Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Ruvuma katika kata ya Mletele Manispaa ya Songea, nako wafuasi wa vyama hivyo walichapana kwa mapanga na fimbo na kusababisha zaidi ya watu watano kujeruhiwa wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo.
Tukio hilo ambalo lilitokea juzi saa tisa jioni huko katika kijiji cha Lihumbu, wafuasi wa CHADEMA akiwemo mbunge wao wa viti Maalumu, Chiku Abwao, walivamiwa na kupigwa na wafuasi wa CCM ambao wanadaiwa kuwa walikuwa na gari ndogo.
Hata hivyo wafuasi wa CHADEMA walifanikiwa kulikamata gari dogo la wafuasi wa CCM akiwemo Mwenyekiti wa UVCCM wa wilaya hiyo, ambayo ndani yake inadaiwa ilikuwa na mapanga, vipande vya nondo, mundu, fimbo na bundi akiwa hai.
Mmoja wa wafuasi wa CHADEMA Frank Mgao alisema kuwa baada ya kukamatwa gari hilo, askari ambao waliongozwa na Mkuu wa Polisi wa Wilaya hiyo, Nico Mwakasanga, waliwakamata na kuwapeleka kituo kikuu cha polisi cha Songea ambako wanaendelea kuhojiwa.
Mgao alisema kuwa baadhi ya wanachama wenzake na wanachama wa CCM wamejeruhiwa kwa kupigwa na panga sehemu mbalimbali za miili yao na wengine wamelazwa katika Hospitali ya Serikali ya Mkoa wa Ruvuma ambako wanaendelea kupata matibabu zaidi.