William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,588
- 10,375
Tatizo hapa ni kuwa CCM tayari imeamua kufanya mabadiliko makubwa ya Katiba mwakani na hivyo kumeza kabisa hoja ya Katiba mpya.
Kwa kuteka hoja ya mabadiliko ya Katiba (nasema "kuteka" kwa sababu mara kadhaa sasa serikali imetoa tamko rasmi kuwa hakuna haja ya mabadiliko ya katiba kwani iliyopo inajitosheleza) CCM inajitengenezea uwanja wa kushinda kwa urahisi na hivyo hata wapinzani wakisema "tunataka Katiba Mpya" CCM inasema hakuna haja "tayari tunaifanyia mabadiliko katika mswada wa "mabadiliko ya 22 ya Katiba" na wale wenye mapendekezo wayatoe kwa wizara ya Katiba na Sheria."
Hivyo, hoja ya mabadiliko ya Katiba haiendi popote kwani ni hoja ambayo CCM wameshajua kuwa itawatengenezea ujiko mkubwa zaidi kuliko mambo ya ufisadi. HIvyo kama kuna nguvu nje ya CCM basi siamini kuwa zitatokana na mjadala wa Katiba, CCM is too smart for that.
Mkuu MMJ,
Heshima mbele, ninakubali hoja zako nyingi kwenye hii post kwa sababu zinajitosheleza, lakini bado nina tatizo kidogo hapo juu kuhusu katiba na CCM,
- Tunao mfano mzito sana wa ripoti ya Hosea na Richimonduli, kwa sababu ni clear kwamba Lowassa alijaribu kuwa too smart kama unavyowabatiza CCM hapa, lakini mbele ya nguvu ya wananchi hakuweza kutushinda,
Sasa hata kwenye hili la katiba, CCM haiwezi kushindana na nguvu ya wananchi iliyoshikamana na kusimama imara, lakini one thing sisi wananchi hatuwezi kutegemea nguvu ya wanachama wachache ndani ya CCM, kutusaidia kuleta mabadiliko kwa wananchi wote wa Tanzania, infact historia iko wazi kwamba tunahitaji kuwa waangalifu sana maana kwa mtaji huo wa watu wachache tunaweza kuangukia kwenye ule mtego uliotaka kuwapata wa-China na lile kundi la watu wanne.