endapo mgombea ubunge amepita bila kupingwa, kura za mgombea Urais wa chama cha mbunge zitachukuliwa kuwa ndizo kura halali za mbunge huyo. Kama hakina mgombea Urais, asilimia 51 ya idadi ya wapiga kura walioandikishwa zitachukuliwa kuwa ndizo kura halali za mbunge wa chama husika. Hata hivyo, chama kinaweza kupata nafasi ya viti maalumu cha mbunge mwanamke endapo kimepata 5% ya kura zote halali za uchaguzi wa wabunge.
 
Hii sio sahihi kabisa. Mchanganuo wa kupata wabunge wa viti maalumu ni kama ifuatavyo:

Kulingana na Ibara Na. 66 na 78 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 Vyama vya Siasa vitapendekeza kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi majina ya wanawake ambao Tume inaweza kuwatangaza kuwa Wabunge kama ikiridhika kwamba wana sifa zinazostahili.

Tume inatakiwa kutangaza majina ya wanawake kwa idadi isiyopungua asilimia 30 ya Wabunge wote kwa ajili ya viti maalumu kwa wanawake. Mgawanyo huo utazingatia uwiano wa kura ambazo kila chama kimepata katika uchaguzi wa Bunge. Endapo mgombea ubunge amepita bila kupingwa, kura za mgombea Urais wa chama cha mbunge zitachukuliwa kuwa ndizo kura halali za mbunge huyo. Kama hakina mgombea Urais, asilimia 51 ya idadi ya wapiga kura walioandikishwa zitachukuliwa kuwa ndizo kura halali za mbunge wa chama husika. Hata hivyo, chama kinaweza kupata nafasi ya viti maalumu cha mbunge mwanamke endapo kimepata 5% ya kura zote halali za uchaguzi wa wabunge.
Pamoja na sahihisho lako lakini hofu bado iko palepale ya kupoteza viti vingi maalumu tofauti na 2005.
 
Back
Top Bottom