CCM siyo mama yangu-Maige!!!!!

kwa habari za kuaminika ni kwamba hawa jamaa watashitakiwa pamoja na makatibu wao na wakurugenzi wa wizara.
 
Baada ya kupigwa chini na JK sasa mh Maige ni kama kachanganyikiwa...kuna baadhi ya watu wake waliokua wakimpa pole ya kuvuliwa ubosi amewambia kwamba ccm siyo mama yake eti aipigie magoti na haoni tatizo kupigwa chini maana kafanywa mbuzi wa kafara!!!!!

Kauli hii inaonyesha alijaribu kumbembeleza mkulu lakini kamchomolea.


Swali langu sasa ni je Ule mkopo USD400,000 atalipa na income za yale malori mawili?????????????

Kazawadiwa na wale alowazawadia twiga
 
Yule jamaa anae lipwa bila kufanya kazi atashangilia kutoswa kwa gamba laini hili
 
Mie natamani hao walioachwa,waanze kuanika uozo wa wenzao + boss wao,ili tuendelee kupata sababu za kutosha kuwamaliza!!
 
du, huyu asuburi chadema ishike nchi 2015 apandishwe kizimbani kwa kuliibia Taifa bila huruma.
 
kama david mataka alishtakiwa mahakamani kwa kutoongoza vyema shirika la ndege,na hawa mabwana washtakiwe kwa kuliingizia hasara taifa.:A S-baby:
 
Maige aburuzwe mahakamani atueleze wananchi alikopata hizo mali lukuki alizopata. Asipoburuzwa wakati huu, itakuwa ni kipolo. Makamanda wakichukua nchi mnamo 2012 lazima kieleweke.
 
kama david mataka alishtakiwa mahakamani kwa kutoongoza vyema shirika la ndege,na hawa mabwana washtakiwe kwa kuliingizia hasara taifa.:A S-baby:

Dah! Hiyo kutoongoza nilijuwa yale mambo fulani kumbe ni kuto ongoza!!
 
Huyu jamaa si ana majumba mawili ya dola 410,000 kila moja....

Na malori yanayomuingizia dolari 20,000 kwa mwezi....

Dude is ballin'


Ina maana huyu gamba hatakuwa na la kujibu mbele ya mahakama jamani.?
Hili haliwezekani kbs ktk jamii ya Watanzania.

Ila nina hofu kwa sababu ya uongozi ulioko madarakani.
 
Alisema bado anadaiwa kulipa mkopo aliokopa CRDB na anategemea kumaliza deni mwaka 2015,kazi anayo

Usijeshangaa deni hilo likahitimishwa kutoka kwenye yale mabilioni ya Kikwete ambayo sijui yalipotelea wapi. Hayakufika uswazi kabisaa...
 
Ina maana huyu gamba hatakuwa na la kujibu mbele ya mahakama jamani.?
Hili haliwezekani kbs ktk jamii ya Watanzania.

Ila nina hofu kwa sababu ya uongozi ulioko madarakani.
La kujibu analo maana mamlaka husika zimeshapewa kibali cha kufanya uchunguzi then kuanza kamata kamata.
 
Ukiona mtu amefanya kosa kisha halijutii kosa lake basi mtu wa namna hiyo ni hatari sana!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom