MawazoMatatu
JF-Expert Member
- Sep 6, 2008
- 505
- 61
TAHADHALI: MTUNDIKO HUU UMETOLEWA KWENYE GAZETI KAMA HAUPENDI MITUNDIKO TOKA MAGAZETINI TAFADHALI ENDELEA NA MITUNDIKO MINGINE!
MWENENDO wa mambo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unazidi kuwa tete, baada ya makada wa chama hicho kushindwa kuvumiliana na kuanza kushambuliana katika vikao mbali mbali vya chama hicho na katika mikutano ya hadhara.
Taarifa za karibuni zinazothibitisha kuwepo kwa hali hiyo, iliifikia Tanzania Daima Jumatano kutoka ndani ya kikao cha wabunge wa CCM kilichofanyika Februari 5 katika ukumbi wa Pius Msekwa ulio ndani ya eneo la Bunge mjini Dodoma.
Taarifa hizo zilieleza kuwa katika kikao hicho kilichokuwa kikiongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Mbunge wa Mvomero, Suleiman Sadiq, alimshutumu Mweka Hazina wa CCM, Amos Makala, kuwa anatumia vibaya madaraka yake kwa kufuja mamilioni ya fedha za chama kwa masilahi yake binafsi.
1.Habari ambazo gazeti hili limezipata kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa kikao hicho kiliitishwa mahususi kwa ajili ya kuwajadili wabunge wawili wa kambi ya upinzani, Dk. Willbrod Slaa, (CHADEMA) na Hamad Rashid (CUF).
Wabunge hao ambao ni viongozi wa kambi ya upinzani waliandaliwa ajenda maalumu ya kuwajadili kuhusiana na nia zao za kuwasilisha hoja binafsi zilinazowahusu viongozi wa sasa wa serikali.
Ilielezwa kuwa, katika kikao hicho, wabunge wa CCM walikuwa wakitafuta msimamo wa pamoja wa namna na kumdhibiti Dk. Slaa atapowasilisha hoja binafsi inayotaka maelezo ya serikali kuhusu hatua ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurence Masha, kuingilia mkachato wa utengenezaji wa vitambulisho vya taifa.
Mbali na Dk. Slaa, kikao hicho pia 2.kilijadili namna ya kumdhibiti kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Hamad Rashid, atakapowasilisha hoja yake binafsi ya kutaka rais apunguziwe madaraka.
Ajenda nyingine, ilikuwa ni 4.kujadili malalamiko kutoka kwa Sadiq kuhusu matumizi makubwa yanayofanywa na mweka hazina wa chama hicho anapokuwa katika safari zake binafsi.
Mmoja wa wabunge wa CCM aliyekuwa ndani ya kikao hicho alilieleza gazeti hili, kuwa ingawa ajenda muhimu katika kikao hicho zilikuwa mbili, za Dk. Slaa na Hamad Rashid zilifunikwa na ajenda ya matumuzi makubwa ya fedha za chama, ambapo Mbunge Sadiq alionya kuwa iwapo hali hiyo haitakemewa na viongozi wakuu wa chama, yeye atalipeleka kwa wananchi.
Alisema, baadhi wa wabunge walikuwa wakitoa tuhuma kwa viongozi wa juu wa CCM kutumia mamilioni ya fedha kwa ajili ya masilahi yao binafsi pasipo kuwataja majina, lakini Sadiq alimtaja moja kwa moja Makala na kutangaza kupambana naye iwapo ataachwa aendelee kuchezea fedha za chama.
Aliyechafua upepo ndani ya kikao ni Sadiq, alisimama na kumwambia waziri mkuu kuwa Makala anatumia fedha za chama kwa masilahi yake binafsi, alisema kwa ukali kwamba kundi la wana CCM wanaochukua fedha za chama na kuzitumia kupandikiza watu wa kuwangoa baadhi ya wabunge katika majimbo wasifikiri kwamba wabunge wanaowaandama hawana fedha.
Alimtuhumu moja kwa moja Makala kuwa katumia zaidi ya sh milioni 100 za chama kuendesha kampeni katika jimbo analolishikilia la Mvomero na kuonya kuwa yeye ana pesa nyingi zaidi ya hizo, hivyo atakapoanza kujibu mapigo kwa kumwaga fedha, kiongozi yeyote wa CCM asimuulize, kwa sababu hatarudi nyuma na akisumbuliwa atakihama chama kwa sababu ana uhakika wa kushinda ubunge akiwa katika chama chochote, alisema mbunge huyo.
Vyanzo vingine vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vilieleza kuwa baadhi ya wabunge walieleza wasiwasi wao kuhusu matumizi makubwa ya fedha za chama hicho na kwamba jambo hilo linawatia mashaka wanachama ambao wamekuwa wakiwahoji wanapokuwa majimboni kuwa viongozi wa CCM wanapata wapi mamilioni hayo ya fedha.
Wasiwasi wetu wabunge ni wananchi, huko majimboni wanahoji kama CCM si mafisadi, tunatoa wapi mamilioni ambayo baadhi ya viongozi wa chama wanayatumia kupiga kampeni kwenye baadhi ya majimbo wakati hata muda wa kampeni haujafika?
Itakuwa ni aibu kubwa kama itagundulika kuwa chama chetu kinahusika na ufisadi wakati hivi sasa tunakanusha, tena kwa nguvu. Ingawa sababu kubwa ni woga wa baadhi ya wabunge kunyanganywa majimbo yao na mafisadi, lakini ni ukweli viongozi wa chama wanatumia vibaya fedha za chama kwa sababu huwa hazikaguliwi, kilisema chanzo kingine cha habari hizi.
Alipoulizwa kuthibitisha kama alitoa kauli hizo katika kikao hicho, Sadiq alijibu kwa ukali: Wewe umeyajuaje mambo yaliyozungumzwa ndani ya kikao chetu, hayo ni mambo yetu ya ndani na wala hupaswi kabisa kuyajua wewe, nenda kwa hao hao wanaona ajabu mtu kueleza kile alichonacho moyoni kwa lengo la kukijenga chama, alijibu kwa ukali huku akiondoka.
Malalamiko ya baadhi ya wabunge wa CCM kuhusu baadhi ya makada wa chama hicho wenye ukwasi wa kutisha kuanza kampeni za uchaguzi mapema huku wengine wakidai wanaandaliwa mkakati wa kuwaangusha katika uchaguzi mkuu yamekuwepo kwa muda sasa.
Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ni mmoja wa wana CCM waliokwisha kusikika akilalamika kuchezewa mchezo mchafu na watu aliodai kuwa ni wapinzani wake kisiasa ndani ya chama hicho, ambao kwa kutumia utajiri mkubwa wa fedha walizonazo, wamekuwa wakiendesha kampeni chafu dhidi yake, ikiwemo kumuweka mtu atakayempinga katika uchaguzi mkuu ujao.
MWENENDO wa mambo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unazidi kuwa tete, baada ya makada wa chama hicho kushindwa kuvumiliana na kuanza kushambuliana katika vikao mbali mbali vya chama hicho na katika mikutano ya hadhara.
Taarifa za karibuni zinazothibitisha kuwepo kwa hali hiyo, iliifikia Tanzania Daima Jumatano kutoka ndani ya kikao cha wabunge wa CCM kilichofanyika Februari 5 katika ukumbi wa Pius Msekwa ulio ndani ya eneo la Bunge mjini Dodoma.
Taarifa hizo zilieleza kuwa katika kikao hicho kilichokuwa kikiongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Mbunge wa Mvomero, Suleiman Sadiq, alimshutumu Mweka Hazina wa CCM, Amos Makala, kuwa anatumia vibaya madaraka yake kwa kufuja mamilioni ya fedha za chama kwa masilahi yake binafsi.
1.Habari ambazo gazeti hili limezipata kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa kikao hicho kiliitishwa mahususi kwa ajili ya kuwajadili wabunge wawili wa kambi ya upinzani, Dk. Willbrod Slaa, (CHADEMA) na Hamad Rashid (CUF).
Wabunge hao ambao ni viongozi wa kambi ya upinzani waliandaliwa ajenda maalumu ya kuwajadili kuhusiana na nia zao za kuwasilisha hoja binafsi zilinazowahusu viongozi wa sasa wa serikali.
Ilielezwa kuwa, katika kikao hicho, wabunge wa CCM walikuwa wakitafuta msimamo wa pamoja wa namna na kumdhibiti Dk. Slaa atapowasilisha hoja binafsi inayotaka maelezo ya serikali kuhusu hatua ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Laurence Masha, kuingilia mkachato wa utengenezaji wa vitambulisho vya taifa.
Mbali na Dk. Slaa, kikao hicho pia 2.kilijadili namna ya kumdhibiti kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Hamad Rashid, atakapowasilisha hoja yake binafsi ya kutaka rais apunguziwe madaraka.
Ajenda nyingine, ilikuwa ni 4.kujadili malalamiko kutoka kwa Sadiq kuhusu matumizi makubwa yanayofanywa na mweka hazina wa chama hicho anapokuwa katika safari zake binafsi.
Mmoja wa wabunge wa CCM aliyekuwa ndani ya kikao hicho alilieleza gazeti hili, kuwa ingawa ajenda muhimu katika kikao hicho zilikuwa mbili, za Dk. Slaa na Hamad Rashid zilifunikwa na ajenda ya matumuzi makubwa ya fedha za chama, ambapo Mbunge Sadiq alionya kuwa iwapo hali hiyo haitakemewa na viongozi wakuu wa chama, yeye atalipeleka kwa wananchi.
Alisema, baadhi wa wabunge walikuwa wakitoa tuhuma kwa viongozi wa juu wa CCM kutumia mamilioni ya fedha kwa ajili ya masilahi yao binafsi pasipo kuwataja majina, lakini Sadiq alimtaja moja kwa moja Makala na kutangaza kupambana naye iwapo ataachwa aendelee kuchezea fedha za chama.
Aliyechafua upepo ndani ya kikao ni Sadiq, alisimama na kumwambia waziri mkuu kuwa Makala anatumia fedha za chama kwa masilahi yake binafsi, alisema kwa ukali kwamba kundi la wana CCM wanaochukua fedha za chama na kuzitumia kupandikiza watu wa kuwangoa baadhi ya wabunge katika majimbo wasifikiri kwamba wabunge wanaowaandama hawana fedha.
Alimtuhumu moja kwa moja Makala kuwa katumia zaidi ya sh milioni 100 za chama kuendesha kampeni katika jimbo analolishikilia la Mvomero na kuonya kuwa yeye ana pesa nyingi zaidi ya hizo, hivyo atakapoanza kujibu mapigo kwa kumwaga fedha, kiongozi yeyote wa CCM asimuulize, kwa sababu hatarudi nyuma na akisumbuliwa atakihama chama kwa sababu ana uhakika wa kushinda ubunge akiwa katika chama chochote, alisema mbunge huyo.
Vyanzo vingine vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vilieleza kuwa baadhi ya wabunge walieleza wasiwasi wao kuhusu matumizi makubwa ya fedha za chama hicho na kwamba jambo hilo linawatia mashaka wanachama ambao wamekuwa wakiwahoji wanapokuwa majimboni kuwa viongozi wa CCM wanapata wapi mamilioni hayo ya fedha.
Wasiwasi wetu wabunge ni wananchi, huko majimboni wanahoji kama CCM si mafisadi, tunatoa wapi mamilioni ambayo baadhi ya viongozi wa chama wanayatumia kupiga kampeni kwenye baadhi ya majimbo wakati hata muda wa kampeni haujafika?
Itakuwa ni aibu kubwa kama itagundulika kuwa chama chetu kinahusika na ufisadi wakati hivi sasa tunakanusha, tena kwa nguvu. Ingawa sababu kubwa ni woga wa baadhi ya wabunge kunyanganywa majimbo yao na mafisadi, lakini ni ukweli viongozi wa chama wanatumia vibaya fedha za chama kwa sababu huwa hazikaguliwi, kilisema chanzo kingine cha habari hizi.
Alipoulizwa kuthibitisha kama alitoa kauli hizo katika kikao hicho, Sadiq alijibu kwa ukali: Wewe umeyajuaje mambo yaliyozungumzwa ndani ya kikao chetu, hayo ni mambo yetu ya ndani na wala hupaswi kabisa kuyajua wewe, nenda kwa hao hao wanaona ajabu mtu kueleza kile alichonacho moyoni kwa lengo la kukijenga chama, alijibu kwa ukali huku akiondoka.
Malalamiko ya baadhi ya wabunge wa CCM kuhusu baadhi ya makada wa chama hicho wenye ukwasi wa kutisha kuanza kampeni za uchaguzi mapema huku wengine wakidai wanaandaliwa mkakati wa kuwaangusha katika uchaguzi mkuu yamekuwepo kwa muda sasa.
Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ni mmoja wa wana CCM waliokwisha kusikika akilalamika kuchezewa mchezo mchafu na watu aliodai kuwa ni wapinzani wake kisiasa ndani ya chama hicho, ambao kwa kutumia utajiri mkubwa wa fedha walizonazo, wamekuwa wakiendesha kampeni chafu dhidi yake, ikiwemo kumuweka mtu atakayempinga katika uchaguzi mkuu ujao.