CCM: Mkoa wa vyuo vikuu kweli kuna lolote?

MchunguZI

JF-Expert Member
Jun 14, 2008
4,006
2,166
Nimeona eti sasa kuna mkoa wa vyuo vikuu. Naelewa wana vyuo hawana la kusikia toka CCM. Unaweza ukakataa lakini hayo ndo yanayoonekana. Ukifika unaweza kupokelewa kwa nyimbo na fulana za jembe na nyundo lakini ukiondoka CCM inawatoka vijana.

Unaweza ukapandisha posho za wanafunzi, lakini vijana hawa, wakisha kaa husahau lengo lako.


Sasa naona yaja mbinu hii ya mkoa wa vyuo vikuu. Kama kawaida, wataingia wale wanaotaka ubunge na uongozi ili wapate posho, mara baada ya posho, CCM itawatoka vichwani.

Huo Mkoa wa Vyuo vikuu, mwenyekiti nani?? Bado ataendelea kuwa mfanyakazi wa chuo chochote au wametafuta mtu toka mitaani kwetu ili vyuo vikuu wamuunge mkono.


Hawa CCM wanaelewa ni watu wa aina gani huungwa mkono vyuo vikuu?


Nawatakia kufufuka kwema.
 
Back
Top Bottom