Mchawi wa CCM si CHADEMA wala operesheni sangara.
CCM imekwishapoteza mwelekeo kama chama cha siasa chenye kuwajibika kwa wananchi Na kuleta Maendeleo ya nchi. CCM sasa ni chama cha watu binafsi kinachosimamia maslahi ya watu binafsi wachache pamoja na familia zao.
Kwa bahati mbaya (nzuri kwa wanaotaka mabadiliko) CCM imeshindwa kujisahihisha ki vitendo na hata imeshindwa kutumia nafasi ya wazi kujivua magamba katika uchaguzi huu Mkuu wa chama unaendelea.
Katika muda wote wa uhai wa CCM, ukiondoa kipindi cha uchaguzi mkuu 2010, ni muda huu ambapo Ufisadi unadhihirisha nguvu yake wazi wazi. Hii yote inafanyika si kwa maslahi ya taifa, Nadhani hata si kwa maslahi ya chama cha CCM, bali kwa maslahi ya watu binafsi wachache.
Kwa CCM yenyewe kupoteza mwelekeo, kuwakumbatia mafisadi, kuwatupilia mbali wakulima na wafanyakazi na kushindwa kujisahihisha hata baada ya kugundua makosa basi haya ndiyo yanaipeleka CCM kaburini.
CCM imekwishapoteza mwelekeo kama chama cha siasa chenye kuwajibika kwa wananchi Na kuleta Maendeleo ya nchi. CCM sasa ni chama cha watu binafsi kinachosimamia maslahi ya watu binafsi wachache pamoja na familia zao.
Kwa bahati mbaya (nzuri kwa wanaotaka mabadiliko) CCM imeshindwa kujisahihisha ki vitendo na hata imeshindwa kutumia nafasi ya wazi kujivua magamba katika uchaguzi huu Mkuu wa chama unaendelea.
Katika muda wote wa uhai wa CCM, ukiondoa kipindi cha uchaguzi mkuu 2010, ni muda huu ambapo Ufisadi unadhihirisha nguvu yake wazi wazi. Hii yote inafanyika si kwa maslahi ya taifa, Nadhani hata si kwa maslahi ya chama cha CCM, bali kwa maslahi ya watu binafsi wachache.
Kwa CCM yenyewe kupoteza mwelekeo, kuwakumbatia mafisadi, kuwatupilia mbali wakulima na wafanyakazi na kushindwa kujisahihisha hata baada ya kugundua makosa basi haya ndiyo yanaipeleka CCM kaburini.