Kasheshe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 4,694
- 787
Kwa mtaji huu wa kukubali kukosolewa CCM yaweza ongoza kwa miaka makumi yajayo....
TahaririHabari zaidi!
Mhariri
Daily News; Monday,March 16, 2009 @19:14
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa waraka maalumu kwa ajili ya kuwaonya na kuwabana viongozi na wanachama wake wanaoendesha kampeni za chinichini kinyume na ratiba ya uchaguzi.
Hatua hiyo inapiga marufuku mgombea na kiongozi wake yeyote kuingiza wanachama wapya kwa ufadhili binafsi kwa kuwanunulia kadi au kuwalipia ada za uanachama, kwa lengo la kutaka wampigie kura.
Hiyo inatokana na uamuzi wa chama hicho kubadilisha utaratibu wa kura za maoni kwa kupanua wigo, ambapo sasa kura hizo zitapigwa katika matawi yake badala ya utaratibu wa zamani wa wajumbe wa mkutano mkuu.
Hii ni hatua mabayo kwa kweli itatoa viongozi wanaotakiwa badala ya zamani ambapo fedha zilitumika kwa majina tofauti tofauti na wagombea, kwa lengo la kurubuni na hatimaye kupitishwa.
Hali hii ndiyo imefanya baadhi ya watu wanaotaka kuwania uongozi kwa tikiti ya chama hicho, kujipitisha kutafuta kuungwa mkono kwa mashinikizo mbalimbali yakiwamo ya kununuliana kadi na kulipiana ada.
Tunaipongeza CCM kuwa imeliona hili na haikutaka kulifumbia macho na mara moja imetoa waraka, ambao utakuwa mwongozo ili kuhakikisha yale inayoyapitisha na kuyasimamia, ndiyo yanayoheshimika na kufuatwa.
Malalamiko ya rushwa yamekuwapo siku zote wakati wa uchaguzi hali ambayo imekuwa ikiichafulia CCM jina na kuonekana kana kwamba ni chafu kupindukia na hivyo kuwapo na haja ya makusudi ya kuhakikisha kuwa haiko hivyo.
Sasa basi hatua hii ya kutoa waraka wa kujibana yenyewe, inaonyesha kuwa inakubali kujisahihisha kwanza kwa kukiri tatizo kuwapo na kulitafutia dawa ya kudumu. Tunaviomba vyama vingine vya siasa nchini vinavyoshiriki uchaguzi na hata visivyoshiriki, kuiona hatua hii ya CCM kama mfano bora wa kuigwa katika mapambano ya rushwa na ufisadi mwingine.
Hivyo navyo havina budi kuja na mwongozo wao kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa na hata uchaguzi mkuu mwakani, kwa sababu navyo si visafi kama ambavyo vitataka wananchi waelewe. Uchaguzi ni uchaguzi na nguvu nyingi halali na haramu hutumiwa na si kwa CCM bali kwa vyama vyote vya siasa na si tu nchini bali duniani kote, hivyo ili kujitoa kimasomaso, vyama vya upinzani navyo havina budi kuweka mambo yao wazi katika hilo.
Kama utoaji fedha na zawadi nyingine wakati wa uchaguzi utadhibitiwa, ni wazi kuwa uchaguzi utafanyika kwa uhuru na haki na kuondoa malalamiko yasiyo ya msingi na hakika watapatikana viongozi wenye uwezo na waadilifu. Kama vyama vya upinzani vitaendelea kudhani kuwa rushwa ya uchaguzi imo ndani ya CCM peke yake, vitajidanganya na kwa upofu huo, rushwa itavitafuna vyenyewe na kujikuta vinakosa viongozi wanaostahili.
TahaririHabari zaidi!
Waraka wa CCM uwe mfano
Mhariri
Daily News; Monday,March 16, 2009 @19:14
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa waraka maalumu kwa ajili ya kuwaonya na kuwabana viongozi na wanachama wake wanaoendesha kampeni za chinichini kinyume na ratiba ya uchaguzi.
Hatua hiyo inapiga marufuku mgombea na kiongozi wake yeyote kuingiza wanachama wapya kwa ufadhili binafsi kwa kuwanunulia kadi au kuwalipia ada za uanachama, kwa lengo la kutaka wampigie kura.
Hiyo inatokana na uamuzi wa chama hicho kubadilisha utaratibu wa kura za maoni kwa kupanua wigo, ambapo sasa kura hizo zitapigwa katika matawi yake badala ya utaratibu wa zamani wa wajumbe wa mkutano mkuu.
Hii ni hatua mabayo kwa kweli itatoa viongozi wanaotakiwa badala ya zamani ambapo fedha zilitumika kwa majina tofauti tofauti na wagombea, kwa lengo la kurubuni na hatimaye kupitishwa.
Hali hii ndiyo imefanya baadhi ya watu wanaotaka kuwania uongozi kwa tikiti ya chama hicho, kujipitisha kutafuta kuungwa mkono kwa mashinikizo mbalimbali yakiwamo ya kununuliana kadi na kulipiana ada.
Tunaipongeza CCM kuwa imeliona hili na haikutaka kulifumbia macho na mara moja imetoa waraka, ambao utakuwa mwongozo ili kuhakikisha yale inayoyapitisha na kuyasimamia, ndiyo yanayoheshimika na kufuatwa.
Malalamiko ya rushwa yamekuwapo siku zote wakati wa uchaguzi hali ambayo imekuwa ikiichafulia CCM jina na kuonekana kana kwamba ni chafu kupindukia na hivyo kuwapo na haja ya makusudi ya kuhakikisha kuwa haiko hivyo.
Sasa basi hatua hii ya kutoa waraka wa kujibana yenyewe, inaonyesha kuwa inakubali kujisahihisha kwanza kwa kukiri tatizo kuwapo na kulitafutia dawa ya kudumu. Tunaviomba vyama vingine vya siasa nchini vinavyoshiriki uchaguzi na hata visivyoshiriki, kuiona hatua hii ya CCM kama mfano bora wa kuigwa katika mapambano ya rushwa na ufisadi mwingine.
Hivyo navyo havina budi kuja na mwongozo wao kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa na hata uchaguzi mkuu mwakani, kwa sababu navyo si visafi kama ambavyo vitataka wananchi waelewe. Uchaguzi ni uchaguzi na nguvu nyingi halali na haramu hutumiwa na si kwa CCM bali kwa vyama vyote vya siasa na si tu nchini bali duniani kote, hivyo ili kujitoa kimasomaso, vyama vya upinzani navyo havina budi kuweka mambo yao wazi katika hilo.
Kama utoaji fedha na zawadi nyingine wakati wa uchaguzi utadhibitiwa, ni wazi kuwa uchaguzi utafanyika kwa uhuru na haki na kuondoa malalamiko yasiyo ya msingi na hakika watapatikana viongozi wenye uwezo na waadilifu. Kama vyama vya upinzani vitaendelea kudhani kuwa rushwa ya uchaguzi imo ndani ya CCM peke yake, vitajidanganya na kwa upofu huo, rushwa itavitafuna vyenyewe na kujikuta vinakosa viongozi wanaostahili.