CCM Nyonyeni Watanzania hadi akili zao zikae sawa.... umaskini na ujinga viliumbwa....

Hossam

JF-Expert Member
Feb 10, 2011
3,538
2,155
Napenda kukipongeza CCM namna kinavyojitahidi kila siku kuja na mbinu mpya ya wizi wa kura na wizi wa maliasili za watanzania, zaidi sana na pesa zetu katika benki kuu yetu na mawizarani. Nafarijika sana kuwaona watoto wa wakubwa wakiishi maisha ya anasa, ubabe na kwa viburi vya baba zao huku wakiwa juu ya sheria kwa sababu sheria za Tanzania zilitungwa kwa ajili ya makabwela na sio wenye nazo.

Binafsi nafurahi sana kuona mafisadi wakubwa wa nchi hii wanatokea CCM na hakuna wa kuwafanya kitu kwa kuwa hakuna sheria wala chombo chochote cha dola chenye uwezo wa kuwakabili. Taasisi ya Urais ya JK nayo ikilegalega napata faraja mno, na zaidi sana napenda kila mara kuona mheshimiwa rais akirandaranda nchi za nje kutafuta chakula kwa watanzania.

Inaleta matumaini sana kuona CCM ikifanya kila hila kulithisha uongozi wa watoto na ndugu zao ili kulinda maslahi yao na kuendeleza unyonyaji kwa Watanzania mambumbumbu wasio na uwezo wa kuhoji, na zaidi sana naoenda kuona nafasi zooote nyeti serikalini zikiendelea kuteuliwa na rais kwa manufaa yake.

Inanipa raha sana kuona mafaili ya wala rushwa na wezi wa pesa za umma yanapotea hovyo kwenye ofisi nyeti serikalini na hakuna wa kuhoji kwa sababu sisi ni mambumbumbu kabisa, na naona raha kabisa mtu mmoja wa CCM akiwapiga mkwara Watanzania milioni 55 bila hata mmoja kuhoji. Hii inanipa raha sana kwa kuwa sasa CCM itatumia watu wachache kuwatisha wananchi kwa kuwa hao wachache ndio walioichafua CCM, yaani win win situation, naona raha kabisa.

Binafsi na familia yangu tunafarijika sana kuwaona Watanzania milioni 55 wakikenua meno wamuonapo rais wao huku kwa hakika hakuna wanachoambulia zaidi ya kuungua na jua na kupanda mafuso ili kujaza watu.

Napenda na naomba mafisadi wazidi kushika makampuni muhimu nchini na tenda hata za ikulu zitolewe kwa upendeleo ili CCM izidi kupendwa na mafisadi. Zaidi sana nasikia raha sana kuona fujo zile za Kivukoni na jinsi watanzania wanavyopoteza muda kusubiria MV Kigamboni na Magogoni, hata daraja lile linalojengwa Kurasini linanipa raha sana kwa kuwa watu sasa hawataweza kwenda huko maana ni ujinga kabisa, hii ina maana serikali ya CCM itajisifu kujenga daraja hilo na lakini itasema hatutaondoa vivuko hivyo anayetaka daraja achome mafuta kurasini ama aendelee kulipia vivuko, sasa kwa sababu njia ya mkato ni vivuko basi daraja litumiwage kwa fujo na daladala za mbagala tu. Hii inanipa raha sana.

Nafarijika mno kuona mheshimiwa rais anatembea na first class ambulance wakati wakazi wa Kibondo na Tabora wanaendelea kufa bila kuwa na vitua vya afya halafu wakimuona kiongozi wa CCM wanakenua tu meno, hii inanipa raha sana.

Mwisho nafarijika kuona maisha yanakuwa magumu na ajira hakuna nchini. Nasikia raha mno kuona sukari inauzwa sasa hadi na polisi kwa kuwa inafaida kwa wenzetu na sio bongo, naona raha pale PM anaposema sasa JWTZ italinda sukari badala ya mipaka maana polisi kazi yao kumbe ni vibaka wadogo wadogo wa kariakoo, hii inanipa faraja sana ikizingatiwa kwamba mkuu wao yaani IGP anafurahia kusifiwa kwamba yeye anaweza sana kula sahani moja na vibaka wa kariakoo na sio wahujumu uchumi halafu akipewa na lile V8 basi anakenua meno tu, nasikia raha sana aiseee.

CCM ikiiba kura, ikiendesha siasa za mwenyenacho mpishe, ubabe, uimla, vitisho na ubaguzi kwangu ni raha sana aisee. Mwigule eehh hivi hakuna mchongo mwingine wa wizi BOT? Nataka na mie kuleta scania langu lina tani 40 nadhani litasaidia ubebaji. CCM raha sana, mungu awatie nguvu aisee muendelee hivyohivyo hadi akili zitusogee!!! Kesho nitaleta ya Chadema, stay tuned.
 
Tuombaje amendment wakati Mungu kaagiza neno lake lisibadilishwe?alisema usiongeze wala kupunguza neno?

Basi huyo ni mungu wako peke yako na sio wetu sisi akina kalume kenge, Mungu ukimuomba kitu anakupa thats why anasema yeye ni wa rehema. Maana yake utaka kusema tutanyonywa hadi siku ya ufufuko eehh?
 
Nyie watu hivi mmemsoma huyo mleta thread hii? Anawauliza watanzania tumerogwa? why dont we fight for our country? Tumekuwa wabinafsi ile mbaya, hivi mmeishajiuliza watoto wetu hali ikiendelea hivi wataikuta nchi hii kweli? Tumelalal mno jamani watanzania tuamke katika usingizi huu mzito!
 
Inabidi hali izidi kuwa mbaya sana ili tupate akili maana sasa ni makalio tu yanafanya kazi
 
Nyie watu hivi mmemsoma huyo mleta thread hii? Anawauliza watanzania tumerogwa? why dont we fight for our country? Tumekuwa wabinafsi ile mbaya, hivi mmeishajiuliza watoto wetu hali ikiendelea hivi wataikuta nchi hii kweli? Tumelalal mno jamani watanzania tuamke katika usingizi huu mzito!

Mkuu tatizo ni umimi ndio unatusumbua watanzania yaani mtu akineemeka anasahau wenzie.
 
Hossam Hassan acha hasira na kukata tamaa kwani hata wewe hufaidi kitu humo.

Mungu hata siku moja hajamuandikia bindamu mateso haya na kudhalilishwa kote bali ni matokeo tu ya uchoyo uliowatembelea baadhi ya wenzetu ndani ya CCM. Hebu kaza buti zaidi mkuu siku si nyingi mambo kujipa nchini mwetu.

Amini tena nakuambia wengi ni wenye imani haba katika 'vita' hivi vya kujiondolea minyororo ya Ukoloni Mamboleo tabaka la Ufisadi.
 
Duh!! Hii Hossam umetoa kali dah!!
Ila ok, ki ukweli watz tumelala sana, lakini kaka kukata tamaa hakutotusaidia, chamsingi mkuu mimi na wewe msomaji tuunge mkono ukombozi kwa wale ambao tiyari wameishaamka, kila mmoja ajiamini kwamba anaweza kuleta mabadiliko.
Si jambo la kukata tamaa!! Tujitoe kwa dhati mabadiliko/ ukombozi umekaribia!!
 
tufanyeje.......pamoja na mazuri yote aliyofanya mwl.jk alisahau moja kubwa yaani kutuondoshea janga la woga.
 
Mtaji wa CCM ni ujinga na umasikini wa watanzania. Laiti ujinga huu ungeondoka viongozi wa CCM wote wangepigwa mawe na kuchomwa moto popote watakapo onekana.ILAANIWE CCM.
 
waache waendelee kutuchokonoa,bado kitambo kidogo tu mambo yatabadilika...Tutachukua vyote walivyotuibia......
 
ndugu zangu tuamini kwamba ukombozi u karibu na wala Wa-Tanzania tusifike mahala tukakata kabi tamaa maana siku zote maisha mema yako kwenye kuendelea kutumaini mabadiliko, kjitolea kwa nguvu zote kwa kila mmoja wetu kuwa chachu wa mabadiliko tunayoyatamani.

Tanzania daima itakwepo ulimwenguni sawa tu na ari yake ila CCM kwa mfano wangu huu ni kama magugu tu kwenye ardhi yenye rutuba ambapo asubuhi moja sisi wakulima tukiamua ni kisi tu cha kuking'oa, kutikisa udongo wote miszizini na kukianika juani kikauke na kufa kabisa.

Ufisadi wao umetukinaisha pomoni wenzetu hawa.


tufanyeje.......pamoja na mazuri yote aliyofanya mwl.jk alisahau moja kubwa yaani kutuondoshea janga la woga.
 
Uchungu wa maisha ukizidi watu watalazimika kufikiri.Nakubaliana sana na wewe mkuu Hossam.
Kama matumaini yakifa,kama upendo ukifa na kama haki ikifa,CCM lazima ife.
 
Siku zote kuongoza kundi la watu waliokta tamaa ni sawa kuongozi kundi la simba jike lenye vijijito jangwani. Wahusika fikirieni juu ya hili.
 
Nadhani tunapo ongelea ukombozi ni lazima wakombolewa na hata mkozi/wakombozi wapitie madhila fulani ambayo kwa namna fulani ndio kichocheo cha kuutaka ukombozi huo. Hata tukiangalia twaweza pata mifano mingi mf.wanawa israel toka utumwani misri, wazawa wa Afrika kusini dhidi ya utawala wa kibaguzi,nk. Ndugu zangu hapana kukata tamaa kwani nuru imeanza kuonekana kwa ishala zilizo wazi,ingawa watawala wanaweza puuza lakini muda utatueleza,kumbuka gaddaf alichelewa kusoma alama na kuendelea kuwabeza waasi kuwa ni panya lakini leo iko wazi. Hapana kukata tamaa ktk kutafuta ukombozi.
 
Back
Top Bottom