Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Diwani wa Kata ya Kisangura (CCM),
Katika Tarafa ya Rogoro wilayani hapa, Joseph Muniko, amelazimika kumwaga machozi mbele ya mkutano wa kijiji cha Bisarara ili kukwepa adhabu dhidi yake kufuatia hatua yake ya kumzaba kibao kijana mmoja kwa `kosa` la kukamata kuku wawili kutokana na vijana wa diwani huyo kutoshiriki shughuli za maendeleo.
Tukio hilo lilianza Februari 8, mwaka huu kijijini hapo baada ya kundi la vijana wanaolingana kwa umri, maarufu hapa kama `saiga` walipokamata kuku wawili wa diwani huyo kama faini kwa kitendo cha watoto wake kugoma kushiriki katika shughuli za maendeleo.
Kwa mujibu wa habari zilizothibitishwa na kaimu katibu tarafa ya Rogoro, Masaga Magesa, kitendo hicho kilimuudhi diwani huyo aliyechaguliwa Oktoba 12, mwaka jana katika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha diwani aliyekuwepo, ambapo aliamua kuwafuatilia kuku wake hao ili kuwarejesha.
Huku uamuzi wa kukamata kuku ama kulipa faini ya sh. elfu 10,000 kwa wanaokwepa kushiriki shughuli za maendeleo ukiwa ni wa kijiji, diwani huyo alifika na kuchuka kuku wake kwa nguvu huku akisema hayuko tayari kulipa kiasi hicho na wala kuku wake kuchukuliwa.
Inadaiwa diwani huyo wakati anachukua kuku hao kibabe, vijana waliokuwa wamemkamata kuku wake waliamua kumtolea uvivu na kumwambia kuwa yeye ni kikwazo cha maendeleo, kauli iliyomuudhi zaidi na kumzaba kibao kijana mmoja wao kisha akaondoka na kuku wake, huku akitamba kuwakomesha.
Imeelezwa kwamba kitendo hicho kiliwaudhi wananchi wengi ambao waliamua kwenda nyumbani kwa diwani huyo, wakachukua ng`ombe wawili zizini akiwemo maksai mmoja na kuwapeleka katika ofisi ya kijiji.
Habari zimesema kwamba diwani huyo aliamua kuchukua sime na kufuata ng`ombe wake kibabe hali iliyopelekea wananchi kuogopa kutokana na jinsi wanavyomfahamu kwamba anaweza hata kuua, hatua iliyomwezesha kuondoka na ng`ombe wake wawili na kurudi nao nyumbani kwake.
Katika Tarafa ya Rogoro wilayani hapa, Joseph Muniko, amelazimika kumwaga machozi mbele ya mkutano wa kijiji cha Bisarara ili kukwepa adhabu dhidi yake kufuatia hatua yake ya kumzaba kibao kijana mmoja kwa `kosa` la kukamata kuku wawili kutokana na vijana wa diwani huyo kutoshiriki shughuli za maendeleo.
Tukio hilo lilianza Februari 8, mwaka huu kijijini hapo baada ya kundi la vijana wanaolingana kwa umri, maarufu hapa kama `saiga` walipokamata kuku wawili wa diwani huyo kama faini kwa kitendo cha watoto wake kugoma kushiriki katika shughuli za maendeleo.
Kwa mujibu wa habari zilizothibitishwa na kaimu katibu tarafa ya Rogoro, Masaga Magesa, kitendo hicho kilimuudhi diwani huyo aliyechaguliwa Oktoba 12, mwaka jana katika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha diwani aliyekuwepo, ambapo aliamua kuwafuatilia kuku wake hao ili kuwarejesha.
Huku uamuzi wa kukamata kuku ama kulipa faini ya sh. elfu 10,000 kwa wanaokwepa kushiriki shughuli za maendeleo ukiwa ni wa kijiji, diwani huyo alifika na kuchuka kuku wake kwa nguvu huku akisema hayuko tayari kulipa kiasi hicho na wala kuku wake kuchukuliwa.
Inadaiwa diwani huyo wakati anachukua kuku hao kibabe, vijana waliokuwa wamemkamata kuku wake waliamua kumtolea uvivu na kumwambia kuwa yeye ni kikwazo cha maendeleo, kauli iliyomuudhi zaidi na kumzaba kibao kijana mmoja wao kisha akaondoka na kuku wake, huku akitamba kuwakomesha.
Imeelezwa kwamba kitendo hicho kiliwaudhi wananchi wengi ambao waliamua kwenda nyumbani kwa diwani huyo, wakachukua ng`ombe wawili zizini akiwemo maksai mmoja na kuwapeleka katika ofisi ya kijiji.
Habari zimesema kwamba diwani huyo aliamua kuchukua sime na kufuata ng`ombe wake kibabe hali iliyopelekea wananchi kuogopa kutokana na jinsi wanavyomfahamu kwamba anaweza hata kuua, hatua iliyomwezesha kuondoka na ng`ombe wake wawili na kurudi nao nyumbani kwake.