CCM: Tujisahihishe au Tugawane Chama

Mchambuzi

JF-Expert Member
Aug 24, 2007
4,850
9,405
Kwa hali tuliyofikia sasahivi, CCM imebakiza option mbili kubwa: Kujisahihisha na tena upesi; au kukivunja Chama katika mapande mawili makubwa ili kutoa vyama viwili tofauti. Nitafafanua baadae kidogo.

Ni muhimu pia niseme kwamba katika haya, ninalindwa na kipengele kifuatacho cha Mwongozo wa Chama Changu Cha Mapinduzi (CCM) 1981: Kipengele Cha 57(5), Ukurasa wa 22 “Kujikosoa na kukosoana ni silaha ya Mapinduzi”.

Miaka karibia 50 iliyopita, Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alitoa kitabu chake cha “TUJISAHIHISHE” (May 1962). Miaka 50 baadae, CCM haina mwarubaini mwingine zaidi ya kumrudia Mwalimu Nyerere ili kujirudisha katika mstari. Badala ya kupoteza muda an kauli butu za tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele, ni muhimu viongozi wa CCM watumie kilele cha ‘sherehe’ za miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika kuanza kuthubutu ili chama chetu cha mapinduzi (CCM) kweli kiweze kusonga mbele.

Katika kitabu chake cha ‘TUJISAHIHISHE’. Mwalimu anasema:
[“Ukiondoa matatizo wayapatayo binadamu kwa sababu kama mafuriko, nzige, kiangazi, n.k, matatizo yao mengi hutokana na unafsi. Unafsi ni wa aina nyingi. Swali ambalo twalisikia mara kwa mara, “Hali yetu ya baadae itakuwaje?”, ni swali ambalo sina shaka kuna wanaouliza kwa nia safi kabisa. Lakini mara nyingi linatokana na unafsi. Mtu anayeuliza anafikiri TANU iliundwa kwa faida yake binafsi. Ni kama kwamba TANU ilipoundwa ilimwahidi kwamba ikiwa atakubali kuwa mwanachama, au kiongozi, basi TANU itamfanyia yeye jambo fulani kama tunzo! Anasahau kabisa kuwa TANU inajishughulisha na haja za Jumuiya kwa ujumla. Lakini kwa mtu wa aina hiyo, hata kama TANU inatimiza madhumuni yake kwa jumuiya, ataona kuwa ni umoja ambao hauna maana kwa sababu haumtimizii haja zote za nafsi yake. Huu ni unafsi. Kama wanachama wa TANU, na hasa viongozi, hawatakihukumu chama chetu kwa mahitaji na nafsi zao wenyewe, chana hakitadumu. Wanachama wa aina hiyo ni ugonjwa katika chama.

Dalili nyingine ya unafsi, na ambayo ni ugonjwa mbaya sana ni fitina. Kanuni moja ya TANU inasema hivi: “Nitasema Ukweli Daima. Fitina Kwangu ni Mwiko.” Lakini bado tunao wanachama ambao ni wafitini wakubwa bila kujitambua. Ni wa aina mbali mbali. Wengine humwona mwenzao anafanya kosa. Badala ya kumwambia pale pale kijamaa kwamba atendalo ni kosa, watanyamaza kimya. Lakini hawanyamazi kabisa. Watakwenda kumteta katika vikundi vya siri. Mateto haya si ya kumsaidia mwenzao, ni ya kumdhuru. Hii ni aina moja ya fitina. Wengine hugawa watu katika mafungu. “Fulani” japo kafanya kosa kubwa sana hasemwi. Lakini “Fulani” wa pili akifanya kosa japo dogo, kosa lile hukuzwa likawa kama mlima Kilimanjaro. Hawa hutafuta sababu ya kumtetea “Fulani” wa kwanza, au za kumaulumu “Fulani” wa pili, ambazo hazifanani kabisa na ukweli. Kwa watu wa aina hii, ukweli ni jambo ambalo hutegemea mtu, si kitu kinachojitegemea chenyewe bila kujali mtu. “Fulani” wa kwanza akisema katika majadiliano kuwa mbili na mbili ni tano, wao watakubali. Lakini “Fulani” wa pili akisema sivyo, mbili na mbili ni nne, watamwona ni mtu mbaya kabisa ambaye hastahili hata kusikilizwa. Hawa hawajali ukweli, hujali nafsi tu. Kwao, ukweli ni maoni yao na matakwa yao. Hatuna budi, hasa katika majadiliano na mazungumzo yanayohusu jumuiya, tujifunze kusikiliza hoja zenyewe zinazotolewa na wenzetu, na kuzijibu zile hoja kwa kuzikubali au kuzikataa, bila kujali kama anaezitoa ni rafiki au si rafiki. Pia wanaopingwa hawana budi wakubali kuwa kinachopingwa ni zile hoja zao, sio wao wenyewe. Bila mazoea haya, mazungumzo hayana maana; yanakuwa ni kupoteza wakati, maana huwa tumekwisha kuzihukumu hoja za mtu hata kabla hajazitamka; kadhalika, hoja zetu zikijibiwa kwa kupingwa halafu tunawakasirikia waliozipinga tunafanya mazungumzo yasiwe na maana, kwa sababu tunapenda hoja zetu zikubaliwe tu hata kama si hoja safi.

Ukweli una tabia moja nzuri sana. Haujali mkubwa wala mdogo; haujali adui wala rafiki. Kwake, watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kulipiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwa.
Wakati mwingine, mtu tunayempinga huwa ana makosa kweli lakini hoja tunazozitoa ni za kinafsi na hazihusiani kabisa na hoja zake. Nikisema mbili na tatu ni sita, nakosa. Lakini ni bora kunionyesha kwamba pengine nafikiri tunazidisha kumbe tunajumlisha. Ni kweli mbili mara tatu ni sita; lakini mbili na tatu ni tano, siyo sit.a Lakini ukijaribu kuwashawishi wenzetu wakatae mawazo yangu na kukubali yako kwa kusema kuwa meno yangu ni machafu, au natoa kamasi daima, utakuwa unatumia hoja ambazo hazina maana. Huu ni mfano wa upuuzi; lakini mara nyingi hoja tunazotumia kuwashawishi watu wakatae mawazo ya wale tusiowapenda, au kukubali mawazo yetu, huwa hazihusiani kabisa na mambo tunayoyajadili.

Makosa yetu mengine hutokana na woga; woga unaotuzuia kumlaumu mkubwa japo tunajua kuwa kakosa, au unaotuzuia kumtetea mdogo anayelaumiwa na wakubwa japo tunajua hana makosa. Na msingi wa woga ni unafsi. Pengine huwa tunaogopa sisi wenyewe kulaumiwa au kupata hasara fulani. Pengine twaweza kuwa hatuna cheo chochote ambacho tunaogopa kupoteza; pengine huwa hatuna tamaa yoyote ya kupata cheo fulani. Lakini woga unaweza kutokana na tamaa ya kila binadamu kupendwa na binadamu wenzake. Sisi sote tunayo tama hii, au sivyo tusingekuwa binadamu. Woga huu huweza kumfanya mtu kuvumilia maovu, hasa kama maovu yale yanatendwa na walio wengi kwa walio wachache, au yanatendwa na wakubwa kwa wadogo. Kwa kuogopa kuwaudhi wengi tunawaacha watende makosa bila kuwasahihisha, wasije wakatuchukia. Huu ni unafsi mbaya sana Ni kweli kwamba demokrasi haiwezi kudumu ikiwa wachache watakubali matakwa ya wengi. Lakini matakwa ya wengi hujulikana katika majadiliano au mazungumzo wa wazi.

Kadhalika, matakwa ya wachache hujulikana katika majadiliano na mazungumzo. Bila wachache kusema wazi wazi matakwa yao, majadiliano hayana maana. Wakati mwingine, hata baada ya majadiliano, wachache – japo wamekubali kutii uamuzi wa wengi wanaweza kuendelea kuamini kwamba mawazo yao ni sawa, na ya walio wengi yamepotoka. Demokrasi inawapa haki, na ukweli unawapa wajibu wa kuendeleza mawazo yao mpaka wengi waone kuwa ni ya kweli. Bila hivyo Maendeleo katika mawazo hayawezekani, kwani mara nyingi wazo zuri hutokana na mtu mmoja tu. Mwanzo laweza likapingwa, pengine kwa nguvu kabisa, na walio wengi, lakini hatimaye wengi hulikubali. Huu ndio msingi wa Maendeleo katika mawazo ya binadamu.
Makosa ni makosa na dhuluma ni dhuluma, japo watendao makosa hayo au dhuluma ile ni wakubwa au ni wengi. Chama kinachopenda ukweli na haki hakina budi kiwape wanachama wake uhuru na nafasi ya kusahihisha makosa na kuondoa dhuluma. Wanachama hawana budi waone kuwa ni wajibu wao kuutumia uhuru huo, na nafasi hiyo. Wanachama wasiotumia uhuru huo na nafasi hiyo, kwa sababu ya kuogopa kuchukiwa au kupoteza nafasi zao, wanafanya kosa kubwa la unafsi, ambalo ni adui wa haki na ukweli.

Kosa jingine linalotokana na unafsi tunalifanya wakati wa kuchagua viongozi. Wakati mwingine hufanywa na wanachama; wakati mwingine hufanywa na viongozi wenyewe, au wale wanaotaka uongozi. Nimesema mahali pengine kwamba viongozi wetu hawana budi watokane na WATU. Viongozi wa TANU hawana budi watokane na wanachama wa TANU wenyewe, bila hila, vitisho, rushwa, au ujanja wa aina yoyote. Lakini mara nyingi wanachama huchagua viongozi bila kufikiri kwa makini kama viongozi hao wanaiweza, au hawaiwezi, kazi wanayochaguliwa kufanya. Wanachama wetu watafanya makosa makuwa sana ikiwa watachagua viongozi wa ovyo tu. Hii ni jambo la hatari kwa demokrasi na chama chetu, na maadui wa TANU wanaweza kusema kwamba demokrasi haina maana kwa sababu haizai viongozi wanaoweza kazi zao. Hii ni kweli, maana wote twajua kwamba demokrasi inaweza kuchagua viongozi wazuri. Lakini ni wajibu wetu katika kuhifadhi demokrasi kuona inachagua viongozi ambao wanaziweza kazi zao. Kazi za kuchagua viongozi ni kazi ya wanachama wetu; lakini viongozi wetu wanaweza kusaidia kwa kuelezea wanachama wetu kwamba jambo la kuchagua viongozi ni kubwa sana. Haifai kuchagua kiongozi kwa sababu ni mjomba, au binamu au ana sauti au sura nzuri. Wala haifai kuacha kumchagua mtu kuwa kiongozi kwa sababu kama hizo. Jambo kubwa ni kuchagua kiongozi mwenye tabia nzuri na anayeiweza kazi. Hatuna budi tutii kanuni hii katika kuajiri wafanya kazi katika TANU au Serikalini. Hawa pia hawana budi wachaguliwe kwa sababu wanaiweza kazi wanayoajiriwa kufanya, na ni watu wenye tabia nzuri.

Kosa jingine ni kutojielimisha. Kanuni yetu moja inasema: “Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu wote na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote”. Wengi wetu hufikiri kuwa kujielimisha ni kwenda Kivukoni, au kupata nafasi kwenda kusoma katika nchi za nje. Wengine hufikiri kuwa kujielimisha ni kujua kusoma na kuandika. Hilo ni kosa, lakini sio kubwa kama la pili. Wengi wetu, hasa baadhi ya viongozi, hufikiri kuwa tunajua kila kitu na hatuna haja ya kujifunza jambo lolote zaidi. Mtaalamu mmoja wa zamani alisema kuwa “mwanzo wa elimu ni kutambua kuwa haujui kitu.”]

Mwalimu Nyerere, Tujisahihishe, kurasa 1- 4, May 1962.
-----
Maneno haya ya Mwalimu kwa kiasi kikubwa (sio chote) ni mwarubaini wa matatizo yanayokiyumbisha CCM na serikali yake. Ni tiba kwa matatizo kama vile:
  • Matatizo katika mchakato wa katiba mpya;
  • Sakata la Kujivua Gamba;
  • Uteuzi wa kidugu katika nafasi za chama na serikali;
  • Mbio za urais 2015 (CCM);
  • Utumishi mbovu wa umma na utendaji mbovu unaopelekea matatizo kama ya sakata la Luhanjo na Jairo;
  • Uwepo wa baadhi ya wabunge wa CCM bungeni wenye tabia ya kuunga hoja hata kama hazina maslahi ya taifa, pengine kutokana aidha na upeo wao mdogo, udhaifu/uvivu wao wa kufikiri au unafiki na ubinafsi wao;
  • Unafiki na ubinafsi wa baadhi ya wajumbe wa NEC & CC ya CCM na hivyo kukisindikiza chama kaburini.
CCM hatuna muda wa kutosha wa kujisahihisha. Lakini Mwalimu bado yupo kutusaidia katika hili. Vinginevyo tujiandae kuachia upinzani (utakaotokana na CCM kuvunjika vipande viwili au Chadema) uongozi wa nchi ifikapo mwaka 2015 sio kwa sababu upinzani wana itikadi au sera bora zaidi, bali kwa sababu sisi hatuna itikadi na hivyo tunaishia kuongoza kwa fitina,woga, ujuaji, ubinafsi, na unafiki. Ni ukweli ulio wazi kwamba hata sera za upinzani na CCM ni zilezile, wote tunanyukana ili tukae kwenye usukani kumkuna mgongo IMF na World Bank; hakuna Chama chenye sera mbadala za kuwakomboa watanzania kwa dhati; Chadema, CCM, wote mwendo utakuwa ule ule; Adui wa Mtanzania sio ufisadi, huyo ni mdogo sana, Adui wa kweli ni CCM iliyoamua kuyatupa hata mazuri ya Azimio la Arusha; hili ndio imezaa mafisadi kwa wingi, ambao wamekuwa wakipeana pongezi na IMF na WorldBank kwani lao ni moja.

Kama alivyoasa Baba wa taifa miaka ya nyuma, Viongozi wenye nia nzuri na Tanzania wasione CCM kama ni mama yao; Ni dhahiri kuna viongozi ndani ya CCM wenye nia ya dhati kuwakomboa maskini kimapinduzi kama inavyoainishwa ndani ya katiba ya Chama; lakini wengine wengi zaizi uongozi wao unasukumwa na fitina, unafiki, chuki, woga, na ubinafsi; Lakini iwapo viongozi wenye nia nzuri na taifa hili wanahisi wamefikia kikomo katika juhudi zao kukirudisha chama kuwa cha wakulima na wafanyakazi, ni muhimu kwa viongozi hao kuthubutu sasahivi kwa kuigawa CCM katika vipande viwili vinavyopishana kiitikadi. Hii sio dhambi, wanaoona ni dhambi lazima watakuwa na mapungufu katika fikra zao. Watakaothubutu watakumbukwa kwa ushujaa wao hata kama mwanzoni watabezwa na wachumia tumbo waliopo ndani ya CCM.

Kama kila mtu anakubaliana na hoja kwamba chama cha siasa kinaendeshwa na kuongozwa na itikadi, suala la CCM kugawanyika haliepukiki, sana sana ni suala la muda tu na la nani aanze zezi hilo – maneno kama yale ya Spika Makinda kuwajibu wabunge kwamba “anza wewe” wanapotishia kwenda kinyume na msimamo wa serikali ya CCM bungeni ni ishara ya woga anaouzumgumzia Mwalimu. Vinginevyo kwa viongozi kubakia kwenye uongozi wa CCM isiyo na dira kwa miaka 20 (tangia azimio la Zanzibar 1992 la kuvunja azimio la arusha) ni ishara kwamba viongozi hao hawajali mustakabali wa chama na wanaowaongoza; wanajali zaidi matumbo yao kuliko wananchi kwani katika mazingira ya Azimio la Arusha Sambamba na Azimio la Zanzibar (1992) hakuna cha zaidi ya fitina, chuki na ubinafsi kwani chama hakina dira. Marehemu Kolimba alibezwa bila sababu. Na matokeo yake ni kwamba hata viongozi wa sasa mfano Nape huwa anaishia kubabaisha na majibu kila mara anapoulizwa CCM inafuata itikadi ipi. Mbaya zaidi, majibu kwamba ni Ujamaa na kujitegemea ni ya kupotosha umma. Hili ni tatizo kubwa sana kwa Chama kuliko ufisadi kwani ufisadi ni uzao wa Azimio la Zanzbar. Na ni bora ufisadi ukapewa jina lingine vinginevyo kwa ruksa ya Azimio La Zanzibar, wapo wengi watakaoitwa mafisadi kwa makosa kwa sababu tu wametumia fursa rasmi ya azimio la Zanzibar kujitafutia riziki wakati wengine wamekosa nafasi kutumia fursa hiyo; sina maana kwamba nahalalisha azimio la Zanzibar au suala la kujilimbikizia mali ovyo kwa kutumia madaraka vibaya, bali naelezea ujinga wetu wa CCM ambao unapelekea chama kuongozwa kwa fitina, wivu, woga na unafiki. Azimio la Arusha lilikataza viongozi kuwa na mishahara miwili, nyumba ya (za) kupanga na kuwa na hisa katika makampuni binafsi; azimio la Zanzibar liliruhusu hayo yote rasmi bila ya mipaka; Ni kiongozi gani wa CCM hivi sasa ambae hana angalau moja ya hayo juu yaliyoruhusiwa na Azimio la Zanzibar? Mgombea urais yupi wa CCM ambae mwaka 2015 hatokuwa na angalau moja wapo ya hayo hapo juu? Lowassa? Membe? Magufuli? Pinda? Migiro? Mwakyembe? Mwandosya? Sitta? Ngeleja? Nimeishiwa majina, tafadhali nisaidieni.

Muda umetupa mkono, CCM Tujisahihishe au Tuvunje chama ili upande mmoja urudie mambo mazuri ya azimio la Arusha na upande mwingine uendelee na Azimio la Zanzibar kama lilivyo. Kwanini mbadala ni kujisahihisha au kuvunja chama? Ni kwa sababu sera za Chadema hazina tofauti na za CCM juu ya nini kila chama kinataka kuwafanyia watanzania, ilani zao zote za uchaguzi mkuu uliopita mengi yalikuwa ni yale yale, tofauti kubwa ni kwamba ya Chadema ilitawaliwa na mambo matatu “Ufisadi, Ufisadi, na Ufisadi, - jambo ambalo katika mwongozo wetu CCM 1981, tunalizungumzia vizuri sana; mfano mwingine ni kwamba suala la elimu bure tokea msingi hadi Chuo Kikuu ambalo lilikipa CDM mvuto sana ni suala ambalo CCM ililifanya kwa miaka mingi sana chini ya Nyerere na kutofanikiwa hali ambayo ilipelekea hata muasisi wa Chadema Mzee Mtei kuona Sera za Mwalimu zilikuwa mbovu na hivyo kujiuzulu na kupewa kazi na IMF kama pongezi.

Labda kama Chadema watabadilika au kama vyama vingine vya upinzani vitakuja na mpango wa kweli wa kuwakomboa watanzania; vinginevyo ule unaotegemea kupakatana na IMF na WorldBank ambao hata mwalimu Nyereer aliukataa kwa hoja zilizo wazi kabisa kuelewa, hautafanya Chadema kuwa tofauti wakichukua uongozi; Ndio maana kwa waelewa wengi, hadi hivi sasa, hakuna mbadala wa kweli kwa CCM kisera, mbadala uliopo ni ule wa kuweza kupata ubunge na udiwani kwa urahisi zaidi mfano ukihamia Chadema; Vinginevyo ndio maana nje ya hoja ya ufisadi na katiba mpya, pamoja na umakini wao na mafanikio yao katika maeneo kadhaa ya hoja ambayo kwa kweli yanayostahili pongezi, Chadema haina hoja za msingi mbele ya umma kwanini Tanzania maskini kwani hata Mzee Mtei akiamua kuwa mkweli juu ya hili, lazima atakubali kwamba kushiriki kwake kuwaruhusu IMF na WorldBank kiholela ilikuwa ni grave mistake na ndio msingi wa matatizo yetu leo; sio siasa ya ujamaa pekee;
CCM, Tujisahihishe au tuvunje chama ili kuwapa fursa wale walio na mapenzi bado na CCM kuyachukua mazuri ya chama chetu na kuyapa meno ili kuyatumia kikamilifu katika siasa hizi za ushindani. Changamoto iliyopo iwapo CCM itavunjika, ni who will choose the right side of history and who will choose the wrong side of history; vinginevyo mpaka tutakapofikia huko, tutazidi kuwindwa na maneno kama ya Spika Makinda ya “Anza Wewe.”
 
Nimesoma makala yako kwa umakini,kwangu mie naona umesahau maswala mkubwa matatu,mosi watu wamekuwa wanajenga makundi ndani ya chama kwa madhumuni ya kujiimarisha kuwa viongozi badala ya kujenga kundi moja ambalo ni CCM,pili viongozi wamekua sio wavu,ilivu wanataka waingie leo kwenye chama kesho wawe wakubwa..na nafasi zinapewa kutokana na kujuana sio uwajibikaji na uzoefu kama ulivyo bainisha kidogo,tatu fitina zingine sahivi ni za kutungiana uongo tena uongo kabisa na kufanya ukweli na viongozi wa kitaifa kuuchukulia ni ukweli bila utafiti.
 
Mkuu Kimbunga,

Si kweli kwamba watu wazuri na wenye uchungu na chama na kusimamia ukweli kama huyu ndugu hapo juu hawapo jpo siku hizi ni wachache mno, lakini ndio kama hivo upendeleo kwa makundi ukishaanza ndio inakua hivo tena.

Kwa taarifa yako, kuna watu wana mawazo mazuri sana huku CCM sio kwamba watu hatuna habari lakini dhubuti kujitokeza uone unavyogombaniwa kama mpira wa kona; demokrasia ya ndani ya chama iliondoka na Mwalimu Nyerere mwenyewe hivi CCM ni kwa wenye nguvu kupishwa.

Na nguvu zenyewe CCM siku hizi haitokani na kukubalika kwako na watu chamani bali ni kwa yule anayezidi dau ndiye yule anayeitisha muziki kuimbwa. Na hii ndio sababu kuu ya kufanya hata watu ambao otherwise walikua ni waadilifu tu kuanza kuingia tamaa ya kusujudiwa hivyo kuanza kukwapulia umma fedha ili kufikia azma hiyo.

Mkuu hapo juu, uchungu moyoni mwako na kusononeka kote huko tumeusoma lakini ujue kwamba kule KULIALIA MUDA WOTE hakukusaidii kitu, njoo tujiunge pamoja kwa njia halali kikatiba tukausukume huu mlango wa chuma ukaangukie baharani ili tukapate hesa safi.

Mkuu naona ulistahili kupata fursa kwenye mkutano wa NEC-CCM ili uwasilishe hii makala yako kwa wajumbe kabla ya mkutano wao labda wangekuelewa.
 
Mkuu Uwezo Tunao kama hali ni hiyo basi tena CCM imefika mahala ife ili izaliwe upya manake naona iimefika ukomo kama nilivyofundishwa na mwalimu wangu wa masoko kuhusu Product Life Cycle!!
 
Wataalam wenyewe wanapaita mahala kama hapo walipofikia kuwa ni PLATEAU STAGE (yaani eneo tambarare kule juu juu mlimani) ambapo hata kufanyike nini hakuna pa kuweza kupanda zaidi sana sana kinachoweza kikatokea ni kuporomoka chini kama si hicho cha 'Kama Vipi Tugawane Chama.'

Mkuu Uwezo Tunao kama hali ni hiyo basi tena CCM imefika mahala ife ili izaliwe upya manake naona iimefika ukomo kama nilivyofundishwa na mwalimu wangu wa masoko kuhusu Product Life Cycle!!
 
Mkuu Kimbunga,

Si kweli kwamba watu wazuri na wenye uchungu na chama na kusimamia ukweli kama huyu ndugu hapo juu hawapo jpo siku hizi ni wachache mno, lakini ndio kama hivo upendeleo kwa makundi ukishaanza ndio inakua hivo tena.

Kwa taarifa yako, kuna watu wana mawazo mazuri sana huku CCM sio kwamba watu hatuna habari lakini dhubuti kujitokeza uone unavyogombaniwa kama mpira wa kona; demokrasia ya ndani ya chama iliondoka na Mwalimu Nyerere mwenyewe hivi CCM ni kwa wenye nguvu kupishwa.

Na nguvu zenyewe CCM siku hizi haitokani na kukubalika kwako na watu chamani bali ni kwa yule anayezidi dau ndiye yule anayeitisha muziki kuimbwa. Na hii ndio sababu kuu ya kufanya hata watu ambao otherwise walikua ni waadilifu tu kuanza kuingia tamaa ya kusujudiwa hivyo kuanza kukwapulia umma fedha ili kufikia azma hiyo.

Mkuu hapo juu, uchungu moyoni mwako na kusononeka kote huko tumeusoma lakini ujue kwamba kule KULIALIA MUDA WOTE hakukusaidii kitu, njoo tujiunge pamoja kwa njia halali kikatiba tukausukume huu mlango wa chuma ukaangukie baharani ili tukapate hesa safi.

Nakubaliana na wewe; ila tatizo mkuu linakuja pale unapogundua kwamba hakuna chama chenye dira na itikadi ya kweli itakayopelekea mwananchi wa kijijini kupata unafuu wa maisha; Wote CCM, Chadema, mitazamo yao ni sawa - kugombania uongozi ili kutekeleza sera za IMF na WorldBank kwa ufanisi zaidi; katika mazingira ya sasa, any improvement ya maisha ya mtanzania alie kijijini kutokana na sera za IMF/WorldBank ni matokeo ya bahati mbaya - sio ya kukusudiwa; sasa tunafanyaje katika hilo? au tunataka kupata tu uongozi ili tutunishe CV zetu, kumwagiwa sifa na jamii kwamba tunawapigania maskini na kuboresha maisha ya wake zetu na watoto? Chama ambacho kitamwokoa mwananchi wa kijijini kitahitaji kuwa very radical, sio kama CCM au Chadema ya sasa; tazama CUF, they have done it kule zanzibar, wamegungua mlango na tusubiri kushuhudia mabadiliko ya maisha ya mzanzibari ndani ya miaka 15; haya ya serikali ya mseto ni siasa tu, sio kikwazo, wanajua wanafanya nini; angalia katiba ya zanzibar - taifa jipya limezaliwa lenye mwamko wa kulinda rasilimali zake; na mapambano yalianza siku nyingi, Jumbe, Seif, hawakuwa wabinafsi, ingawa walikuwa na madaraka makubwa sana ndani ya CCM, walijitoa mhanga kwa vizazi vyao vya baadae ili kuwapatia wananchi wao maisha bora baadae; walifukuzwa kazi, wekwa kizuizini, lakini tazama sasa;
 
Mkuu Uwezo Tunao kama hali ni hiyo basi tena CCM imefika mahala ife ili izaliwe upya manake naona iimefika ukomo kama nilivyofundishwa na mwalimu wangu wa masoko kuhusu Product Life Cycle!!

Well said.
 
Katika chambua chambua yangu ya katiba na miongozo ya CDM na CCM nimeona yafuatayo ambayo kimsingi hayana tofauti kubwa zaidi ya utekelezaji; sana sana ukizingatia kwamba CCM ya leo imeyatupa mengi inayoyataja humu na badala yake inafanya yale yale yanayoimbwa na Chadema yani ya kukumbatia soko huru na kukenulia ujio wa IMF na WorldBank.

Nape Mnauye anapoteza muda na suala la ufisadi ambao chimbuko lake ni Azimio La Zanzibar; Angekuwa ni mtu makini, angejikita zaidi katika ku deal na tofauti hizi na kujenga program zake za itikadi, siasa, na uenezi humu katika mazingira haya ya siasa za ushindani wa hoja; kama akipona na panga la kamati ya maadili au kama uvumi kwamba atateuliwa kuwa mbunge na waziri ili kumfuta machozi au kuwa balozi, akibaki katika nafasi yake, akae chini na kuchambua tofauti hizi hapa chini na kuzifanyia kazi na kushauri accordingly na kuanza kujenga chama; hii ndio kazi yake muhimu kwa sasa; na itamsaidia kuondokana na tatizo la kwenda kwenye midahalo na kukosa majibu ya kujiamini kila anapoulizwa itikadi ya chama chako ni nini; katibu wa itikadi wa Chama anaulizwa itikadi ya chama chako ni nini anatetereka? Hili ni tatizo kubwa sana.

1. CHADEMA ni chama cha itikadi ya MRENGO WA KATI.
· CCM ni chama kinachofuata ITIKADI YA UJAMAA NA KUJITEGEMEA.

2. CHADEMA ni chama kinachoamini kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi kwa kutumia raslimali za nchi yetu bila kuathiri uhuru wa Taifa, na kuhakikisha kuwa umma kwa ujumla unanufaika na raslimali zao.
Kutengeneza sera makini zitazowezesha kukuza maendeleo ya viwanda vya aina zote hasa vinavyotumia malighafi inayopatikana nchini kwa lengo la uzalishaji wa bidhaa kwa matumizi ya ndani na biashara ya nje.
Kujenga na kuimarisha kilimo, hususan cha umwagiliaji, na ufugaji katika lengo la kutosheleza Taifa kwa chakula na kwa ajiri ya masoko ya biashara ya ndani na ya nje ili kuboresha maisha ya wakulima na wafugaji na kuendeleza sera ya kulinda ardhi, maliasili na mazingira kwa manufaa ya kilimo na ufugaji endelevu.

· CCM ni Chama kinachoamini kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi kwa kuanzisha viwanda vinavyotumia bidhaa za asili za kilimo chetu kama ngozi, pamba, katani, korosho, tumbaku, pareto, miwa na kadhakila, lengo likiwa ni likiwa ni kutekeleza sera ya kujitegemea.
· Chama pia kinatilia mkazo utekelezaji wa Agizo la Viwanda Vidogo Vidogo mijini na vijijini. Chama kitahakikisha kuwa kila Mkoa unaandaa mpango wa muda mrefu wa utekelezaji wa Agizo hili la viwanda vidogo.
· Kilimo ndio msingi wa maendeleo yetu ya sasa na ya miaka mingi ijayo. Asilimia themanini na tano ya Wanzania wanaishi kwa kilimo; biashara yetu na nchi za kigeni inategemea zaidi mazao tunayoyatoa katika kilimo, viwanda tulivyonavyo nchini vinategemea mazao ya kilimo uwezekano wa kutoa ziada itakayowezesha nchi kugharimia mapinduzi ya viwanda (kugharimia viwanda vya madawa) upo katika sekta ya Kilimo.
· Kilimo kimepewa umuhimu wake katika mwelekeo wa muda mrefu. Kwa kuelewa kuwa pamoja na miradi mikubwa ya kitaifa ya umwagiliaji, miradi midogo midogo ya vijijini ndiyo ambayo inaweza kutoa matunda ya haraka,hatua za dhati zichukuliwe za kuandaa wataalam wa fani hiyo kwa wingi nchini na ng'ambo na pia kutafuta uwezekano wa kuanzisha kiwanda cha zana za umwagiliaji maji. Wakati huo huo Chama kijizatiti barabara ili kuimudu kazi ya kuwashirikisha wananchi, maana utekelezji wa miradi ya umwagiliaji vijijini utategemea zaidi jasho la wananchi wenyewe kuliko matumizi ya zana za kisasa.
· Siasa ya uchumi ya Chama cha Mapinduzi inasisitiza lengo la kutosheleza mahitaji ya wananchi ya chakula na kulipa Taifa uwezo wa kujitegemea katika mahitaji ya maendeleo ya sasa na ya baadaye.
· Katika sekta ya mifugo, moja ya kazi muhimu za Chama ni kuhakikisha kuwa Serikali inaandaa sera ya kuendeleza mifugo nchini na kuhakikisha kuwa wafugaji wanaelimishwa na wanatekeleza misingi ya ufugaji wa kisasa na kuchukua hatua za dhati za kueneza mbegu bora za ng'ombe wa maziwa na wa nyama.

3. CHADEMA inaamini katika kujenga na kuimarisha uchumi wa soko huru, utakaoheshimu na kulinda haki na mali za watu, biashara huru na sekta ya watu binafsi bila kupoka mamlaka ya umma katika maeneo nyeti hususani pale penye hitilafu ya soko au penye maeneo nyeti ya kiuchumi. Tunaamini katika soko huru sio soko holela.
· CCM inaamini katika kujenga na kuimarisha uchumi wa kijamaa, kwa umma kushika njia kuu za uchumi ili kupunguza migongano ya maslahi ya kitabaka ambayo imejitokeza nchini, mizizi yake ikiwa ni ubepari unaotishia maslahi ya wakulima na wafanyakazi na kupandikiza mbegu za ubinafsi na ubwanyenye. Tunaamini katika umma kushika njia kuu za uchumi kama mabenki, biashara ya nje na mashamba makubwa ya mabepari na kuunda mashirika ya umma na viwanda vyama umma kama njia ya kusaidia chama kuunda mfumo mpya wa uchumi unaofanana na hali halisi ya watanzania.

4. CHADEMA inaamini kuhakikisha matumizi bora ya raslimali asilia za nchi ili zichangie kikamilifu katika pato la taifa na hasa kuboresha huduma za kiuchumi zinazotumiwa na wananchi wote.
· Sehemu ya 90 (5) ya Mwongozo wa CCM:
"CCM inatambua kwamba kumekuwa na ongezeko kubwa la uhalifu wa aina mbalimbali nchini tangu tupate uhuru. Uhalifu wenye kutia wasiwasi maalum ni uhalifu katika uchumi. Wizi wa mali ya umma umeanza kuwa jambo la kawaida. Kumekuwa na matukio ya baadhi ya maafisa kuhusika na kuidhinisha mikataba na kampuni za nchi za nje bila kujali maslahi ya Taifa. Wakati huo huo vipusa, dhahabu na na mali mbalimbali za taifa zinatoroshwa nje ya nchi kwa magendo na kusabisha hasara kubwa kwa Taifa. Chama kitahakikisha kuwa serikali inachukua hatua kali za kupambana na vitendo hivi vinavyodhoofisha uchumi wa Taifa. Iko haja pia kwa sasa ya kubuni sheria maalum zitakazoelekezwa kwenye vita dhidi ya uhalifu katika uchumi unaozidi kuongezeka."

5. CHADEMA inaamini katika kujenga uwezo wa wazawa katika kumiliki na kuendesha uchumi.
· CCM ni muungano wa wakulima na Wafanyakazi wa mstari wa mbele kaika mapambano ya kujenga Ujamaa Tanzania. Mfumo wetu wa kisiasa na kijamii unajengwa kwa mujibu wa msingi na mahitaji ya nchi inayojenga ujamaa. Lengo ni kujenga mfumo wa demokrasia ya kijamaa ambamo wakulima, wafanyakazi, washirika na watu wote wanaoishi kwa jasho lao sio tu kuwa watashirikiana na kuwa na kauli ya mwisho katika mambo ya siasa na ya jamii ya nchi yao bali wakati huo huo watamiliki na kudhibiti uchumi wa Taifa kwa kupitia Serikali, Mashirika ya umma, Vijiji vya ujamaa na vyama vya ushirika.
6. CHADEMA – Kulipa kipaumbele suala la hifadhi na ulinzi wa mazingira katika mipango yote yamaendeleo ya kiuchumi na kijamii.
· CCM - Hali ya vijiji vingi ingali duni kwa ustawi wa jamii na utamaduni. Chama kitalishughulikia suala la kuleta mapinduzi ya mazingira vijijini katika fani hiyo.
Hali ya afya ya wananchi wengi vijijini inaathiriwa na tabia na mila ambazo zinapingana na maendeleo ya jamii kama vile tabia ya kutotumia vitanda, tabia ya kuishi katika nyumba moja na mifugo, tabia ya kutotumia vyoo, tabia ya kunywa maji yasiyochemshwa, miiko mbalimbali,na kadhalika. Wakati huo huo Chama kitatilia mkazo suala la usafi wa mazingira mijini vijijini pamoja na umuhimu wa kuwepo kwa vyoo vya umma mijini.

7. CHADEMA – Kutoa mkazo katika Utafiti, Sayansi na Teknolojia na kusambaza matokeo yake kwa walengwa ili kuchochea maendeleo endelevu.
· CCM – Mpango wa Chama unatoa mwelekeo wa maendeleo ya sayansi na teknolojia, kwani sayansi na teknolojia ni msingi muhimu kwa maendeleo ya
kisasa. Chama kijihusishe zaidi na mipango ya kuwapata wanasayansi na wanateknolojia wenye uwezo wa viwango mbalimbali vyautaalamu na msimamo sahihi wa siasa. Wakati huo huo, Chama kishughulikie ustawi wa wataalamu na mabingwa tulionao hivi sasa nchini ili kuhakikisha kuwa wanaishi katika mazingira yanayowawezesha kutoa mchango wao kwa ukamilifu katika ujenzi wa Taifa letu.

8. CHADEMA – Kujenga misingi imara ya ajira kwa kuongeza fursa na uwezo wa wananchi kujiajiri wenyewe, kujenga mazingira ya kupanuka kwa sekta binafsi na kuhakikisha kipato cha waajiriwa katika sekta rasmi za uchumi na huduma kinalingana na jasho au juhudi za muajiriwa.
· CCM – kuwahamasisha vijana kuanzisha miradi ya kiuchumi na kujiunga katika vikundi vya ushirika wa kuweka na kukopa (SACCOS) na VICOBA na kuziwezesha kimitaji;
Kuwahamasisha vijana kujiunga na vyuo stadi ili wapate stadi za kuwawezesha kujiajiri wenyewe.
 
Naona vijana ndani ya CCM sasa wanaanza kuona sababu za kutafuta mabadiliko ya kweli kwa faida yetu sote.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Mkuu mchambuzi umenena maneno mazito na mwenye macho asome aelewe. Nchi yetu inahitaji mabadiliko makubwa ya kiitikadi na kisera. Vyama vyetu vya siasa vyote vimejaa wasaka tonge sijaona Chama makini chenye nia ya dhati ya kuleta ukombozi wa pili katika nchi yetu. CCM inahangaika na ufisadi eti inawamulika watu watatu tu!! Sijui kama hao wakiondoka maisha ya watanzania yataboreka. Tutafute kiini cha tatizo. Nadhani Mwenyekiti wa CCM aliposema kujivua gamba hakuwa na maana finyu kama ambavyo wanataka kutuaminisha. Nadhani alikuwa na maana pana ya kufanya mabadiliko makubwa ndani ya CCM kama dhana kamili ya nyoka kujivua gamba.

Jamani CCM isipoangalia itakuwa kama KANU, UPC, MPC, UNIP, nk.
 
Ulikuwa wapi MCHAMBUZI siku zote hizo mpaka chama kimebaki makapi?
Tunataka watu wa aina yako kwa kipindi hiki kigumu.
 
Well said.

Mchambuzi hayo unayonena ni kweli lkn yamenenwa sana na watu wengi tuu,nakubaliana na wewe kuwa hata CDM waliowengi wakubwa kwa vijana waliopo madarakanai hawana utashi wa kweli kuleta maendeleo katika nchi hii (I mean non political statistical development). Nashnagaa hata wazee wa CCM wanashindwa kutukemea viongozi waliopo madarakani, yupo wapi Mkapa,Mwinyi,Salim,Warioba,Malecela, na hata Mh. Kikwete...Utasikia wanaogopa kutoa maelekezo makali kwa viongozi wetu wanaoabudu matumbo yao shv eti kwasababu nao wamefanya madhabi...that is not true na hata kama wanaogopa hilo basi nashindwa kuelewa..kwani baba yako akifanya makosa ndio hatakiwi kukuelekeza we mwanaye njia sahihi ya kupita??kufanya makoso ndio experience hiyo wanayotakiwa ku share na kurekebisha mwenendo wa viongozi wetu. Baba wa taifa mbona alisema kuna makosa aliyatenda kwenye uongozi wake lkn bado alikemea sana maovu ndani ya chama na nchi wakati wa uhai wake...iwe vp wazee wetu waliobaki kutofanya hivyo? Anyway hata Nyerere akiwa kijana alipambana na mkoloni Mzungu na na hata watawala machifu waafrica...so my take...tuache kulalalama na kuongea sana desturi ya Tanzania ni hiyo na CDM nao ndio vivyo hivyo maneno mengii tu ndo maana bado naamini CCM yenye mabadiliko ndio nuru ya taifa letu...tudiscuss nini cha kufanya sio kulalama na kuandika kasoro sasa wewe kama kijana wa CCM mwenye mawazo mbadala what should be our way forward??????/
 
Nafikiri kuna a clear ideological divide katika CCM haswa baada ya wanamtandao kusweep into power.....Kuna wale wanaotaka mazuri ya mwalimu yarejeshwe haswa katima maadili ya uongozi (siasa na biashara nk) hawa naweza kuwaita NEO-CONSERVATIVES na kuna wale walionufaika sana sana na kujilmbikizia mali au wenye uroho wa mali na madaraka na hawataki kitu kubadilika ikiwemo mfumo huu wa kifisadi ulioanza muda wa mwinyi na kuimarika muda wa MKapa hawa naweza kuwaita ni STATUS-QUO...kitu kibaya wote wana fikiri wakijitoa ndani ya chama nguvu zao zitapungua au kuzimwa (mfano wa Mrema) na hii inakipa shida chama sasa...nakubaliana na wewe CDM siyo mbadili wa CCM, wapizani wa kweli watatoka humo humo CCM, (kumbuka Maalima seif na Dr SLaa)
 
Kwa kawaida mtu mzima akikupa kauli yake tena kwa maandishi ustaarabu tu wa kawaida unatuambia, huna sababu ya kuwa na wasiwsi.

Lakini hili la kuruka kauli yako mwenyewe ndani ya masaa 24 tu ni rekodi ya aina yake kwa Rais Kikwete. Hivyo swali sahihi ni watu kujiuliza tu kwamba je Rais Kikwete, unatupeleka wapi kama taifa juu ya swala zima la katiba?

Na pale tunapogeuka kumuuliza tena mjeruhiwa swali kama hili basi hapo ndipo mnaposikia watu kuitwa wanafiki tena wazandiki wakubwa.

Kuna kila dalili kwamba Rais Kikwete 'Katiba Mpya tena inayotufaa Wa-Tanzania' tayari anayo mfukoni ni kiasi tu cha kufanya geresha la hapa na pale ili akauchomoe na kuuweka mezani jinsi atakavyopendezendezewa mwenyewe.

Si kweli kwamba ukiwa ni rais sasa ufanye kila kitu jinsi upendavyo tu mwenyewe; kuna mipaka ya ki-katiba!!
 
Mchambuzi,

Umechambua vizuri sana, nakupongeza.

Tatizo kubwa lililotufikisha hapo ni ubinafsi wa viongozi. Kuna uwezekano mkubwa kwamba viongozi wengi wa chama hawajui hata itikadi ya chama. Hii inathibitishwa na serikali kukumbatia sera za kibepari kinyume na itikadi ya chama.
Mawazo ya kujiendeleza kwa faida ya wote sasa yamegeuzwa kwa faida binafsi, familia, ndugu, jamaa na marafiki.

Vyama vyote vina miongozo, ilani, sera ambazo kwa ujumla zinafanana kwa lengo moja kuu la kuwalendeleza wananchi. Tofauti ni watendaji.

Tusitegemee miujiza ya kujisahihisha tukiwa na watendaji wale wale. Ni muhimu kujua kwamba kupigania uhuru au ukombozi ni jambo endelevu na hivyo ni wakati muafaka kwa wananchi wanyonge walio wengi kuungana kupambana na tabaka la wachache waliotupoteza njia ili kurudi kwenye mstari.
Kuwa na mawazo kwamba watu hao hao waliotupoteza wanaweza kuturudisha kwenye muelekeo sahihi ni utumwa wa fikra.
 
Kwa mtaji tu wa hayo maneno machache kwenye wino mwekundu hapo chini, mkuu YOU HAVE MADE MY DAY!! Spot on!!!!!!!!!!!!

Mchambuzi,

Umechambua vizuri sana, nakupongeza.

Tatizo kubwa lililotufikisha hapo ni ubinafsi wa viongozi. Kuna uwezekano mkubwa kwamba viongozi wengi wa chama hawajui hata itikadi ya chama. Hii inathibitishwa na serikali kukumbatia sera za kibepari kinyume na itikadi ya chama.
Mawazo ya kujiendeleza kwa faida ya wote sasa yamegeuzwa kwa faida binafsi, familia, ndugu, jamaa na marafiki.

Vyama vyote vina miongozo, ilani, sera ambazo kwa ujumla zinafanana kwa lengo moja kuu la kuwalendeleza wananchi. Tofauti ni watendaji.

Tusitegemee miujiza ya kujisahihisha tukiwa na watendaji wale wale. Ni muhimu kujua kwamba kupigania uhuru au ukombozi ni jambo endelevu na hivyo ni wakati muafaka kwa wananchi wanyonge walio wengi kuungana kupambana na tabaka la wachache waliotupoteza njia ili kurudi kwenye mstari.
Kuwa na mawazo kwamba watu hao hao waliotupoteza wanaweza kuturudisha kwenye muelekeo sahihi ni utumwa wa fikra.
 
Nashuhudia mkiweweseka.Leo ndio mnamkumbuka Mwl, tena kwa njia ya kuweweseka kiasi hicho!! Poleni maana kumekucha nanyi bado mko kwenye lepe la usingizi.Watanzania, wamewaacha kama mwanamke mzinzi, mmejaa soni. Mmebaki kuwashikia na kuwaelekezea mitutu ya bunduki na mabomu ya machozi.Hata wakati tunaelewa nchi yetu ni muflisi, jambo mnalolijuwa ni kuongeza magari ya deraya ya polisi ili kuwafunga midomo wananchi, na kununua mitambo ya kijasusi kuwadhibiti wananchi wenu!!
Leo adui wa ccm si ujinga, maradhi na umaskini ila adui mkubwa wa ccm ni wananchi waliowachoka kwa vile mmeshindwa kuongoza na sasa mnataka kutawala. Hatutaki kwa maneno, hatutaki kwa silaha. Sisi ni watu huru.Down with ukoloni mweusi wa ccm.
Kumekucha!!
Unakiri kwamba CDM inaweza kushika uongozi wa nchi.Wananchi wanajuwa hilo hata bila ya nyinyi kukubali.Lakini, acheni kuwapangia CDM sera, siyo kazi yenu. Iwapo sera zenu zimetufikisha hapo leo mnataka kuwapangia wenzenu sera, zipi??Ondokeni salama. Tanzania itasimama tena.
Wakati anafariki London, Mwl alisema "Najuwa nitakufa,Watanzania mtanililia sana, lakini naenda kuwaombea" Haijawahi kutokea mtu akayasema haya akaribiapo kufa.
Kwa vile hamkujuwa Mwl mmefika hapo mlipo,kurarurana hadharani kama mbwa mwitu. La ajabu mnakwenda kaburini kwake sijui kutambika? Mwl alikuwa mcha Mungu.Hakuna kujikosoa, maana mmechafuka mno.Magamba you are cursed!!! Mlipowapokea waliolaaniwa na Mwl leo yamewafika. Yule aliyelaaniwa na MWL ndiye chanzo cha kuanguka ccm.Mlifikiri mna hekima na busara kuliko Mwl haya sasa jiokoeni tuwaone. Kwishnei!
Kwa heri ya kuonana mwaka 2015.
 
Back
Top Bottom