Jamani Mwanza hakukaliki,leo askari wamevamia duka la furniture kenyatta road na kubeba karibu 1/2 ya mali yote.Tena wanavamia kwa kunyatia kama vibaka.Mfanyabiashara huyu alikua amedisplay seti moja tu ya meza ya ofisi mbele ya duka lake,dhahma aloipata inasikitisha sana,i wish ningekua na cemera niwaonyeshe yanayoendelea nchi hii.Najua pengine sheria hairuhusu kudisplay nje mlango wa duka,lakini nguvu ilotumika na hasara alopata haifanani kabisa na kosa lake,wamebeba mpaka bidhaa ilokua ndani kabisa,huu si ubinadamu,ifikie hatua askari wawe na reasonable thinking.kila askari aliondoka na chake pale.Je huu ni uungwana?Serikari ya CCM inanyang'nya hata kidogo walichonacho wananchi,CHADEMA wanapita mtaani kuwatuliza wananchi na kuwapa pole kwa yanayowakuta,wakichukizwa na hila za askari kuvizia na kuiba badala ya kuwaendea wavunja sheria kisheria.Mimi binafsi nimeumia sana.