Moja ya mambo yanayosikitisha ni pale mtu unayemtegemea kuwa anauwezo au akili fulani au busara lakini unakuja kukuta kinyume chake.
Ndugu zangu watanzania napenda kuanza kwa kusema ule msemo kuwa Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe na sio mwekezaji, wala mzungu bali ni mtanzania ataamua kujenga au kubomoa. Nayazungumza haya kwa machungu makubwa kwa kuwa naona Watanzania tunaelekea kubaya kwa sababu tuu ya watu wachache wenye uchu wa madaraka. Mtu mwenye akili timamu ni lazima atambue kuwa duniani Mungu ametuumba tofauti kunakuzidiana kiakili,kiuwezo wa hali namali, kuna wakati wa kupanda na kuna wakati wa kushuka, kuna wakati wa kiangazi kwa maana mambo huwa yanabadilika.
Kutokana na hayo mabadiliko kwa mtu mwenye busara huwa anajiandaa na mabadiliko, mtu mjinga ataendelea kushangaa na na kuendelea kupambana akidhani anaweza kuzuia madadiliko.
Nimeyazungumza hayo hapo juu kwa lengo la kuwashauri viongozi wa CCM na CHADEMA kuwa ni vizuri wakaelewa kuwa wao ndio wanaweza kusababisha amani ikawepo au ikatoweka kwa sababu tuu ya uchu wa kutawala wengine. Tutumie akili zetu vizuri kwa kujenga utamaduni wa kukubali pale mwenzio anapokuzidi na tuwe na moyo wa kusema kwa dhati kabisa katika hili, au kipindi hiki au wakati huu, au karne hii wenzetu wamenizidi kiaakili, kiuwezo na kisera pale inapodhihiri.
Nimeyasema haya kwa sababu dalili si nzuri kwa viongozi wa CCM , yenyewe niwaonavyo wanafikiri ndio wenye hati miliki ya kutawala, hata pale dalili za wazi zinapoonyesha kuwa ni wakati wa kulia. Mimi niwashauri kuwa ni vizuri wakacheza siasa za kistarabu na haki kwa maana ya kujenga hoja kwa hoja wakishinda safi, mkishindwa sawa lakini Taifa likabaki na amani na watanzania wakaendelea kuwa wamoja (Taifa mbele chama baadaye). Na ndugu zangu tatizo liko kwa viongozi, wana CCM wakawaida hawana matatizo, mbona tupo wote humu mitaani tunashirikiana kwenye harusi na misiba. CCM mambo ya ukabila, udini, ukanda ili mradi tubaki madarakani tuyakatae ni hatari (Bomu baya sana).
Ndugu zangu ni nyinyi wenyewe mlianzisha sera ya soko huru kuwa litaleta unafuu kwa mtumiaji wa mwisho na hivyohivyo waoneni wapinzani kama washindani wenu katika kuboresha maisha ya mtanzania na pale mnapozidiwa kubalini hamkuzaliwa mtawale milele hizo ni akili za watu wasio na upeo. CCM huu ni ushauri wangu bado ninawapenda kama watanzania wenzangu.
Mungu Ibariki Tanzania
Ndugu zangu watanzania napenda kuanza kwa kusema ule msemo kuwa Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe na sio mwekezaji, wala mzungu bali ni mtanzania ataamua kujenga au kubomoa. Nayazungumza haya kwa machungu makubwa kwa kuwa naona Watanzania tunaelekea kubaya kwa sababu tuu ya watu wachache wenye uchu wa madaraka. Mtu mwenye akili timamu ni lazima atambue kuwa duniani Mungu ametuumba tofauti kunakuzidiana kiakili,kiuwezo wa hali namali, kuna wakati wa kupanda na kuna wakati wa kushuka, kuna wakati wa kiangazi kwa maana mambo huwa yanabadilika.
Kutokana na hayo mabadiliko kwa mtu mwenye busara huwa anajiandaa na mabadiliko, mtu mjinga ataendelea kushangaa na na kuendelea kupambana akidhani anaweza kuzuia madadiliko.
Nimeyazungumza hayo hapo juu kwa lengo la kuwashauri viongozi wa CCM na CHADEMA kuwa ni vizuri wakaelewa kuwa wao ndio wanaweza kusababisha amani ikawepo au ikatoweka kwa sababu tuu ya uchu wa kutawala wengine. Tutumie akili zetu vizuri kwa kujenga utamaduni wa kukubali pale mwenzio anapokuzidi na tuwe na moyo wa kusema kwa dhati kabisa katika hili, au kipindi hiki au wakati huu, au karne hii wenzetu wamenizidi kiaakili, kiuwezo na kisera pale inapodhihiri.
Nimeyasema haya kwa sababu dalili si nzuri kwa viongozi wa CCM , yenyewe niwaonavyo wanafikiri ndio wenye hati miliki ya kutawala, hata pale dalili za wazi zinapoonyesha kuwa ni wakati wa kulia. Mimi niwashauri kuwa ni vizuri wakacheza siasa za kistarabu na haki kwa maana ya kujenga hoja kwa hoja wakishinda safi, mkishindwa sawa lakini Taifa likabaki na amani na watanzania wakaendelea kuwa wamoja (Taifa mbele chama baadaye). Na ndugu zangu tatizo liko kwa viongozi, wana CCM wakawaida hawana matatizo, mbona tupo wote humu mitaani tunashirikiana kwenye harusi na misiba. CCM mambo ya ukabila, udini, ukanda ili mradi tubaki madarakani tuyakatae ni hatari (Bomu baya sana).
Ndugu zangu ni nyinyi wenyewe mlianzisha sera ya soko huru kuwa litaleta unafuu kwa mtumiaji wa mwisho na hivyohivyo waoneni wapinzani kama washindani wenu katika kuboresha maisha ya mtanzania na pale mnapozidiwa kubalini hamkuzaliwa mtawale milele hizo ni akili za watu wasio na upeo. CCM huu ni ushauri wangu bado ninawapenda kama watanzania wenzangu.
Mungu Ibariki Tanzania