CCM waenda mikoani kuukana ufisadi; Wapeleka ujumbe wa NEC mkoa kwa mkoa

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797




*Wapeleka ujumbe wa NEC mkoa kwa mkoa
*Nape asema watapambana hadi washinde


Na Edmund Mihale, Dodoma

CHAMA Cha Mpinduzi (CCM) kimeanza ziara mikoani kupeleka ujumbe wa
Halmashauri Kuu ya CCM kwa wanachama kuwa kimedhamiria kupambana na ufisadi ndani na nje ya chama hadi kishinde.

Katibu wa Itikadi na Uenezi, Bw. Nape Nnauye aliyasema hayo Makao Makuu ya chama hicho mjini Dodoma jana, wakati akitangaza ratiba ya mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Wilson Mukama na Sekretarieti ya chama hicho mkoani hapa.

Alisema chama hicho kimeandaa ziara kwa ajili ya kufikisha ujumbe wa Halmashauri Kuu kwa wanachama wake kuanzia leo ambapo watafanya makutano katika Uwanja wa Nyerere Square na kesho Mkoani Morogoro.

Alisema kuwa mapokezi hayo yataendelea katika Mkoa wa Pwani Wilaya ya Kibaha ambapo yatapokelewa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete. Alisema kuwa siku hiyo hiyo yataendelea katika Mkoa Dar es Salaam na Aprili 17 mwaka huu yatakuwa Zanzibar.

"Tutapambana na ufisadi hadi tushinde," alisema Bw. Nnauye.

Alisema kuwa CCM haitavumilia kuona inachafuliwa na watu wachache na kuwataka wanachama waliohama kwa hasira kutokana na kashfa ya ufisadi kurudi kundini.

Alisema uamuzi uliofikiwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa utafanyiwa kazi.Alisema uamuzi wa kuwachukulia hatua wanaojihusisha na ufisadi uko pale pale, hivyo wasidhani kuwa chama kimeishia hapo.

"Ndugu zangu Halmashauri Kuu iliamua kuwa tutapambana na ufisadi hadi tushinde, hivyo kama alivyozungumza mwenyekiti, wanaotuhumiwa wajiandae, tumefunga milango na madirisha yote, ili kuhakikisha tunashinda," alisema Bw. Nnauye.
 
Nape yupo kitengo cha propaganda cha CCM hivyo anafikiri kujivua kwao magamba ni kitu cha kwenda kuwaambia wananchi na anadhani kuwa ni kitu cha kushagiliwa na watu. CCM ni sikio la kufa, kila wanachofanya ni usanii tu.
 
Tatizo la CCM wanadhani tatizo ni kubadilisha sura za watu ndio ufumbuzi wa tatizo; wakati tatizo ni mfumo wa kutumia rasilimali na vyombo vya usalama vya umma kulinda CCM na ufisadi wake halafu wanakurupuka na kuondoa kamati kuu na sekretariati pamoja na watu 3 wanaodhani ni mafisadi basi wako safi. Wanacheza hawa, ufisadi kwa CCM uko institutionalised mpaka ndani ya serikali. Kwa hiyo kinachotakiwa ni kufumua mfumo na sio kubadilisha sura, lakini wajidanganya wao kwanza halafu wanadhani watawadanganya na watanzania. Nasema hawa wamepotoka kabisa!!
 
Walishawahi kufanya ujinga huu wa kuwapeleka mawaziri kuitangaza bajeti isiyokidhi maendeleo sasa wanakuja na hoja hii tena. Bila shaka wanapoteza muda na hakuna wa kuwasikiliza hiki ni kipindi cha mvua watangazie wananchi kulima katika kilimo kwanza na sio muda wa siasa huu. Pumbafu kabisa hawa.
 
Baada ya kufanya wanachokiita kujivua gamba CCM wasitegemee kwamba mtanzania mwenye akili timamu ataamini akiambiwa kwamba sasa ufisadi umekwisha CCM. Muda wa kuwadanganya watu kwa kukubali kila kinachosemwa umepita , sasa hivi watu wanaelewa na wanaona hivyo wanataka matendo zaidi kuliko porojo na ngonjera.
 
May be i can honestly say it is too late......

Wamechelewa, ufisadi CCM hauko kwenye magamba, uko ndani kwenye damu.....

Watoe damu waweke nyingine ndipo nitaanza kuwaamini........subirini pamoja nami na mtaniambia....

Nape mtoto mdogo sana, kama Makamba na vile vitoto vya UVCCM vilimuweza ije kuwa RA na EL...akamuulize baba yake JK atamwambia....

Hii ngoma bado mbichi, haijaiva bado, utavimbiwa chijana mapemaaaa
 
it wont work.. Nyoka ni nyoka tu hata akijivua gamba atabaki kuwa nyoka tena mkali zaidi, anyway nawatakia kila la kheri.. ila Nape pamoja na uwezo wake jukumu alilopewa ni gumu sana hicho chama kimeoza mno kiasi kwamba ni mzigo kwa huyu dogo
 
it wont work.. Nyoka ni nyoka tu hata akijivua gamba atabaki kuwa nyoka tena mkali zaidi, anyway nawatakia kila la kheri.. ila Nape pamoja na uwezo wake jukumu alilopewa ni gumu sana hicho chama kimeoza mno kiasi kwamba ni mzigo kwa huyu dogo
Unastahili senksi yangu maana wanapoteza muda bure na vijisenti ukumbuke sasa wanataka kupambana na wanaowachangia fedha za kuzunguka mikoani na fedha za umma tunazitazama kwa macho yetu katika mkamati ya Zito Mrema na Cheyo
 
watuambie kwanza kagoda ni ya nani na pesa zirudi, watuweke wazi kuhusu ufisadi wa meremeta, deep green, dowans na tuone watu wakiwajibishwa kisheria, kisiasa na wafilisiwe, then ndipo watakapopata guts za kuja mikoani kutueleza. Huwezi kubadilisha safu ya uongozi ukasema umemaliza kazi, kubadilisha safu ni jambo la kawaida kwenye taasisi yeyote ile.
 
Kuleni chakula bora cha kuujenga mwili na kujenga nyumba safi pa kulala pawe bora? CCM wanashangaza sana wanashindwa kutambua kuwa binadamu anaona mazuri yote na wao kwa kuwa wana serikali ni jukumu lao kutoa maisha bora na kupinga vita rushwa sasa kama wanatunza wala rushwa wanadhani nani atawasikiliza eti kwa kuwa Nape kasema? Tunataka tuwaone wala rushwa mahakamani kama wana ubavu wa kufanya hivyo.
 




*Wapeleka ujumbe wa NEC mkoa kwa mkoa
*Nape asema watapambana hadi washinde


Na Edmund Mihale, Dodoma

CHAMA Cha Mpinduzi (CCM) kimeanza ziara mikoani kupeleka ujumbe wa
Halmashauri Kuu ya CCM kwa wanachama kuwa kimedhamiria kupambana na ufisadi ndani na nje ya chama hadi kishinde.

Katibu wa Itikadi na Uenezi, Bw. Nape Nnauye aliyasema hayo Makao Makuu ya chama hicho mjini Dodoma jana, wakati akitangaza ratiba ya mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Wilson Mukama na Sekretarieti ya chama hicho mkoani hapa.

Alisema chama hicho kimeandaa ziara kwa ajili ya kufikisha ujumbe wa Halmashauri Kuu kwa wanachama wake kuanzia leo ambapo watafanya makutano katika Uwanja wa Nyerere Square na kesho Mkoani Morogoro.

Alisema kuwa mapokezi hayo yataendelea katika Mkoa wa Pwani Wilaya ya Kibaha ambapo yatapokelewa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete. Alisema kuwa siku hiyo hiyo yataendelea katika Mkoa Dar es Salaam na Aprili 17 mwaka huu yatakuwa Zanzibar.

"Tutapambana na ufisadi hadi tushinde," alisema Bw. Nnauye.

Alisema kuwa CCM haitavumilia kuona inachafuliwa na watu wachache na kuwataka wanachama waliohama kwa hasira kutokana na kashfa ya ufisadi kurudi kundini.

Alisema uamuzi uliofikiwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa utafanyiwa kazi.Alisema uamuzi wa kuwachukulia hatua wanaojihusisha na ufisadi uko pale pale, hivyo wasidhani kuwa chama kimeishia hapo.

"Ndugu zangu Halmashauri Kuu iliamua kuwa tutapambana na ufisadi hadi tushinde, hivyo kama alivyozungumza mwenyekiti, wanaotuhumiwa wajiandae, tumefunga milango na madirisha yote, ili kuhakikisha tunashinda," alisema Bw. Nnauye.

http://www.google.com/imgres?imgurl=http://i826.photobucket.com/albums/zz188/JamiiForums/kikwete_rostam1.jpg&imgrefurl=https://www.jamiiforums.com/tanzania-2010-2015/76301-igunga-kikwete-amnadi-rostam-picha-3.html&h=473&w=710&sz=60&tbnid=5-WBF3xiZRx-jM:&tbnh=93&tbnw=140&prev=/search%3Fq%3Dkikwete%2B%2526%2Brostam%2Bpictures%26tbm%3Disch%26tbo%3Du&zoom=1&q=kikwete+%26+rostam+pictures&hl=en&usg=__GEFr-PWW5R43kAxYqfvOVBY2Aw8=&sa=X&ei=mrmmTZz9EsGbhQfY8Y3ZCQ&ved=0CCIQ9QEwAg
 
http://
 




*wapeleka ujumbe wa nec mkoa kwa mkoa
*nape asema watapambana hadi washinde


na edmund mihale, dodoma

chama cha mpinduzi (ccm) kimeanza ziara mikoani kupeleka ujumbe wa
halmashauri kuu ya ccm kwa wanachama kuwa kimedhamiria kupambana na ufisadi ndani na nje ya chama hadi kishinde.

Katibu wa itikadi na uenezi, bw. Nape nnauye aliyasema hayo makao makuu ya chama hicho mjini dodoma jana, wakati akitangaza ratiba ya mapokezi ya katibu mkuu wa ccm, bw. Wilson mukama na sekretarieti ya chama hicho mkoani hapa.

Alisema chama hicho kimeandaa ziara kwa ajili ya kufikisha ujumbe wa halmashauri kuu kwa wanachama wake kuanzia leo ambapo watafanya makutano katika uwanja wa nyerere square na kesho mkoani morogoro.

Alisema kuwa mapokezi hayo yataendelea katika mkoa wa pwani wilaya ya kibaha ambapo yatapokelewa na mwenyekiti wa ccm, rais jakaya kikwete. Alisema kuwa siku hiyo hiyo yataendelea katika mkoa dar es salaam na aprili 17 mwaka huu yatakuwa zanzibar.

"tutapambana na ufisadi hadi tushinde," alisema bw. Nnauye.

Alisema kuwa ccm haitavumilia kuona inachafuliwa na watu wachache na kuwataka wanachama waliohama kwa hasira kutokana na kashfa ya ufisadi kurudi kundini.

Alisema uamuzi uliofikiwa katika kikao cha halmashauri kuu ya taifa utafanyiwa kazi.alisema uamuzi wa kuwachukulia hatua wanaojihusisha na ufisadi uko pale pale, hivyo wasidhani kuwa chama kimeishia hapo.

"ndugu zangu halmashauri kuu iliamua kuwa tutapambana na ufisadi hadi tushinde, hivyo kama alivyozungumza mwenyekiti, wanaotuhumiwa wajiandae, tumefunga milango na madirisha yote, ili kuhakikisha tunashinda," alisema bw. Nnauye.

mwenyekiti gani ndio huyu anayewainua mikono mafisadi au mwingine, kwanza arejeshe fedha za epa zilizomuingiza ikulu 2005.
 

Attachments

  • Kikwete & Lowassa.jpg
    Kikwete & Lowassa.jpg
    7.4 KB · Views: 22
  • Kikwete & Rostam.JPG
    Kikwete & Rostam.JPG
    37.9 KB · Views: 27
Watanzania wa leo hawataki kudanganyika kwa maneno wanataka vitendo; Mukama kama kweli amedhamilia kupambana na ufisadi kazi yake ya kwanza nikuweka mkakati wa kukirudisha chama kwa wenyewe wakulima na wafanyakazi. Pili Mukama afanyae kama alivyokuwa anafanya Phillip Mangula, asikubali kutumia rushwa kwa kuwahonga/ kuwanunua wapinzani kujiunga na CCm kwani kufanya hivyo kunadhoofisha chama kwa kuunda makundi ya WAKUJA kama wakina Tambwe Hiza, Msabaha na Walid Kaborou na wale wazamani!! Hao mercenaries/ mamluki wanakuwa hawana mapenzi kwa chama bali kwa wale waliowanunua!!
 
Hawa jamaa wanadhani bado wanadhani watu wanaoongozwa wa enzi za mwalimu. Tunasubiri vitendo na sio maneno kama zamani.....
 
Ufisadi wa ccm upo mioyoni na migongoni mwa wana-ccm wote kwa hiyo kuzunguka nchi nzima nikujichoresha zaidi...............wangewakamata mafisadi na kuwafilisi mali zao na kila mtanzania akaona live hilo lingesaidia................hizi longolongo sidhani km zitaendelea kuwahadaa watz kwani waliisha ng'amua janja ya ccm............ili sisiemu ionekane na iwe safi inabidi hadi kikwete ajiuzuru kwani naye yupo kwenye list of shame ambayo hajawahi kuikanusha..............kinachotaka kufanyika ni kuwatolea mhanga baadhi kwa mlango wa mbele lakini wanapita kirahisi kwa mgongo wa nyuma
 
Ufisadi haupingwi kwa kupepeta mdomo majukwaani. Kinachotakiwa ni kukamata mali za mafisadi na kuwaburuza mahakamani. Vinginevyo ni utapeli mtupu.
 
watuambie kwanza kagoda ni ya nani na pesa zirudi, watuweke wazi kuhusu ufisadi wa meremeta, deep green, dowans na tuone watu wakiwajibishwa kisheria, kisiasa na wafilisiwe, then ndipo watakapopata guts za kuja mikoani kutueleza. Huwezi kubadilisha safu ya uongozi ukasema umemaliza kazi, kubadilisha safu ni jambo la kawaida kwenye taasisi yeyote ile.

Umesema sahihi mkuu, wanataka kutupiga changa la macho- wajue waTZ wa leo sio wa jana-tumeshagundua janja yao
 
Back
Top Bottom