The Hunter
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 1,049
- 305
Mwisho wa ubaya ni aibu
Toka asimamishwe ubunge wa Arusha mjini, Godbless Lema amekuwa akifanya harakati kubwa sana za kisiasa dhidi ya CCM, akipita kijiji kwa kijiji akitumia uwezo wake wa kuzungumza kwa ujasiri na hoja zinazogusa wananchi wa ngazi ya chini kabisa,
Sio siri tena athari kadhaa kubwa zimeanza kuonekana waziwazi kwenye kila eneo alilopita, kwa mfano:
1/Makada wengi kutoka CCM wamejiunga na Chadema.
2/Chadema imeanza kuota mizizi vijijini.
3/Chuki dhidi ya Serikali imeongezeka.
4/Woga wa kifikra miongoni mwa wananchi umeanza kutoweka.
5/Chadema imepata wanachama wengi sana maeneo mapya.
*Swali langu kuu kwa viongozi na makada wa CCM, mmejipangaje kukabiliana na hii hali, maana msipochukua hatua sasa mwisho wa siku ni kilio.