William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,588
- 10,375
Jamani tusiwe vipofu ktk hoja ambayo ni muhimu..Field marshall Es kasema ukweli mtupu ambao hauhitaji maelezo mengi..
Kama CCM ni kisiki itakuwaje mtu usubiri hadi kimeguke!.. hali hiyo itatokana na kitu gani? tusubiri hali ya hewa ya ukame ama!..
Kama alivyosema kuanzishwa kwa vyama vya Upinzani kulitokana na Ulazima uliotakiwa toka nchi za nje na CCM walijenga vyombo hivi kuuhadaa Ulimwengu.. Mrema na Seif Sharrif walitoka wakiwa na uhakika na nafasi za juu zenye posho na mshiko safi kama vile wako CCM.. tatizo lilikuja tu pale tamaa za kibinadamu zilipoingia kwa hawa jamaa. Mrema aliona upenyo wa kuweza kushinda Uchaguzi, akafanya kweli nje ya makubaliano.. Seif Pia aliona upenyo wa kuchukua Uongozi Zanzibar, CCM wakabadilisha Uwakilishi ktk serikali ya Muungano...Bahati yake ni kwamba hadi leo jhii bado ni tishio kubwa kwa CCM lakini wmeshamtafutia dawa..
CCM haiwezi kumeguka kirahisi wakubwa zangu kwani kila mkulu alipo ndani ya CCM anakatiwa chake kisawasawa, huku nje hakuna nuru na wale wote waliojaribu kujimegua wamerudi wenyewe..
Wee fikira tu majuzi Kikwete amekebehi UJAMAA wakati huu ndio mwongozo wa chama chake na Imani ya chama inasema - Ujamaa na kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru!..
Lakini la kuchekesha viongozi wote ndani ya chama walimpigia makofi na kumshangilia wakati akikitukana chama chake mwenyewe akitumia neno Upinzani..Na ajabu kubwa ni kwamba Upinzani hawakurudisha majibu.
Mkuu wangu kisiki hiki hakiwezi kuondoka bila zana maalum za kung'oa visiki na watu wenye moyo na imani kubwa isiyofungamana na woga wa Uchawi..
CCM sio tu kisiki cha mkorosho, hiki ni kisiki sawa na ule mbuyu wa St. Peters, njia panda kwenda Masaki.
Tumejenga barabara kuuzunguka, measure zetu ni kutazama kama uwezekano wa usafiri bado unawezekana bila kukiondoa kisiki hicho..
Mkuu Bob,
Heshima mbele mkuu kwa kuuona ukweli, sina la kuongeza mkuu!