CCM na madai mapya dhidi ya OCD Arumeru.

Losambo

JF-Expert Member
Nov 8, 2011
2,612
864
Chama cha Mapinduzi (CCM) haileweki kuwa ni kuweweseka au vipi, maana habari za chini ya kapeti lakini zilizothibitishwa zinasema kumeanza shutuma mpya dhidi ya kamanda mkuu wa Arumeru kuwa ni CDM na hakisaidii chama kikamilifu.

Nilipokihoji chanzo hicho ni msaada gani hasa wanaotaka CCM zaidi ya ulinzi na usalama katika mikutano yao? Chanzo hicho kilisema kuwa OCD Arumeru ni kama ana mapenzi na CDM pamoja na askari wake hivyo hawatoi msaada unaotakiwa na wanamashaka siku ya tarehe moja wanaweza kushindwa kuthibiti vurugu ambazo zinaweza kujitokeza eti kutokana na kuonekana kuwa na mapenzi na CDM!!!!!

Baada ya kupata taarifa niliingia porini kuthibitisha madai ya chanzo hicho na kubaini yafutayo;

1.0 Ongezeko la askari wengi wageni toka mikoa ya karibu na Arusha, lengo likiwa ni kuongeza nguvu. Askari hao ni mashushushu (UWT) na polisi wenyewe kwa lengo la kushauriana jinsi ya kuweza kuona jindi ya kuokoa jahazi lisizame.
2.0 OCD wa Arumeru siyo kweli ni mtu wa CDM bali ni jinsi anavyotenda kazi kwa kufuata maadili ya kutoegemea upande wowote imepelekea kutiliwa mashaka eti ni CDM. Hali kadhalika askari wengi wameonekana kukubwa na kiroho cha kuhamishwa endapo CCM itashindwa!!!! Ikumbukwe vyombo vyote vya ulinzi na usalama havipaswi kushabikia chama chochote kile.
3.0 Ni kama CCM imeshagundua itashindwa Arumeru kwenye kura la box na kilichobaki ni kutoka kupitia mlango wa nyuma ambao ni fitna nje ya uwanja wa kura. Hii kwa wao wanaamini inawezekana kwa sababu wanajeshi linalowasupport.

Angalizo;

Madai kama haya hayana msingi kwa chama kama CCM, ni bora muda ulibaki ikajitahidi kushawishi wapiga kura ili wakipigie chama chao siku ya uchaguzi kuliko kujikita zaidi na hisia ambazo zinaweza kuwahukumu watu kinyume na makosa yao.

Nawasilisha kwa majadiliano.
 
Uhuni tuu huo OCD ni mwajiliwa wa CCM!
Sasa lawama wanamtupia nani Mwema?
Yaani siku ya CCM kupokwa madaraka kitaifa kuna haja ya kuwafungulia kesi kwa jinsi wanavyofnya watu wakiuke maadili yao ya kazi!
 
Magamba hawaamini kwamba hawakubaliki, wanataka power by force. Lakini hiyo haitawasaidia sana kwa baadae, maana wenye busara walisema who the cap fit let them weir it.
 
Uhuni tuu huo OCD ni mwajiliwa wa CCM!
Sasa lawama wanamtupia nani Mwema?
Yaani siku ya CCM kupokwa madaraka kitaifa kuna haja ya kuwafungulia kesi kwa jinsi wanavyofnya watu wakiuke maadili yao ya kazi!

Mkuu OCD ni mwajiriwa serikali na si CCM na hasa vyombo vya ulinzi na usalama havina chama, hivyo madai ya haya hayana msingi zaidi ya kupenda mteremko na mbeleko katika siasa.
 
Mkuu OCD ni mwajiriwa serikali na si CCM na hasa vyombo vya ulinzi na usalama havina chama, hivyo madai ya haya hayana msingi zaidi ya kupenda mteremko na mbeleko katika siasa.
Hizi wangekuwa siyo waajiliwa wa CCM ndenge ya jeshi la nchi nyingine wanguja hapa nchini na kubeba wanya wetu, hivi wangekuwa siyo waajiliwa wa CCM wangekuwa hawamjui mmiliki wa RICHMOND...naona povu linakutoka...Polisi,mahakama,jeshi, usalama wa taifa, TAKUKURU wote ni waajiliwa wa CCM na siku hawa watu wakigundua kuwa hatupaswi kuajiliwa na CCM basi hii nchi itapata maendeleo
 
Mkuu OCD ni mwajiriwa serikali na si CCM na hasa vyombo vya ulinzi na usalama havina chama, hivyo madai ya haya hayana msingi zaidi ya kupenda mteremko na mbeleko katika siasa.

usipingane na ukweli fuatilia uchaguzi Mwanza .Jamaa alipata taabu sana ila baada wakampandisha cheo, huon wanavyotumia mali za serikali kwa shughuli za chama.Au jinsi wakuu wa vituo vya polisi wanavyohongwa ili waipendelee ccm!mfano polisi Bugurun gari yayotembelea tshs 200 m wa chin yake wanalala kwenye suti za mabat na joto hili inakuwaje?acha papara chambua hoja kwa kufanya tafit funguka kijana.
 
Makanda nashauri tuendelee kua makini sana iyo pia nimbinu chafu za ccm,ilo nichanga la macho ndugu zangu.tuwe makini kulinda kura natusi anzishe fujo.ila tukionewa tusikubali kuonewa.
 
usipingane na ukweli fuatilia uchaguzi Mwanza .Jamaa alipata taabu sana ila baada wakampandisha cheo, huon wanavyotumia mali za serikali kwa shughuli za chama.Au jinsi wakuu wa vituo vya polisi wanavyohongwa ili waipendelee ccm!mfano polisi Bugurun gari yayotembelea tshs 200 m wa chin yake wanalala kwenye suti za mabat na joto hili inakuwaje?acha papara chambua hoja kwa kufanya tafit funguka kijana.

Mkuu umemuelewa Losambo au umekurupa tu kumwambia afunguke ili hali yeye anasema kwa jinsi nilivyomuelewa kuwa CCM wanataka mbeleko katika uchaguzi huo wa Arumeru licha ya kujua OCD hatakiwi kupendelea upande wowote ule.

 
hichi chama sijui vipi ... hata pale moshi walimlaumu sana marehemu Ngohoboko kwamba hakuwathibiti CDM
 
Siku moja kabla ya uzinduzi wa kampini zao walitaka kufanya mkesha kwenye uwanja ambao walipanga kufanyia uzinduzi lakini OCD aliwakatalia baada ya viongozi wa chadema kwenda kumlalamikia...

Hawajui aliwazuia kwa faida yao wenyewe maana usiku hauna macho. Ila wao ni wagumu sana kuelewa.
 
Back
Top Bottom