CCM na CHADEMA wagombana usiku Arumeru...

bibikuku

JF-Expert Member
Feb 16, 2011
832
495
Usiku huu timu ya kampeni ya CCM na ile ya CHADEMA wamejikuta wakipambana kwa dakika kadhaa katika eneo la Meru Garden wilayani Arumeru ambapo ilidaiwa kuwa CCM walikuwa pale kutoa hongo kwa watu kadhaa na kisha Chadema kugundua mchezo huo na kuvamia kwa lengo la kuwakamata na kuwasambaratisha.

Ugomvi huo unadaiwa kusababisha gari la Violet kuvunjwa vioo kwa mawe na kisha CCM wakaenda kuripoti jambo hilo polisi na kudai kuwa wamevamiwa wakati wakiwa katika starehe zao Bar.

Taarifa zaidi juu ya tukio hili tutazipata asubuhi na maendeleo yake. Lakini kwa ufupi hivyo ndivyo mambo yalivyotokea usiku huu
 
Wajameni mbona kugawa rushwa kwa CCM is the oder of the day Chadema ugomvi wa nini?. Kama ni kweli CCM walikutana pale kuoeana rushwa, sasa Chadema wanaingilia nini?, au siku hizi Chadema ndio Takukuru!.

Wana Chadema, waacheni wananchi wa a Arumeru waneemeke na migao fedha safi za chama tawala ili nao japo waambulie ambulie, naamini wa Meru sio waendekeza njaa kivile mpaka kurubuniwa kwa shibe ya siku moja!,

Waacheni wapokee pesa ila kura wanajua watampigia nani!.
 
chadema kweli ni wapenda vurugu kwanini baada ya kusikia habari hizo wasiwaiite TAKUKURU?Kweli watu washindwe kufanza starehe zao kweli?siasa za majitaka hizo,mnatuletea yaleyale ya IGUNGA..!MBOWE kashawahusia anataka siasa safi siyo ya kupigana mawe!tunabishana kwa hoja na sio mabavu
 
Wajameni mbona kugawa rushwa kwa CCM is the oder of the day Chadema ugomvi wa nini?. Kama ni kweli CCM walikutana pale kuoeana rushwa, sasa Chadema wanaingilia nini?, au siku hizi Chadema ndio Takukuru!.

Wana Chadema, waacheni wananchi wa a Arumeru waneemeke na migao fedha safi za chama tawala ili nao japo waambulie ambulie, naamini wa Meru sio waendekeza njaa kivile mpaka kurubuniwa kwa shibe ya siku moja!,

Waacheni wapokee pesa ila kura wanajua watampigia nani!.

Were you listening to yourself while writing this?
 
Nakubaliana nawe Pasco! Chadema, why the heck do you have to get involved in physical fights? Ina maana hamna contact ya takukuru hapo? Ingetosha tu kutuambia mmeona nini na kuchukua hatua ya kuripoti hata kama haitofanyiwa kazi!
Ngoja tusubiri ripoti ya magazeti.
 
Kama ni kweli CCM walikutana pale kuoeana rushwa, sasa Chadema wanaingilia nini?, au siku hizi Chadema ndio Takukuru!.
Labda walitaka kufanya citizen arrest? Au hawaruhusiwi?
 
Nakubaliana nawe Pasco! Chadema, why the heck do you have to get involved in physical fights? Ina maana hamna contact ya takukuru hapo? Ingetosha tu kutuambia mmeona nini na kuchukua hatua ya kuripoti hata kama haitofanyiwa kazi!
Ngoja tusubiri ripoti ya magazeti.
Takukuru? Polisi! Wananchi wanapokosa imani na vyombo vya dola tutegemee nini!
 
Wajameni mbona kugawa rushwa kwa CCM is the oder of the day Chadema ugomvi wa nini?. Kama ni kweli CCM walikutana pale kuoeana rushwa, sasa Chadema wanaingilia nini?, au siku hizi Chadema ndio Takukuru!.

Wana Chadema, waacheni wananchi wa a Arumeru waneemeke na migao fedha safi za chama tawala ili nao japo waambulie ambulie, naamini wa Meru sio waendekeza njaa kivile mpaka kurubuniwa kwa shibe ya siku moja!,

Waacheni wapokee pesa ila kura wanajua watampigia nani!.

Watu hufika mahali wakajichukulia hatua mikononi baada ya kuona vyombo vya dola havifanyi kazi. TAKUKURU wakipigiwa simu na wapinzani huwa hawaendi au wanawasaka kwanza wanaotuhumiwa ili kuwashitua na kuwaambia waondoke. Kwa hiyo CHADEMA wakiamua kuchukua sheria mkononi ni matokeo ya kukosa imani na vyombo vya dola ambavyo vyote vinafanya kazi kwa maslahi ya chama tawala.

Asilimia kubwa ya fedha za CCM ni chafu, huko ndiko zilikoenda baadhi ya fedha za EPA, Stimulus Package na nyinginezo nyingi ambazo zilipatikana kwa njia haramu.
 
Usiku huu timu ya kampeni ya CCM na ile ya CHADEMA wamejikuta wakipambana kwa dakika kadhaa katika eneo la Meru Garden wilayani Arumeru ambapo ilidaiwa kuwa CCM walikuwa pale kutoa hongo kwa watu kadhaa na kisha Chadema kugundua mchezo huo na kuvamia kwa lengo la kuwakamata na kuwasambaratisha.

Ugomvi huo unadaiwa kusababisha gari la Violet kuvunjwa vioo kwa mawe na kisha CCM wakaenda kuripoti jambo hilo polisi na kudai kuwa wamevamiwa wakati wakiwa katika starehe zao Bar.

Taarifa zaidi juu ya tukio hili tutazipata asubuhi na maendeleo yake. Lakini kwa ufupi hivyo ndivyo mambo yalivyotokea usiku huu
Hawa Chadema wawe makini sana ...tayari mkakati wa ccm wa IGunga unaendelea ...kwa kutumia genge la wahuni 200 waliosafirishwa toka Mara....vijana Hawa Wana silaha....bastola,mapanga,visu ,sime ,bisbisi ,acid etc...

LENGo...

1.kuchoma moto nyumba za wenyeji ambao ni wana ccm na kusingiZia ni Chadema.
2.kuteka na kupora wana ccm ionekane ni Chadema
3.kurushia mawe magari ya ccm wenzao na kusingiZia Chadema
4.kuteka watu na kuwauwa...ie Hawa kule IGunga waliua zaidi ya watu 15..-ambao baada ya uchaguzi Maiti za watu walopotea ziliendelea kuonekana.
5.kumwagia watu tindikali zionekane ni Chadema
6.kufanya vurugu wakati matokeo ya awali yanaanZa kutoka ili ccm wapate Mwanya wakuite ffu .....warushe mabomu,ffu watakuja wakiwa na mabox tayari na wakati watu wanajifunika na moshi wa mabomu wao watabadili matokeo...

NINI Kifanyike?

Chadema wahubiri Amani mikutanoni..
Wawasisitize vijana wao kuwa makini na watu wanaowachikoza au wanaovaaa Sare Zao sio wote ni Chadema ...wengine wapo kundi la "al shabaab"
Wakazi wawe makini na wahamiaji ambao wapo kwenye kundi hii wanaosambazwa vijijini mwao........kwa kuwa wa wanafahamiana,itakuwa rahisi kutambua wageni miongoni mwao Wenye nia mbaya ...

Onyo kwa Dola...

Hatua ya ccm Kukodi mercenaries ni dalili mbaya .....Kama iliyokuwa ikifanywa na KAnu kuwakodi Mungiki....ni dalili za mwisho za chama kinachokufa...ie kutumia mamluki,kutumia siasa za majitaka...,kutumia dola ..etc..,....Hatua hizi hazitakuwa na faida kwa ccm zaidi zitaaharakisha kifo......kuna tofauti kubwa ua uelewa kati ya Arumeru na IGunga.......ccm wasitegemee propaganda ,vijarida...,mauwaji ,tindikali ...zitawasaidia kupata ushindi.....sanasana hata wakiwavika wafanya vurugu Sare za Chadema ....tayari wananchi wameshagundua .....na utafiti wa kiiteligensia unaonyesha wananchi wanawafuatilia kwa karibu sana ....Hawa mamluki...,wakazi wa Arumeru wana ushirikiano wa kipekee nje ya chama ......msishangae mkaamka asubuhi mkakuta Hao mamluki 200 wote wamechinjwa na mapanga na wameru ......kwani hii Siri imeshaliki hata kwa wananchi wa kawaida....na Hao wamekuwa common enemy wa kuwachonganisha wameru ....nao hawataki kuuliwa Kama Wana IGunga .

Watu wa usalama wa Taifa ingilieni haraka kusaidia Hawa mamluki warudi makwao haraka......WAmeru watawachinja........na IKULU ITABEBA LAWAMA......KWANI HII TAARIFA KWA SASA INAFUATILIWA HADI NA VUOMBO VYA NJE NCHI....HAO MAMLUKI KILA WAMESHAWEKEWA SURVEILLANCE YA KITAALAMU KABISA NA KILA MWENENDO WAO ...UNADAKWA NA KUREKODIWA .....NA MUDA SI MREFU WATAZINGIRWA..NA MAAFA YATAKUWA MAKUBWA SANA....NA HII INAWEZA KUSABABISHA WAKUU WA USALAMA ,POLISI NA HATA RAIS WETU APELEKWE THE HAGUE ..SIKU AKITOKA MADARAKANI...

CHUKUENI TAHADHARI......! Anaepata ujumbe huu ..Amuambie na mwenzake....!!! Amani ya nchi yetu ,na umoja wetu Kama taifa ni muhimu kuliko tamaa ya ccm kushinda Arumeru!!!!! Wekeni tu uwanja sawa na haki .mshindi wa jimbo la Arumeru ...hatakuwa RAIS WA JAMHURI,!
 
Kuwaacha ni sawa na kuhalalisha rushwa, kuwakamata nako nikujiingiza kwenye mitego yao ambayo wanajua wenyewe pale mambo yanapowawia ngumu. CDM lazima wacheze hii ngoma kwa akili sana, ni kiasi cha kubadili frequency kidogo tu tena bila nguvu kubwa au kuhatarisha maisha yao!! Tatizo kubwa kwa sasa ni vijana wengi wenye sifa za kupiga kura hawako kwenye daftari la kupiga kura, hivyo kushinda chaguzi kama hizi inabidi kutumia akili za hali ya juu.
 
Nakubaliana nawe Pasco! Chadema, why the heck do you have to get involved in physical fights? Ina maana hamna contact ya takukuru hapo? Ingetosha tu kutuambia mmeona nini na kuchukua hatua ya kuripoti hata kama haitofanyiwa kazi!
Ngoja tusubiri ripoti ya magazeti.

Takukuru ni sawa na jibwa lisilo na meno. Kama waliwakamata wapambe wa sioy wakigawa fedha lakini hakuna kesi iliyofunguliwa hadi hii leo halafu unataka chadema iwaachie majukumu ya kupambana na rushwa?

Dawa yao ccm ndio hiyo hiyo, kwenda nao ng'andu kwa ng'adu!
 
Back
Top Bottom