CCM: Tujisahihishe au Tugawane Chama

CCM imeenda kinyume na katiba yake kuingia mseto na CUF; Jamani, hata katiba ya chama nayo viongozi wanakosa umakini kwa jambo ambalo pengine linahitaji kikao kimoja tu kusahihisha? Angalau suala la CCM kuacha itikadi ya chama kwenye katiba yake ibaki kusomeka 'ujamaa na kujitegemea' kidogo inaeleweka ingawa ni bado sio sahihi kosa, hata hili la mseto?

KAKA MCHAMBUZI NA CCM WENGINE,NAOMBA NIULIZE SWALA MOJA PIA AMBALO HALINA DIRECT CONNECTION NA POST YAKO,SWALI LANGU AMBALO LBD WADAU WAKIJADILI HUMU PIA INAWEZA SAIDI...NI JE NINI MANTIKI YA MAGEUZI AMBAYO TUNAAMBIWA CCM INAFANYA SHV?YAANI KUBADILISHA UTARATIBU WA KUMPATA MGOMBEA URAIS,KUUNDA CHOMBO CHA WASHAURI YAANI MA RAIS WASTAAFU,NA KUUNDA TENA SIJUI KUBORESHA KAMATI YA MAADILI YA CHAMA NA MENGINE NIISHIE HAYO.

KWA MTAZAMO WANGU WAMBALI NAONA MAMBO HAYA HAYANA TIJA KWA CCM,SABABU NINAZO KWANZA KAMATI YA MAADILI IPO KWANINI IUNDWE NYINGINE?ILIYOPO HAUFAI?NA KAMA NDIO KWANINI?PILI MARAIS NA VIONGOZI WAKUU WA NCHI YETU KWAKAWAIDA NI WASHAURI TAYARI ..SO JE KUNA ULAZIMA GANI WAKUWA AUTHORISE KWA KUWAUNDIA CHOMBO?SIO KUONGEZA GHARAMA SIZIZO ZA MSINGI? NA MOVE HII NAONA KAMA CHAMA KINAELEKEA KUPOKONYWA MAMLAKA YA MAAMUZI KWA WANACHAMA NA BADALA YAKE MAAMUZI MENGI YAWE YANAFANYA NA WACHACHE, MIE KWELI NAWAZA HIVYO WKT TUNAONGELEA KATIBA KUPUNGUZA MAMLAKA KWA WATU WACHACHE NAONA KAMA CCM KAMA INAKAZANA THE OTHER WAY AROUND YAANI KUTOA KWA WENGI KUPELEKA KWA WACHACHE..PENGINE LBD MIE SIJAELEWA NA TAFSIRI YANGU SI SAHIHI NAOMBENI WENYE UELEWA PENGINE ZAIDI KTK HILI TUWEKANE SAWA....[/QUOTE]

Sidhani kama nina jibu la moja kwa moja lakini pengine maoni;

  1. Kuhusu suala la kumpata mgombea urais, utaratibu uliopo ni mbovu sana kwani mianya ya rushwa ni mipana mno; wanaopigia kura jina la mgombea urais ni wajumbe wa mkutano mkuu wa taifa toka mikoa yote, hawapungui wajumbe 2,000; ni hawa hawa pia ndio uchagua wajumbe wa NEC;

Siku moja jaribu kupanda treni kutoka Mwanza kuja DSM kupitia Dodoma atika nyakati za chaguzi za Urais au NEC; kinachotembea mle ni bahasha, konyagi, chips mayai, whisky na bia; wenye pesa wanatuma mawakala wao mle ambao safari nzima kinachishindaniwa ni dau tu; mpaka treni ifike Dodoma, tayari wajumbe wana msimamo juu ya mgombea fulani kutokana na msimamo wa matumbo yao na mifuko yao; Kwa mgombea mwenye pesa nyingi ni rahisi sana kuwakamata wajumbe wengi kama sio wote kutoka Mwanza, Mara, Shinyanga, na Kagera; na ukijipanga kwa wajumbe wa treni ya Kigoma, Tabora, kuja Dodoma, ndio umemaliza kazi; wajumbe toka mikoa ya kusini, nyanda za juu kusini ukiokota okota kadhaa na huko haukosi ushindi;

Kwa maoni yangu utaratibu huu lazima ubadilishwe ingawa sina uhakika kama mabadiliko ynayozungumzwa yatalenga haya ninayozungumza; Pengine niseme pia kwamba ni sahihi kabisa wajumbe hawa kuchagua wagombea urais, NEC kwani inapanua demokrasia katika michakato hiyo ndani ya Chama; lakini ingekuwa busara zaidi kama wajumbe hawa wangefanyiwa utaratibu wa kupiga kura huko huko mikoani kwao bila ya kuwapa wenye pesa mianya ya kuwakusanya wote kwenye matreni na mabasi; na utaratibu wa kuwapigia kura wagombea huko mikoani lakini sio kabla wagombea wote hawajapitishwa mikoani kujieleza wasifu wao, kuruhusu wajumbe waulize maswali yote yenye shaka juu ya uadilifu wa mgombea n.k.

Kwa mfano, ni suala la ajabu sana katika kura za maoni udiwani, ubunge, hata Urais kwa wajumbe/wanachama kukatazwa kuuliza maswali about the integrity ya wagombea uongozi; in my opinion, it is the basic right of the electorate kutosheka na personal integrity and commitement of a candidate; sidhani kama kuna mtu yoyote wants to vote for a self – seeking, corrupt, power hungry candidate; to question and demand of a candidate to account for his/her past performance in public life (and to an extent private), is legitimate, in my opinion; and this should not remain only at the accusations and allegations levels, but wapiga kura have a right to be fully informed of the background of the candidate; ni matumaini yangu mabadiliko yanayozungumzwa yatalenga huko pia;


  1. Kuhusu kamati ya washauri, sijui kwa undani sana suala hili lakini ninachoweza kusema ni kwamba KATIBA ya sasa haielezei nafasi ya wazee katika Chama kwa ufasaha; wanatajwa kidogo sana kwenye sehemu ya nne ya katiba chini ya heading WAZEE NA JUMUIYA ZA WANANCHI:
"Kutakuwa na sehemu ya wazee ambamo watakuwepo wazee wote wanaokubali imani, malengo na madhumuni ya CCM."
This is too narrow in my view. Wazeee wastaafu ni muhimu wawekwe kwenye chombo chao in my opinion; wapo wanaosema kwamba itawapunguza nguvu, but mimi naona it is the other way round kwani badala ya kusema mfano Mzee karume alisema hili na lile kwenye NEC/CC, sasa itakuwa msimamo wa wazee wa CCM ni this and that, hence kuleta uzito zaidi;

  1. Kuhusu kamati ya maadili, pia sina uelewa sana wa nini kinaendelea katika hilo lakini jambo lililo wazi ni kwamba kamati hii kwa sasa ni ‘A Toothless Dog;'
 
Mkuu, wewe ni sauti ya mtu aliyeachwa mwituni peke yake baada ya wenzake kubadilisha mwelekeo wa njia na malengo ya safari yao. Ni miaka 20 tangu wenzako ( CCM) walipobadilisha njia na malengo. Mtazamo wako ulishakuwa historia na kugawana hiyo CCM ikabaki salama ni vigumu sana. Subirini mambo ya KANU na UNIP.
 
kwa mfano, ni suala la ajabu sana katika kura za maoni udiwani, ubunge, hata urais kwa wajumbe/wanachama kukatazwa kuuliza maswali about the integrity ya wagombea uongozi; in my opinion, it is the basic right of the electorate kutosheka na personal integrity and commitement of a candidate; sidhani kama kuna mtu yoyote wants to vote for a self – seeking, corrupt, power hungry candidate; to question and demand of a candidate to account for his/her past performance in public life (and to an extent private), is legitimate, in my opinion; and this should not remain only at the accusations and allegations levels, but wapiga kura have a right to be fully informed of the background of the candidate; ni matumaini yangu mabadiliko yanayozungumzwa yatalenga huko pia;

  1. kuhusu kamati ya washauri, sijui kwa undani sana suala hili lakini ninachoweza kusema ni kwamba katiba ya sasa haielezei nafasi ya wazee katika chama kwa ufasaha; wanatajwa kidogo sana kwenye sehemu ya nne ya katiba chini ya heading wazee na jumuiya za wananchi:
"kutakuwa na sehemu ya wazee ambamo watakuwepo wazee wote wanaokubali imani, malengo na madhumuni ya ccm."
this is too narrow in my view. Wazeee wastaafu ni muhimu wawekwe kwenye chombo chao in my opinion; wapo wanaosema kwamba itawapunguza nguvu, but mimi naona it is the other way round kwani badala ya kusema mfano mzee karume alisema hili na lile kwenye nec/cc, sasa itakuwa msimamo wa wazee wa ccm ni this and that, hence kuleta uzito zaidi;
  1. kuhusu kamati ya maadili, pia sina uelewa sana wa nini kinaendelea katika hilo lakini jambo lililo wazi ni kwamba kamati hii kwa sasa ni ‘a toothless dog;'

nimekupata mawazo yako,ngoja tuvute subira tuone uhalizia wa mabadiliko yenyewe basi maana kujadili kabla ya kuwekwa wazi tutabashiri mambo.itakuwa vizuru wasipoguza democracy ambayo mie naona kwa mbali kama mfuo huu utawapa nguvu baadhi waliopo na waliowahi kuwa kwenye madaraka maamuzi makubwa.anyway let us wait n see
 
Mkuu, wewe ni sauti ya mtu aliyeachwa mwituni peke yake baada ya wenzake kubadilisha mwelekeo wa njia na malengo ya safari yao. Ni miaka 20 tangu wenzako ( CCM) walipobadilisha njia na malengo. Mtazamo wako ulishakuwa historia na kugawana hiyo CCM ikabaki salama ni vigumu sana. Subirini mambo ya KANU na UNIP.

Unaposema ni miaka 20 tangia Chama kibadilishe njia na malengo, Je, hayo wanachama huko vijijini au huko kwenye kata ambapo ndio mizizi ya chama ipo wanajua hilo? kwanini wanawapokea viongozi wao kwa nyimbo za kulinda ujamaa na kujitegemea? Kwanini wanapepea azimio la Arusha?

Sielewi hoja yako ya kugawanya chama na kubakisha chama salama ni nini; salama kwa maana ipi? vinginevyo uwezekano wa kugawanya chama kiwe vipande viwili vinavyopishana kwa itikadi ni jambo jema tu- and not only inevitable at this juncture but desirable; Uwezekano wa CCM kukubaliana juu ya itikadi moja kwa vitendo kwa sasa ni ngumu sana; njia pekee ya kubakisha chama kuwa kimoja ni kwa kuendelea kuwaadaa wananchi na wanachama kwamba itikadi yetu ni ya ujamaa; vinginevyo ni jambo lililo dhahiri kwamba CCM kurudi kwa mkulima na mfanyakazi kwa dhati na vitendo ni vigumu sana; vinginevyo uwepo wa hali ya siasa ambapo kwa upande mmoja viongozi wa CCM waliopo meza kuu ni mabepari na mabwanyenye na kwa upande mwingine wanachama wa kwenye hadhara wanaimba kwa shangwe na kutimua vumbi kwa kauli zao za kuapa kulinda siasa ya ujamaa, is a timing bomb and a much bigger problem to the party than Ufisadi; Tutakuja ona hili siku moja;

Suala la KANU, UNIP, kwa mazingira ya Tanzania haiwezekani; rejea historia ya CCM kikatiba na sera za awali za nchi hii utagundua hilo; kwani Kenya wao baada ya Mkoloni waliendeleza sera zile zile za mkoloni za 'soko huria', kwahiyo baada ya mfumo wa vyama vingi kuingia Kenya, tatizo la ideological clash kwa Chama tawala halikuwa la msingi, na sio hilo lililokimaliza KANU bali sababu nyingine kabisa; Sisi Tanzania CCM ilituonjesha siasa na sera za ujamaa na kujitegemea kwa miaka 19 na tukaona faida zake lakini tukugundua kwamba hasara zake zilichangiwa na mapungufu katika utekelezaji na pia njama za mabepari wa humu humu ambao wao walishashiba na hawakuwa tayari kuingia katika siasa za Mwalimu Nyerere za 'tuanze sote pamoja kama taifa jipya na huru'; Leo hii CCM inaimba siasa za ujamaa majukwaani, kivitendo CCM ni chama cha kibepari, kama ilivyo Chadema;
 
Serikali ya umoja kati ya CCM na CUF Zanzibar si ni serikali ya mseto au? Pengine nina uelewa mdogo katika hili; Na katika mazingira ya kawaida, si katiba ya Chama inatakiwa iwe ina anticipate hayo and therefore have that provision? Swali langu la msingi hapa ni je, ni katika mwongozo upi au katiba ipi suala la CCM kuunda serikali ya mseto na chama cha upinzani linafafanuliwa kama vile Chadema wanavyofanya katika katiba yao? Au kwa CCM suala hili lilitokana tu na azimio la kikao. Hoja yangu ya msingi ni kwamba, suala la mseto linahitaji mwongozo na ni lazima uwepo kikatiba;unless CCM zanzibar na CCM bara wana katiba tofauti;
Unatakiwa kikatiba (na wananchi wa Z'bar) kuunda serikali ya umoja wa kitaifa. Hii haijali kaa umetokea chama gani, usipounda serikali ya umoja, mahakama kuu itatengua cabinet yako.
haijali wewe unatoka chama gani.
Mkuu, ujue kuwa hivi vyama vyote vya upinzani, vilikutana Zanzibar kuanzisha NCCR-Mageuzi ili kuleta mageuzi ya katiba ya nchi na walikubaliana wasishiriki uchaguzi kabla ya katiba kurekebiswa. Ila wananchi ndiyo wanaowafanya washiriki kwenye hizi chaguzi, la sivyo vingekufa kama '63.
Same thing, CCM haina budi kufuata katiba ya Zanzibar, ila haiwezi kubadili katiba yake ili iwape mwanya mivyama mingine iingie ubia na CCM kwenye seikali ya muungano.
Basically, weirdness ya serikaliya CCM, can best be attributed to preserving the Union, as I've said earlier.
 
Unatakiwa kikatiba (na wananchi wa Z'bar) kuunda serikali ya umoja wa kitaifa. Hii haijali kaa umetokea chama gani, usipounda serikali ya umoja, mahakama kuu itatengua cabinet yako.
haijali wewe unatoka chama gani.
Mkuu, ujue kuwa hivi vyama vyote vya upinzani, vilikutana Zanzibar kuanzisha NCCR-Mageuzi ili kuleta mageuzi ya katiba ya nchi na walikubaliana wasishiriki uchaguzi kabla ya katiba kurekebiswa. Ila wananchi ndiyo wanaowafanya washiriki kwenye hizi chaguzi, la sivyo vingekufa kama '63.
Same thing, CCM haina budi kufuata katiba ya Zanzibar, ila haiwezi kubadili katiba yake ili iwape mwanya mivyama mingine iingie ubia na CCM kwenye seikali ya muungano.
Basically, weirdness ya serikaliya CCM, can best be attributed to preserving the Union, as I've said earlier.

Nimekusoma; ila nina swali - mantiki ya chama kama Chadema kuweka kwenye katiba yake provision juu ya kuingia mseto na vyama vingine ikibidi ni nini?
 
Nimekusoma; ila nina swali - mantiki ya chama kama Chadema kuweka kwenye katiba yake provision juu ya kuingia mseto na vyama vingine ikibidi ni nini?
Hata CUF wanayo hiyo, lakini nadhani uliona debate ya Mbowe na Hamad.
Ukiwa bado mchanga na huna uhakika wa kupata majority, utajaribu kuweka milango wazi,this is not necessary when you think you can easily sweep an election at any time.
And definately, that option is usually ignored after you get the majority as is the case with CDM in the making of opposition camp.
 
Mchambuzi,

..lakini nadhani hata nyie mnaojiita waumini wa Azimio la Arusha sidhani kama mna guts za kulifuata kama alivyobainisha Mwalimu Nyerere.

..sasa hebu kuwa honest na utueleze unafikiri ni sehemu ipi ya azimio la arusha bado iko relevant in the times and era that we live today.
 
Unaposema ni miaka 20 tangia Chama kibadilishe njia na malengo, Je, hayo wanachama huko vijijini au huko kwenye kata ambapo ndio mizizi ya chama ipo wanajua hilo? kwanini wanawapokea viongozi wao kwa nyimbo za kulinda ujamaa na kujitegemea? Kwanini wanapepea azimio la Arusha?

Sielewi hoja yako ya kugawanya chama na kubakisha chama salama ni nini; salama kwa maana ipi? vinginevyo uwezekano wa kugawanya chama kiwe vipande viwili vinavyopishana kwa itikadi ni jambo jema tu- and not only inevitable at this juncture but desirable; Uwezekano wa CCM kukubaliana juu ya itikadi moja kwa vitendo kwa sasa ni ngumu sana; njia pekee ya kubakisha chama kuwa kimoja ni kwa kuendelea kuwaadaa wananchi na wanachama kwamba itikadi yetu ni ya ujamaa; vinginevyo ni jambo lililo dhahiri kwamba CCM kurudi kwa mkulima na mfanyakazi kwa dhati na vitendo ni vigumu sana; vinginevyo uwepo wa hali ya siasa ambapo kwa upande mmoja viongozi wa CCM waliopo meza kuu ni mabepari na mabwanyenye na kwa upande mwingine wanachama wa kwenye hadhara wanaimba kwa shangwe na kutimua vumbi kwa kauli zao za kuapa kulinda siasa ya ujamaa, is a timing bomb and a much bigger problem to the party than Ufisadi; Tutakuja ona hili siku moja;

Suala la KANU, UNIP, kwa mazingira ya Tanzania haiwezekani; rejea historia ya CCM kikatiba na sera za awali za nchi hii utagundua hilo; kwani Kenya wao baada ya Mkoloni waliendeleza sera zile zile za mkoloni za 'soko huria', kwahiyo baada ya mfumo wa vyama vingi kuingia Kenya, tatizo la ideological clash kwa Chama tawala halikuwa la msingi, na sio hilo lililokimaliza KANU bali sababu nyingine kabisa; Sisi Tanzania CCM ilituonjesha siasa na sera za ujamaa na kujitegemea kwa miaka 19 na tukaona faida zake lakini tukugundua kwamba hasara zake zilichangiwa na mapungufu katika utekelezaji na pia njama za mabepari wa humu humu ambao wao walishashiba na hawakuwa tayari kuingia katika siasa za Mwalimu Nyerere za 'tuanze sote pamoja kama taifa jipya na huru'; Leo hii CCM inaimba siasa za ujamaa majukwaani, kivitendo CCM ni chama cha kibepari, kama ilivyo Chadema;

Mkuu Mchambuzi,
Nimejaribu kufuatilia michango yake kwenye hii thread, na naona pamoja na kwamba kichwa cha mada ni Tujisahihishe au Tugawane Chama. Wewe mwenyewe umeonesha kukata tamaa option ya kwanza(ya Tujisahihishe) na mara kadhaa umeonesha why umepata huo mtazamo.

Vilevile kupitia thread hii nimeweza kusoma kwamba kwa sasa hivi, kisera hakuna tofauti ya msingi kati ya CCM na CHADEMA, vyote ni vyama vinavyopigania kutekeleza kwa ufanisi zaidi sera za Bretton Woods institutions. Kwa maana nyingine kisera ni vyama vya kibepari.(wanaCHADEMA naomba kukosolewa kama nimekosea).

In short, ni kama unakumbukia the good old days za striving for self reliance and development. Sasa napenda kujua what are your thoughts on the way forward? Je kuna haja ya kuanzisha chama chenye mrengo wa kushoto zaidi(socialist leaning), na kama ni hivyo, tayari ndani ya CCM asilimia 75% ya wanachama wake watakua tayari kuhamia huko. Sababu ni viongozi na wapambe wao wa karibu ndiyo wanaonufaika na hili soko holela(huria).

Au unasubiria the small spark that leads to the big bang ya CCM kupasuka?

But alll in all its a good analysis ya hali ya kisiasa ndani ya CCM,...
 
Mkuu Mchambuzi,
Nimejaribu kufuatilia michango yake kwenye hii thread, na naona pamoja na kwamba kichwa cha mada ni Tujisahihishe au Tugawane Chama. Wewe mwenyewe umeonesha kukata tamaa option ya kwanza(ya Tujisahihishe) na mara kadhaa umeonesha why umepata huo mtazamo.

Vilevile kupitia thread hii nimeweza kusoma kwamba kwa sasa hivi, kisera hakuna tofauti ya msingi kati ya CCM na CHADEMA, vyote ni vyama vinavyopigania kutekeleza kwa ufanisi zaidi sera za Bretton Woods institutions. Kwa maana nyingine kisera ni vyama vya kibepari.(wanaCHADEMA naomba kukosolewa kama nimekosea).

In short, ni kama unakumbukia the good old days za striving for self reliance and development. Sasa napenda kujua what are your thoughts on the way forward? Je kuna haja ya kuanzisha chama chenye mrengo wa kushoto zaidi(socialist leaning), na kama ni hivyo, tayari ndani ya CCM asilimia 75% ya wanachama wake watakua tayari kuhamia huko. Sababu ni viongozi na wapambe wao wa karibu ndiyo wanaonufaika na hili soko holela(huria).

Au unasubiria the small spark that leads to the big bang ya CCM kupasuka?

But alll in all its a good analysis ya hali ya kisiasa ndani ya CCM,...
Hata mimi nilitaka kujua mtazamo wake. Mkuu njoo utoe maoni yako.
But Mr. Alwattan, the Big Bang Theory usually huwa inaleta migawanyiko ambayo haitabase on ideology, rather than mere tribal, religious, regional and class warfare. Very, very, bad.
Instead, the route that the ANC Youth League is taking is more prefferable and highly practical in Tanzania. We have the fan base, so let's do it!!!
 
Mchambuzi,

..lakini nadhani hata nyie mnaojiita waumini wa Azimio la Arusha sidhani kama mna guts za kulifuata kama alivyobainisha Mwalimu Nyerere.

..sasa hebu kuwa honest na utueleze unafikiri ni sehemu ipi ya azimio la arusha bado iko relevant in the times and era that we live today.

Jokakuu, asante kwa swali zuri;

Kwanza, ni muhimu ieleweke wazi kwamba mimi sio muumini wa Azimio la Arusha Per Se, lakini nina amini kabisa kwamba tukilichambua azimio la Arusha kuna mambo mengi ambayo bado yana nafasi kubwa sana ya kumletea mwananchi wa kijijini ahueni ya maisha kwani muundo wa sasa wa soko huria limemtupa mwanakijiji huyu moja kwa moja; baadhi ya marekebisho muhimu ni pamoja kuhimiza demokrasia, uhuru na haki kwa raia kisiasa, kijamii na kiuchumi, haki ambazo zitalindwa in practice katika katiba mpya itakayotokana na wananchi wenyewe;

Mwalimu alipokea Tanzania toka kwa wakoloni ikiwa na watu takriban milioni 9; takwimu zinaelezea kwamba 95% ya watanganyika walikuwa wanaishi vijijini – sawa na kama watanganyika 850,000, na 5% mijini – sawa na takriban watanganyika 50,000; hali ya maendeleo nchini kama historia inavyotueleza, katika nyanja za miundo mbinu, viwanda n.k ilikuwa ni ya chini sana kulinganisha na mataifa mengine mengi yaliyotawaliwa na wakoloni; kwa maana hii, asimilia 95 ya nchi ya Tanganyika ilikuwa ni kijiji au mapori yenye binadamu wakiishi maisha duni;

Hali hii ilipelekea Mwalimu kutamka haya just before independence:
"If we allow land to be sold like a robe, within a short period, there would only be a few Africans possessing land in Tanganyika and all others would be tenants"

Na mbaya zaidi, katika kitabu kimoja by Samir Amin, anaelezea kwamba by 1959, European and Asian Settlers who formed barely 1.3% of the total population in Tanganyika owned 1,270,000 Hectares of fertile land and Africans owned 1,800,000 Hectares; hii inamaanisha kwamba watu 117,000 wa Tanganyika walikuwa wanamiliki karibia 50% ya ardhi yote yenye rutuba; na wengine kama milioni 8 na ushehe walikuwa wanamiliki the other 50% of fertile land in Tanganyika;

Ni dhahiri kwamba nchi ilikuwa katika a big imbalance at independence; lakini tunaona Nyerere jinsi gani aliachia ‘soko huru' liendelee 1962, 63, 64, 65, 66 kuona performance yake, na baadae kugundua kuna tatizo, kwani unlike nchi nyingine kama vile Kenya ambako wakoloni waliwekeza sana, Mwalimu akaona mbali kwamba – iwapo Tanganyika tungeiga tembo kupiga msamba ingetupeleka katika balaa kubwa siku za mbeleni.

Mwalimu kwenye kitabu chake cha TANU na RAIA ambacho ndicho kilimpelekea kuja na Azimio La Arusha muda mfupi baadae anasema hivi (UK 5-8):

["Tulipoanzisha TANU shabaha yetu ya kwanza ilikuwa kuleta UHURU wa watanganyika; Hatukutaka kuwaletea uhuru huo viongozi wachache wa TANU, au wanachama wachache wa TANU, na raia wengine wote wawe ni watumwa wao au raia wao, Uhuru wetu ni Uhuru wa raia wote wa Tanganyika; Ndiyo maana baadhi ya watu fulani walipoonyesha kwa vitendo vyao kwamba hawaelewi kuwa uhuru wetu, na heshima inayotokana na uhuru huo, ni kwa raia wote, bila ubaguzi, basi, Serikali ya TANU ilichukua hatua za kuwaondoa mashaka kabisa watu hao;

Leo tumeanza kupiga baragumu la pili; na baragumu hili ni baragumu la kuongeza utajiri wa nchi yetu. Kama vile mwanzo tulimwomba kila mwananchi kushirikiana na wenzake kuondoa umaskini. Swali ambalo hatuna budi tujiulize ni hili: Tunamwomba kila raia kufanya kazi kwa bidii tuondoe umaskini wa nani? Umaskini wa viongozi wa TANU? Au wa watumishi wa serikali? Au wa watu wachache wenye elimu, au nguvu, au bahati au ujanja? Au shabaha yetu ni kuondoa umaskini wa kila mtu kama vile shabaha yetu ya kwanza ilikuwa ni kuleta uhuru na heshima kwa kila mtu?

Najua kuwa tukiulizwa swali hili wote tutajibu bila kusita, na bila unafiki, kwamba shabaha yetu ni kuondoa umaskini wa kila mtu; Lakini tunaweza tukawa tunajidanganya bila kutambua kuwa tunajidanganya; baadhi ya vitendo vyetu vyaweza vikaipotosha shabaha yetu, bila sisi wenyewe kutambua kuwa shabaha yetu inapotosha;

Nitajaribu kueleza. Tulipokuwa tunatawaliwa na wakoloni tuligawanywa katika mafungu matatu; Wazungu walikuwa juu, wahindi walikuwa katikati na waafrika walikuwa chini, kwa hali zao za elimu, mali na vyeo. Yawezekana wachache wa kundi fulani la chini walipata bahati ya kuwa miongoni mwa kundi la juu; laini kwa ujumla hivyo, ndivyo tulivyokuwa;

Shabaha ya TANU na serikali ya TANU ni kuondoa makundi haya. Milango ya elimu, mali na vyeo, ambavyo jana ilikuwa imefungwa kwa waafrika leo inafunguliwa. Wazungu ha wahindi ambao jana walipita katika milango hiyo kwa urahisi kwa sababu cheti cha kupita kilikuwa ni rangi tu, wanaona kwamba cheti hicho siku hizi hakitoshi kumpitisha mtu asiyestahili kupita; Mambo haya tunayatenda hivi sasa na tutaendelea kuyatenda mpaka mafungu yale tuliyorithi kwa mkoloni yawe yameondoka; Jambo ambalo hatuna budi kujiuliza ni hili: Je, vitendo hivi vina shabaha gani? Ni Shabaha ya kuinua wanyonge wote wa jana? Au ni shabaha ya kuwatia Waafrika wachache katika nafasi ya wazungu na wahindi? Shabaha yetu ni kuondoa makundi kati ya raia, au ni kuunda makundi mapya? Tutakuwa na kundi la Waafrika ambao hawajambo katika hali na mali, elimu na vyeo, na kundi la waafrika ambao ni taabani katika mambo yote hayo;

Tuchukue mfano wa mishahara. Wakoloni walipokuwa hapa walipanga mishahara bila kujali uwezo wa watu wetu kuilipa mishahara hiyo, na bila kuilinganisha mishahara hiyo na mapato ya watu wetu; Lakini ilikuwa ni ada yao kufanya hivyo; serikali ya wageni haiwezi kujali maisha ya raia; serikali yao ilikuwa ni serikali ya ubwana na ufahari; na walijitimizia ubwana wao na fahari yao, bila kujali uwezo wa watu wetu wa kugharamia ubwana huo na fahari hiyo;

Lakini baadhi yetu tulikuwa hatutambui jambo hilo. Waafrika wengi tulikuwa tumekwisha kusahau kwamba mzigo ule wa ubwana na fahara ni mzito mno na watu hawawezi kuubeba; Kilichokuwa kikituuma ni kwamba ubwana ule na fahari ile wazungu waligawana wenyewe tu, bila kutugawia na sisi pia; baadhi yetu hatukuwa tunadai uhuru ili uwapunguzie watu wetu mzigo huu wa ubwana na ufahari, bali tama yetu ilikuwa ni kukali viti vile vya ubwana na ufahari; tama yetu haikuwa kushika vyeo tu, vilivyokuwa vinashikiliwa na wazungu hapo zamani, tulitaka na mishahara pia iliyokuwa ikifuatana na vyeo hivyo bila kujali kama watu wanaweza kulipa mishahara hiyo, na bila kujali maisha ya watu wetu;

Tulipopunguza mishahara ya mawaziri, tulisifiwa kwamba tumefanya jambo zuri; na ni kweli kwamba tulifanya jambo zuri; mshahara wa waziri wa kikoloni ulikuwa zaidi ya Shs 5,000/= kwa mwezi; juu ya hiyo kulikuwa na matumizi mengine ya kikazi ambayo hata sisi hatukuondoa; sisi tulipunguza mshahara huo na kuufanya Shs 3,000/= kwa mwezi kwa kila waziri pamoja na waziri mkuu pia; Mshahara huu ukilinganisha na mishahara wanayopata mawaziri katika sehemu nyingine za Africa au dunia, ni mshahara mdogo sana; lakini kulinganisha mishahara ya mawaziri wetu na mishahara ya mawaziri wan chi nyingine, ambayo yaweza kuwa tajiri kuliko Tanganyika, siyo njia safi ya kulinganisha; Njia inayofaa kutumiwa, njia ambayo wana TANU na wananchi wote hatuna budi tuitumie, ni kulinganisha mshahara huo na pato la ndugu zetu;

Nitajaribu kuwaonyesheni na sina shaka natumaini mtastuka; pato la nchi yetu kama tukigawana kila mtu sawa sawa, basi kila raia wa Tanganyika atapata Shs 400/= kwa mwaka; Tuseme nyumba ina watu wane – yaani mke, mume na watoto wawili; basi pato lao lingekuwa shs 400/= mara 4 kwa mwaka, yaani shs 1,600/=. Pato hili ni kiasi cha Shs 133/= kwa mwezi;
Lakini tunalifikiaje pato hili? Tunalifikia pato hili kwa kuchanganya pato la Tanganyika nzima, na kuligawa sawa sawa; Ukweli wenyewe ni kwamba pato hili la shs 133/= kwa mwezi ni pato la karatasi tu; Watu wetu hawalipati. Tulipoingia serikalini tulikuta watu wengi wanapata mshahara wa Shs 1/75 kutwa ambao ni kiasi cha Shs 45/50 kwa siku 26 za kazi; tuliongeza mshahara huu ukawa shs 2/75 kwa siku, ambao ni kiasi cha shs 71/50 kwa siku 26 za kazi; watumishi wa juu ya hao walikuwa wakipata kiasi cha shs 107/= kwa mwezi; Ni wakati wa kukubali mishahara iliyotokana na uchunguzi wa bwana Adu ndipo tulipoongeza mshahara ukawa shs 132/= kwa mwezi;

Basi njia safi ya kujua kama mshahara wa shs 3,000/= kwa mwezi ni mkubwa au mdogo si ile ya kulinganisha mishahara ambayo mawaziri wa nchi nyingine hupokea; Njia bora ni kulinganisha shs 3,000/= kwa mwezi na shs 71/50 au shs 132 kwa mwezi; Hapana mtu anayeridhika na fedha; Kwahiyo mawaziri wetu wanazo shida kubwa, na tunazijua; lakini shida zao ni za aina mbali mbali kabisa na shida ya mtu ambaye anapata sh 71/50 kwa mwezi;

Nimetaja mawaziri kama mfano tu; lakini maneno haya yanawahusu waafrika wote wenye hali nzuri; Leo Permanent Secretary mwafika mshahara wake ni shs 4,000 kwa mwezi; Hatujali permanent secretary kupata mshahara mkubwa kuliko waziri wake; sababu ni kwamba hatutaki mawaziri wetu walingsanishe mishahara yao na ma – permanent secretary wao, na kusema ni midogo; Tunataka mawaziri wetu walinganishe mishahara yao na wale vibarua wanaopata Shs 71/50, na watambue kuwa ni mikubwa; hatutaki waziri wetu awe na tama ya kupunguza tofauti ya pengo kati ya mshahara wake wa Shs 3,000/= kwa mwezi na ule wa kibarua wa shs 71/50 kwa mwezi; kadhalika mshahara wa Permanent secretary mzungu ni shs 4,800/= au zaidi; hatutaki permanent secretary mwafrika aseme kuwa huu ni ubaguzi, na kudai yeye pia apate mshahara huo; tunataka afikirie njia za kusaidia kupunguza tofauti iliyopo sasa kati ya mshahara wake wa shs 4,000/= kila mwezi na ule wa kibarua was shs 71/50 kwa mwezi; tunataka kila mwafrika ambae sasa hivi hali yake ni nzuri ailinganishe hali yake na wale wengi ambao hali yao ni mbaya;

Leo tuko Waafrika maelfu hapa Tanganyika ambao hali yetu ni nzuri sana ukilinganisha na ile ya ndugu zetu vibarua na wakulima; na hesabu yetu itazidi kuongezeka kila mwaka; Baadhi yetu ni wakubwa wa siasa, wengine ni watumishi wa serikali kuu, au serikali za mitaa, wengien ni watumishi wa makampuni, au wanafanya shughuli zao wenyewe. Sisi sote hao tuko katika kundi la juu la waafrika ambao hawajambo; na mara nyingi tunayo manung'uniko mengi sana; Lakini ni mara ngapi ambapo manung'uniko hayo ni ya kutaka hali yetu, ambayo ni nzuri, ifanywe nzuri zaidi, na tofauti iliyopo sasahivi kati yetu na ndugu yetu wa chini izidi kuwa kubwa?
Ikiwa jitihada yetu itakuwa ni jitihada ya kupunguza tofauti iliyopo kati ya wale walio juu na wale walio chini, basi hapo hatuna haja kuwa na wasiwasi sana tunapowahimiza ndugu zetu kufanya kazi kwa bidii; kwani tunakuwa hatuwahimizi wawafanyie kazi watu wa juu, bali tutakuwa tunawaomba wajifanyie kazi wao wenyewe; lakini watu wa juu wasipojali tofauti iliyopo baina ya hali zao na hali za watu wa chini, basi hapo kuwahimiza watu wa Tanganyika kufanya kazi ni kuwahimiza wawafanyie kazi watu wa juu; Na serikali ya TANU ikikubali mambo hayo, basi hapo serikai ya TANU itakuwa siyo tofauti na Serikali ya Kikoloni;

Ikiwa TANU inataka kuunda nchi ya ‘UJAMAA' kwa kweli basi, tunaitazama TANU kuendelea na jitihaha ya kupunguza tofauti iliyopo sasa kati ya watu wenye hali ya juu, na wale wenye hali ya chini; Kama nilivyosema hapo juu, kila mtu hupenda fedha nyingi, na hakuna mtu yeyote, tangu waziri mpaka kibarua, ambaye hapendi pato lako lizidi kuongezeka kila siku; Kwahiyo, ikiwa serikali ya TANU itachukua hatua kuzuia tofauti iliyopo sasa kati ya watu wa juu na watu wa chini, sina shaka watu wote walio juu hawatapenda; hata mimi ninayeyaandika maneno haya, sitapenda; kwani hata mimi napenda kuwa tajiri! Lakini kitachotuwezesha kujenga nchi safi siyo tamaa yangu mimi kuwa tajiri; bali ni vitendo ambavyo, ingawa tunajua kuwa vitawaudhi wachache, tunayo hakika kuwa ni vya manufaa kwa ndugu zetu walio wengi."]

-----------------------------MWISHO----------------------------------


Tunaona jinsi gani maneno ya Mwalimu bado ni very relevant kwa hali ya sasa:
· Mfano leo hii hata CHADEMA wamekuwa wanaibana serikali kwa matumizi holela ya fedha za walipa kodi;
· Tunaona jinsi gani leo hii, soko huria lililoletwa kwa kasi bila kuwaandaa watanzania walio wengi, soko ambalo kwa raha zote CCM na CDM wamelikumbatia, linawadidimiza mamilioni ya watanzania katika umaskini, hususan 75% ya watanzania ambao ni wanavijiji;
· Nini ni tofauti ya msingi kati ya mkoloni anaemsemea Mwalimu na Serikali inayokubali kupakatwa na IMF/WorldBank, vyombo ambavyo wote CCM na CHADEMA wanapigana vikumbo kwenda ikulu kuvitumikia?
Ndiyo maana nahimiza umuhimu wa CCM kumeguka ili tupate chama kipya chenye itikadi inayochukua mazuri ya Azimio La Arusha; CCM ya sasa haiwezi kamwe kubadilika na kuyachukua mazuri ya Azimio La Arusha na kuyafanyia kazi kwa vitendo;

Dhana ya Azimio la Arusha imekuwa inapotoshwa sana kupelekea hali ya kuwatisha baadhi ya watu bila sababu za msingi; Azimio La Arusha lilikuwa na mapungufu yake, Lakini Azimio La Arusha Per Se halikuwa na ubaya; Ndio maana Mwalimu aliumia sana aliposikia limeuawa huko Zanzibar na kuhoji kwenye interview on TV kwa tabasamu kidogo la mshangao, ‘Nasikia Wameliua Azimio La Arusha huko Zanzibar, kwani lilikuwa na Ubaya kiasi gani?'

Binafsi I am of the opinion kwamba tofauti na miaka ya nyuma, leo Tanzania tuna rasilimali tosha za kutuwezesha kusonga mbele kwa kuchukua mazuri ya Azimio La Arusha – leo tuna geologists, engineers, economists etc; tuna madini na rasilimali tele; we are ready to take off ikiwa tutapata viongozi wenye ‘political will', integrity, patriotism and commitment na nchi yao; na ambao watakuwa tayari kuyafanyia kazi mambo mazuri ya Azimio La Arusha; kwani hata Mwalimu alishakiri wazi kwamba:
"Kuna mazuri niliyafanya lakini pia yapo ya kipumbavu niliyafanya, lakini cha kushangaza ni kwamba awamu zilizonifuatia zinaacha mazuri na kuchukua ya kipumbavu?".

Katika mazingira haya mapya pia ni muhimu kuyapa masuala haya kipaumbele: demokrasia; uhuru na haki za binadamu kijamii, kiuchumi na kisiasa; na haya yasichomekwe tu kiholela ndani ya katiba bali yapewe meno ndani ya katiba mpya itakayotokana na wananchi wenyewe ambao kimsingi ndio waajiri wa viongozi na watumishi wa umma;
 
Hata mimi nilitaka kujua mtazamo wake. Mkuu njoo utoe maoni yako.
But Mr. Alwattan, the Big Bang Theory usually huwa inaleta migawanyiko ambayo haitabase on ideology, rather than mere tribal, religious, regional and class warfare. Very, very, bad.
Instead, the route that the ANC Youth League is taking is more prefferable and highly practical in Tanzania. We have the fan base, so let's do it!!!

Soby, would you care kufafanua kidogo zaidi juu ya big bang theory based on tribal, religions, regional and class warfare rather than ideology? You might have a point; my take ni kwamba kitachopelekea kwenda huko ni kukosekana wa ideology;vita dhidi ya ufisadi ni mfano mmoja wapo; na nina uhakika kama hatutakuwa makini na kuacha CCM ikiendeleza migogoro inayosukumwa na nguvu za pesa, taratibu, vita hivi vitahamia kwa ndugu zetu wapemba, wahindi....;
 
Mkuu Mchambuzi,
Nimejaribu kufuatilia michango yake kwenye hii thread, na naona pamoja na kwamba kichwa cha mada ni Tujisahihishe au Tugawane Chama. Wewe mwenyewe umeonesha kukata tamaa option ya kwanza(ya Tujisahihishe) na mara kadhaa umeonesha why umepata huo mtazamo.

Vilevile kupitia thread hii nimeweza kusoma kwamba kwa sasa hivi, kisera hakuna tofauti ya msingi kati ya CCM na CHADEMA, vyote ni vyama vinavyopigania kutekeleza kwa ufanisi zaidi sera za Bretton Woods institutions. Kwa maana nyingine kisera ni vyama vya kibepari.(wanaCHADEMA naomba kukosolewa kama nimekosea).

In short, ni kama unakumbukia the good old days za striving for self reliance and development. Sasa napenda kujua what are your thoughts on the way forward? Je kuna haja ya kuanzisha chama chenye mrengo wa kushoto zaidi(socialist leaning), na kama ni hivyo, tayari ndani ya CCM asilimia 75% ya wanachama wake watakua tayari kuhamia huko. Sababu ni viongozi na wapambe wao wa karibu ndiyo wanaonufaika na hili soko holela(huria).

Au unasubiria the small spark that leads to the big bang ya CCM kupasuka?

But alll in all its a good analysis ya hali ya kisiasa ndani ya CCM,...

Upo sahihi; heading ya thread inaonyesha kwamba kuna two options - aidha tujisahihishe au tupasuke huku content that I present inaegemea zaidi towards kupasuka na kuonyesha kukata tama kwamba there is no way back; kwa maoni yangu, CCM kujisahihisha na kurudi kilipotoka na kuyachukua mazuri ya azimio la arusha na kuyaacha ya kipumbavu ambayo hata Nyerere aliyataja, kwa mtazamo wangu ni vigumu sana kwa sasa; chances ni very slim kwani kwa miaka 20 sasa (since azimio la ZNZ 1992) kimekuwa chama cha kibepari - chama cha wafanyabiashaha wakubwa, wakulima wakubwa na wafanyakazi wenye kazi za kudumu, vipato vya juu na wenye elimu; the majority ambao ni wafanyabishara ndogo ndogo, wakulima wadogo wanaopinda migongo yao juani tokea uhuru, na wafanyakazi wenye hali za chini ambao TUCTA inawapigania kila siku, wengi wao wakiwa wanyonge kielimu na kwa kipato kwa sasa hawana chama cha siasa cha kuwatetea; Chadema imekuwa just a fall-back position, but kimsingi hakiendani na hali na matakwa yao; iwapo CCM itameguka na kuleta upande mmoja CCM ya bwana wakubwa, na kingine CCM ya mabwana wadogo, wote watapata support base ya kutosha ingawa hiki cha watu wadogo ndicho kitakachopata mafanikio ya haraka zaidi;

Otherwise kama nilivyokwisha sema, kwa sasa mbadala wa wengi ni Chadema ambao kimsingi bado sio chama kinachoweza kukidhi matakwa ya watu hawa wadogo naowasema kwani chama cha kukidhi matakwa yao lazima kile kitacho demand IMF na WorldBank kwamba sasa tunataka ku-own our development agenda; chama ambacho kitatekeleza mambo mengi mazuri ya azimio la Arusha kwa vitendo; Swali linakuja, now if we agree kwamba the support base is there, which method is more appropriate? Je ni: Top - Bottom approach whereby we should wait for viongozi ndani ya CCM ya sasa kumeguka, viongozi wenye nia ya dhati na nchi hii, viongozi waadilifu? Kwa mtazamo wangu, Nape makes a good candidate hapa, ninachopingana nae ni kwamba anapigana na vita ambavyo mzizi wake ni itikadi kuwa blurred kwani he is the marketing manager wa chama chenye brand ya Ujamaa na ubepari at the same time; brand equity hapa haiwezi kuwa forthcmong; so the top - bottom approach ni njia moja wapo; alternatively kuna bottom - up approach whereby baada ya wafanyakazi wanyonge kimapato na kielimu na kimaisha, wafanyabiashara wanyonge (machinga), na wakulima wadogo wanaopindisha migongo yao kwenye jua, na vijana wengi wa UVCCM ambao wanaimba kuilinda siasa ya Ujamaa na kujitegemea huku viongozi mabepari na mabwanyenye wamekaa meza kuu wanatuma SMS kenye Blackberry zao kufuatilia miradi yao kwenye simu, baada ya hawa wooooote kupewa elimu husika juu ya nini kinaendelea na nini CCM asili can do for them, ni wao sasa kwa umoja wao kupitia some sort of a movement waanza to demand CCM asili, izaliwe, wapate viongozi na siasa za ushindani kuendelea…;

Kwa mtazamo wako, njia ipi ni sahihi na rahisi?
 
Mcahambuzi said:
.......Katika mazingira haya mapya pia ni muhimu kuyapa masuala haya kipaumbele: demokrasia; uhuru na haki za binadamu kijamii, kiuchumi na kisiasa; na haya yasichomekwe tu kiholela ndani ya katiba bali yapewe meno ndani ya katiba mpya itakayotokana na wananchi wenyewe ambao kimsingi ndio waajiri wa viongozi na watumishi wa umma

Mchambuzi kuna kitu imoja kinakosekana hata vyote vikikamilika. Ni ubunifu. Hakuna viongzi wanfikiria new, efefctive and efficient way of doing things.

Unajua tuna tatizo viongzi wetu kudhani wanahitaji kufanya mambo makubwa saaaaana ndiyo yanahitaji kuleta mabaiiko. Kumbe somtime ni vitu vidogo tu vinaweza kuwa trigger ya kumletea maendeleo

hata wale viongzi tunoadhani ni mfano hawaonyeshi au hawana ubunifu wa kuepeleka maendeleo vijijini.

Sita ni kati ya viongozi wa CCM ambao ananafuu. Lakini sita huyu kwenye majukwaa anayeongolea ajira za vijana .Lakini hata yeye ofisi yake ya bunge viti na samani zimetoka dar(Alikosa ubunifu wa kutoa ajira kwa vijana) . Na dar wamegiza kutoka china. Mkoa wa Tabora una mbao. Mkoa wa tabora haukosi fundi au mafundi ambao wagewezeshwa kwa utangazwa local tender kutengeza japo meza.Matokeo yake vijana wa mikoani ujuzi wao unabki kufunga bolt na kubeba samani kupelea kwenye maofisi.

Nimemtolea mfano wa Mh six si wamba ninashida naye sana lakini huu ni mfano kwa wabunge wote, ofisi za miko yote na wilaya zote. Ok hatukatai viti vya waheshimwa vya kuzunguka labda watu wetu hawawezi. Lakini hata meza ya wilayani inatoka china, Hata viti vya wageni kwenye ofisi za mikoa na wizara zinatka china??Majibu ya viongozi waliokariri na wasiouwa wabunifu na wasiokuwa wazalendo ni kuambiwa mshindi anapatikana kwa tender na kwenye tener hakukuwa na tatizo wala upendeleo.

Sio siri sometim e nachukia nikisa wanaosema soko huria. Upendeleo unatakiwa kuwepo kwenye sehemu fulani fulani. Samani za ikulu zitoke ulaya/china , samani za wizara zitoke ulaya/china Za mikoa zitoke ulaya Za wilaya zitoke ulaya. Duh Tender gani isiyokuwa na vigezo. Hivi hauna nafasi ya kuwapendelea product made by and in Tanzania wilayani na mkoani? Hata PM wa uk inawezekana binafis anapend agetumia Marcedes bez lakini Uzalend unafanya aatumie brand ya UK. Sasa sisi iweje viongozi wetu washindwe kubeba kazi za vijana made in and bt Tanzanian kwa kisingizo cha tender. Yaani hata Wilayani.??????

Inahitaji kiongozi mzallendo kufanya baadhi ya vituvidgo vidogo kukuza ajira za moja wa moja .

Huko Italy nasikia katu kinachotengenzwa na fundi kwa mkono ni cha bei ghali zaidi. Lakin hapa kwetu ni mbunge gani au mwanasiasa gani au mimina wewe tuko tayari aonekane japo na pair ya kiatu cha fundi wa sinza. Jibu rahisi utaambiwa quality Lakini ukweli hatuna uzalendo nahiyo hata sisi wnanchi wa kawaida. Lainivigzi wanasisa wako kwenye nafasinzuri ya uwawezesha watu. Nikisia zitto kabwe, nape, membe baadhi ya suti zao zinashonwa na fundi zuberi basi tutakuwa tunaokoa $$$ kadhaaa na kukuza ajira za ndani.

Mawaziri na maofisa wakuu serikalini wanatumia VX. Hawa nimawaziri aktaakwenda mwanza anapanda ndege. Wenda arusha anapanda ndege gari inamfuata. Sometimenajuliza hiiymawziri na viogozi wauu utumia VX from masaki posta ni sheria ilipitishwa na bunge. Ni agizo la Ikulu.
Waziri yeyote mbunifu na mzalendoo anaweza kuagiza anataka atumie vitara. Kama kwa wiki VX inawekewa lita kama 200 . ina maana kwa vitara anaweza kutumia lita 100 au 75. Sasa chukulia mfan kila wizara VX mbili au tatu za viongozi wakuu zinakuwa vitara. kiasi gani kitaokolewa kwenye mandeleo badala ya adminsitratin cost.

Lakini hawawezi na kuna baadhi wanaweza kuwa demorolised kuitwa mawaziri alafu watumie vitara. Kwa wengine hilo ni tusi. But jibu ni sbabu hawana uzalendo.

Nimeona picha za ukutani wenye Ukumbi kiwekte alitumia kukutana a CDM na CUF. Ni picha za kuchora kaa sikosei . Haraka haraka niajiuliza hizi picha zimechorwa na msanii gani. Kam ni mtanzania pogezi yake . Kama imported sababu ya quality mhhh...

Kifup binafsi naamin viongozi wanaweza kufanya vitu vidogo vidogo tu na vikaleta mabadiliko kwenye jamii. We are too much import oriented hata kwa vitu vya ajabu. Kisa bajeti ipo na soko huria na quality
 

Mchambuzi kuna kitu imoja kinakosekana hata vyote vikikamilika. Ni ubunifu. Hakuna viongzi wanfikiria new, efefctive and efficient way of doing things......


Sita ni kati ya viongozi wa CCM ambao ananafuu. Lakini sita huyu kwenye majukwaa anayeongolea ajira za vijana .Lakini hata yeye ofisi yake ya bunge viti na samani zimetoka dar(Alikosa ubunifu wa kutoa ajira kwa vijana) . Na dar wamegiza kutoka china. Mkoa wa Tabora una mbao. Mkoa wa tabora haukosi fundi au mafundi ambao wagewezeshwa kwa utangazwa local tender kutengeza japo meza.Matokeo yake vijana wa mikoani ujuzi wao unabki kufunga bolt na kubeba samani kupelea kwenye maofisi.

Sio siri sometim e nachukia nikisa wanaosema soko huria. Upendeleo unatakiwa kuwepo kwenye sehemu fulani fulani. Samani za ikulu zitoke ulaya/china , samani za wizara zitoke ulaya/china Za mikoa zitoke ulaya Za wilaya zitoke ulaya. Duh Tender gani isiyokuwa na vigezo. Hivi hauna nafasi ya kuwapendelea product made by and in Tanzania wilayani na mkoani? Hata PM wa uk inawezekana binafis anapend agetumia Marcedes bez lakini Uzalend unafanya aatumie brand ya UK. Sasa sisi iweje viongozi wetu washindwe kubeba kazi za vijana made in and bt Tanzanian kwa kisingizo cha tender. Yaani hata Wilayani.??????

Huko Italy nasikia katu kinachotengenzwa na fundi kwa mkono ni cha bei ghali zaidi. Lakin hapa kwetu ni mbunge gani au mwanasiasa gani au mimina wewe tuko tayari aonekane japo na pair ya kiatu cha fundi wa sinza. Jibu rahisi utaambiwa quality Lakini ukweli hatuna uzalendo nahiyo hata sisi wnanchi wa kawaida. Lainivigzi wanasisa wako kwenye nafasinzuri ya uwawezesha watu. Nikisia zitto kabwe, nape, membe baadhi ya suti zao zinashonwa na fundi zuberi basi tutakuwa tunaokoa $$$ kadhaaa na kukuza ajira za ndani....

Mawaziri na maofisa wakuu serikalini wanatumia VX. Hawa nimawaziri aktaakwenda mwanza anapanda ndege. Wenda arusha anapanda ndege gari inamfuata. Waziri yeyote mbunifu na mzalendoo anaweza kuagiza anataka atumie vitara. Kama kwa wiki VX inawekewa lita kama 200 . ina maana kwa vitara anaweza kutumia lita 100 au 75. Sasa chukulia mfan kila wizara VX mbili au tatu za viongozi wakuu zinakuwa vitara. kiasi gani kitaokolewa kwenye mandeleo badala ya adminsitratin cost....

Lakini hawawezi na kuna baadhi wanaweza kuwa demorolised kuitwa mawaziri alafu watumie vitara. Kwa wengine hilo ni tusi. But jibu ni sbabu hawana uzalendo........

Nimeona picha za ukutani wenye Ukumbi kiwekte alitumia kukutana a CDM na CUF. Ni picha za kuchora kaa sikosei . Haraka haraka niajiuliza hizi picha zimechorwa na msanii gani. Kam ni mtanzania pogezi yake . Kama imported sababu ya quality mhhh...

Kifup binafsi naamin viongozi wanaweza kufanya vitu vidogo vidogo tu na vikaleta mabadiliko kwenye jamii. We are too much import oriented hata kwa vitu vya ajabu. Kisa bajeti ipo na soko huria na quality..........

Zing, well put; uzalendo ndio jambo la msingi – we need leaders who have love for their country and willingness to sacrifice for it; hili kwa viongozi wetu wengi kwa kweli halipo; Kama ulipata nafasi ya kusoma my earlier post ukurasa huu huu, Mwalimu alikuwa mtu wa ajabu sana, mtu wa pekee; kwa maneno yake alizungumza kwamba hata yeye sio kwamba hapendi kuwa tajiri, ikiwa na maana kwamba hakuuchukia utajiri per se bali hakutaka utajiri unaotokana na wizi na ufisadi, tena katika mazingira ambayo walipa kodi waliokupa dhamana ya kuwaongoza wanaishi maisha ya ufukara wa kupindukia; Ni yake ilikuwa kuona wananchi wanainuka wote kwa faida ya wote; ni viongozi wachache sana wenye huruma ya namna hii, mimi nadhani hakuna kiongozi wa namna hii dunia ya leo, kwani hata nyumba yake ya msasani nasikia alikopesha hela benki lakini muda si mrefu deni likamshinda, ikabidi kuiuza ili kumaliza mkopo wake benki na kukwepa fedheha; hata wakati amestaafu, nyumba yake nyavu za mbu kwa muda mrefu sana zilikuwa zimetoboka na pia vitu vingi sana vilikuwa vimeisha, na kwa sababu hakuwa na uwezo wa kufanya any major repairs, aliishi hivyo hivyo kwa mud asana, mpaka baadae serikali ilipoamua kumsaidia, ingawa kwa muda fulani ni kama ilimtupa; wapi utapata kiongozi kama huyu? Baada ya kushindwa kulipa deni la nyumba ile na kuamua kuiuza akiwa bado Rais, serikali ikamwonea huruma miaka ya mwisho mwisho ya uongozi wake na kumpa kama zawadi; alipoulizwa kwanini unakaa msasani wakati una hekalu ikulu, alikuwa anajibu kwamba pale sio nyumbani kwangu, ni kwamba tu sina jinsi;

Mawaziri wa Nyerere na wa sasa hawafanani kiuadilifu, kiuzalendo, na hata kiutendaji; mawaziri wengi wa sasa ni wababaishaji; Nyerere alijitahidi sana kutengeneza mazingira ya kuwa na serikali yenye mawaziri wenye moyo wa kizalengo, wenye kuwajibika na government machinery ilikwenda kweli kweli; lakini tazama leo, ni uchwara mtupu;

Kuhusu suala la viongozi kukosa ubunifu - nakubaliana na wewe katika hili, mimi nadhani njia ya kurekebisha hili ni kuanza kupata mawaziri wasiotokana na wabunge; kuna watanzania wengi sana kwenye jamii wenye uwezo mkubwa sana kuongoza sekta/wizara mbalimbali kwa ufanisi lakini hawapati nafasi hizo kutokana na kisiki cha ubunge; haina maana kwamba hakuna wabunge wenye uwezo, wapo, lakini mchanganyiko wa mtu kuwa waziri na mbunge unaathiri sana ufanisi na uwajibikaji;
 
Mchambuzi,

..lakini nadhani hata nyie mnaojiita waumini wa Azimio la Arusha sidhani kama mna guts za kulifuata kama alivyobainisha Mwalimu Nyerere.

..sasa hebu kuwa honest na utueleze unafikiri ni sehemu ipi ya azimio la arusha bado iko relevant in the times and era that we live today.
I think every word in that Declaration is still relevant.
 
Soby, would you care kufafanua kidogo zaidi juu ya big bang theory based on tribal, religions, regional and class warfare rather than ideology? You might have a point; my take ni kwamba kitachopelekea kwenda huko ni kukosekana wa ideology;vita dhidi ya ufisadi ni mfano mmoja wapo; na nina uhakika kama hatutakuwa makini na kuacha CCM ikiendeleza migogoro inayosukumwa na nguvu za pesa, taratibu, vita hivi vitahamia kwa ndugu zetu wapemba, wahindi....;
YEAH,
It's not quite healthy kusubiri a lil spark itakayoanzisha Big bang kama Alwattan alivotoa hiyo option. Ukianzisha kundi ndani ya chama, wapinzani wako wataanza kutumia udini, ukabila etc... ku counter attack regardless of the ideology behind that spark.
If you really have an ideology (I'm talking about a very radical ideology, not centrist like CDM) IT'S BETTER TO JUST GO AHEAD AND START COLLECTING SIGNATURES (especially in Zanzibar), and start a new party.
Republicans were once democrats......
 
Kwa hali tuliyofikia sasahivi, CCM imebakiza option mbili kubwa: Kujisahihisha na tena upesi; au kukivunja Chama katika mapande mawili makubwa ili kutoa vyama viwili tofauti. Nitafafanua baadae kidogo.

Ni muhimu pia niseme kwamba katika haya, ninalindwa na kipengele kifuatacho cha Mwongozo wa Chama Changu Cha Mapinduzi (CCM) 1981: Kipengele Cha 57(5), Ukurasa wa 22 “Kujikosoa na kukosoana ni silaha ya Mapinduzi”.

CCM, Tujisahihishe au tuvunje chama mwandishi. Changamoto iliyopo iwapo CCM itavunjika, ni who will choose the right side of history and who will choose the wrong side of history; vinginevyo mpaka tutakapofikia huko, tutazidi kuwindwa na maneno kama ya Spika Makinda ya “Anza Wewe.”

Kila ninapokutana na maneno kama haya hubaki nikijiuliza hivi Watanzania tuna laana gani. Hii hoja ukiitafakari kwa ndani unabaki tu unajiuliza mwandishi alitaka kufikisha ujumbe gani na kwa wasomaji wa aina gani. Je mwandishi huo ujumbe ameuelekeza kwa Watanzania kwa ujumla wao bila kujali itikadi zao au wana CCM peke yao. Kwa vyovyote vile na bila kujali ujumbe uliwalenga watu wa aina gani kuna mapungufu makubwa kwenye ujumbe huu ambayo ni vigumu kuyanyamazia.

Picha ninayopata kwa haraka haraka ni kuwa yawezekana mwandishi, kama walivyo wananchi wengi, anaamini kutoka moyoni mwake kuwa Tanzania bila CCM haiwezekani. Kabla sijaendelea kuchangia kwenye hii mada namwomba mwandishi atoe ufafanuzi kidogo kuhusu mchango wa watu kama sisi ambao tunaamini kwa dhati kabisa kuwa tatizo kubwa linalotukabili Watanzania sio sera wala itikadi bali utawala madhubuti unaoheshimu sheria, ambao CCM imeshindwa kuusimamia kwa miaka 27.
 
Back
Top Bottom