CCM pawaka moto Dodoma

Watanzania tuna tatizo .
japo wengi wanajaribu kurusha mpira kwa watu wa kijijini ,eti waelimishwe kweli mie mtoto wa kijijini nafadhaishwa sana na kauli za namna hii.

Nakubali ,kweli na hakika ni tabia ya binadamu asiye mwelevu(yani mpumbafu) akifikiri yeye ni mwelevu. Binadmu huyu ana tabia ya kuhamisha tatizo ya kwamba lazima tatizo hili nililonalo limesababishwa na fulani na wala si yeye.

fuatilia tu, binadamu mpumbafu hata kama akiwa amebeba bilauli yake ya maji na bahati mbaya akaidondosha na kupasuka ,binadamu mpumbafu lazima atatafuta wa kumtushwa tatizo hilo.mfano mbona umeweka kiti hapa, ama kitambaa hiki ndo kimesababisha .

binadamu mpumafu siko zote hatafuti chanzo cha tatizo, na mara zote atatafuta jibu jepesi kabisa nalo ni kumtwika hilo zigo mtu fulani.

Jamani nawaombeni kwa niaba ya wanakijiji wenzagu ,mtupe kalikizoeti ya kwamba mnataka kutuelimisha,eti ya kwamba sisi ndo chanzo cha matatizo,eti ya kwamba sisi ndo tunaiweka ccm madarakani.

One moment
Lakini nikijaribu kufunua na kuperuzi kumbukukumbu na wanakijiji wenzagu naona kumbukukumbu zinaleta takwimu ya kwamba sisi wavijijini, tusio na elimu tuna historia nzuri ya kupeleka wabunge wa upinzani bungeni ,tofauti na wasomi na watu wa mjini .

Ehe
Sisi wanakijiji tunachojiuliza je tatizo la tanzania ni sisi wanakijiji,tusio na elimu? ama tatizo ni wamjini na wasomi ?
kwanini sisi wa vijijini tunabebeshwa mizigo? je ni kwa sababu hatuna media kama jamiiforums.com ama ITV?

Je tatizo lina mizizi yake i mingine tofauti ila kwa sababu ya upumbafu wa watanzania wote hasa wasomi na wamjini wanajaribu kutafuta jawabu rahisi kuhalalisha upumbafu wao.?
MkamaP,
Mkuu, Kiswahili lugha yangu, lakini hoja na mafumbo uliyotoa hapojuu naona yako nje ya mstari hayalingani kabisa na Hoja iliyopo mezani. Naomba ufafanuzi ili tuendeleze mjadala na kusaidiana.
 
Pasco hilo la Sitta kutoka nje ni la kweli kuna gazeti moja la hapa Tanzania nadhani ni Mwanachi limeripoti kuwa Sitta, Anna Kilango, Dr Mwakyembe walitoka nje na wakaingia kwenye ofisi moja na humo walikaa zaidi ya saa moja na nusu wakijijadiliana na badaye walirudi kwa nyakati tofauti akianza Mwakyembe, baadaye Kilango na mwisho Sitta.

Mimi hawa jamaa wa 16 na mwenzake Kileo naamini sehemu kubwa waliyokuwa wakiongea ni ya UKWELI ila sijui wanaongea kwa maslahi ya nani! Saa nyingine huwa najiuliza hawa jamaa wanaoshinikiza akina wa 16 walete vitu ni kweli wanavitaka hivyo vitu au 'kimtindo' hawavitaki na wanachofanya ni vitisho vya 'kimtindo??

JF!!!! I dare to listen!!!

Hiyo ya kutoka nje kwa hao unaowasema ili ripotiwa jana J3 na magazeti na walitoka nje siku ya Jumapili siku ya kwanza ya kikao cha NEC si jana J3 wakati hiyo thread ya kilewo ni ya jana J3 acheni fix zenu hata hivyo hatuhitaji tena audio yake tumeshapata ajenda zake
 
Angalia sana haya magazeti ya Bongo mengi siku hizi yanatumia JF kama chanzo cha habari

RayB,

Ninachofanya hapa ni kuunga mambo. Hawa jamaa wa 16/Kilewo walisema Sitta alikunywa maji glasi nzima na kutoka nje ambako alikaa muda mrefu bila kurudi. Gazeti la Mwananchi linaripoti Sitta alitoka ndani ya kikao na kuwa na kikao kingine cha faragha na Mwakyembe na Kilango. Kilewo nadhani anawish kuandika 'mamboz' ila huenda anaandika kwa wasiwasi au hata kutype kwenye kompyuta kwake ni tatizo... rejea maandishi yake.. typos nyingi laini zake hazizidi tano.
 
Hiyo ya kutoka nje kwa hao unaowasema ili ripotiwa jana J3 na magazeti na walitoka nje siku ya Jumapili siku ya kwanza ya kikao cha NEC si jana J3 wakati hiyo thread ya kilewo ni ya jana J3 acheni fix zenu hata hivyo hatuhitaji tena audio yake tumeshapata ajenda zake

Luteni,

Hata kama hukubaliani na kinachosemwa lugha za kibabe hapa sio mahali pake! Ushafahamu! Hata sisi twazijua. Kwani Kilewo alitaja Sitta alitoka ndani lini? Au kwa sababu aliongea j3 na kwa hiyo lazima Sitta alitoka ndani j3 na si j2? Kama tunavyokusikiliza wewe ni haki yako na mtu mwengine yoyote ana haki ya kusikilizwa. Sasa kama wewe umeshapata hizo ajenda mbona hujatuletea hapa?? Nina imani Uluteni wako ni wa 'kiukweli' na si kama wa kina Makamba!!
 
Luteni,

Hata kama hukubaliani na kinachosemwa lugha za kibabe hapa sio mahali pake! Ushafahamu! Hata sisi twazijua. Kwani Kilewo alitaja Sitta alitoka ndani lini? Au kwa sababu aliongea j3 na kwa hiyo lazima Sitta alitoka ndani j3 na si j2? Kama tunavyokusikiliza wewe ni haki yako na mtu mwengine yoyote ana haki ya kusikilizwa. Sasa kama wewe umeshapata hizo ajenda mbona hujatuletea hapa?? Nina imani Uluteni wako ni wa 'kiukweli' na si kama wa kina Makamba!!

Gottee
Fuatilia post zangu sina lugha za kibabe lakini huwa mdadisi sana
Hizi ndizo agenda za kilewo unazotaka tuziamini unauhakika RA aliongea jana?

Kilewo: agenda za kipuuzi walizo kuwa nazo jana ni 1. kuhakikisha upnzani haukuwi kwasababu wanawafanya waonekaniki silolote wa chochote mbele ya jamii kitu ambacho sitta alikataa alipokuwa anachangia na kuhoji mulianzisha vyama vingi vya nini, si ilikurekebisha pale tunapokosea na kuleta maendeleo kwa wananchi, 2.kutobadili sheria za uchaguzi na kutumia uchaguzi wa serikali za mitaa kama kupima upepo wa kisiasa kuwa wankubalika au laa, kulikuwa na kauli moja ilyo tolewa na mjumbe mmoja kuwa kwanini chaguzi zisiunganishwe ilkuokoa fedha zinazotumika hovyo kwenye changuzi za serikali za mitaa? hapa wale ambao hawapo kambi ya ufisadi waliunga mkono huku wengi wale mafisadi wakibisha wakisema kufanya hivyo nikukiangusha chama alisema......... rostarm

kulikuwa hata hamna la maana ilawalikuwa wanajaribu kujiokoa ila wakashindwa ndiyo amri ikatoka kuwa watumie vyombo vya habari kuwa mambo nishwari ila hakuna ufumbuzi kama ufumbuzi upo kwanini mwinyi waongezewe muda? angalieni mbali jamani, na wateteeni watanzania wa lalahoi kwa kupitia vyombo mbalimbali kwa kujadili kama hapaz jf naamini ipo siku itawezekana
 
Luteni,

Hata kama hukubaliani na kinachosemwa lugha za kibabe hapa sio mahali pake! Ushafahamu! Hata sisi twazijua. Kwani Kilewo alitaja Sitta alitoka ndani lini? Au kwa sababu aliongea j3 na kwa hiyo lazima Sitta alitoka ndani j3 na si j2? Kama tunavyokusikiliza wewe ni haki yako na mtu mwengine yoyote ana haki ya kusikilizwa. Sasa kama wewe umeshapata hizo ajenda mbona hujatuletea hapa?? Nina imani Uluteni wako ni wa 'kiukweli' na si kama wa kina Makamba!!

Ni haki ya mtu kusikiliza na kusikilizwa lakini si haki kudanganya wengine kama unahitaji ajenda zilizozungumzwa angalia post no 298 ya bumbumbile hizo ndizo tunazitaka kuzichambua haijarishi kama ni nzuri au mbaya

habari unayoizungumzia ilitoka jana gazetini matukio aliyokuwa anatuletea kiwelo na wa 16 ni ya jana ina maana gazeti liliandika matukio ya siku hiyo hiyo na kutoka siku hiyo hiyo lazima nijulize legitimacy ya habari mnazotuletea vinginevyo nitakuwa napoteza muda tu hapa JF nitakuwa useless kama napokea chochote mradi kimeletwa na JF members

Date::2/15/2010
Kikao cha NEC-CCM ngoma nzito Dodoma
na Habel Chidawali, Dodoma

MKUTANO wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec), umeanza mjini hapa ukiwa umefunikwa na usiri mkubwa kutokana na mambo mazito yanayojadiliwa wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba.
.........................................................................................
Mnamo saa 12:15 hivi jioni Spika Sitta, Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Same Mashariki Anne Kilango Malecela walitoka ndani ya chumba cha mikutano na kukaa kwenye chumba kimoja kwa pamoja wakijadili jambo linaloonekana kuwa ni zito kwa muda wa takribani saa nzima.

Baada ya kuketi pamoja kwa muda huo, baadaye waliamua kuingia ndani ya kikao, haikufahamika kama waliitwa au la, lakini alianza kuingia Dk Mwakyembe akifuatiwa na mama Kilango na baadaye Spika Sitta.
 
..hakuna chochote kilichotokea ni business as usual. kama ulifuatilia kikao cha bunge na maazimio yaliyopitishwa basi utaelewa kwamba wananchi tumepigwa changa la macho.

NB:
..pia fuatilieni mahojiano kati ya Dr.Ndulu na kamati ya bunge mtajua tuna wabunge wa aina gani Tanzania. hawa watu wakishafika Idodomya wana-loose touch na maisha ya wa-Tanzania masikini.
 
.
Alibaba, asante kutujulisha, kumbe sasa angalau mnalala?. Basi nitamweleza Invi na wanabodi wengine na sisi to relax.

Asante pia kujitambulisha kwa kutupatia hakikisho la habari yenye uhakika asilimia 99% ili kutuonyesha wewe ndio namba 2 chini ya Othman, maana kama hata huyo namba 3 hawezi kuwa na uhakika na namba 2.

Tumekusikia kumbe hizi ni kelele tuu za mlango... ngoja nasi tujilalie, kumbe wenyewe wamelala na hawakosi usingizi!.

Angalizo kwako Alibaba, usijekuta kumbe wewe ndio mfungua geti hapo nje, hivyo wala hujui mle ndani kinaendelea nini, ukishaona tuu wamezima taa na kufunga ofisi, basi umejiridhisha wemeshafunga kazi, hivyo wamekwenda kulala, na wewe unajifungia zako geti ukiwasubiri asubuhi waje kazini, asubuhi ikifika unawafungulia geti ukiamini ndio wametoka kuamka na ndio wanaingia kazini!, na wewe ndio unatoka shifti na kwenda kujilalia!.

Asante kwa taarifa hizi!.
Mkuu Pasco,

Hili mbona halihitaji Hesabu kali au roket sayans, kwani kila siku tunabweka humu, kuna jambo lolote uliloliona au kusikia kuwa UWT wamewajibika kwa sababu ya kelele au vielelezo walivyochukua toka JF? Upo uwezekano wa Afisa fulani kupita Jf kwa wakati wake na pengine pia akawa mchangiaji kama mimi na wewe, lakini aliyewekwa/waliowekwa Rasmi kwa kazi ya kumonita JF hakuna.Mimi si no 2 wala mfungua na mfunga geti kwa hesabu za Bongo ni kuweka mbili na mbli na jibu liko wazi.

Ndio mana nikasema ili washughulikie maswala tunayoyapigia kelele ni lazima tutafute mbinu nyingine ya kuwahusisha na kuwafanya wahusike. Na ikiwa tutaweza kufanya hivyo basi iwe kwa TAASISI zote muhimu tukianzia Ofisi ya Rais, Waziri mkuu, Bunge, Mahakama ,Polisi, Tukukuru na nyinginezo, Usitegemee Taasisi zote hizo hususan UWT ati watakaa wakingojea mimi na wewe tukerwe tuandike na wao wawe kazini, Hayendi hivyo mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom