CCM Mambo yazidi kuwa Magumu: Ni kuhusu rasimu ya katiba mpya

dodoma.jpg

Chama kinataka kugawanyika vipande vipande. haya tusubiri yetu macho na masikio!
Poor thinking.
 
Mkuu Mchambuzi,

Nimechukua hiyo para ya kwanza tu ili tuweze kuijadili kwa marefu na mapana dhana nzima ya haya mabadiliko. Wajumbe wa NEC ambao watakuwa ni full time job ni wa kutoka wilayani tu. So, mawaziri na wabunge bado wana opportunity ya kuingia kwenye NEC na CC kupitia matundu yafuatayo:



Kwa hiyo mawaziri na wabunge bado wanaweza kupitia kwenye tundu la NEC (Taifa), wawakilishi wa wabunge wa CCM au kupitia kwenye Jumuiya za Chama na haswa UWT.

Tatizo la mabadiliko haya ya Katiba, hayalengi kuipatia CCM viongozi waadilifu wala kupunguza mlundikano wa vyeo kwa mtu mmoja. Mfano mdogo tu, je, baada ya haya mabadiliko, Januari Makamba, Mwigulu Nchemba na Chilligati watabaki kuwa wajumbe wa Secretariat ya NEC ambao wanahudhuria vikao vyote na bado ni wabunge? Mwenyekiti wa UWT Taifa ni waziri, mjumbe wa NEC na CC. Anna Makinda ni Mbunge, Spika, Mjumbe wa CC na NEC, Eng. Stella Manyanya ni Mkuu wa Mkoa, Mbunge na Mjumbe wa NEC kupitia UWT.

Katiba za UWT, Wazazi, na UVCCM hazijabadilishwa katika kuweka sifa za wagombea wa ujumbe wa NEC kupitia Jumuiya hizo. Wala wagombea wa NEC Taifa haijasemwa kwamba wasiwe mawaziri. Contradiction iko kwenye kundi la wawakilishi wa wabunge, what if mwakilishi wa wabunge ni Waziri?

Kwa mtazamo wangu, mabadiliko haya hayajafanyiwa kazi kwa kina na kwa umakini. Wangeweka wazi kwamba nafasi za NEC Taifa wabunge wote hawaruhusiwi kugombea. Pia futa kundi la wawakilishi wa wabunge kwenye NEC.

Haya ni matunda ya kushindikana kwa operation vua gamba kwa kuwa tayari Chama kilishatekwa na matajiri na hawajui namna ya kukirudisha kwa walalahoi. Kila njia wanayopendekeza inaonekana kama vile haifanyi kazi. Walianza na kuvua magamba, imeshindwa. Wamekuja na mabadiliko ya Katika, nayo itashindwa bado kuna watu wataendelea kuwa na influence kwenye vikao vya NEC na CC. Mwisho wanataka kuunda Kamati ya Maadili na Nidhamu [ingawa ilikuwepo ambayo ilikuwa inaongozwa na JK]. Sasa kwa sababu JK hataki kuonekana yeye ni mbaya, anataka kusukumia watu wengine wafanye kazi ya kudhibiti mafisadi. Sasa kama NEC na CC wameshindwa kuwadhibiti, hiyo Kamati mpya ya maadili itawezaje kuwashughulikia wale wote ambao wanaonekana kwamba ni magamba?

Keil,

Niwie radhi kama sitaeleweka vizuri kwani sijatulia sana hapa nilipo sasahivi.
Una hoja za msingi sana, kwani ni kweli bado tiba kamili haijapatikana chini ya mabadiliko haya kutibu ugonjwa husika. Nikianza na suala la kina Mwigelu na wenzake ambao kwa sasa ni wabunge na wapo kwenye NEC na CC, kama umeona katika haya mabadiliko, kuna maelezo ambayo yanawakandamiza na mkono wa kulia, halafu yanawanyayua na mkono wa kushoto. Sikumbuki maneno hayo exactly lakini the bottom line ni kwamba kuna ile element ya “unless vinginevyo…”, ikiwa na maana kwamba, pamoja na mabadiliko husika, bado kuna uwezekano wabunge fulani fulani wakaendelea kuwa wajumbe wa NEC iwapo itahitajika hivyo. Hiki ni kigeu geu geu. Lakini iwapo hawatabwebwa na kigeu geu hiki, wabunge hawa ambao kwa sasa ni wajumbe wa NEC na CC wana wakati mgumu sana wa kuchagua kugombea au kutogombea nafasi hizo, kwani come 2015, watakuwa bado ni wajumbe wa NEC hadi 2017, na hii itawapa wapinzani wao ndani ya chama katika kura za maoni huko majimboni, silaha kubwa ya kuwamaliza kisiasa kwa kutumia hoja kwamba kuwa na kofia mbili ‘full time’ kunapunguza ufanisi wa mhusika, ni kinyume na matakwa mapya ya chama n.k.

Pia hoja yako kwamba bado kuna upenyo kwa wabunge na mawaziri kuendelea kuwa wajumbe wa NEC, upo sahihi lakini upenyo huu ni mdogo sana. Kwanza, wakithubutu kugombea ujumbe wa NEC na wakapita, maana yake ni kwamba watakuwa wajumbe wa NEC mpaka 2017. Ikifika uchaguzi mkuu 2015, itakuwa vigumu kwa wao kupita ubunge kwa sababu ambazo tumeshaziona. Unajua wabunge wengi kupenda kuwa NEC kwa sababu, nje ya posho, hiki ndio kikao cha maamuzi kwa mambo kama uteuzi wa wagombea ubunge baada ya kura za maoni, kwa hiyo mbunge akiwa mjumbe NEC, then yupo jikoni nah ii itarahisisha sana kwa jina lake kuteuliwa, ukifananisha na kama atakuwa ni ‘outsider’. Lakini vilevile, ujumbe wa NEC hiyo ndiyo njia pekee ya kujijengea uzoefu ndani ya chama, kitu ambacho kinahitajika sana iwapo una malengo ya kuwania Urais. Ubunge pekee sio kigezo cha ‘uzoefu’ ndani ya chama.

Kitu kingine cha muhimu pia ni kwamba, chini ya mfumo mpya, ushindani kuwania vile viti kumi utakuwa ni kubwa sana, kwani ina maana wanasiasa wote ambao sio wabunge hivi sasa, kina mama a kina kaka na baba watakuwa wanawania hizo nafasi kumi tu. Humo kuna kina mama mbalimbali ambao wana nguvu kisiasa ingawa hawana nguvu UWT, pia kuna vijana ambao wameshavuka miaka 35 n.k. Yote hii itazidi kuwabana wabunge/mawaziri.

Pia suala la viti vya UVCCM NEC kupunguzwaa kutoka 20 hadi 10 ina madhara makubwa sana juu ya nguvu ya jumuiya hii kwenye vikao vya maamuzi, hasa NEC. Hii itaathiri sana vurugu zao ambazo tuliziona kuanzia enzi ya Guninita mpaka miaka sasa. Kwa UWT, kwa kweli pamoja na umuhimu wa wanawake katika siasa zetu, UWT kama taasisi imepoteza sana hadhi na haina influence kubwa both, kwa wanawake wenyewe, na hata katika maamuzi ndani ya vikao vya chama. Hata wanawake wenyewe wanaidharau siku hizi.

Na mwisho ni kuhusu hiyo kamati ya nidhamu. Upo sahihi kwani Kamati Kuu chini ya katiba iliyopo ina meno ya kumfukuza mtu yoyote. Ibara ya kumi sehemu ya 7 inasema kwamba kazi ya kamati kuu itakuwa pamoja na: “Kumsimamisha uongozi kiongozi yeyote isipokuwa mwenyekiti wa CCM na makamo mwenyekiti endapo itaridhika kwamba tabia na mwenendo wake vinamwondolea sifa za uongozi.”

Sasa suala la kuunda kamati mpya ya nidhamu inatoa tafsiri kwamba ndani ya CCM kuna viongozi ambao wapo juu ya mwenyekiti na makamo mwenyekiti wa chama, hivyo kamati kuu pia haiwezi kuwagusa hawa pia.
 
Mfumo wa Uhongaji ndani ya CCM hauhitaji uwepo wa mhusika mkuu, bali ni swala la mhusika mkuu kutafuta mtu wake na kuhakikisha kwamba anasimamia kila kitu ili kuhakikisha kwamba mgombea wao anashinda.

Mfumo huu wa sasa utawabeba wenye fedha tu!! Unajua wajumbe wengi kule mawilayani hawakuingia katika nafasi hizo kupigania chama bali kutafuta ulaji. Ndiyo maana katika kura za maoni pesa inatembea katika majimbo kama njugu. Sasa wameongezewa tena kiosk kingine cha wajumbe wa NEC. Hvyo wanaotaka nafasi watapaswa kuwa na fedha ili kuchaguliwa mawilayani. Kama hawana fedha itabidi watafute mapema godfather. Hapo ndipo hao wazee watakapoingia. Wao wala hawataenda mawilayani. siku hizi mpaka m pesa na tigo pesa zinapeleka hela. Unadhani nani ata monitor mambo haya?
 
Mfumo huu wa sasa utawabeba wenye fedha tu!! Unajua wajumbe wengi kule mawilayani hawakuingia katika nafasi hizo kupigania chama bali kutafuta ulaji. Ndiyo maana katika kura za maoni pesa inatembea katika majimbo kama njugu. Sasa wameongezewa tena kiosk kingine cha wajumbe wa NEC. Hvyo wanaotaka nafasi watapaswa kuwa na fedha ili kuchaguliwa mawilayani. Kama hawana fedha itabidi watafute mapema godfather. Hapo ndipo hao wazee watakapoingia. Wao wala hawataenda mawilayani. siku hizi mpaka m pesa na tigo pesa zinapeleka hela. Unadhani nani ata monitor mambo haya?

Well said.
 
Mkuu Mchambuzi,

Nimekupata vyema, ngoja tusubiri kama mabadiliko haya yatasaidia kupunguza nguvu za wagombea urais kwenye vikao vya juu NEC na CC.

CCM mna kazi ngumu ya kukirejesha chama kwa wanachama. Kwa sasa chama kimetekwa na wenye fedha na hawako tayari kukiacha na ndio maana wenye fedha na viongozi wa juu wa chama wamewekana "mateka", kwamba mkinitema nitawalipua na viongozi nao wanaogopa kulipuliwa, maana wataishia kuumbuka.

Kaazi kweli kweli!
 
Mfumo huu wa sasa utawabeba wenye fedha tu!! Unajua wajumbe wengi kule mawilayani hawakuingia katika nafasi hizo kupigania chama bali kutafuta ulaji. Ndiyo maana katika kura za maoni pesa inatembea katika majimbo kama njugu. Sasa wameongezewa tena kiosk kingine cha wajumbe wa NEC. Hvyo wanaotaka nafasi watapaswa kuwa na fedha ili kuchaguliwa mawilayani. Kama hawana fedha itabidi watafute mapema godfather. Hapo ndipo hao wazee watakapoingia. Wao wala hawataenda mawilayani. siku hizi mpaka m pesa na tigo pesa zinapeleka hela. Unadhani nani ata monitor mambo haya?

Salama ya CCM ni kwamba influence yake kwa siasa za nchi hii inaporomoka kwa kasi sana kwa hiyo baada ya miaka michache ni watu wachache watavutiwa kutafuta vyeo vya kisiasa kupitia CCM. Mimi naona uamuzi wa kuwa na wajumbe wa NEC kuanzia ngazi ya wilaya hauna maana sana sana wanajiongezea gharama za uendeshaji wa chama,ambazo zitakuja kuwa shubiri ukizingatia kuporomoka kwa umaarufu wa chama na zaidi ikitokea kikaondolewa madarakani.
 
Back
Top Bottom