CCM Uchikimbia Nchale Uchichimama Nchale! Baada ya kushinda kesi Segerea watapata uungwaji mkono?

Kasimba G

JF-Expert Member
Jan 19, 2011
3,428
2,609
Wahenga walishasema lakuvunda halina ubani, CCM wameshinda kesi ya ubunge segerea! je watapata uungwaji mkono kwa kutumia hukumu hiyo? Nadhani mambo yatakuwa magumu zaidi kwao, kwa kweli kama mkaazi wa segerea, naona kama imeamsha chuki mbaya kabisa dhidi ya CCM.

Hata baadhi ya wanachama wa CCM wameshangaa na kutahayari, sasa CCM watapoteza zaidi tofauti na matarajio yao, wamekosa charisma, wangefocus kidogo isingekuwa kama mambo yalivyo leo, anyway siasa za kiafrika huwa hawajali, wanaona kwa kuwa muda huu jamaa kashinda basi, lakini ina madhala makubwa kwa chaguzi zitakazo fuatia, inaweza ikawa mala ya mwisho kwa CCM kushinda kiti cha ubunge siyo segerea tuu bali hata sehemu nyingine nyingi ambazo walijua mambo yalivy jiri segerea.

Kwa wakati huu yes ni mbaya saana kwa CCM na No nayo ni mbaya zaidi kwa CCM, ndio maana nimechukua msemo wa walinzi wa zamani wa kimachinga, uchikimbia nchale uchichimama nchale!

Nawasilisha
 
.. Kasimba G, wanalijua hilo na ndio maana wanatumia kila hila inayowezekana kubaki.
Mtu yeyote aliekata tamaa hufanya lolote pasi na kuzingatia madhara yatayojitokeza.
CCM wamekataa tamaa, wapo tayari kwa lolote.
 
Last edited by a moderator:
dah nimehudhunika sana kwa hii hukumu, mbona mambo yalikuwa wazi sana?? naona ccm sasa ni rahisi kuwashinda katika uchaguzi hasa tukilinda kura zetu kuliko kuwapeleka mahakamani.
yawezekna vipi watu waanze sherehe yahukumu hii tangu jana? hawa mafisadi walijuaje?? yawezekana hata hukumu wamekuwa nayo kitambo.
napendekeza katika katiba ijayo hawa majaji ajira zao zipatikane kwa kuapply kama tunavyoomba kazi nyingine wawe interviewed na maconsultants waliokubuu wa sheria na sio mfumo wa sasa raisi anateua maswahiba pia makada wa chama CCM kuwa majaji hawa ni wahujumu tu wademokrasia, hii ni hujuma, tulinde kura zetu jamani.
leo sina raha kabisa jamani
 
Mimi nadhani wanapoteza umaarufu zaidi, mshauri wao wa mambo ya siasa hana charisma, haoni mbeleeee, alitakiwa awe anaweza kuona mbele madhala ili kulinda image ya chama chao
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom