CCM kidedea umeya Sumbawanga

KAUMZA

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
699
237
Kwa mara nyingine tena CCM kimetwaa kiti cha umeya ktk manispaa ya Sumbawanga baada ya meya wa awali kujiuzulu kutokana na "kashfa" ya kuwa na elimu ndogo.
 
Kwa mara nyingine tena CCM kimetwaa kiti cha umeya ktk manispaa ya Sumbawanga baada ya meya wa awali kujiuzulu kutokana na "kashfa" ya kuwa na elimu ndogo.
toa habari iliyokamilika,mfano uchaguzi umefanyika lini na wapiga kura walikuwa walikuwa wangapi.
 
Kaumza wewe ni seniour jf member toa habari kamili ubabaishaji hausaidii jamvini
 
BARAZA la madiwani la Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa limemchagua Sabas Katepa ambaye ni diwani wa kata ya Ntendo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Meya mpya wa manispaa hiyo.

Uchaguzi wa kumpata Meya umefanyika kwenye ukumbi wa manispaa hiyo, ambapo Mkurugenzi wa uchaguzi huo, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga, Silvia Siriwa alimtangaza Kapeta kuwa mshindi kwa kupata kura 16 akimshinda, Field Kasitu aliyegombea kwa tiketi ya Chadema na kuambulia kura 4.

Diwani mmoja wa CCM hakupiga kura kutokana na kuwa na udhuru. Uchaguzi huo umefanyika kufuatia kujiuzulu Januari 28 mwaka huu kwa aliyekuwa Meya wa Manispaa hiyo, Samwel Kisabwiti kupitia CCM kwa madai ya kulinda heshima yake binafsi na ya chama chake.

Kisabwiti ambaye ana elimu ya darasa la saba alifikia uamuzi huo baada ya kutambua kwamba meya ni mtu muhimu na anatakiwa kuwa na elimu ya kutosha ili aweze kufanya kazi kwa ufanisi, alihitaji kupata muda wa kutosha ili ajifunze.

Meya huyo amedumu katika nafasi hiyo kwa mwezi mmoja na nusu, alichaguliwa kushika nafasi hiyo Desemba 17, mwaka jana ambapo alikuwa mgombea pekee baada ya mgombea wa
Chadema kujitoa.

Akizungumza mara baada ya kuchaguliwa na madiwani hao, Katepa alisema kuwa uchaguzi ulikuwa mgumu kwa upande wake, lakini anashukuru Mungu kwa kupata nafasi hiyo na hatakikisha anasimamia kwa ukaribu mapato na matumizi ya halmashauri hiyo ambayo ina vyanzo vichache vya mapato, lakini vikisimamiwa vizuri vitasaidia kuondoa kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Aliongeza kuwa katika kipindi chote akiwa kwenye nafasi hiyo atajitahidi kuhakikisha manispaa haipati hati chafu, inayoweza kusababishia kukosa fedha za ruzuku kutoka Serikali kuu.

Halmashauri hiyo ina madiwani 21 kati yao 16 ni wa CCM, wanne wa Chadema na mmoja ni diwani kupitia tiketi ya DP.

Source: HabariLeo
 
Kulikuwa hakuna element za kuchakachua...maana hawa jamaa ni moja ya sera zao......
 
Ongera zao maana siasa si chuki wala vita kama walistahili ushindi na wameshinda wanastahili pongezi pia
 
BARAZA la madiwani la Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa limemchagua Sabas Katepa ambaye ni diwani wa kata ya Ntendo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Meya mpya wa manispaa hiyo.

Uchaguzi wa kumpata Meya umefanyika kwenye ukumbi wa manispaa hiyo, ambapo Mkurugenzi wa uchaguzi huo, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga, Silvia Siriwa alimtangaza Kapeta kuwa mshindi kwa kupata kura 16 akimshinda, Field Kasitu aliyegombea kwa tiketi ya Chadema na kuambulia kura 4.

Diwani mmoja wa CCM hakupiga kura kutokana na kuwa na udhuru. Uchaguzi huo umefanyika kufuatia kujiuzulu Januari 28 mwaka huu kwa aliyekuwa Meya wa Manispaa hiyo, Samwel Kisabwiti kupitia CCM kwa madai ya kulinda heshima yake binafsi na ya chama chake.

Kisabwiti ambaye ana elimu ya darasa la saba alifikia uamuzi huo baada ya kutambua kwamba meya ni mtu muhimu na anatakiwa kuwa na elimu ya kutosha ili aweze kufanya kazi kwa ufanisi, alihitaji kupata muda wa kutosha ili ajifunze.

Meya huyo amedumu katika nafasi hiyo kwa mwezi mmoja na nusu, alichaguliwa kushika nafasi hiyo Desemba 17, mwaka jana ambapo alikuwa mgombea pekee baada ya mgombea wa
Chadema kujitoa.

Akizungumza mara baada ya kuchaguliwa na madiwani hao, Katepa alisema kuwa uchaguzi ulikuwa mgumu kwa upande wake, lakini anashukuru Mungu kwa kupata nafasi hiyo na hatakikisha anasimamia kwa ukaribu mapato na matumizi ya halmashauri hiyo ambayo ina vyanzo vichache vya mapato, lakini vikisimamiwa vizuri vitasaidia kuondoa kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Aliongeza kuwa katika kipindi chote akiwa kwenye nafasi hiyo atajitahidi kuhakikisha manispaa haipati hati chafu, inayoweza kusababishia kukosa fedha za ruzuku kutoka Serikali kuu.

Halmashauri hiyo ina madiwani 21 kati yao 16 ni wa CCM, wanne wa Chadema na mmoja ni diwani kupitia tiketi ya DP.

Source: HabariLeo
inasikitisha sana kusikia na kuona poeples power wakipata kura 4 tu kat ya 21. mimi naanza kulia na wengine mnifuatilizie hiiiiiihiiiiiiiiiiii!
 
inasikitisha sana kusikia na kuona poeples power wakipata kura 4 tu kat ya 21. mimi naanza kulia na wengine mnifuatilizie hiiiiiihiiiiiiiiiiii!

usilie mbona kwenye maandamano watu wanaajaga.
 
Back
Top Bottom