wakuu, nimeletewa hii kitu hebu isomeni kwa makini na haswa kuhusu maneno yaliyotumiwa na hawa viongozi halafu fanya tafakuri ya kina nini kinaendelea ndani ya CCM na taifa kwa ujumla , pia hili kundi lilikuwa linapeleka ujumbe gani kwa taifa na wanaCCM wenzao.
KIKAO CHA CCM NA WANAVYUO MBEYA- KILICHOFANYIKA KIWIRA MOTEL 16/07/2011
MADA: VIJANA MUSTAKABALI WA TAIFA:
Mwakyembe.-Alisema alifuatwa na chama maarufu cha upinzani nyumbani kwake na akaambiwa ahame ccm akagoma.
-Anasema ni yeye aliyekuwa mkurugenzi wa NBC na akaiamuru ifungwe kwa miezi minne kwasababu ya ufisadi lakini kwasababu yuko imara hakuweza kubabaishwa na mtu yeyote.ndio maana ccm wanashindwa kumfukuza sababu analindwa katiba ya ccm ibara 81.
-Anasema yeye ataendelea kubaki ccm. -Anasema amefanya mengi ya kukosoa chama lakini bado hakufukuzwa ccm, na atabaki ccm .
Samweli Sita.
-Chama chetu kiliota gamba nami nikiwemo serekalini, kwahiyo ndugu wanachuo na wanafunzi tunaomba radhi.-Tumefika pabaya mpaka chama cha CHADEMA/ upinzani ndio wanamnukuu baba wa Taifa na kuiga baadhi ya matendo yake.
-Chama cha mapinduzi ndicho kinachostahili kujenga Taifa hili nasio chama kingine.-Chama chochote cha siasa hususani ccm lazima kiwe na mizizi mirefu.
-Baadhi ya wenzetu ndio waliotupoteza .
-Nikiwa ndani ya kikao cha nec nilishangaa baadhi ya watu wanataka nirudishe kadi yaani watu ambao wameota magamba(mafisadi).
-Aliendelea kukiri kuwa vita yao ambayo wanapigana sasa ni ngumu sana kwa kuwa wao ni wengi watashinda tu.
-Mkoa wa Mbeya unatosha kuitwa nchi kwani unajitosheleza kwa kuwa una -Kilimo -Maji -Rasilmali(madini)
-Wamepanga kuanza mradi mkubwa wa kilimo utakaoanzia Tunduma hadi morogoro.
-Akasema inashangaza kuna hekari 20, za maua Arusha kwa Tanzania nzima lakini Kenya wana hekari 100. lakini mbeya pekee yaweza kuwa na hekari 600 za maua.
-Akasema ccm inaweza kuwa matajri mpaka kujenga maghorofa kama chama cha ANC kama tutatokomeza mafisadi
-Wapinzani wanachekelea kwakuwa tunamatatizo kibao. Nani aliwaambia kuna kusoma bure? wanakufulu hata vitabu vya mwenyezi Mungu hakuna kitu cha bure. Huo ni upuuzi tu.
Nape Nauye
-Dr Slaa anangangania mke asiye wake, kwani mwenye mke yuko ikulu. Kwahiyo yeye akangangania siatakuwa kibaka
-Chadema hawana huruma (ni baba wa kambo kwani wanawadanganya watu tuandamane ili msipate muda wa kufanya kazi, kwani wao wamepata pesa na kuishi kwenye viyoyozi.
-Akasema kuna mtu Zanzibari (makamu wa kwanza wa Rais Seif) alikuwa mbishi lakini tulipomwambia ukikubali mapinduzi sisi tutakulipa, basi tukamlipa ndio maana anapendeza na tukamtunza kama waziri, kiongozi mstaafu wa serikali ya mapinduzi, akasema lakini chadema ni chama cha msimu tu. Ambacho nacho wataacha na watapotea tu.
Mary Mwanjelwa.-Tuimarishe chama chetu cha mapinduzi .
Ole sendeka.-Waliwaambia vijana kuwa umefika wakati wa kupeana zamu za uongozi na vijana.
Nyalandu.
-Lazara aliongelea kuwa maisha yanakusudi kwamba kijana lazima uwe na kusudi la maisha yako .-Akawaambia vijana hasa wanachuo kuwa ndio rasilimali ya taifa.
-Akaendelea akisema kwamba kila mwanadamu anauwezo mkubwa lakini huwa anatumia 10% tu ya uwezo wake.
-Akasema vijana wa CCM wana mashaka hata wanaogopa kuvaa nguo za CCM.
-Alikiri kuwa ndani ya CCM kuna watu wanokiharibu chama akasema watawashughulikia wanao kiharibu chama cha mapinduzi.
-Aliwaambia wanachuo wafikirie juu ya Tanzania yao.
Hitimisho.
-Hata hivyo vyuoni wakuu wa vyuo bila aibu wanawatishia wana vyuo, wafanyakazi, kuwa hatutamaliza vyuo kwani watatufukuza, wanasema tuhamie CCM Lakin mwalimu mmoja Allawi Dean of student ndiye aliyefanya kazi kuhakikisha mkutano na wanavyuo unafanikiwa kati ya viongozi hao wa CCM na wanachuo wa Teku Mbeya ikiwa ni pamoja na kutumia Serikali ya chuo yaani TEKUSO, kufanikisha kufanyika kwa semina ya CCM.
Mytake ; Vita ni kubwa sana ndani ya CCM na waasisi wa CCJ hawako tayari kurudi nyuma na wanajua kuwa kama hawatapata mtu wao kugombea na ama kushinda Urais watakuwa kwenye wakati mgumu sana hivyo hali ni mbaya ndani ya CCM .