Nyambala
JF-Expert Member
- Oct 10, 2007
- 4,465
- 1,170
Wakuu,
Chama kile kikongwe naona kiko desperate mpaka inachekesha.......... Jisomee hapa chini for details.
Mtoto wa Makalla kuwania Uenyekiti chipukizi
na Nasra Abdallah
MTOTO wa Mweka Hazina wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla, Gabriel Makalla, amejitokeza kuwania nafasi ya uenyekiti wa chipukizi taifa ndani ya chama hicho kwa upande wa Tanzania Bara.
Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Desemba 29 katika Chuo cha Ualimu Kigurunyembe mkoani Morogoro, ambapo nafasi hiyo wamejitokeza jumla ya wagombea tisa - watano kutoka Tanzania Bara na wanne Visiwani.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Makao Makuu ya Ofisi za Umoja wa Vijana, Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Taifa, Esther Bulaya, aliwataja wagombea wengine waliojitokeza na mikoa wanayotokea kwenye mabano kuwa ni Ally Mbaraka (Kagera), Asnail King (Dar es Salaam), Hayani Mkambuga (Kagera) na Paulina Lucas Kasonso (Mtwara).
Kwa upande wa Tanzania Visiwani waliojitokeza ni Abdallah Ali Abdallah, Harith Juma Mwinyi, Harith Mohamed Mohamed na Mohamed Gharib Mohamed, wote kutoka Mkoa wa Mjini Magharibi.
Kwa mujibu wa Bulaya, vigezo ambavyo vinazingatiwa katika kugombea nafasi hizo ni kwa mgombea kuwa na umri kati ya miaka mitatu hadi 13 na awe na kadi ya uanachama.
Aidha, alisema mbali na nafasi ya uenyekiti, nafasi nyingine zinazogombewa katika uchaguzi huo ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa atakayewakilisha chipukizi (nafasi mbili - moja Tanzania Bara nyingine Tanzania Visiwani).
Nafasi nyingine ni ya mjumbe wa Mkutano Mkuu wa UVCCM Taifa ambapo nafasi zinazogombewa ni tatu - mbili Tanzania Bara na moja Zanzibar, huku nafasi za wajumbe wa Kamati ya Uendeshaji Taifa ni tatu - moja kutoka Tanzania Bara na mbili Zanzibar. "Ni kawaida na taratibu za uongozi wa chipukizi kufanya uchaguzi mkuu kila baada ya miaka mitatu, ambapo mkutano huu ni wa tano tangu kuanzishwa kwa chipukizi. "Hata hivyo mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu wa chipukizi ngazi ya matawi, kata, wilaya, mikoa hadi taifa na katika ngazi ya matawi hadi mkoa tayari wamekwishakamilisha chaguzi hizo," alisema Bulaya.
source: freemedia.co.tz
My take:
1. Ina maana hao wanachama wa CCM tunaoaminishwa ni 4 million includes babies born in 2006???????
2. What is the significance ya kuwa na mwenyekiti wa chipukizi nchi nzima? What are their roles?
3. Hivi hii chipukizi iliffufuka lini? Na hizi taratitibu zilianza lini, enzi zile sikuwahi kusikia haya mambo.
4. Is this not indoctrination of babies into the green party??????
Chama kile kikongwe naona kiko desperate mpaka inachekesha.......... Jisomee hapa chini for details.
Mtoto wa Makalla kuwania Uenyekiti chipukizi
na Nasra Abdallah
MTOTO wa Mweka Hazina wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla, Gabriel Makalla, amejitokeza kuwania nafasi ya uenyekiti wa chipukizi taifa ndani ya chama hicho kwa upande wa Tanzania Bara.
Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Desemba 29 katika Chuo cha Ualimu Kigurunyembe mkoani Morogoro, ambapo nafasi hiyo wamejitokeza jumla ya wagombea tisa - watano kutoka Tanzania Bara na wanne Visiwani.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Makao Makuu ya Ofisi za Umoja wa Vijana, Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM Taifa, Esther Bulaya, aliwataja wagombea wengine waliojitokeza na mikoa wanayotokea kwenye mabano kuwa ni Ally Mbaraka (Kagera), Asnail King (Dar es Salaam), Hayani Mkambuga (Kagera) na Paulina Lucas Kasonso (Mtwara).
Kwa upande wa Tanzania Visiwani waliojitokeza ni Abdallah Ali Abdallah, Harith Juma Mwinyi, Harith Mohamed Mohamed na Mohamed Gharib Mohamed, wote kutoka Mkoa wa Mjini Magharibi.
Kwa mujibu wa Bulaya, vigezo ambavyo vinazingatiwa katika kugombea nafasi hizo ni kwa mgombea kuwa na umri kati ya miaka mitatu hadi 13 na awe na kadi ya uanachama.
Aidha, alisema mbali na nafasi ya uenyekiti, nafasi nyingine zinazogombewa katika uchaguzi huo ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa atakayewakilisha chipukizi (nafasi mbili - moja Tanzania Bara nyingine Tanzania Visiwani).
Nafasi nyingine ni ya mjumbe wa Mkutano Mkuu wa UVCCM Taifa ambapo nafasi zinazogombewa ni tatu - mbili Tanzania Bara na moja Zanzibar, huku nafasi za wajumbe wa Kamati ya Uendeshaji Taifa ni tatu - moja kutoka Tanzania Bara na mbili Zanzibar. "Ni kawaida na taratibu za uongozi wa chipukizi kufanya uchaguzi mkuu kila baada ya miaka mitatu, ambapo mkutano huu ni wa tano tangu kuanzishwa kwa chipukizi. "Hata hivyo mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu wa chipukizi ngazi ya matawi, kata, wilaya, mikoa hadi taifa na katika ngazi ya matawi hadi mkoa tayari wamekwishakamilisha chaguzi hizo," alisema Bulaya.
source: freemedia.co.tz
My take:
1. Ina maana hao wanachama wa CCM tunaoaminishwa ni 4 million includes babies born in 2006???????
2. What is the significance ya kuwa na mwenyekiti wa chipukizi nchi nzima? What are their roles?
3. Hivi hii chipukizi iliffufuka lini? Na hizi taratitibu zilianza lini, enzi zile sikuwahi kusikia haya mambo.
4. Is this not indoctrination of babies into the green party??????