Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,466
- 113,548
Wanabodi,
Katika mapumziko ya long week-end hii, nilipata kajinafasi, nikaamua kubadili upepo, this time, nikaenda mitaa ya Moshi Vijijini,
Nilianzia Njia Panda, nikapandisha Marangu, nikasimama kidogo Marangu Mtoni, Mamba na kupanda juu mpaka kule Marangu National Park. Kesho yake nikateremkia Kilema, kupitia bara bara ya Kawawa, nikaanzia Legho Kilema, nikaja Legho, Iwa Mission, nikaremkia Nduoni, nikashuka Tella, nikapita Sumi, nikaja Uparo na kuchomokea Kawawa Rd inapoungana na barabara ya Moshi Dar.
Nilifanya hojaji isiyo rasmi kuhusu watanchagua nani, huwezi amini, asilimia klubwa chaguo lao ni Mrema, CCM hawana kitu kabisa. Mtu wa pili kwa kukubalika ni mgombea wa Chadema akifuatiwa na NCCR -Mageuzi.
Imani kubwa waliyonayo ndugu zangu hawa kwa Lyatonga, bado wanaamini anaweza kufanya mambo. Hawajaamini kuwa amechoka, hana sera wala hana jipya ukilinganisha na yule wa Chadema. Wachagga wanachagua mtu, siyo chama, siyo sera, siyo uwezo, bali jina, na kwa Moshi Vijijini, mtu wao ni Mrema, Hawaoni hawaskii wala mtu hawaambii kitu!, kama ilivyo kwa Ndesa na jimbo la Moshi Mjini.
Cha ajabu anachokifanya Mrema huyu, sio tuu anajipigia debe kuchaguliwa, bali anampigia chapuo la kiaina JK, kwamba ubunge mnichague mimi, ila kura za urais, mchagueni Kikwete!.
Licha ya chama chake kuweka mgombea urais, na kuzinduliwa kwa kampeni zao jijini, Mrema kama Mwenyekiti wa chama, alipaswa kuwepo, lakini yeye alikacha, akiendelea na kampeni zake kule Kiraracha!.
Angalizo, TLP, CHADEMA na NCCR, wasijeishia kugawana kura kama vita vya panzi, na furaha ikawa ni kwa kunguru!
Katika mapumziko ya long week-end hii, nilipata kajinafasi, nikaamua kubadili upepo, this time, nikaenda mitaa ya Moshi Vijijini,
Nilianzia Njia Panda, nikapandisha Marangu, nikasimama kidogo Marangu Mtoni, Mamba na kupanda juu mpaka kule Marangu National Park. Kesho yake nikateremkia Kilema, kupitia bara bara ya Kawawa, nikaanzia Legho Kilema, nikaja Legho, Iwa Mission, nikaremkia Nduoni, nikashuka Tella, nikapita Sumi, nikaja Uparo na kuchomokea Kawawa Rd inapoungana na barabara ya Moshi Dar.
Nilifanya hojaji isiyo rasmi kuhusu watanchagua nani, huwezi amini, asilimia klubwa chaguo lao ni Mrema, CCM hawana kitu kabisa. Mtu wa pili kwa kukubalika ni mgombea wa Chadema akifuatiwa na NCCR -Mageuzi.
Imani kubwa waliyonayo ndugu zangu hawa kwa Lyatonga, bado wanaamini anaweza kufanya mambo. Hawajaamini kuwa amechoka, hana sera wala hana jipya ukilinganisha na yule wa Chadema. Wachagga wanachagua mtu, siyo chama, siyo sera, siyo uwezo, bali jina, na kwa Moshi Vijijini, mtu wao ni Mrema, Hawaoni hawaskii wala mtu hawaambii kitu!, kama ilivyo kwa Ndesa na jimbo la Moshi Mjini.
Cha ajabu anachokifanya Mrema huyu, sio tuu anajipigia debe kuchaguliwa, bali anampigia chapuo la kiaina JK, kwamba ubunge mnichague mimi, ila kura za urais, mchagueni Kikwete!.
Licha ya chama chake kuweka mgombea urais, na kuzinduliwa kwa kampeni zao jijini, Mrema kama Mwenyekiti wa chama, alipaswa kuwepo, lakini yeye alikacha, akiendelea na kampeni zake kule Kiraracha!.
Angalizo, TLP, CHADEMA na NCCR, wasijeishia kugawana kura kama vita vya panzi, na furaha ikawa ni kwa kunguru!