CCM kumeguka ni muhimu kwa Taifa!

Mkuu Kitila,

Heshima mbele, maneno yako mengi ni ya kishujaa sana, kuna mzee mmoja aliyekwua CCM aliyafuata maneno yako exactly, akajiunga na waasisi wa upinzani na kuanzisha upinzani, akiwa CCM alikuwa vyeo vingi vya bure hasa kwenye bodi ili kumpa kula, alipotoka tu CCM wakamnyofoa vyote, na kubaki tupu!

Ambacho hakujua ni kwamba wenziwe wote aliojiunga nao, either walikuwa wameshachota kule CCM na kuwa na miradi binafsi mikubwa kwa hiyo hawakuwa na wasi wasi na mlo, au wengine walikuwa ni mapandikizi wa CCM tu, masikini mzee wa watu akaishia kua lofa hoe hae huku wenziwe wakipeta tu, siku moja mdogo wake ambaye naye alikuwa na vyeo huko CCM, naye akawa frustrated kidogo na Diria, akaamua kutoka na kuingia upinzani,

Ninakumbuka huyu mzee, yaani kaka mtu akimlilia sana mdogo wake asifanye, makosa kama yake ya kurukia upinzani na abaki huko huko CCM, maana wakati bado, alsema nilifikiri wakati ulikuwa umefika, lakini sikuwa-read vizuri wananchi wa Tanzania kwamba bado hawako tayari kwa mabadiliko.

Ninamkumbuka sana huyu mzee, ambaye sasa ni marehemu, maneno yako Kitila ni ya kishujaa sana, lakini sio kwa mazingara ya bongo, sawa kama unavyosema kwamba ni vyema kuwa-recruit wapya kwa ajili ya the future, ni idea ambayo hapa JF kwenye quick fix kama za Europe na USA, haikubaliki kwa hiyo ni kaaazi kweli kweli!

Mzee FMES,

Kwanza naomba usichukulie binafsi kutumia maneno yako kujenga hoja zangu kuwa ni vita baridi, maana hapa watu hawachelewi kuanzisha zogo!

nikirudi kwenye jibu lako kwa Kitila, kinachonitatiza kutokana na kauli yako ambayo ndiyo hali halisi ya mfumo wetu wa Siasa na Uongozi ni ile dhana ya kusema mtu anakuwa mwanasiasa au kiongozi ile "ale" au ajipatie!

Je kujituma na kutumikia Taifa kuna nafasi gani tena? Jee kulitumikia Taifa kwa moyo kwa kuwa mtu ni mzalendo na mwaminifu wa nchi yake kunageuzwaje kuwa mradi wa kujipatia mali?

Nafahamu fika wewe ni mmoja wa wale wanaolipinga Azimio la Arusha, ingawa sijawahi kuelewa kwa maoni yako ni kwa nini unalipinga Azimio la Arusha. Lakini nitakuambia hivi, kwenye Azimio la Arusha ambalo lilivunjwa kwa kuundwa kwa Azimio la Zanzibar, ndiko kulikoandikwa miiko ya uongozi kuzuia watu kukimbilia uongozi kuwa ni sehemu ya kujipatia kipato ama kwa kutumia nafasi zao za kazi au kujipangia manufaa ya binafsi na si ya Taifa.

Huyo mzee unayemzungumzia, namfahamu, nami nilishawahi kumpa saluti yangu kwa kuwa jasiri na kwenda Upinzani.

Tatizo la uoga na unafiki wa WanaCCM wengi ambao ni viongozi, wabunge na wawakilishi ni kuwa wamekimbilia kazi zao si kulitumikia Taifa, bali ni kujipatia kipato na kushughulikia maslahi binafsi!

Hili ndilo tatizo kuu na ndio maana wengi wao wanaingia kwenye mtego wa kuogopa kuihama CCM au kufa masikini kwa kuwa wameshajenga nadharia kuwa ni lazima wawe na mali nyingi au uhakika wa mali na mapato ili waweze kulitumikia Taifa.

Badala ya Viongozi na WanaCCM kufanya kazi na kulitumikia Taifa na kuacha mapato au kipato kiwe matokeo ya kazi zao, wao wameweka maslahi na kipato mstari wa mbele kuwa ni muhimi kabla ya kufanya kazi yeyote.

Ndio maana niliposema CCM ni adui wa Maendeleo ya Tanzania na Watanzania ni kutokana na hii sasabu nyingine iliyozaa utamaduni wa watu kukimbilia siasa kama tegemeo pekee la kujipatia MAISHA BORA.

Ugonjwa na Utamaduni huu umeliharibu Taifa letu. Kama Mwanakijiji alivyoeleza, Watanzania tumeshazoea kuishi KIFISADI na KIHUJUMU na hivyo vita dhidi ya Ufisadi na Uhujumu inakuwa ngumu kwa kuwa tumefanya mazoea ya kuishi kwa kutegemea mapato ya ziada na ya ujanja ujanja na si kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

Narudia tena nilichomwambia Pasco na wewe kuwa ni mpaka pale baadhi ya Viongozi waasisi na walioko madarakani wa CCM watakapoachana na woga na kuukumbatia Utamaduni huu mbovu wa unyonge wa mali kuwa ndio kigezo cha kuogopa kuondoka CCM na kufanya kilicho sahihi, Tanzania kamwe haitaweza kuendelea au kupata mafanikio inayoyataka.

Utamaduni huu pamoja na kuwa unawaathiri Watanzania wengi hata wale walioko katika vyama vya upinzani, lakini kama tunataka uharamia huu uishe mara moja na si kutumia miaka 100 kubadilika, atakayeweza kulibadili hili na kufuatwa kwa urahisi kabisa ni CCM!

Ndiyo maana nimekuwa mkali kwa wanaojiita CCM mageuzi kwa kuwa wanaukumbuatia mfumo mbovu kulitumikia Taifa!
 
1.
FMES,

Kwa nini unavunjika moyo kirahisi na kuruhusu adui akuvuruge akili kwa vitisho? Ulichokisema hapa cha kina mke wa Mao na wenzake, ndicho kinachotumiwa na CCM kukaba makoo kina Mwakyembe, Killango, Seleli, Manyanya na wengine wanaotaka kuachana na mfumo butu na chama sakala.

- Unajua mkuu Rev, ninasikitishwa na tabia moja ya ajabu sana, kwamba nikitoa mawazo yangu, yanakuwa ya CCM au ya Kiongozi flani, lakini ya kwako yanakua ya kwako, WHY is that? Ni wapi unapopajua upaweke hapa JF as ushahidi kwamba CCM imewahi kutumia kundi la wanne kule China kama fimbo against hao viongozi uliowataja?

- Kwamba nimevunjika moyo? Hapana I am being reelistic baada ya kuona mifano mingi sana bongo, nimewaona kina Mrema wakijitolea kufa na kupona, na wananchi walivyoshia kuwabeza kama ni vichaa!, Nimeona Kasaka Njelu, akisimama kidete na kudai Tanganyika in the process akiwakusanya wananchi wengi nyuma yake, na nimemuona akiingia mitini kimya kimya baada ya kupewa cheo na CCM hakuna cha Tanganyika wala kudai mabadiliko, nimewaona wananchi wakiwakimbia kina Ngaiza walioyataka kuwaokoa,

- Ninaifahamu vizuri sana siasa na tabia za wananchi wa bongo, ndio maana sishangazwi na maneno mengi hapa ya kishujaa ya kuwatukana kina Mwakyembe, wanaojitahidi angalu to do something kuliko kupiga domo hapa JF, mkuu ndio kwanza nimemaliza kampeni yangu ya OIC ambapo nimeweza kuwa-reach out viongozi karibu 80% wa NEC, niliyopambana nayo mengine ni aibu hata kusema jinsi hawa viongozi wetu wasivyoelewa, recently nime- spent a lot of hours kwenye ofisi za OIC kujifunza exactly who they are na kujaribu kuwaelimisha wanaohusika, ndio maana ninakataa kujivika mkenge kuhusu wananchi wa bongo, kusema hapa JF ni one thing na kutimiza katika bongo ni another story of its own, muulize Kitine unajua siku hizi hata viongozi humkimbia kwa kuogopa wasionekane naye mbele ya public, that is bongo yaani Tanzania, that is what we are sasa naishndwa kuelewa mawazo kama yako yanaweza kufanyika boingo hii ya sasa au wapi?

- Nimesikia mara kwa mara, kwamba wananfunzi wa Mlimani huwa wanazuiwa wasiandamane maana wakifika mitaani wananchi watajiunga nao, nonesense! Nimeona under Mwinyi wananfunzi wakiandamana kupitia mitaani mpaka kufika Wizara ya elimu ya juu, hakuna mwananchi hata mmoja aliyejiunga, nimeona wananchi wakiwazomea kuwa ni wajinga, huku FFU wakiwala fimbo!

- Kama haya yote hayakutoshi, nilipokuwa Secondari nilikuwa kiongozi wa upinzani wa kila kitu kisichofaa, kuanzia chakula kibovu, kulimishwa kama mbwa, kutoruhusiwa kwenda mjini week end, one time nilianzisha mpaka mgomo wa chakula na kulima, mambo yalipochacha wanafunzi wote wakanikimbia nikabaki peke yangu mbele ya Pilato, wakanitisha weee lakini walipoona sibadiliki, Pilato akamua ku-make a deal kwamba sitaguswa tena ninaweza kufanya ninalotaka mradi tu niwape heshima waalimu na nisiwashawishi na wengine, yes form that day I was free, jamaa wakienda kulima mimi naingia town, chakula nikawekwa permanent kwenye list ya maseule mpaka miaka mitatu yangu liyobaki ya kumaliza shule,

Kwa hiyo mkuu hii njia ya upinzani na bongo ninaifahamu vizuri sana kwa sababu nimeipitia mara nyingi sana, ndio maana ninaishi na realities za bongo sio imagination!
 
Rev. Kishoka,
Mkuu taratibu mkuu wangu taratibu.... ebu pumua kidogo kabla hujasoma yangu maanake nataka utazame upande wa pili wa shilingi hiyo ya watu kama Field Marshall Es..
Nitakupa mfano wa dini yako mwenyewe ambayo nina hakika wewe ni Rev na utaweze kunipa somo vizuri..
Hivi kama viongozi wa Kanisa wakiwa na mapungufu yote uliyoyaandika hapo juu... wewe kama muumini wa dini ya Kikristu utajiondoa ktk dini hiyo kwa sababu ya matendo ya viongozi hao!
Je, Biblia uliyofundishwa itakuwa na mafundisho yapi muhimu ktk kukuongoza wewe ikiwa matendo ya binadamu wachache waliochaguliwa ama kubahatika kuongoza ndio wametumia vibaya msahafu huo kujineemesha..
Navyofahamu mimi mtu kama Field Marshall ES ni muumini wa kweli wa CCM isipokuiwa anaelewa mapungufu ya baadhi viongozi wa chama chake na hawezi kukiharamisha chama kizima kwa sababu ya matendo machafu ya baadhi ya viongozi waumini wa msahafu ule ule wa chama CCM..

Bob Mkandara,

Mtu anapojirudi na kujisahihisha na kuanza kufuata njia iliyo bora na njema, ni rahisi sana kukubalika. Hata Mchungaji, Padiri au mhubiri kama amefanya makosa na waumini tukayaona, naye akaja ungama kwetu na kwa nadhiri ya kweli akajisahihisha na kutenda yale yaliyomema, atapokelewa na kupewa nafasi ya mara ya pili.

Inapokuwa Mchungaji huyu, anafumbia macho maovu ya watu wake au yake mwenyewe na kukataa katu katu kuwa mnyenyekevu na kujisahihisha hata kuomba toba si kwa Mungu pekee bali hata kwa waumini na wafuasi wake, basi ni ama Mchungaji huyu aondolewe madarakani kwa kufukuzwa, au kupigiwa kura ya kutokuwa imani au hatari kubwa zaidi kama Mchungaji huyu ana mizizi ambayo haikatiki, ni waumini kumuachia hilo kanisa lake mwenyewe.

Sasa CCM kama ni Kanisa au Msikiti, lina viongozi, wawe Wachungaji, Mashekhe, Wainjilisti, Wahubiri, Mapadiri,Imamu au Masharifu. Wanaposhindwa kuliongoza Kanisa au Msikiti, inawapasa waachie ngazi ili wengine wenye uwezo na wenye kuaminiwana waumini, waongoze chombo hiki.

Lakini kama CCM, tuna makanisa na misikiti ambayo viongozi wake wamekwaza roho za waumini kwa madhambi ya ajabu ajabu, iwe ni wizi, uzembe, uzinzi, uasherati, ulawiti, dhuluma, unafiki, fitina au kukosa mwamko wa kiroho kuongoza makanisa na misikiti hii na hivyo kurutubisha imani za waumini wa masikiti na misikiti hii.

Viongozi hawa ama hufuatwa kwa uungwana kuombwa wajirudi, na mara nyingine huombwa wajiondoe kutoka uongozi. Wanapokuwa wagumu na kukata kuona makosa na udhaifu wao, migogoro na migongano inaanza kutokea.

Lakini kizuri katika misikiti na makanisa ni kuwa waumini ni rahisi kujitenga na kwenda kuanzisha misikiti na makanisa mapya huku wakitafuta viongozi wapya bila woga wa kuambiwa kuwa uumini na imano zao zitakuwa batili kwa kuwa wamejiondoa kutoka makanisa na misikiti ambayo wanaona kuwa imepotoka.

Nimekusoma sana Mzee mwenzangu Mkandara, sawa na nilivyomsoma FMES na Mwanakijiji, lakini najiuliza, tumekuwa tukiongea kuhusu haya mambo kwa miaka mingi, na kuna wengi wanatusikia pamoja na uchache wetu iwe kule Nyenzi, BCS, TEF, Jambo na sasa Jamii.

Sasa kama kulonga kwetu na kujadili na hata kufundisha kuwa tunaweza kubadilika na hata kujaribu kuwafikia wale waliopewa dhamana na kuwaambia ukweli wa mambo tunaendelea kupuuzwa na zaidi kuanza kuitwa wahaini au kutafutwa na vyombo vya dola, kwa nini tuendelee kuremba michubuko na vidonda na vaselini na tusiwe wakali?

Mtanzania nikitumia ile tafsiri yako ninayoipenda ya Watu na Mazingira, anaweza kubadilika kwa kufuata anachoona kwa kiongozi wake.

December 9 ya mwaka huu itakuwa ni mwaka wetu wa 47 tangu tupate Uhuru. Mtanzania bado anaamini kuwa TANU iliyompa Uhuru na CCM wanamuongoza. Anachoshindwa Mtanzania kuelewa ni kuwa CCM haimtumikii yeye tena na haina nia ya kuboresha maslahi ya Mtanzania huyu tena. CCM imebadili mwelekeo na kuwa ni kikuni kinacholinda maslahi ya wajanja wachache ambao wamepewa mamlaka makubwa na hata kura ndani ya CCM yenyewe kupitia Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na hata jumuiya zake.

Ndiyo maana unaona ni rahisi kwa watu kukimbilia Uongozi ndani ya chama maana huko wakishalishana viapo, kuna upenyo mkubwa sana wa kuneemeka kimaslahi na wala si kulitumikia Taifa na kujipatia kipato kwa uhalali.

Ndio maana nimeamuwa kuwa mkali na kama kauli na maneno yangu ni makali mno, ni kutokana na kuchoshwa kufanywa mjinga na watu ambao nimewapa dhamana ya kuliongoza Taifa langu.
 
1.
Umenihoji hapo awali kuwa nimekuwa mkali na kutoa maneno makali, je jukumu na wajibu huo wa kuwa mkali kwa wanaohujumu nchi ni wa nani?
Ndiyo, maneno yangu ni makali kwa kuwa ni hasira na uchungu wa kuendelea kupuuzwa na kudharauliwa. Haki yangu inanyanyaswa na kuzibwa pumzi kisa wajibu wa mwanachama wa CCM ni kwa Chama kwanza na si Taifa!
Ni aibu sana kwa wale ambao wako katika vyama vya siasa na hasa CCM na ambao wametoa viapo vya maisha kuwa kamwe wao hawataachana na CCM! Aibu hii itawaingia siku CCM uozo wake utakapokifanya kisambaratike.

- Tatizo ni kwamba wote tunaweza kutumia lugha ya ukali, then tutaelewana kweli hapa? Mimi niko radhi kusikiliza na kujadili hoja kama zinavyowekwa hapa, simuogopi mtu hapa hata siku moja, heshima siku zote huchukuliwa kama uoga, kama umeamua kutoa ukali wako basi ukautoe panapotakiwa kuliko ku-generalize sisi wote wanachama wa CCM kwamba we are this or that, Mwanakijiji mtoa mada hajamkaripia mtu wala kumtukana mtu hapa, lakini tunajdiliana bila matatizo na hoja zake zinaonekana na zetu pia zinaonekana, ndio hasa maana ya mjadala wa wanaoelewa kuliko wananchi wa mtaani,

- Lakini sikuzuii kutoa ukali, ila tu kumbuka kua owte tunaweza kuongea lugha ya ukali, kuheshimiana sio kuogopana na sio lazima tuheshimiane au tushirikiane, hapana!

2.
Sijui hawa wazee Salim, Warioba, Kawawa, Malecela, Msuya na wenginewe ambao wanazidiwa kete kila siku na wajanja wanaomiliki CCM watasemaje na viapo vyao siku CCM itakapokuja umbuka kuwa pamoja na kutuletea uhuru na mengine yote yaliyokuwa ya maana, CCM ilibadilika kuwa jinamizi mhujumu na fisadi.

- On this one kwangu ni very easy, kwanza ninaheshimu sana hawa wazee kwa yote waliyokwisha yafanya, sasa ni zamu yangu kuongeza mazuri yao na kupigania kurekebisha mabpovu yao, lakini no way ninaweza kukaa kuwalamu eti kwa nini hawasimami, ninayetakiwa kusimama sasa ni mimi, hao wamemaliza kazi yao, they are out sasa kushindwa kwangu siwezi kuwasingizia wao, ila ninatakiwa nikubali kuwa nimeshindwa!

3. [
B]Swali langu kwa hawa Wazee ni hili, wako tayari kufa kuilinda CCM na si Tanzania? Ni maslahi gani wanayoyalinda ikiwa kwa zaidi ya miaka karibu 15 tunajua kuwa CCM imepoteza dira na muelekeo? Hivi hawa wazee wanategemea kweli na kutokuwa kwao na madaraka au kutumia busara na kuachana na CCM wataweza kuibadilisha CCM iwe kila chama tulichokishangilia February 5 ya mwaka 1977? Wazee hawa ni heri wakihame CCM au waachane na CCM kuliko kuja poteza sifa na heshima zao na kuitwa WASALITI kwa kuwa waliogopa kukihama CCM wakati walipokuwa na fahamu zao kuwa CCM si chama cha mapinduzi wala si chama cha Wakulima na Wafanyakazi.[/B]

- Hapa wasliti ni sisi wenyewe vijan na wananchi wa Tanzania ambao tumeshindwa kuwaunga mkono walipotaka kutusaidia, walipokuwa wanafanyiwa ujaunja na CCM sisi wananchi tulikuwa wapi?

- Wahame chama ambacho kimewafikisha walipo? Kwa ajili ya nani sisi wananchi tuliokuwa tukiwacheka wakati wakifanyiwa ujanja na CCM? Kwani wenye tatizo hapa ni nani wao au sisi wananchi? Eti wasaliti? WAsaliti ni nani hapa kati ya wao na sisi wananchi? Leo kwa sababu tuna shida ndio watakiwa kutuokoa, mkuu kama sisi wananchi tuna matatizo tutafute njia za kujiondoa kwenye hayo matatizo lakini sio kuwalilia hao wazee, matatizo ni yetu sio yao!

4.
Sauli wa Tarsu, alikula kiapo cha milele kuitumikia Roma, akawa akiwanyanyasa Wayahudi na hata kufumbia macho vitendo viovu. Lakini siku ile alipokuwa akienda Damesiki (Damascus), Biblia inatuambia mbingu ikafunguka na Bwana Yesu akamuuliza, "ilhali vipi wawanyanyasa watu wangu? wamekukosea nini unawapa mateso?" Sasa sisi na sauti zetu za kutaka CCM imeguke na hawa wanaojiita CCM mageuzi waachane na Roma yao, ndiyo inayolia, "kwa nini hawa wanaojiita watetezi wa haki bado wanaendelea kulewa mvinyo na CCM ambayo haiwajali Watanzania tena bali ni kujali matumbo yao na marafiki zao?

- Sauli alikuwa anaua waumini wa Yesu, sasa hawa wazee unasema wanaua wananchi waumini wa upinzani au what? I do not get it?

- Watetezi wa haki wa CCM wanajua what time is, kwa hiyo hawawi wajinga na kwenda kama vichaa, I support them kwa sababu wananchi wa Tanzania sio kama wa nchi nyingine yoyote duniani, ni wananchi wa bongo unaenda nao pole pole, bongo sio USA au Europe, it just bongo!

5.
Umeniuliza maana ya kuleta mfano wa Somaiya kulipia mkutano mkuu wa UVCCM kwa kutoa shilingi milioni 400. Nikuulize, hizo hela ni kwa mapenzi gani? ni nani ananunuliwa au analipwa fadhila na hizo hela? Iweje CCM leo iweze kupata fedha za kuendesha mkutano na uchaguzi wa jumuiya yake ambayo si jambo la msingi kwa Taifa lakini inajivutavuta kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya kweli yanayowasibu Wananchi wa Tanzania na Taifa la Tanzania?

- vyama vyetu vyote vya siasa vinapokea misaada kila siku kutoka kwa wahindi, wazungu, na wazawa na hakuna kelele, sasa ninauliza why this one unaleta makelele?

6.
Nikianza na orodha ya haraka haraka, kuna mgomo wa wanafunzi, mgomo wa waalimu (huu sijui baada ya mwaka ndio Serikali inapata pesa na kuwalipa!), kuna wastaafu, kuna shida ya maji, shida ya umeme, madawa hakuna, njaa kila kona, ajira hakuna, ufisadi na dhuluma zinapeta, lakini kikao cha UVCCM kimepata umuhimu na ujiko wa hali ya juu (priority) na pesa zikapatika haraka ili achaguliwe mwenyekiti wa jumuiya? Nitaongea kwa ukali kwa kuwa CCM ya leo, si CCM iliyonilea, CCM iliyonifunza kuuthamini utu na jirani, kujivunia Utaifa wangu. CCM ya leo imezingirwa na inaongozwa na kundi la Wasaliti, Wahaini, Wazembe, Walafi, Wezi, Wavivu, Wahuni, Wanafiki, Waongo, Wahujumu, Mafisadi na sifa nyingine mbovu ambazo si njema kwa Tanzania hata wale WanaCCM ambao bado wanatongotongo kwenye macho.

- Matatizo unayoyasema yalikuwepo hata under Mwalimu, hakukuwa na migomo kwa sababu tunajua yaliyowapata waliojaribu kugoma au kumuuliza Mwalimu, sasa yes yapo mpaka leo, lakini leo tuko huru unaweza kugoma na ukapeta tuu, kwa nini hapa tunaingia kwa majina ya bandia? Ni kwa sababu tunaogopa, tunaogopa nini ni kwa sababu tunajua yaliyotokea toka enzi zile za awamu ya kwanza, matatizo yalikuwepo siku zote na matatizo siku zote yanazidiana, lakini tofauti ni kwamba leo tunaweza kugoma na kusema wazi tukasikika.

- Binafsi ninarudia tena siamini kwamba CCM yote imejaa viongozi wabovu, ninaamini kuwa kuna wachache sana, ambao wakithibitiwa na kuondolewa kama anavyotaka Kinana, CCM itakuwa bora na safi, lakini ni haki yako kuamini as you say, ndio demokrasia.

7.
Wanaojiita CCM mageuzi, tunawataka wafanye hivi kama sisi Wakristo tunavyosema tunapotubu, "wamkatae Shetani na mambo yake, kazi zake, fadhila zake na wema wake" watubu kuwa walikosea na wanapaswa kuoshwa, nasi tutawasamehe na kuwaenzi kama mashujaa. Kinyume cha hapo, wataendelea kunuka uozo na kuoza kama vile kapu la samaki linavyovunda kwa samaki mmoja kuoza.

- Kwangu haya ni maneno ya hasira za mkizi, kwa sababu Tanzania sio tu ya hao viongozi wanamageuzi, ni ya kwetu sisi wananchi wote millioni 40, hao wanamageuzi wameshajaribu wawezavyo sasa ni wakati wa sisi wananchi ku-take it to the next level, lakini mimi siwezi kukaa kuwalaumu hao viongozi wachache wa CCM, wanaotukanwa kila siku na sisi wananchi wanaojaribu kutusaidia, kwanza sio lazima wafanya wanayoyafanya.

Kama tumeshindwa vyema kukubali kuwa tumeshindwa as wananchi, wananchi millioni 40, sasa tunajaribu kuwashambulia viongozi wasiozidi watano tu kwamba ndio tatizo letu kwa sababu magezui yao sio fast enough kama tunavyotaka, as if ni lazima wawe hivyo wanamageuzi, wakuu tutafute mbinu za kujiokoa taifa ni letu sio la wanamageuzi au anybody ni letu sisi wananchi wa Tanzania, kama tumeshindwa bora tuache lakini tuisisngizie viongozi wanamageuzi au anybody, matatizo ni yetu wananchi.
 
Something has to be wrong in CCM other than Kikwete, Lowassa, Chenge and others including FMES.

Hizi name calling zako na nonesense ndio zinanifanya siku zote nikuite miaka 60 lakini akili ya mtoto wa miaka 10. Ulipokuwa rafiki wa Kikwete kabla hajakufukuza hukujua kua Tanzania ina matatizo je ulifanya nini? Taarabu sasa zimekuchosha maana umeona sikujibu sasa umerudi tena kutaja jina langu maana hii obssesion sijawahi kuona, huwezi kuandika bila FMES, na taarabu na gonjera as if I care mimi nipo tena imara, anytime ukinitaja tu nipo!

Mimi sio rais wa Tanzania, ila ni raia wa Tanzania I hope you are tooyaani raia wa Tanzania kama mimi!
 
1.
Mzee FMES,

Kwanza naomba usichukulie binafsi kutumia maneno yako kujenga hoja zangu kuwa ni vita baridi, maana hapa watu hawachelewi kuanzisha zogo!

- Hukuwa na sababu ya ksuema haya, kwa sababu mimi sio mtoto mdogo ninajua kinachoendelea, tena siku nyingi. Sio lazima niwe na uhusiano na mtu yoyote hapa JF ili kutoa mawazo yangu hapa, heshima sio uog it just heshima tu na inaweza kuvunjwa anytime na life ikawa kama ilivyokuwa mwanzoni na isiwe taabu vile vile!

2.
nikirudi kwenye jibu lako kwa Kitila, kinachonitatiza kutokana na kauli yako ambayo ndiyo hali halisi ya mfumo wetu wa Siasa na Uongozi ni ile dhana ya kusema mtu anakuwa mwanasiasa au kiongozi ile "ale" au ajipatie! Je kujituma na kutumikia Taifa kuna nafasi gani tena? Jee kulitumikia Taifa kwa moyo kwa kuwa mtu ni mzalendo na mwaminifu wa nchi yake kunageuzwaje kuwa mradi wa kujipatia mali?

- I have no clue na haya, nijuavyo ni kwamba huwezi kuwa kiongozi huku ukiwa na shida na ndilo tatizo letu na uongozi bongo, sasa wewe utalishughulikaje hilo la uongozi na umasikini, lakini siamini kwamba dawa ni kuwashambulia wanaoamini hivyo labda wewe uonyeshe mfano wa kuwa kiongozi masikini na mwenye shida.

3.
Nafahamu fika wewe ni mmoja wa wale wanaolipinga Azimio la Arusha, ingawa sijawahi kuelewa kwa maoni yako ni kwa nini unalipinga Azimio la Arusha. Lakini nitakuambia hivi, kwenye Azimio la Arusha ambalo lilivunjwa kwa kuundwa kwa Azimio la Zanzibar, ndiko kulikoandikwa miiko ya uongozi kuzuia watu kukimbilia uongozi kuwa ni sehemu ya kujipatia kipato ama kwa kutumia nafasi zao za kazi au kujipangia manufaa ya binafsi na si ya Taifa.
Huyo mzee unayemzungumzia, namfahamu, nami nilishawahi kumpa saluti yangu kwa kuwa jasiri na kwenda Upinzani.

- Sina uhakika kama haya yanahusika na kumeguka wka CCM kama the last resort ya kutuokoa wananchi wa bongo, tatizo sio Azimio sasa hivi tatizo ni kwamba nchi inakwenda kombo, sasa sisi wananchi tufanye nini maana kwangu naamini kwamba ni tatizo letu sisi wananchi sio viongozi wachahce ndani ya CCM au upinzani?

4.
Tatizo la uoga na unafiki wa WanaCCM wengi ambao ni viongozi, wabunge na wawakilishi ni kuwa wamekimbilia kazi zao si kulitumikia Taifa, bali ni kujipatia kipato na kushughulikia maslahi binafsi! Hili ndilo tatizo kuu na ndio maana wengi wao wanaingia kwenye mtego wa kuogopa kuihama CCM au kufa masikini kwa kuwa wameshajenga nadharia kuwa ni lazima wawe na mali nyingi au uhakika wa mali na mapato ili waweze kulitumikia Taifa. Badala ya Viongozi na WanaCCM kufanya kazi na kulitumikia Taifa na kuacha mapato au kipato kiwe matokeo ya kazi zao, wao wameweka maslahi na kipato mstari wa mbele kuwa ni muhimi kabla ya kufanya kazi yeyote. Ndio maana niliposema CCM ni adui wa Maendeleo ya Tanzania na Watanzania ni kutokana na hii sasabu nyingine iliyozaa utamaduni wa watu kukimbilia siasa kama tegemeo pekee la kujipatia MAISHA BORA. Ugonjwa na Utamaduni huu umeliharibu Taifa letu. Kama Mwanakijiji alivyoeleza, Watanzania tumeshazoea kuishi KIFISADI na KIHUJUMU na hivyo vita dhidi ya Ufisadi na Uhujumu inakuwa ngumu kwa kuwa tumefanya mazoea ya kuishi kwa kutegemea mapato ya ziada na ya ujanja ujanja na si kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa. Narudia tena nilichomwambia Pasco na wewe kuwa ni mpaka pale baadhi ya Viongozi waasisi na walioko madarakani wa CCM watakapoachana na woga na kuukumbatia Utamaduni huu mbovu wa unyonge wa mali kuwa ndio kigezo cha kuogopa kuondoka CCM na kufanya kilicho sahihi, Tanzania kamwe haitaweza kuendelea au kupata mafanikio inayoyataka. Utamaduni huu pamoja na kuwa unawaathiri Watanzania wengi hata wale walioko katika vyama vya upinzani, lakini kama tunataka uharamia huu uishe mara moja na si kutumia miaka 100 kubadilika, atakayeweza kulibadili hili na kufuatwa kwa urahisi kabisa ni CCM!
Ndiyo maana nimekuwa mkali kwa wanaojiita CCM mageuzi kwa kuwa wanaukumbuatia mfumo mbovu kulitumikia Taifa!

- Mimi kama nimemuelewa Mwanakijiji ni kwamba kumeguka kwa CCM anaona ndio the last resort ya kutatua tatizo letu wananchi wa Tanzania, tatizo tulilonalo bongo ni pamoja na yote haya unayoyasema ndiyo yamemfanya MMJ aseme CCM inahitaji kumeguka, sasa nilifikiri tunajaribu kutafuta solution, mimi nikashauri kwamba kubadilika kwa katiba kupewa kipaumbele kwanza kabla ya yote, so far sijakuelewa exactly solution yako ni ipi hasa?
 
- Unajua mkuu Rev, ninasikitishwa na tabia moja ya ajabu sana, kwamba nikitoa mawazo yangu, yanakuwa ya CCM au ya Kiongozi flani, lakini ya kwako yanakua ya kwako, WHY is that? Ni wapi unapopajua upaweke hapa JF as ushahidi kwamba CCM imewahi kutumia kundi la wanne kule China kama fimbo against hao viongozi uliowataja?

FMES, sijasema kuwa unazungumza kwa niaba ya mtu au kiongozi fulani, hiyo ni hali halisi ambayo mimi ninaifahamu ambayo iko ndani ya CCM. Nimeshukuru kuwa umeleta mfano wa karibu wa mke wa Mao na genge kuonyesha jinsi gani CCM ilivyo. Kama unafahamu vizuri hadithi ya genge la wanne kule China, ungeelewa maana yangu ya kusema kina Mwakyembe na Wenzake kufanywa kama genge la wanne. Genge la wanne lilikuwa ndani ya chama cha Kikomunisti, wakaja kugeukwa kutokana na msimamo wao. Hata pamoja na kuwa msimamo wao ulikuwa si sawa, lakini kitendo cha wao kufanywa kondoo ni kitu ambacho CCM inakiweka kama mtego kwa yeyote ndani yake atakayediriki kuachana nao.

Alikuwepo Jumbe, Sefu Hamad, Natepe, Kasyupa, Mrema, Kolimba, Kitine, Iddi Simba, hata Warioba, walipoamua kujitenga, "madhambi" yao yakatangazwa na wamefanywa wahaini na ndio wanakimbiwa kama ukoma!

Hata Nape, Mamuya na wenginewe kama uliowataja kina Kasaka nao wameingia kwenye mtego huo huo wa kutengwa kwa kuwa na misimamo tofauti.

- Kwamba nimevunjika moyo? Hapana I am being reelistic baada ya kuona mifano mingi sana bongo, nimewaona kina Mrema wakijitolea kufa na kupona, na wananchi walivyoshia kuwabeza kama ni vichaa!, Nimeona Kasaka Njelu, akisimama kidete na kudai Tanganyika in the process akiwakusanya wananchi wengi nyuma yake, na nimemuona akiingia mitini kimya kimya baada ya kupewa cheo na CCM hakuna cha Tanganyika wala kudai mabadiliko, nimewaona wananchi wakiwakimbia kina Ngaiza walioyataka kuwaokoa,

Ni nani basi aliyeongoza vita ya kuwabeza hawa jamaa kama si CCM? si majuzi tumemsikia Chiligati akimbeza Mbowe kwa kudai yeye ni mchezesha kamari na disko? sasa kama CCM wakiambiwa ukweli au wakiona mtu anajijenga kwa kutofungamana nao nao wanamfanya msaliti na kuhakikisha kuwa anaangamia si kisiasa pekee bali ni hata utu na kimaisha, ni nani basi anapaswa kusahihisha dhana hii mbovu ambayo inawaingia Wananchi?

CCM wanatumia dola, vyombo vya habari, serikali na nguvu nyingine nyingi kuhakikisha wanakandamiza na kuwazika wote wale wenye sauti tofauti. Anzia vitisho vya TRA, kukatiwa maji na umeme, kunyang'anywa nyumba na mali hata kufukuzwa kazi! Hili ni kosa na si demokrasia na kama kuna watu ndani ya CCM wanafurahia hii tabia alimradi Chama chao kiendelee kushika hatamu, basi hao wote waliomo ndani na wanalipuuzia jambo hili la uonevu hawafai kuthaminiwa au kupewa heshima na enzi. Infact tunapaswa kuwaita wasaliti wa utu kitu ambacho tumekiimba kwenye imani ya chama na hata katiba.

- Ninaifahamu vizuri sana siasa na tabia za wananchi wa bongo, ndio maana sishangazwi na maneno mengi hapa ya kishujaa ya kuwatukana kina Mwakyembe, wanaojitahidi angalu to do something kuliko kupiga domo hapa JF, mkuu ndio kwanza nimemaliza kampeni yangu ya OIC ambapo nimeweza kuwa-reach out viongozi karibu 80% wa NEC, niliyopambana nayo mengine ni aibu hata kusema jinsi hawa viongozi wetu wasivyoelewa, recently nime- spent a lot of hours kwenye ofisi za OIC kujifunza exactly who they are na kujaribu kuwaelimisha wanaohusika, ndio maana ninakataa kujivika mkenge kuhusu wananchi wa bongo, kusema hapa JF ni one thing na kutimiza katika bongo ni another story of its own, muulize Kitine unajua siku hizi hata viongozi humkimbia kwa kuogopa wasionekane naye mbele ya public, that is bongo yaani Tanzania, that is what we are sasa naishndwa kuelewa mawazo kama yako yanaweza kufanyika boingo hii ya sasa au wapi?

Mapinduzi ya fikra huanza kwa kuachana na unyonge na uoga wa kuwa sauti ya kudai mapinduzi haitakaa isikike. Nyerere alipoanza kudai Uhuru, mawazo yake yalikutana na vizingiti vya ndani na nje, wafuasi waliokuwa na mashaka ya alichokuwa akikisema, woga wa kuachana na mfumo wa Kikoloni na kuwa nchi Huru yenye kujitegemea.

Kama Watanzania tutaendelea kusema kuwa hatuwezi kuwa na mawazo endelevu eti kwa kuwa mandhari na mazingira hayaruhusu, basi tutaendelea kuwa Watumwa wa fikra na wanyonge ambao tunatawaliwa kwa ridhaa zetu na CCM ambayo sasa hivi haina tofauti na mkoloni.

Siasa za compromise, zina nyakati zake, kama nilivyomjibu Mkandara, inapofikia mahali kuwa watu wamegeuza mashavu kunaswa vibao wamechoka na hakuna compromise tena.

Tunachokikataa kutoka kwa hawa kina Mwakyembe ni kile tulichokiona kwa Kasaka na Kolimba, kuruhusu "ushujaa" wao kuyeyuka kutokana na vitisho ndani ya Chama au kuundiwa mikakati.

Kama CCM ni chama safi, basi kiachane na wale wachafu! Kama si hivyo basi kina Mwakyembe waondoke, maana hakieleweki kuwa leo hii ndani ya CCM kuwa Chenge, Lowassa na Rostam wana nguvu za ajabu na ushawishi mkubwa kuliko Mwakyembe, Killango, Sitta au Seleli!

- Nimesikia mara kwa mara, kwamba wananfunzi wa Mlimani huwa wanazuiwa wasiandamane maana wakifika mitaani wananchi watajiunga nao, nonesense! Nimeona under Mwinyi wananfunzi wakiandamana kupitia mitaani mpaka kufika Wizara ya elimu ya juu, hakuna mwananchi hata mmoja aliyejiunga, nimeona wananchi wakiwazomea kuwa ni wajinga, huku FFU wakiwala fimbo!

Wakulaumiwa hapa ni sisi maana tayari tumeshashibishwa na pilau na kachumbari inayosema wanafunzi wanachofanya ni batili. Baada ya ule mkwala waliopigwa kina Winfred Mwabulambo na Nyerere miaka ya 70, na zile sifa za UWT kufuatilia kila Mtanzania na vitisho, Watanzania tumeendelea kuwa wanyonge na waoga kuogopa vyombo vya dola kiasi tumefikia hatua kuwa tunapuuzia kile ambacho ni cha msingi ambacho kama hakituhusu, basi hatutoki jasho wala kuona umuhimu wa kusimama kidete kutetea haki za jirani.

- Kama haya yote hayakutoshi, nilipokuwa Secondari nilikuwa kiongozi wa upinzani wa kila kitu kisichofaa, kuanzia chakula kibovu, kulimishwa kama mbwa, kutoruhusiwa kwenda mjini week end, one time nilianzisha mpaka mgomo wa chakula na kulima, mambo yalipochacha wanafunzi wote wakanikimbia nikabaki peke yangu mbele ya Pilato, wakanitisha weee lakini walipoona sibadiliki, Pilato akamua ku-make a deal kwamba sitaguswa tena ninaweza kufanya ninalotaka mradi tu niwape heshima waalimu na nisiwashawishi na wengine, yes form that day I was free, jamaa wakienda kulima mimi naingia town, chakula nikawekwa permanent kwenye list ya maseule mpaka miaka mitatu yangu liyobaki ya kumaliza shule,

Sasa mfano wako wa kuachwa solemba na wenzio na kisha kupewa compromise na mkuu wa shule, unaonyesha wazi ni jinsi gani mfumo wa devide and rule ulivyoshika mizizi.

Ulipopewa chako, basi vita dhidi ya uonevu ukaicha kwa wengine. Je ilikuwa ni kuwalipa kwa usaliti wao kukuacha pekee yako? Au kwa kuwa ulishapata ulichotaka hukuona sababu au manufaa ya kuendeleza vita vya ukombozi dhidi ya uonevu?

Kwa hiyo mkuu hii njia ya upinzani na bongo ninaifahamu vizuri sana kwa sababu nimeipitia mara nyingi sana, ndio maana ninaishi na realities za bongo sio imagination!

Realities za Bongo haziwezi kuwa permanent, they can change, ndio maana unaona nimekuwa mkali maana nimechoka mazoea!

Lakini jukumu hili la kubadilisha fikra za Mtanzania ni la kika mtu. Ndiyo Mwanakijiji kaleta hoja nzuri sana kuhusu umuhimu wa CCM kupoteza madaraka ili Taifa letu liweze kubadilisha mwelekeo. Sasa ni wajibu wetu wote kwanza kuwa na imani kuwa hilo linawezekana pamoja na ugumu wote uliopo.

Ninapoongea kwa Ujasiri na Ukali, hata kama siko ground zero, kuna wanaojifunza na kunisikia. Kuna wanaopata tumaini na kufundishika kuwa hakuna haja ya kuwa na woga kudai haki yako au kutetea maslahi ya Taifa.

Nikiendelea kuishi kwa dhana kuwa realities za Bongo kuwa kamwe hatutakuwa na mabadiliko basi ni heri niukane Utaifa wa Tanzania na nijongomee kwingine na hata niache kuongea hapa kwa maana eti hakutakuwa na mabadiliko.

Wote tuko safari moja, lakini tunatumia mbinu tofauti. Wewe unakutana na watu wa NEC, mimi naongea na kila mwenye masikio, that is the difference.
 
- Binafsi ninarudia tena siamini kwamba CCM yote imejaa viongozi wabovu, ninaamini kuwa kuna wachache sana, ambao wakithibitiwa na kuondolewa kama anavyotaka Kinana, CCM itakuwa bora na safi, lakini ni haki yako kuamini as you say, ndio demokrasia.

FMES,

Ikiwa ni wachache ndani ya CCM ni wabovu, kwa nini CCM inakuwa na kigugumizi kuwashughulikia? Iweje hawa wachache wawe na nguvu za ajabu na kukitia madoa CCM mpaka kinafanya kila aliyendani aonekane kuwa ni mshiriki?

Si ndani ya CCM kuna vikao na kura? Je ni kura ngapi zinahitajika kuwaondoa hao wachache ili Chama kijirudi na kuwa na taswira safi?

Sasa kama mpaka leo Lowassa, Chenge na Rostam ambao wametuhumiwa na kuonekana wana madoa bado wana nguvu au sauti ndani ya chama, itaelewekaje kwa mtu mweye akili timamu kusema CCM ni safi?

Ni ugumu gani ulioko kuwaondoa hawa watatu na wafuasi wao kama kina Kingunge, Nchimbi, Serembuka, Kisumo, Yona, Mkapa na wengine?

Kama leo hii ndani ya mfumo mpya wa siasa na demkorasia, CCM bado kuna ububu, utata na ugumu kufanya demokrasia ya kweli kuwaondoa hawa wachache waharibifu, tutakuwaje na tumaini kuwa CCM mageuzi itafanya kweli na kuleta mabadiliko ya kweli kwa Taifa letu?

Ndio maana napiga baragumu kuwa kama CCM Mageuzi wameshindwa kuwaondoa hawa wachache, kwa nini wasijiondoe na kuunda chama kipya au kujiunga na vinginevyo ili kuleta upinzani wa kweli?

Tukirudi kwenye hoja ya Katiba, bado Wananchi hawatakuwa na uwezo wa kuleta mabadiliko kama ndani ya CCM yenyewe hakuna mfukuto wa kweli na si wa kizandiki au kufuata malengo ya chama kuleta mabadiliko ya Katiba.
 
Kama njia ni kumeguka CCM, kitu chepesi ni kwa wanaotaka CCM imeguke ni kujiunga na CCM na kujaribu kupigania nafasi za juu katika CCM na baadaye kukimegua chama.

Mtu kuwa CHADEMA na baadaye kumuomba Mungu kuwa migogoro itokee CCM ya kumegua chama hicho doesnt make any sense to me.

Pluralism sio lazima iwe ya vyama vingi. Hata ndani ya chama kimoja ikitokea migongano ya kifikra uwezekano wa kupata pluralism utakuwepo.

Vilevile tukumbuke kuwa wakati wa mfumo wa chama kimoja kuna watu wengi walioachana professions zao na kujiingiza kwenye siasa. Watu hawa pamoja na rais JK, na marais wengine waliomtangulia hawakuwahi kufanya kazi katika professions zao na hawawezi kutafuta maisha bila kuwa wanasiasa. Hivyo wao kubakia CCM ni moja ya survival skills. Hawako CCM kwa nia ya kuwa na debate ya kujenga au kuangalia masilahi ya nchi. Hili ndio kundi kubwa na halina mpango wowote wa kumegua chama.
 
Well, Hivi kama mnataka chama chenye wanachama (5 millions) kati ya 40 kimeguke yaani kuwe na vyama viwili kimoja 2.5mil na kingine 2.5mil mnatakia kweli taifa mema? Yale yale mambo ya kuombea mabaya yatoke ili tupate mambo yakuongea. Kwa upande wangu ningependa angalau CCM ingekuwa na wanachama 10 millions na chama kingine 10 millions hapo sasa tungekuwa tunaongelea siasa kwa maendeleo ya taifa. Kwa maneno mengine "CCM is too weak to be divided."
Kama kumbukumbu zangu ni nzuri, nadhani ilikuwa 2003 au 2004 mkapa aliulizwa swali kwenye mahojiano kwenye TV kuhusu katiba mpya. Kwa maneno yake mwenyewe alisema serikali haikatai kuandika katiba mpya lakini aliwaomba wanasiasa wampelekee sababu au mambo ambayo wanadhani ni muhumu kuandika katiba mpya. Mpaka anaondoka madarakani hakuna mwanasiasa aliyempelekea na wote si wanaingia humu ndani waniambie kwamba ni nani alimpelekea kitu wanachofanya ni kufanya issue hii iwe wa kisiasa ili wawe na kitu cha kuongea majukuani. Pure nonsense.
Let just consider that we have the need ya katiba mpya. Kwa upande wangu huwa sioni ni kivipi hiyo katiba itaandikwa. Tuchukulie nchi yetu in demokrasia ya kutosha na kuamua kuwashirikisha wananchi katika kuandika katiba. Don't you think that 80% of the population watasema tunataka CCM kiwe chama pekee cha siasa nchini? Unapota mabadiliko ya namna hii lazima uwe na watu wanaotaka mabadiliko kwanza, siyo wewe Mwanakijiji, Mrema, na Lipumba tu. The changes will wipe you out from the political map. Tumeshaona sehemu nyingi duniani, ukishakuwa na watu wa kutosha kutakuwa hakuna haja tena ya kuipigia magoti CCM au serikali eti tunaomba katiba mpya.
 
Well, Hivi kama mnataka chama chenye wanachama (5 millions) kati ya 40 kimeguke yaani kuwe na vyama viwili kimoja 2.5mil na kingine 2.5mil mnatakia kweli taifa mema? Yale yale mambo ya kuombea mabaya yatoke ili tupate mambo yakuongea.

don't even start.. hivyo kumeguka kwa CCM ni jambo baya kwa Tanzania? how is that?

Kwa upande wangu ningependa angalau CCM ingekuwa na wanachama 10 millions na chama kingine 10 millions hapo sasa tungekuwa tunaongelea siasa kwa maendeleo ya taifa. Kwa maneno mengine "CCM is too weak to be divided."

Not really, CCM is weak enough to be divided!

Kama kumbukumbu zangu ni nzuri, nadhani ilikuwa 2003 au 2004 mkapa aliulizwa swali kwenye mahojiano kwenye TV kuhusu katiba mpya. Kwa maneno yake mwenyewe alisema serikali haikatai kuandika katiba mpya lakini aliwaomba wanasiasa wampelekee sababu au mambo ambayo wanadhani ni muhumu kuandika katiba mpya.

You are confirming my point.. "Wampelekee" yeye kwa misingi gani?

Mpaka anaondoka madarakani hakuna mwanasiasa aliyempelekea na wote si wanaingia humu ndani waniambie kwamba ni nani alimpelekea kitu wanachofanya ni kufanya issue hii iwe wa kisiasa ili wawe na kitu cha kuongea majukuani. Pure nonsense.

Yaani mapendekezo ya Katiba mpya yapelekwe kwa Rais na wewe unaona sawa hilo? Kuunga mkono wazo hilo is (using your own words) "pure nonsense".


Let just consider that we have the need ya katiba mpya. Kwa upande wangu huwa sioni ni kivipi hiyo katiba itaandikwa.

Umeshasema wazo la kumpelekea Rais kwanza! a.k.a Mwenyekiti wa CCM

Tuchukulie nchi yetu in demokrasia ya kutosha na kuamua kuwashirikisha wananchi katika kuandika katiba. Don't you think that 80% of the population watasema tunataka CCM kiwe chama pekee cha siasa nchini? Unapota mabadiliko ya namna hii lazima uwe na watu wanaotaka mabadiliko kwanza, siyo wewe Mwanakijiji, Mrema, na Lipumba tu. The changes will wipe you out from the political map. Tumeshaona sehemu nyingi duniani, ukishakuwa na watu wa kutosha kutakuwa hakuna haja tena ya kuipigia magoti CCM au serikali eti tunaomba katiba mpya.

well nchi yetu haina demokrasia ya kutosha and thus your whole argument is negated.
 
Kumeguka kwa KANU hakukuisaidia sana Kenya. Hadi leo hawana KATIBA mpya, ufisadi uko palepale, UCHAGUZI uliopita nchini humo ulikuwa wa ovyo kabisa kuliko zilizotangulia.
Tuimarishe vyama vya upinzani vilivyopo ili tupate Uongozi mpya kabisa wa nchi. Tatizo ni vyombo vyetu vya DOLA kama UwT, TPDF na POLISI. Nje ya CCM havioni kama kuna mtu mwingine anaweza kuwa RAIS wa Nchi hii!
 
Kumeguka kwa KANU hakukuisaidia sana Kenya. Hadi leo hawana KATIBA mpya, ufisadi uko palepale, UCHAGUZI uliopita nchini humo ulikuwa wa ovyo kabisa kuliko zilizotangulia.
Tuimarishe vyama vya upinzani vilivyopo ili tupate Uongozi mpya kabisa wa nchi. Tatizo ni vyombo vyetu vya DOLA kama UwT, TPDF na POLISI. Nje ya CCM havioni kama kuna mtu mwingine anaweza kuwa RAIS wa Nchi hii!

Siyo tu kumeguka "megu" halafu yanakwisha. Mmeguko wa Kenya siyo wa kuufuatia.. ni lazima uwe mmeguko wa Tannzania. Siasa za Tanzania huwezi kuzilinganisha na Kenya. Naangalia zaidi zile za South afrika na yale yanayoikuta ANC sasa hivi ndiyo yanayoweza kutokea Tanzania..
 
Zuma wetu hapa atakuwa nani? EL? NAPE? MWAKYEMBE? OLE SENDEKA? SITTA? SAS?
Mzee ndani ya CCM hakuna mtu jasiri kama alookuwa nao MREMA 1995.
 
Ninapoongea kwa Ujasiri na Ukali, hata kama siko ground zero, kuna wanaojifunza na kunisikia. Kuna wanaopata tumaini na kufundishika kuwa hakuna haja ya kuwa na woga kudai haki yako au kutetea maslahi ya Taifa. Nikiendelea kuishi kwa dhana kuwa realities za Bongo kuwa kamwe hatutakuwa na mabadiliko basi ni heri niukane Utaifa wa Tanzania na nijongomee kwingine na hata niache kuongea hapa kwa maana eti hakutakuwa na mabadiliko. Wote tuko safari moja, lakini tunatumia mbinu tofauti. Wewe unakutana na watu wa NEC, mimi naongea na kila mwenye masikio, that is the difference.

Mkuu ninakusikia sana, lakini so far bado sioni your solution kulingana na hali mbaya ya kisiasa tuliyonayo bongo, mimi sio tatizo wala sio kiongozi, nina mawazo tofauti na yako, ninaamini kwamba wananchi wa Tanzania tunahitaji kulilia mabadiliko ya katiba kwanza, sasa wewe unasemaje on the solution side kwa sababu haya mengi unayoyasema yananihusu mimi tu, mimi sio rais wala anything mimi ni mwananchi kama wewe! Toa mapendekezo ya kuwasaidia wananchi namna ya kujikwamua na situation tuliyonayo!
 
Ikiwa ni wachache ndani ya CCM ni wabovu, kwa nini CCM inakuwa na kigugumizi kuwashughulikia? Iweje hawa wachache wawe na nguvu za ajabu na kukitia madoa CCM mpaka kinafanya kila aliyendani aonekane kuwa ni mshiriki? Si ndani ya CCM kuna vikao na kura? Je ni kura ngapi zinahitajika kuwaondoa hao wachache ili Chama kijirudi na kuwa na taswira safi? Sasa kama mpaka leo Lowassa, Chenge na Rostam ambao wametuhumiwa na kuonekana wana madoa bado wana nguvu au sauti ndani ya chama, itaelewekaje kwa mtu mweye akili timamu kusema CCM ni safi? Ni ugumu gani ulioko kuwaondoa hawa watatu na wafuasi wao kama kina Kingunge, Nchimbi, Serembuka, Kisumo, Yona, Mkapa na wengine? Kama leo hii ndani ya mfumo mpya wa siasa na demkorasia, CCM bado kuna ububu, utata na ugumu kufanya demokrasia ya kweli kuwaondoa hawa wachache waharibifu, tutakuwaje na tumaini kuwa CCM mageuzi itafanya kweli na kuleta mabadiliko ya kweli kwa Taifa letu? Ndio maana napiga baragumu kuwa kama CCM Mageuzi wameshindwa kuwaondoa hawa wachache, kwa nini wasijiondoe na kuunda chama kipya au kujiunga na vinginevyo ili kuleta upinzani wa kweli?
Tukirudi kwenye hoja ya Katiba, bado Wananchi hawatakuwa na uwezo wa kuleta mabadiliko kama ndani ya CCM yenyewe hakuna mfukuto wa kweli na si wa kizandiki au kufuata malengo ya chama kuleta mabadiliko ya Katiba.


Katiba ya Jamhuri ni mbovu sana inampa power ya ajabu rais ambaye ndiye mwenyekiti wa CCM, ndio maana unaona kikundi kidogo ndani ya CCM cha wabovu kina sumbua owte ni kwasababu kuna mkono wa mwenyekiti unawakinga, ndio maana ninasema bila kubadili katiba ni kazi ya bure!

Tatizo ni letu wananchi millioni 40 wa Tanzania, sio kikundi cha viongozi wachache wanamegeuzi ndani ya CCM, wao wameshafanya part yao angalu ndogo je sisi wananchi tumefanya nini? Au tutafanya nini? Kumeguka wka CCM hakutakupwepo karibuni, labda next generation hayo ni mawazo yangu tu!
 
Kama njia ni kumeguka CCM, kitu chepesi ni kwa wanaotaka CCM imeguke ni kujiunga na CCM na kujaribu kupigania nafasi za juu katika CCM na baadaye kukimegua chama.

Mtu kuwa CHADEMA na baadaye kumuomba Mungu kuwa migogoro itokee CCM ya kumegua chama hicho doesnt make any sense to me.

Tupo ukurasa mmoja hapa mkuu.
 
4.

- Sauli alikuwa anaua waumini wa Yesu, sasa hawa wazee unasema wanaua wananchi waumini wa upinzani au what? I do not get it?

Mukulu wa Kaya,

Umesahau mauaji ya Pemba, Mwembechai, Kilombero na Bulyankhulu? Je kibano kilichotokea Tunduru, Kiteto na majuzi Tarime hukukiona?

Sina maana kuwa wazee hawa na wale CCM mageuzi ndio waliosababisha umwagaji damu au kipigo kwa wale wanaoipinga CCM, bali wao wakiwa ndani ya CCM kama viongozi na kukaa kwao kimya huku Chama kupitia dola kinawanyanyasa wale wanaokipinga ndio kosa.

Ndiyo maana nikaleta mfano wa Sauli, maana Sauli alikuwa mtumishi wa Roma. Alikuwa akifuata utii kutoka kwa Kaisari mkuu wa Roma kunyanyasa Wakristo.

Wamenufaika directly au indirectly kutokana na maamuzi mabovu na yasiyo ya haki ambayo yamefanywa na wengine. Sasa kama utaniambia hiyo ndiyo cost ya kuwa politician, then Politics of Tanzania have no ethics or morals!
 
Mkuu ninakusikia sana, lakini so far bado sioni your solution kulingana na hali mbaya ya kisiasa tuliyonayo bongo, mimi sio tatizo wala sio kiongozi, nina mawazo tofauti na yako, ninaamini kwamba wananchi wa Tanzania tunahitaji kulilia mabadiliko ya katiba kwanza, sasa wewe unasemaje on the solution side kwa sababu haya mengi unayoyasema yananihusu mimi tu, mimi sio rais wala anything mimi ni mwananchi kama wewe! Toa mapendekezo ya kuwasaidia wananchi namna ya kujikwamua na situation tuliyonayo!

Mkuu,

Unataka kusema sijawahi kutoa mawazo ya kuwa solution za kuleta maendeleo Tanzania au kuboresha mfumo wa siasa?

Naomba nikukumbushe kwanza kwa kukuomba usome Marshal Plan ya Mchungaji na hasa kipengele cha Uongozi
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-plan-restoration-recovery-plan-tanzania.html

Kisha soma Dynamic Productivity https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/11205-dynamic-productivity-tija-na-maarifa.html

Endelea na Why Vita vya Ufisadi will not win election https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-ufisadi-failed-will-never-win-election.html

KUna Money Matters https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...maendeleo-ubunifu-maadili-na-kujitegemea.html

Pia kuna nyingine tatu za Focus 2010, Chadema must reform na Azimio Jipya, sizioni tena naona mods wamechanganya hoja hivyo sijapata linki zake.

NInachojaribu kuonyesha hapa ni kuwa nimekuwa nikimpigia kelele Kikwete na kumtupia lawama kwa ukali, lakini hata kama ni Amiri Jeshi MKuu, yeye si pekee katika uongozi na CCM ilipaswa kuwa makini kumuongoza hata Mkapa, Mwinyi na Nyerere.

Katika hizo thread nilizokuonyesha hapo juu, solution zake si kwa ajili ya CCM, bali ni kwa ajili ya Taifa zima.

Solution kwa CCM kujisafisha ni kwa watu kuacha kuoneana haya na woga na wafanye kweli ama wafukuze au wajiondoe.
 
Mukulu wa Kaya,

Umesahau mauaji ya Pemba, Mwembechai, Kilombero na Bulyankhulu? Je kibano kilichotokea Tunduru, Kiteto na majuzi Tarime hukukiona?Sina maana kuwa wazee hawa na wale CCM mageuzi ndio waliosababisha umwagaji damu au kipigo kwa wale wanaoipinga CCM, bali wao wakiwa ndani ya CCM kama viongozi na kukaa kwao kimya huku Chama kupitia dola kinawanyanyasa wale wanaokipinga ndio kosa. Ndiyo maana nikaleta mfano wa Sauli, maana Sauli alikuwa mtumishi wa Roma. Alikuwa akifuata utii kutoka kwa Kaisari mkuu wa Roma kunyanyasa Wakristo. Wamenufaika directly au indirectly kutokana na maamuzi mabovu na yasiyo ya haki ambayo yamefanywa na wengine. Sasa kama utaniambia hiyo ndiyo cost ya kuwa politician, then Politics of Tanzania have no ethics or morals!

Mkuu Rev,

- Una maana kwamba maovu yote ya serikali yaliyofanyika Mwalimu akiwa hai yeye anahusika directly? sina hata sababu ya kuyaruida maana ni mengi sana.

- Halafu kama hii mifano yako ni valid basi hawa viongozi wote tulionao leo ni wanafunzi wa nani? Sasa what that tells us kuhusu aliyekuwa Mwalimu wao?

Binafsi sikubaliani kabisa na mifano yako, ambayo ninaiona haielekei kutafuta solutions, badala yake inazidi kutupa lawama kwa wengine, badala ya kukubali our political responsibility kama wananchi, ni sisi wenyewe ndio tumeruhusu kufikishwa tulipo na viongozi wetu,

- sasa Mwanakijiji anaamini kwamba solution ni kumeguka wka CCM, mimi ninasema katiba kwanza ibadilishwe, Mkandara kama ninamuelewa anasema wananchi wabadilike au wabadilishwe political attitude waliyonayo, haya yote kwangu ni part of solutions,

- Sasa ninashindwa kukuelewa exactly kama uko kwenye part ya solutions au unataka kuendelea na upande wa matatizo, maana Tanzania sio ya viongozi wachache walioko ndani ya CCM tu, ni taifa letu hili eti leo 2008 tusubiri Salim na Malecela ndio waje kutuokoa, you got to be kidding me mkuu una maana basi tumeshindwa basi tuwaachie mafisadi!

- Halafu lets say kwamba kilio chako na viongozi wa CCM kuwa wauaji ni cha kweli, hebu niambie ni nani aliyewafundisha kuua wapinzani wao kama hoja yako ni kweli na inaweza kusimama kama solution ya matatizo tuliyonayo sasa bongo? Yaani unataka kusema kuwa walianza tu wenyewe bila mafundisho somewhere?

Mkuu ongea solutions acha hizi political short cuts ideas, tunachotaka ni kujitoa kwenye shimo sasa sio kulaumu nani ametufikisha maana ukweli ni kwamba tumejifikisha wenyewe wananchi wa Tanzania.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom