Hivi karibuni kwenye taarifa ya habari TBC1 Manumba alisikika akitamka kwamba Zitto anatishiwa kuuawa! Ni habari ya kuogopesha na kushangaza kwa vile watanzania hatuna utamaduni wa mauaji. Hadi mkuu wa jeshi la polisi atoe kauli kama hiyo, upelelezi wa kina umekwishafanyika na ushahidi wa uhakika na wa kutosha upo! Tena tunaamini mkuu wa namna hiyo hawezi kuropoka ovyo!
Suala la njama za mauaji si la kufumbiwa macho hata kidogo. Liwekwe hadharani na watuhumiwa wafikishwe mahakamani na sheria ichukue mkondo wake. Manumba asipofanya hivyo, akiri hadharani kwamba aliropoka na kisha ajiuzulu.
Kwa mawazo yangu, kwa kuwa jeshi la polisi limekuwa la CCM, matamshi ya namna hii yanaweza kuwa maandalizi ya awali ya kuwahadaa wananchi ili baadae CCM wenyewe watekeleze mauaji na kisha wawasingizie wapinzani wao ili kuwamaliza kisiasa. Huu ndio mwendelezo uleule wa umafia wa Mahita kwa chama cha CUF alipoonyesha kisu kupitia taarifa ya habari ya ITV chenye rangi ya bendera ya CUF siku moja kabla ya uchaguzi miaka kadhaa iliyopita na watanzania wakaamini habari ile ya uzushi..
CCM wanafahamu kwa sasa hali yao ni mbaya na uchaguzi wa 2015 ni patashika. Kauli ya Manumba ni maandalizi ya uzushi mwingine ili baadae watekeleze mauaji ya Zito kisha wawasingizie CHADEMA ili kuwamaliza kisiasa. Wanatafuta namna ya kuua mijadala ya katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. Manumba atoe majina ya watuhumiwa wa mauaji hadharani. Ee Mungu utuepushe na huyu pepo mchafu aliyeivamia nchi yetu!
Suala la njama za mauaji si la kufumbiwa macho hata kidogo. Liwekwe hadharani na watuhumiwa wafikishwe mahakamani na sheria ichukue mkondo wake. Manumba asipofanya hivyo, akiri hadharani kwamba aliropoka na kisha ajiuzulu.
Kwa mawazo yangu, kwa kuwa jeshi la polisi limekuwa la CCM, matamshi ya namna hii yanaweza kuwa maandalizi ya awali ya kuwahadaa wananchi ili baadae CCM wenyewe watekeleze mauaji na kisha wawasingizie wapinzani wao ili kuwamaliza kisiasa. Huu ndio mwendelezo uleule wa umafia wa Mahita kwa chama cha CUF alipoonyesha kisu kupitia taarifa ya habari ya ITV chenye rangi ya bendera ya CUF siku moja kabla ya uchaguzi miaka kadhaa iliyopita na watanzania wakaamini habari ile ya uzushi..
CCM wanafahamu kwa sasa hali yao ni mbaya na uchaguzi wa 2015 ni patashika. Kauli ya Manumba ni maandalizi ya uzushi mwingine ili baadae watekeleze mauaji ya Zito kisha wawasingizie CHADEMA ili kuwamaliza kisiasa. Wanatafuta namna ya kuua mijadala ya katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. Manumba atoe majina ya watuhumiwa wa mauaji hadharani. Ee Mungu utuepushe na huyu pepo mchafu aliyeivamia nchi yetu!