Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Tatizo si Upinzani, CCM haitaondolewa madarakani kwa njia ya kura - huu ndio ukweli!
Naam, huo ndio ukweli ingawa mchungu, CCM hawako tayari kuachia madaraka kwa njia ya amani, period. CCM inaamini kuwa ina hati miliki katika uongozi wa taifa la Tanzania na iko tayari kutumia kila linalowezekana kuilinda inachodai ni haki hiyo hata kama kwa kufanya hivyo inavunja sheria. Kuna mifano michache inayoonyesha kuwa CCM iko tayari kufanya chochote kile kuwalinda wafadhili wake hata ikibidi kumtoa kafara mwananchi yeyote yule anayekuwa tishio kwake.
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CCM. Horace Kolimba alipojaribu kuikaba CCM kwa uongozi usio na dira na kukataa kusalimu amri mbele ya kikao maalum Dodoma, alipotelea mbali. Baba wa taifa alipoonekana amekuwa mwiba kwani alianza kuukandia wazi wazi uongozi wa CCM, hakuishi kushuhudia uchaguzi wa 2000 ambao nina hakika haungemrudisha Mkapa madarakani. Kwa kuwa hawa wawili walikuwa hawawezi kununulika, CCM haikuwa na njia bali kuhakikisha sauti zao hazisikiki tena.
Lakini kwa walioweza kununulika ama kutishwa kama Edward Barongo kazi ilikuwa ndogo tu na hii leo idadi ya watu kama hao inaongezeka kila kukicha. Ndani ya CCM wapo wanaopayuka bungeni na kuitwa wapiganaji ndani ya chama lakini wanapowekwa kiti moto kwenye vikao wananywea kama vile hawapo. Ndani ya Upinzani wapo pia wanaochachamaa na kuleta matumaini kwa taifa lakini moto wao huanza kufifia ama kwa kumeza ndoana au kukosa ujasiri kama wa Mbunge wa Kararu (heko Dr. Slaa).
Wana JF kubaki madarakani kwa CCM kumekuwa jambo la kufa na kupona kwani hatma ya taifa waliokabidhiwa wameiweka rehani kwa wenye fedha kwa tamaa ya mali. Matokeo yake hawafanyi kitu bali kwa maagizo ya waliowaweka madarakani na uchaguzi hauna maana tena. Bunge linafanya kazi kama kamati ya CCM na mahakama imedhihirika inatoa maamuzi kwa maelekezo ya CCM. Juzi tumemshuhudia Tendwa wa ofisi ya msajili naye akitekeleza matakwa ya CCM na hivo hivyo Jaji Makame wa tume ya uchaguzi.
Kwa kuwa ni wazi CCM haiwezi kuondolewa madarakani kwa njia ya kura, ni njia moja tu tunayo - mapinduzi, kwani tunashuhudia watawala wetu wanaanza kuwapandikiza watoto wao na vijukuu vyao madarakani. Lazima ama tuachane na woga au tukubali kuwa watumwa ndani ya ardhi yetu wenyewe. Bila mapinduzi Marekani, Urusi na Ufaransa zingekuwa wapi ? Nina hakika wananchi wanaochukia ufisadi ni wengi ila woga wao ndio unaowafanya wawe wanyonge na kuwalamba miguu akina Jeetu Patel - vya bure vina gharama.
Naam, huo ndio ukweli ingawa mchungu, CCM hawako tayari kuachia madaraka kwa njia ya amani, period. CCM inaamini kuwa ina hati miliki katika uongozi wa taifa la Tanzania na iko tayari kutumia kila linalowezekana kuilinda inachodai ni haki hiyo hata kama kwa kufanya hivyo inavunja sheria. Kuna mifano michache inayoonyesha kuwa CCM iko tayari kufanya chochote kile kuwalinda wafadhili wake hata ikibidi kumtoa kafara mwananchi yeyote yule anayekuwa tishio kwake.
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CCM. Horace Kolimba alipojaribu kuikaba CCM kwa uongozi usio na dira na kukataa kusalimu amri mbele ya kikao maalum Dodoma, alipotelea mbali. Baba wa taifa alipoonekana amekuwa mwiba kwani alianza kuukandia wazi wazi uongozi wa CCM, hakuishi kushuhudia uchaguzi wa 2000 ambao nina hakika haungemrudisha Mkapa madarakani. Kwa kuwa hawa wawili walikuwa hawawezi kununulika, CCM haikuwa na njia bali kuhakikisha sauti zao hazisikiki tena.
Lakini kwa walioweza kununulika ama kutishwa kama Edward Barongo kazi ilikuwa ndogo tu na hii leo idadi ya watu kama hao inaongezeka kila kukicha. Ndani ya CCM wapo wanaopayuka bungeni na kuitwa wapiganaji ndani ya chama lakini wanapowekwa kiti moto kwenye vikao wananywea kama vile hawapo. Ndani ya Upinzani wapo pia wanaochachamaa na kuleta matumaini kwa taifa lakini moto wao huanza kufifia ama kwa kumeza ndoana au kukosa ujasiri kama wa Mbunge wa Kararu (heko Dr. Slaa).
Wana JF kubaki madarakani kwa CCM kumekuwa jambo la kufa na kupona kwani hatma ya taifa waliokabidhiwa wameiweka rehani kwa wenye fedha kwa tamaa ya mali. Matokeo yake hawafanyi kitu bali kwa maagizo ya waliowaweka madarakani na uchaguzi hauna maana tena. Bunge linafanya kazi kama kamati ya CCM na mahakama imedhihirika inatoa maamuzi kwa maelekezo ya CCM. Juzi tumemshuhudia Tendwa wa ofisi ya msajili naye akitekeleza matakwa ya CCM na hivo hivyo Jaji Makame wa tume ya uchaguzi.
Kwa kuwa ni wazi CCM haiwezi kuondolewa madarakani kwa njia ya kura, ni njia moja tu tunayo - mapinduzi, kwani tunashuhudia watawala wetu wanaanza kuwapandikiza watoto wao na vijukuu vyao madarakani. Lazima ama tuachane na woga au tukubali kuwa watumwa ndani ya ardhi yetu wenyewe. Bila mapinduzi Marekani, Urusi na Ufaransa zingekuwa wapi ? Nina hakika wananchi wanaochukia ufisadi ni wengi ila woga wao ndio unaowafanya wawe wanyonge na kuwalamba miguu akina Jeetu Patel - vya bure vina gharama.