Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Wakati tukielekea kwenye Uchaguzi Mkuu, naona mchecheto unazidi kukikumba moja ya chama Kikongwe kabisa barani Afrika yaani CCM, nasikia Mkuu wa Kitengo cha Propaganda ( Hivi inakuwaje chama kinakuwa na Dipatmenti kama hii ? Mh ngoja niwaachie wenyewe) Bwana Tambwe Hizza ambaye chama chake kimemuona hafai kuwa mwakilishi wa Wananchi yaani Mbunge na kumtoselea mbali amekanusha vikali kwamba Rais Jk hakuzikana kura za Wafanyakazi.
Je Hizi Kauli za Kutapatapa zinazotolewa na Viongozi wa CCM zinaonyesha kwamba wameanza kukata tamaa ya kushindana na CHADEMA iliyo chini ya mgombea anayeonekana na Watanzania wengi kama Musa au Nyerere wa pili?
Je CCM wamnyamazishe Tambwe kwa maana kauli zake zinazidi kuwatia Hasira Wafanyakazi, yaani anawafanya wafanyakazi wa Tanzania ambao wote ni Wasomi kuwa ni Mazuzu yasikuwa na Uwezo wa kusikia na kuelewa kitu alichozungumza Rais
Je Kuna haja ya CCM kuomba jukwaa kama lile na kuwaomba Radhi Wafanyakazi kwa Kuwadhalilisha?
Nataka kusikia maoni ya wana CCM
Je Hizi Kauli za Kutapatapa zinazotolewa na Viongozi wa CCM zinaonyesha kwamba wameanza kukata tamaa ya kushindana na CHADEMA iliyo chini ya mgombea anayeonekana na Watanzania wengi kama Musa au Nyerere wa pili?
Je CCM wamnyamazishe Tambwe kwa maana kauli zake zinazidi kuwatia Hasira Wafanyakazi, yaani anawafanya wafanyakazi wa Tanzania ambao wote ni Wasomi kuwa ni Mazuzu yasikuwa na Uwezo wa kusikia na kuelewa kitu alichozungumza Rais
Je Kuna haja ya CCM kuomba jukwaa kama lile na kuwaomba Radhi Wafanyakazi kwa Kuwadhalilisha?
Nataka kusikia maoni ya wana CCM