Elections 2010 CCM Kuilalamikia Chadema NEC

The Invincible

JF-Expert Member
May 6, 2006
6,003
3,269
Katika taarifa ya habari ya TBC1 saa mbili usiku huu, makamu mwenyekiti wa CCM bara Pius Msekwa amenukuliwa akisema kwamba Chadema wameanza kampeni kabla ya muda.

Kutokana na hilo, katibu wa CCM taifa, Yusufu Makamba atapeleka malalamiko yao huko tume ya taifa ya uchaguzi, yaani NEC.

Mambo yameanza. Ngoma inogile.
 


Bahati mbaya sana inaonekana wote hawa hawajui sheria! kwa sababu kama hilo ni kweli itabidi waelezee na kutetea yale waliyoyafanya kwa kuwatembeza wagombea wao vijijini katika kura za maoni. Wataelezea ni tofauti gani kati ya "kumtambulisha mgombea wa CCM" na hotuba za JK aliposema kuwa "endapo mkinichagua".. Waache uhuni wa kisiasa; kama kampeni hazikuanza wakati CCM wanatafuta wadhamini, na kumtambulisha mgombea wao basi kampeni hazijaanza kwa Chadema kutafuta wadhamini na kumtambulisha mgombea wao..

Vinginevyo, itakuwa ni yale ya "mkuki kwa nguruwe mtamu..."

Hizi ni picha za tukio hilo la leo toka wavuti.com

1386426.jpg
Dk.Wilbrod Slaa akionesha fomu za ugombea kiti cha Uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania punde tu baada ya kuzichukua kutoka katika ofisi za NEC alipokabidhiwa na Jaji Lewis Makame.









Hadi kufikia tarehe ya leo, vyama tisa vimewakilishwa na wagombea wao kuchukua fomu za kinyang'anyiro cha Uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.​

credit source: http://www.wavuti.com/4/post/2010/08/wilbroad-slaachadema-wachukua-fomu-toka-nec.html#ixzz0w8y6bwO4
 
Last edited by a moderator:
CCM wamesahahu hii

attachment.php


Wakati wa mkutano ule wa Dodoma, Kikwete alisema mengi mazuri ambayo serikali yake imefanikiwa kuyafanya na akaahidi kufanya mazuri zaidi akichaguliwa tena kuendelea na urais, je hiyo ilikuwa kampeini? tena alikuwa akitangazwa wazi wazi kwa taifa zima kupitia vyombo vya habari vya serikali.

MbioZaUchaguzi.jpg
 


Bahati mbaya sana inaonekana wote hawa hawajui sheria! kwa sababu kama hilo ni kweli itabidi waelezee na kutetea yale waliyoyafanya kwa kuwatembeza wagombea wao vijijini katika kura za maoni. Wataelezea ni tofauti gani kati ya "kumtambulisha mgombea wa CCM" na hotuba za JK aliposema kuwa "endapo mkinichagua".. Waache uhuni wa kisiasa; kama kampeni hazikuanza wakati CCM wanatafuta wadhamini, na kumtambulisha mgombea wao basi kampeni hazijaanza kwa Chadema kutafuta wadhamini na kumtambulisha mgombea wao..

Vinginevyo, itakuwa ni yale ya "mkuki kwa nguruwe mtamu..."


Mkuu Mwanakijiji nilianzisha Thread hapa nikasema CCM wameanza kampeni kwa Mwamvuli wa kura za maoni ( Ila siioni ile thread) nikaonya NEC wasije baadaye wakawa mbogo endapo vyama vingine navyo vikafanya hivyohivyo sasa naona yanatimia
 
Last edited by a moderator:
Hawa wazee wa CCM naona akili zao zimezeeka

Mkuu wamezeeka kama chama chao kilivo zeeka na kuoza, kinapumua kwa oxygeni ya nguvu ya dola jesh na TISS period!
By the way hii inatia moyo kwamba woga umeisha wajaa wanaanza kulia lia sasa!, tulizoe kusikia vyama pinzani vikilalamika nao wakivibeza kwamba ni walalmishi tu, sasa ngoma inogile.. wamenza onja joto ya upinzani kabla ya 31 ocotber!

Go, go our president Dr. Wa slaa
 
Tatizo la nyani haoni kundule. CCM wenyewe wanafikiri ni smart sana lakini tatizo hawajui kwamba wameishapitwa na wakati.
 
Hizi ni dalili za mwanzo kuwa mambo si shwari huko CCM.MAJI YA SHINGO....
 
hayawi hayawi mwisho karibu yanakuwa, zamani ilikuwa sisi leo wao.
Hawa jamaa Msekwa na Makamba hawana hata mshipa wa aibu vurugu zote walizofanya wakati wa kura za maoni hazitoshi.........walidhani kura ya maoni itafunika vyama vingine kumbe imewafunika wao kwa rushwa, sasa wanaanza kulialia LOL! makubwa mazima hamnazo kabisa kwishneiy.

ngoja niimbe kidogo......wameuona mpilipili na maua yake mchikicha.....oooo hayo.....nimesahau unavyoendelea.......
 
Mkuu wamezeeka kama chama chao kilivo zeeka na kuoza, kinapumua kwa oxygeni ya nguvu ya dola jesh na TISS period!
By the way hii inatia moyo kwamba woga umeisha wajaa wanaanza kulia lia sasa!, tulizoe kusikia vyama pinzani vikilalamika nao wakivibeza kwamba ni walalmishi tu, sasa ngoma inogile.. wamenza onja joto ya upinzani kabla ya 31 ocotber!

Go, go our president Dr. Wa slaa
kwa kawaida ukiona mtu ameanza woga na kutetemeka tisha kama unamsogelea anaweza kujikoj......(samahani). Kinachotakiwa sasa Chadema iendelee kutisha nakuwasogelea hadi jikoni wampelekee kadi hata Makamba ikiwezekana, si mbali trh 14 mtikisiko unakuja wautumie huo baada ya hapo kitakachobaki ni kama kumsukuma mlevi.
 
Hili ni tatizo lazima tuliseme. CCM km wamefanya kampeni ni kosa na haimaanishi basi na CHADEMA wafanye. Kuna sheria na suala la msingi ni kuangalia sheria zinasemaje? Ukweli kinachofanyika ni kampeni. Mf km wafanyakazi nipeni kura zenu, kina mama nk. Dr Slaa sio wa kwanza kuomba wadhamini lakini style inayotumika ni kampeni. Kwahiyo km CCM wamelalamika, kwanini CHADEMA hawakulalamika??? Ni vyema kama kuna sheria sote tujifunze kuishi kwa sheria maana two wrongs...
 
Hili ni tatizo lazima tuliseme. CCM km wamefanya kampeni ni kosa na haimaanishi basi na CHADEMA wafanye. Kuna sheria na suala la msingi ni kuangalia sheria zinasemaje? Ukweli kinachofanyika ni kampeni. Mf km wafanyakazi nipeni kura zenu, kina mama nk. Dr Slaa sio wa kwanza kuomba wadhamini lakini style inayotumika ni kampeni. Kwahiyo km CCM wamelalamika, kwanini CHADEMA hawakulalamika??? Ni vyema kama kuna sheria sote tujifunze kuishi kwa sheria maana two wrongs...
Kikwete kule Dodoma hakuomba kura ili aendeleze mafanikio ambayo hayapo unataka kutuambia nini au unajifanya hukumbuki acha kuleta za kuleta watu wanakumbukumbu tunazo hadi kanda zake tutazirusha BBC mkikatalia redio zenu, mwaka huu kama kudata tumedata mmezoea sana nyie.
 
Kikwete kule Dodoma hakuomba kura ili aendeleze mafanikio ambayo hayapo unataka kutuambia nini au unajifanya hukumbuki acha kuleta za kuleta watu wanakumbukumbu tunazo hadi kanda zake tutazirusha BBC mkikatalia redio zenu, mwaka huu kama kudata tumedata mmezoea sana nyie.
Labda ni kueleze sina sababu ya kuleta za kuleta maana hata sizijui hizo za kuleta. Mwishoni nimesema two wrongs......Lakini pia CCM wanaweza kuwa na hoja kuwa wao walikuwa kwenye mkutano wao wa KICHAMA ambao unahusisha wanachama wa chama husika na ridhaa alikuwa akiiomba ndani ya CHAMA. Lakini hili la Slaa ni kwamba ridhaa inaombwa kwa Watanzania. Ingawa kiuhalisia ni vigumu kuwaomba wananchi udhamini bila kuwaeleza utawafanyia nini, lakini wakati wa kuomba udhamini huo unaweza kuwa umepitiliza kwenye kampeni kama utagusia CHAMA kingine. Its abit technical lakini hili lisitufanye viziwi kuwa hatutambui uwepo na mamlaka ya Taasisi zetu. Maana kama hatutaheshimu taasisi zilizopo kisheria basi kwa vyovyote vile malengo yetu pia yanakuwa ni yenye mashaka.
 
Hivi si ni hawa walisema hawaigopi CHADEMA wala Dr. Slaa????????????? I would have thought wangelalamika kama Lipumba na CUF wangekuwa wamefanya hivyo kwani Makamba alitwambia hao ndiyo tishio................

Would CCM bother lets say Mziray akitembea nchi nzima kuomba udhamini???????????

Yaani hizi kweli ni dalili za ulevi, pamoja na mminyo wote huu wa media bado jamaa wanalalamika? Tatizo kubwa la CCM as of now ni ile feeling ya entitlement, they just feel they are entitled to rule, kushangiliwa, kupigiwa makofi, kuaminiwa, kupendwa etc. And if some guy or an organization seem to be about that basi wanaweweseka.

Shame on you CCM.
 
Hili ni tatizo lazima tuliseme. CCM km wamefanya kampeni ni kosa na haimaanishi basi na CHADEMA wafanye. Kuna sheria na suala la msingi ni kuangalia sheria zinasemaje? Ukweli kinachofanyika ni kampeni. Mf km wafanyakazi nipeni kura zenu, kina mama nk. Dr Slaa sio wa kwanza kuomba wadhamini lakini style inayotumika ni kampeni. Kwahiyo km CCM wamelalamika, kwanini CHADEMA hawakulalamika??? Ni vyema kama kuna sheria sote tujifunze kuishi kwa sheria maana two wrongs...

sheria zina aply kama kuna fair ground of competition, kama chadema walio kuwa ccm wamecheza rafu wanajua kuwa kulalamika kwa NEC kuwa ccm wamefanya rafu ni sawa na kupoteza muda kwani NEC ni mtoto wa ccm. Walichofanya chadema waka retaliate. Kama wagombea wa ubunge ccm wamefanya mikutano ya wazi ikaonekana sawa. Leo chadema yaonekana imekiuka taratibu ah! Sitaki kuamini
i-reverse two wrong... Into two right... Maana chadema walifuata utaratibu wao ndani ya chama kama ccm walivyofanya
 
Hili ni tatizo lazima tuliseme. CCM km wamefanya kampeni ni kosa na haimaanishi basi na CHADEMA wafanye. Kuna sheria na suala la msingi ni kuangalia sheria zinasemaje? Ukweli kinachofanyika ni kampeni. Mf km wafanyakazi nipeni kura zenu, kina mama nk. Dr Slaa sio wa kwanza kuomba wadhamini lakini style inayotumika ni kampeni. Kwahiyo km CCM wamelalamika, kwanini CHADEMA hawakulalamika??? Ni vyema kama kuna sheria sote tujifunze kuishi kwa sheria maana two wrongs...

....inafurahisha zaidi kuona kuwa unatambua kuwa hata anayeenda kushitaki NEC u/anajua kuwa na ye alikosea..............
 
1. Hotuba za kejeli zilizotolewa na wajumbe wa mkutano mkuu maalumu Dodoma
2. Mbango yaliyobandikwa njiani, (why CHADEMA wasiyakusanye hayo kama ushahidi?)
3. Kura za Maoni huku vijijini (mfano wilayani Makete) Kila mwananchi aliruhusiwa kushiriki kusikia wagombea wa CCM wakijinadi na tuliuliza maswali bila hata kuulizwa kama tuna kadi za CCM
4. Kumtangaza mgombea mwenza wa CCM, Jamhuri Dom, Unguja, Pemba na Jangwani
5. CCM imefanya kampeini kubwa zaidi kwani kila Tawi wamefika na wagombea wao wa ubunge na madiwani.
6. Matumizi ya TBC1

Nadhani CHADEMA wasilishe malalmiko yao kimya kimya watakapokuja na yao iwe kazi ya NEC Kusuruhisha.
 
Bahati mbaya sana inaonekana wote hawa hawajui sheria! kwa sababu kama hilo ni kweli itabidi waelezee na kutetea yale waliyoyafanya kwa kuwatembeza wagombea wao vijijini katika kura za maoni. Wataelezea ni tofauti gani kati ya "kumtambulisha mgombea wa CCM" na hotuba za JK aliposema kuwa "endapo mkinichagua".. Waache uhuni wa kisiasa; kama kampeni hazikuanza wakati CCM wanatafuta wadhamini, na kumtambulisha mgombea wao basi kampeni hazijaanza kwa Chadema kutafuta wadhamini na kumtambulisha mgombea wao..

Umenena sawa kabisa MMKJ. Naona NEC itafanya mkutano Dar na viongozi wa pande zote na kutatua hili. Wametoa taarifa ya huo mkutano. Ni sala yangu kwamba NEC hawatakubali kuwa vibaraka wa CCM.

Ila zikishaanza kampeni, itabidi CHADEMA iangalie sana muda wanaopewa CCM kwenye vyombo vya habari. Ukiangalia kwenye website ya NEC uatona hivi:

The National Electrol Commission of Tanzania - Homepage

"The Candidate for the office of the President and Vice-President of the United Republic of Tanzania and Political Parties participating in an election have the right to use public-owned media during the official period of elections campaigns.

The Commission, after consultation with the candidate and Political Parties concerned and officers responsible for the public owned media coordinates the programmes of broadcasting.

Every public-owned media which publishes or broadcasts any information relating to the electoral process is guided by the principle of total impartiality and shall refrain from any discrimination in relation to any candidate and in the amount of space dedicated to them".

The emphasis is mine
 
Back
Top Bottom