Taarifa kwa WanaJF mlizoea kusema vibaya dhidi ya CCM wakati huo mkiwapa misifa CDM;
CCM kama chama mama nchini mwetu tunaendesha mambo yetu kisayansi kwa kukaa chini na kutafakari kupitia vikao vya ndani ambavyo havihitaji kuandikwa kwenye magazeti. Ikumbukwe huu ni mwaka wa uchaguzi ndani ya chama ikiwa lengo kuu la uchaguzi ni kuwachuja makapi na kupanga timu ya USHINDI kuelekea 2015.
Wapenzi na wakereketwa wa CCM mkae mkao wa KULA PWEZA ili kucharge nguvu, tupate mvurumisha CDM na vyama vyote vya upinzani.
Msije kuumiza vichwa kutokana na ziara zisizo na tija zinazofanywa na askari uchwara wa CDM huku mikoani, hizo ziara zimepangwa kwa nia ya kuboresha mifuko ya viongozi wao kwa kulipana posho tu. Hizo mbinu za kufungua matawi papo kwa hapo pasipo uchambuzi yakinifu zimepitwa na wakati. Haingii akilini leo hii kwenda kijijini Mtwara kumuuzia mwanakijiji sera ya chama na siku hiyohiyo kufungua tawi!!!!!!!
Kidumu chama cha mapinduzi na sera zake za kuwapa nuru watanzania.
Nadhani mwanzisha hoja hakuwa na hoja bali a,epost ilio chama tawala kisionekane hakifanyi lolote. Nashauri usubiri wakati kwani utasema ukweliWananchi wameanza kurudisha imani kutokana na:
1. Kuwatosa mawaziri ambao ni wakala wa ufisadi
2. Iddi Simba kapelekwa Kisutu
Pia tunafanya mchakato wa watoa siri nyeti ndani ya serikali na wakala wote wa CDM tunapiga chini