Kizimkazimkuu
JF-Expert Member
- Nov 8, 2007
- 337
- 234
Kikao kilichoitishwa na Katibu wa CCM mkoa wa K'njaro ndg. KAZIDI, wiki chache kabla ya kuanza kwa kampeni za uchaguzi na kuhudhuriwa na wanafunzi wa vyuo kadhaa vya mjini Moshi, kiliazimia kuwa kila mhudhuriaji atafute orodha ya wanafunzi ambao wamejiandikisha kupiga kura katika jimbo la moshi mjini lakini hawataweza kupiga kupiga kura kufuatia kuwa likizo nje ya manispaa ya Moshi na kuiwakilisha orodha hiyo kwake na wanafunzi hao watapewa fedha za nauli (go and return) na fedha za kujikimu wakati wakisubiri kupiga kura.
Hii itawahusu wanafunzi wote popote walipo Tanzania hii,ilimradi walijiandikisha kupiga Kura Moshi mjini. Katika kikao hicho, wahudhuriaji walipewa sh 10,000 za 'soda' na kuhakikishiwa kuwa kampeni zitakapoanza fedha itakuwa sio tatizo! Ndg. KAZIDI alieleza kuwa CCM moshi mjini itafanya kampeni kutumia wasomi ambao wanaelewa kwani inaonekana watu wa kawaida hawaambili juu ya mzee Ndesamburo!
Hii itawahusu wanafunzi wote popote walipo Tanzania hii,ilimradi walijiandikisha kupiga Kura Moshi mjini. Katika kikao hicho, wahudhuriaji walipewa sh 10,000 za 'soda' na kuhakikishiwa kuwa kampeni zitakapoanza fedha itakuwa sio tatizo! Ndg. KAZIDI alieleza kuwa CCM moshi mjini itafanya kampeni kutumia wasomi ambao wanaelewa kwani inaonekana watu wa kawaida hawaambili juu ya mzee Ndesamburo!