zakaria masanja
New Member
- Nov 16, 2008
- 1
- 0
ZITTO HAJAPOTEZA WALA HAJAKOSA SIFA KUWA RAIS WA TZ!
Kwanza nakubaliana nanyi kuwa Tanzania kama Taifa tuna uhaba wa viongozi. Sababu kubwa ni hofu. Kwamba kuna baadhi ya watu waliostahili kuwa viongozi lakini kwasababu ya hofa na udhaifu wa kufikiria katika mstari mmoja wa CCM imewawia vigumu kujua kama wanaweza kuwa viongozi ktk nafasi ya Urais nje ya CCM.. Ndio maana binafsi naamini kwamba kwa kadiri tunavyokwenda, tunaweza kutoka nje ya kufikiria CCM, na kuona wanao onesha uwezo nje ya CCM. Nikweli kwamba baada ya Ushindi wa Obama zimeibuka hisia kwa kiwango cha juu kuhusu uwezekano mkubwa wa kijana au vijana wachache wenye dhamira na uwezo kuelekea dhamira zao kuweza kuliokoa Taifa hili. Ni bahati mbaya au nzuri kwamba kwa sehemu kubwa kadiri ninavyokumbana na hisia hizo, Jina Zitto limepata kuwa na nafasi kubwa.
Wanaompinga Zitto wamekuwa wanasukumwa na sababu kubwa mbili, kwanza ni umri wake usiokidhi matakwa ya kikatiba, lakini pia wamekuwa wakihoji sana uzoefu wa Zitto katika kusimamia masuala tete ya Kitaifa. Kwamba pengine utatuzi wa matatizo makubwa ya kitaifa yanahitaji uzoefu mkubwa kuliko alionao Zitto. Nionavyo mimi kwa mazingira ya kisiasa tulionayo, Zitto au mtu aina ya Zitto anaweza kuwa Rais bora kuliko Kikwete na walio wengi kama sio wote ndani ya CCM kwasababu zifuatazo;
1. Kusema Zitto hana umri unao ruhusiwa kikatiba ni sawa na kusema Watanzania wapo kwa ajili ya Katiba badala ya Katiba kuwepo kwa ajili ya Watanzania. Na mpaka sasa sioni mantiki yoyote ya msingi kwanini umri wa mgombea urais kuwa miaka 40 na sio miaka 35 au hata 30. Labda wengine watachangia uzoefu wa nchi zingine duniani ktk hili. Lakini hii bado ni changamoto kwa vijana na wazee watanzania kuendelea kutafakari kama kuna uhusiano kati ya uwezo wa mtu kuwa Rais na Umri wa miaka 40.
2. Kwamba Zitto hakuonesha umakini kukubali uteuzi wa Rais kwenye Kamati ya Bomani, na hivyo hafai kuwa Rais ni sawa nakumuonea bure kijana huyu. Labda ili tutoe hukumu halali katika hili tujiulize, Hivi ushiriki wa Zitto kwenye Kamati ya Bomani umeleta hasara na faida gani? na Je, kama asingeshiriki Taifa lingepata hasara au faida gani?. Nadhani huu ndio msingi wa kupima usahihi na ama udhaifu wa uamuzi wa Zitto. Labda changamoto inayoweza kuendelea kujadiliwa ni kama baada ya Zitto kushiriki ktk kamati hiyo anafanya nini zaidi kuhakikisha alichokitaka kinatokea kweli.
3. Ni kweli kwamba Zitto hana uzoefu kama alinao Kikwete, Lakini faida ya uzoefu ni nini?. Maana kimsingi uzoefu unamsaidia kiongozi kujua masuala mengi kwa kina na hivyo kujmweka kwenye nafasi ya kufanya maamuzi kwa haraka na kwa usahihi mara kwa mara kama sio wakati wote. Lakini ukimtazama Kikwete na walio wengi ndani ya CCM hawana uzoefu kwasababu hiyo. Zitto ni kijana anayebadilika kwa kasi katika jinsi anavyoyatazama mambo. Nikikumbuka siku ya mjadala wa buzwagi bungeni alivyokuwa anawadhibiti wabunge wa CCM kwa hoja na vielelezo kutoka kwenye mabuku mbalimbali aliyokuwa amerundika mezani kwake, ilitosha kujua kuwa kijana huyu ana uwezo mkubwa wa kupambambanua mambo...Lakini tusishau kuwa Zitto amewahi kuwa kwenye timu inayomshauri Rais wa Ujerumani kuhusu masuala ya uchumi, na Sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mashirika ya Umma, kazi ambayo hapana shaka ufanisi wake sio wakuhojika sana kama ingebidi tuzingatie umri na uzoefu wake...Na hivi karibuni tumeambiwa amechaguliwa kwenye timu ya wabunge wanaoshughulikia migogoro ya kisiasa duniani...Nakiri kwamba kama Zitto akigombea urais hii inaweza kuwa hoja, lakini bado kuna mengi ya kutafakari kuhusu nafasi ya urais mbele zaidi ya uzoefu...Kama wamarekani walivyomtazama Obama mbele zaidi ya Uzoefu wa Mac Cain, ndivyo ilivyo kwa Zitto. Kumshindaniosha Zitto na Kikwete ktk eneo la Uzoefu ni kama ambavyo mtu angemshindanisha Obama na Mac Cain katika eneo moja la uzoefu na kufanya uamuzi.
4. Lakini zaidi ya hapo, Zitto anawakilisha tabaka la wasomi vijana wazalendo, aliyeamua kufanya kazi ya kujenga upinzani tangu awali, na hakuna rekodi tofauti ktk uamuzi huo. viongozi wa namna hii hawana mizigo kama walionayo CCM ya kutoka awamu moja kwenda nyingine. Ndio maana siamini kama kiongozi mbadala anaweza kutoka ndani ya CCM. Ndani ya CCM ni visasi na malumbano ya nani ni nani katka awamu gani? basi. Nachokubali ni kwamba CCM ikipasuka itarahisisha upinzani kushinda na kujenga uongozi mbadala, lakini upinzani usije kurogwa kusumbili viongozi wa kuongoza Taifa hili kwa maana ya urais kutoka ndani ya CCM. Litakuwa kosa kubwa kutokea. Na historia itawahukumu vibaya. tunahitaji damu isiyofungamana na mizigo ya hisia chafu, fitina za awamu hadi awamu, wala mizigo ya ufisadi kutoka awamu moja hadi nyingine.
5.Kikubwa ninachokiona kwa Zitto ni kuwa mtu mwenye dhamira isiyohijika kirahisi, kijana mwenye moyo wa simba anapopambana, mwenye kutazama siasa juu ya vyama, aliyepata bahati ya kukubalika na hivyo fursa ya kushawishi mabadiliko(hii ni bidhaa adimu sana na muhimu sana), asiyehofu kufanya maamuzi magumu ambayo yanaweza yasiupendeze Umma au jamii inayomzunguka ktk wakati fulani(Unpopular decision) lakina anayasimamia, na wakati huohuo kuwa tayari kubadili maamuzi yake anapobaini hayakuwa kwenye misingi sahihi.
6. Ni kweli kwamba akiwa mwanadamu, na katika umri wa ujana anaweza kuwa na mapungufu kadhaa wa kadhaa..Lakini muhimu tutafakari Taifa letu linataka nini kwasasa? na hivyo ni kiongozi wa aina gani anahitajika kwa majukumu hayo, kisha tuwapime viongozi tulionao katka hayo...Lakini kitu kimoja muhimu ni kwamba kwa vigezo vyovyote anuai vinavyoweza kuwekwa, ni jambo dhahiri kwamba Zitto atamshinda Kikwete kwa mbali kabisa....Labda CCM ilete mtu mwingine ashindanishwe na Zitto, Siyo Jakaya Jamani!..... Huyu Kikwete?...Tuendelee kujadili.
NDIYO, TUNAWEZA!
Kwanza nakubaliana nanyi kuwa Tanzania kama Taifa tuna uhaba wa viongozi. Sababu kubwa ni hofu. Kwamba kuna baadhi ya watu waliostahili kuwa viongozi lakini kwasababu ya hofa na udhaifu wa kufikiria katika mstari mmoja wa CCM imewawia vigumu kujua kama wanaweza kuwa viongozi ktk nafasi ya Urais nje ya CCM.. Ndio maana binafsi naamini kwamba kwa kadiri tunavyokwenda, tunaweza kutoka nje ya kufikiria CCM, na kuona wanao onesha uwezo nje ya CCM. Nikweli kwamba baada ya Ushindi wa Obama zimeibuka hisia kwa kiwango cha juu kuhusu uwezekano mkubwa wa kijana au vijana wachache wenye dhamira na uwezo kuelekea dhamira zao kuweza kuliokoa Taifa hili. Ni bahati mbaya au nzuri kwamba kwa sehemu kubwa kadiri ninavyokumbana na hisia hizo, Jina Zitto limepata kuwa na nafasi kubwa.
Wanaompinga Zitto wamekuwa wanasukumwa na sababu kubwa mbili, kwanza ni umri wake usiokidhi matakwa ya kikatiba, lakini pia wamekuwa wakihoji sana uzoefu wa Zitto katika kusimamia masuala tete ya Kitaifa. Kwamba pengine utatuzi wa matatizo makubwa ya kitaifa yanahitaji uzoefu mkubwa kuliko alionao Zitto. Nionavyo mimi kwa mazingira ya kisiasa tulionayo, Zitto au mtu aina ya Zitto anaweza kuwa Rais bora kuliko Kikwete na walio wengi kama sio wote ndani ya CCM kwasababu zifuatazo;
1. Kusema Zitto hana umri unao ruhusiwa kikatiba ni sawa na kusema Watanzania wapo kwa ajili ya Katiba badala ya Katiba kuwepo kwa ajili ya Watanzania. Na mpaka sasa sioni mantiki yoyote ya msingi kwanini umri wa mgombea urais kuwa miaka 40 na sio miaka 35 au hata 30. Labda wengine watachangia uzoefu wa nchi zingine duniani ktk hili. Lakini hii bado ni changamoto kwa vijana na wazee watanzania kuendelea kutafakari kama kuna uhusiano kati ya uwezo wa mtu kuwa Rais na Umri wa miaka 40.
2. Kwamba Zitto hakuonesha umakini kukubali uteuzi wa Rais kwenye Kamati ya Bomani, na hivyo hafai kuwa Rais ni sawa nakumuonea bure kijana huyu. Labda ili tutoe hukumu halali katika hili tujiulize, Hivi ushiriki wa Zitto kwenye Kamati ya Bomani umeleta hasara na faida gani? na Je, kama asingeshiriki Taifa lingepata hasara au faida gani?. Nadhani huu ndio msingi wa kupima usahihi na ama udhaifu wa uamuzi wa Zitto. Labda changamoto inayoweza kuendelea kujadiliwa ni kama baada ya Zitto kushiriki ktk kamati hiyo anafanya nini zaidi kuhakikisha alichokitaka kinatokea kweli.
3. Ni kweli kwamba Zitto hana uzoefu kama alinao Kikwete, Lakini faida ya uzoefu ni nini?. Maana kimsingi uzoefu unamsaidia kiongozi kujua masuala mengi kwa kina na hivyo kujmweka kwenye nafasi ya kufanya maamuzi kwa haraka na kwa usahihi mara kwa mara kama sio wakati wote. Lakini ukimtazama Kikwete na walio wengi ndani ya CCM hawana uzoefu kwasababu hiyo. Zitto ni kijana anayebadilika kwa kasi katika jinsi anavyoyatazama mambo. Nikikumbuka siku ya mjadala wa buzwagi bungeni alivyokuwa anawadhibiti wabunge wa CCM kwa hoja na vielelezo kutoka kwenye mabuku mbalimbali aliyokuwa amerundika mezani kwake, ilitosha kujua kuwa kijana huyu ana uwezo mkubwa wa kupambambanua mambo...Lakini tusishau kuwa Zitto amewahi kuwa kwenye timu inayomshauri Rais wa Ujerumani kuhusu masuala ya uchumi, na Sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mashirika ya Umma, kazi ambayo hapana shaka ufanisi wake sio wakuhojika sana kama ingebidi tuzingatie umri na uzoefu wake...Na hivi karibuni tumeambiwa amechaguliwa kwenye timu ya wabunge wanaoshughulikia migogoro ya kisiasa duniani...Nakiri kwamba kama Zitto akigombea urais hii inaweza kuwa hoja, lakini bado kuna mengi ya kutafakari kuhusu nafasi ya urais mbele zaidi ya uzoefu...Kama wamarekani walivyomtazama Obama mbele zaidi ya Uzoefu wa Mac Cain, ndivyo ilivyo kwa Zitto. Kumshindaniosha Zitto na Kikwete ktk eneo la Uzoefu ni kama ambavyo mtu angemshindanisha Obama na Mac Cain katika eneo moja la uzoefu na kufanya uamuzi.
4. Lakini zaidi ya hapo, Zitto anawakilisha tabaka la wasomi vijana wazalendo, aliyeamua kufanya kazi ya kujenga upinzani tangu awali, na hakuna rekodi tofauti ktk uamuzi huo. viongozi wa namna hii hawana mizigo kama walionayo CCM ya kutoka awamu moja kwenda nyingine. Ndio maana siamini kama kiongozi mbadala anaweza kutoka ndani ya CCM. Ndani ya CCM ni visasi na malumbano ya nani ni nani katka awamu gani? basi. Nachokubali ni kwamba CCM ikipasuka itarahisisha upinzani kushinda na kujenga uongozi mbadala, lakini upinzani usije kurogwa kusumbili viongozi wa kuongoza Taifa hili kwa maana ya urais kutoka ndani ya CCM. Litakuwa kosa kubwa kutokea. Na historia itawahukumu vibaya. tunahitaji damu isiyofungamana na mizigo ya hisia chafu, fitina za awamu hadi awamu, wala mizigo ya ufisadi kutoka awamu moja hadi nyingine.
5.Kikubwa ninachokiona kwa Zitto ni kuwa mtu mwenye dhamira isiyohijika kirahisi, kijana mwenye moyo wa simba anapopambana, mwenye kutazama siasa juu ya vyama, aliyepata bahati ya kukubalika na hivyo fursa ya kushawishi mabadiliko(hii ni bidhaa adimu sana na muhimu sana), asiyehofu kufanya maamuzi magumu ambayo yanaweza yasiupendeze Umma au jamii inayomzunguka ktk wakati fulani(Unpopular decision) lakina anayasimamia, na wakati huohuo kuwa tayari kubadili maamuzi yake anapobaini hayakuwa kwenye misingi sahihi.
6. Ni kweli kwamba akiwa mwanadamu, na katika umri wa ujana anaweza kuwa na mapungufu kadhaa wa kadhaa..Lakini muhimu tutafakari Taifa letu linataka nini kwasasa? na hivyo ni kiongozi wa aina gani anahitajika kwa majukumu hayo, kisha tuwapime viongozi tulionao katka hayo...Lakini kitu kimoja muhimu ni kwamba kwa vigezo vyovyote anuai vinavyoweza kuwekwa, ni jambo dhahiri kwamba Zitto atamshinda Kikwete kwa mbali kabisa....Labda CCM ilete mtu mwingine ashindanishwe na Zitto, Siyo Jakaya Jamani!..... Huyu Kikwete?...Tuendelee kujadili.
NDIYO, TUNAWEZA!