nimepata tabu sana kumuelewa huyu ndugu na hasa kwenye issue zake ajira milioni moja na shule za sekondari. ajira milioni moja hazikuzalishwa kama anavyodai na ushahidi mkubwa ni kuongezeka kwa un employment rate ndani ya nchi kwani kila mwaka vijana laki saba wanamaliza darasa la saba bila ya kwenda secondari kwahiyo kwa miaka mitano hao ni zaidi ya watu milioni tatu na nusu bila ya kuhesabu wale wanaomaliza form 4 na 6 kwahiyo kama hizo ajira kweli milioni moja zilitengezwa ukitoa na idadi ya wanaomaliza shule kwa miaka mitano tu ni vijana milioni mbili unusu wanabaki bila ya kazi. kuhusu mafanikio ya kujenga shule nyingi karibu kila kata na shule hizo kutokuwa na vitendea kazi wakiwemo walimu nafikiri matunda yake tumeyaona zaidi na ya nusu ya wanafunzi wote waliomaliza sekondari mwaka 2010 walipata division zero na pia ukichanganya nawaliopata division 4 kwa ujumla asilimia 88 ya wanafunzi wote hawakwenda kokote sasa kama matokeo haya huyu bwana anayaita mafanikio basi tuna matatizo makubwa sana ndani ya nchi yetu.