kessy kyomo
Member
- Feb 1, 2011
- 72
- 11
Ya Igunga, CCM na jeuri ya madaraka!
Na Mashaka Mgeta, 26th August 2012
Waliokuwa wajanja, walishiriki kikamilifu kukionya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika hatua za awali za kampeni zake kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge, jimbo la Igunga mkoani Tabora uliofanyika mwaka jana. Waliionya CCM kupitia viongozi na makada wao, kwamba kutokana na kauli na vitendo vya hovyo, vilivyojikita katika taswira ya jeuri ya kuwepo madarakani, wanazidi kuuchukiza umma.
Vitendo kama vilivyohusu utoaji misaada hasa ya chakula, vitisho vya kuikosesha jamii haki za msingi ikiwa watamchagua mgombea asiyetokana na CCM, kutembea na kuonyesha hadharani bastola, ni miongoni mwa yaliyotajwa kutokukistahili chama tawala.
Yalisemwa mambo mengi katika kuionya CCM, hata sasa bado yanasemwa mengi pale ukiukwaji wa haki za raia unapofanywa, lakini kwa jeuri na dharau, miongoni mwa wasiostahili kuvishiriki vitendo hivyo, wanatenda.
Yaliandikwa mambo mengi na mengine kutangazwa kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, badala ya kujifunza ili wayaepuke, CCM wakayaendeleza, wakayachochea na kuyafanya kuwa ‘mambo ya kawaida' kwao. Pole kwa aliyetangazwa mshindi wa Igunga kupitia CCM, Dk Peter Kafumu, kwa maana alish iriki kampeni kwa njia za kistaarabu, lakini akachafuliwa. Wanaoshindwa kuuona mwanga wa mabadiliko unaolimulika taifa hili, wakajikita katika ‘kuzivuruga' kampeni za Dk Kafumu, hatimaye mahakama imeutengua ushindi wake.
Yapo mambo ya kujifunza kutokana na hatua ya mahakama kutengua ushindi wa Dk Kafumu, mtaalamu wa madini ambaye pasipo shaka, uwepo wake bungeni ulikuwa na maana pana kwa nchi na watu wake. Pasipo kujadili msukumo na shinikizo za kisiasa, bali ukweli unabaki kuwa mtaalamu wa madini, sekta inayopigiwa kelele kila kukicha, anapokuwa ndani ya chombo cha maamuzi kama Bunge, inasaidia zaidi hasa anapokuwa miongoni mwa wanaojali maslahi ya umma.
Ingawa ni hivyo, watawala kupitia CCM wanapaswa kutambua kwamba kuwepo madarakani ni dhamana inayotokana na umma, hivyo kitendo cha aina yoyote kinacholenga kuudhalilisha, kuufedhehesha, kuulaghai na kuutisha (umma) lazima `uzale' adhabu inayotokana na umma.
Ninatambua dhahiri kwamba wapo watu miongoni mwa watawala, wanaotambua na kutenda ipasavyo, wakitimiza wajibu wao pasipo kuathiriwa na jeuri, kiburi ama majigambo ya kisiasa, kwamba kwa sababu wanatawala, wanaweza kufanya lolote lile. Kwa siku za hivi karibuni CCM imejipambanua kwa kukosa viongozi na makada wenye uwezo wa kupanda jukwaani, wakihutubia na kuushawishi umma ili pasipo hila, ghiliba na vitisho, kiendelee kukubalika na kutawala. CCM imejikuta ikiwa na wanasiasa walio mfano wa ‘waigizaji', kwamba hata wanapokuwa kwenye majukwaa ya siasa, si rahisi kukubali mara moja kwamba wanaistahili sifa na heshima ya kuwa watawala. Pengine wangebaki ‘vijiweni' kuongoza mijadala inayohusu hali ya siasa nchini.
Lakini wasiokuwa na uwezo wa kuushawishi umma ndani ya CCM, wameotesha mizizi, wameunda mitandao na kushiriki fitina zinazowafanya wateuliwe na hatimaye kuchaguliwa kuwa viongozi wa umma. Badala ya kuutumikia umma, wakaudhalilisha umma.
Mathalani, CCM ilishafanya tathimini kubaini gharama zilizotumika kuwasafirisha viongozi wa serikali kwenda Igunga, ikalinganisha gharama hizo na thamani ya kujieneza kwake ili kikubalike zaidi kwa umma?
Kama viongozi wakiwemo mawaziri wanatumia rasilimali za umma, kupitia dhamana walizokabidhiwa wanashindwa kuielezea itikadi ya CCM, dira ya CCM, mwelekeo wa CCM, ilani ya uchaguzi ya CCM, tena kwa kuwianisha na mipango na mikakati ya maendeleo.
Badala yake wanashiriki kutoa kauli za vitisho, kuonyesha silaha hadharani na uozo mwingine unaokigharimu chama tawala hata kufikia ‘kupigwa chini' kwa Mbunge anayetokana na chama hicho, kuna manufaa gani. Mwishoni mwa wiki niliandika kwenye mtandao wa kijamii wa Wanabidii, nikachapisha utenzi huu ambao kwa ujumla, unahusiana na kadhia ya Igunga:
Anguko la Kafumu na Mapinduzi ndani ya CCM
Kafumu amevuliwa ubunge,
Makosa Ya 'wahafidhina' wa CCM,
Wale wasioyaona mabadiliko,
Wasiotaka kuyaishi mabadiliko,
Wasioyakubali mabadiliko.
Wamefanya 'uvundo wa kisiasa',
Wameukasirisha umma,
Wameumbuliwa na Mahakama,
Pole sana Kafumu!
Pole sana mwana mawasiliano mwenzatu.
Kwa jeuri na ulevi wa madaraka,
Wasiostahili, wamekusababishia usichostahili.
Hukumu imeshatoka,
Taji la ubunge umevuliwa,
Mjengoni hawatakuona,
Pumzika, anza upya.
Ole wako CCM,
Ole kwa jeuri ya waliomo ndani yako,
Wakitumia rasilimali za umma,
Wanakiuka yaliyo ya umma.
Wanajivisha jeuri ya kutoguswa,
Wafanye wanalolitaka,
Watishie pasipo soni,
Wakiuke kwa matarajio,
Kwamba watadumu siku zote.
Amka enyi mlio wa CCM,
Mapinduzi ya haki myaibue,
Hasira zenu ziwaondoe wasioistahili jamii.
Watoke, watoke kabla hamjatoka.
Msibwete enyi wana wa CCM,
Mkayaona mabaya na kuyaacha,
Kwa vile yanatendwa na wenye majina,
Mkashindwa kuwakemea, kuwatimua.
Mtayaonja mauti ya kisiasa,
Kwa uzembe wa wasio haki,
Wakitisha na kukiuka,
Ubunge wenu mkavuliwa.
Kazi kwenu.
Na Mashaka Mgeta, 26th August 2012
Waliokuwa wajanja, walishiriki kikamilifu kukionya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika hatua za awali za kampeni zake kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge, jimbo la Igunga mkoani Tabora uliofanyika mwaka jana. Waliionya CCM kupitia viongozi na makada wao, kwamba kutokana na kauli na vitendo vya hovyo, vilivyojikita katika taswira ya jeuri ya kuwepo madarakani, wanazidi kuuchukiza umma.
Vitendo kama vilivyohusu utoaji misaada hasa ya chakula, vitisho vya kuikosesha jamii haki za msingi ikiwa watamchagua mgombea asiyetokana na CCM, kutembea na kuonyesha hadharani bastola, ni miongoni mwa yaliyotajwa kutokukistahili chama tawala.
Yalisemwa mambo mengi katika kuionya CCM, hata sasa bado yanasemwa mengi pale ukiukwaji wa haki za raia unapofanywa, lakini kwa jeuri na dharau, miongoni mwa wasiostahili kuvishiriki vitendo hivyo, wanatenda.
Yaliandikwa mambo mengi na mengine kutangazwa kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, badala ya kujifunza ili wayaepuke, CCM wakayaendeleza, wakayachochea na kuyafanya kuwa ‘mambo ya kawaida' kwao. Pole kwa aliyetangazwa mshindi wa Igunga kupitia CCM, Dk Peter Kafumu, kwa maana alish iriki kampeni kwa njia za kistaarabu, lakini akachafuliwa. Wanaoshindwa kuuona mwanga wa mabadiliko unaolimulika taifa hili, wakajikita katika ‘kuzivuruga' kampeni za Dk Kafumu, hatimaye mahakama imeutengua ushindi wake.
Yapo mambo ya kujifunza kutokana na hatua ya mahakama kutengua ushindi wa Dk Kafumu, mtaalamu wa madini ambaye pasipo shaka, uwepo wake bungeni ulikuwa na maana pana kwa nchi na watu wake. Pasipo kujadili msukumo na shinikizo za kisiasa, bali ukweli unabaki kuwa mtaalamu wa madini, sekta inayopigiwa kelele kila kukicha, anapokuwa ndani ya chombo cha maamuzi kama Bunge, inasaidia zaidi hasa anapokuwa miongoni mwa wanaojali maslahi ya umma.
Ingawa ni hivyo, watawala kupitia CCM wanapaswa kutambua kwamba kuwepo madarakani ni dhamana inayotokana na umma, hivyo kitendo cha aina yoyote kinacholenga kuudhalilisha, kuufedhehesha, kuulaghai na kuutisha (umma) lazima `uzale' adhabu inayotokana na umma.
Ninatambua dhahiri kwamba wapo watu miongoni mwa watawala, wanaotambua na kutenda ipasavyo, wakitimiza wajibu wao pasipo kuathiriwa na jeuri, kiburi ama majigambo ya kisiasa, kwamba kwa sababu wanatawala, wanaweza kufanya lolote lile. Kwa siku za hivi karibuni CCM imejipambanua kwa kukosa viongozi na makada wenye uwezo wa kupanda jukwaani, wakihutubia na kuushawishi umma ili pasipo hila, ghiliba na vitisho, kiendelee kukubalika na kutawala. CCM imejikuta ikiwa na wanasiasa walio mfano wa ‘waigizaji', kwamba hata wanapokuwa kwenye majukwaa ya siasa, si rahisi kukubali mara moja kwamba wanaistahili sifa na heshima ya kuwa watawala. Pengine wangebaki ‘vijiweni' kuongoza mijadala inayohusu hali ya siasa nchini.
Lakini wasiokuwa na uwezo wa kuushawishi umma ndani ya CCM, wameotesha mizizi, wameunda mitandao na kushiriki fitina zinazowafanya wateuliwe na hatimaye kuchaguliwa kuwa viongozi wa umma. Badala ya kuutumikia umma, wakaudhalilisha umma.
Mathalani, CCM ilishafanya tathimini kubaini gharama zilizotumika kuwasafirisha viongozi wa serikali kwenda Igunga, ikalinganisha gharama hizo na thamani ya kujieneza kwake ili kikubalike zaidi kwa umma?
Kama viongozi wakiwemo mawaziri wanatumia rasilimali za umma, kupitia dhamana walizokabidhiwa wanashindwa kuielezea itikadi ya CCM, dira ya CCM, mwelekeo wa CCM, ilani ya uchaguzi ya CCM, tena kwa kuwianisha na mipango na mikakati ya maendeleo.
Badala yake wanashiriki kutoa kauli za vitisho, kuonyesha silaha hadharani na uozo mwingine unaokigharimu chama tawala hata kufikia ‘kupigwa chini' kwa Mbunge anayetokana na chama hicho, kuna manufaa gani. Mwishoni mwa wiki niliandika kwenye mtandao wa kijamii wa Wanabidii, nikachapisha utenzi huu ambao kwa ujumla, unahusiana na kadhia ya Igunga:
Anguko la Kafumu na Mapinduzi ndani ya CCM
Kafumu amevuliwa ubunge,
Makosa Ya 'wahafidhina' wa CCM,
Wale wasioyaona mabadiliko,
Wasiotaka kuyaishi mabadiliko,
Wasioyakubali mabadiliko.
Wamefanya 'uvundo wa kisiasa',
Wameukasirisha umma,
Wameumbuliwa na Mahakama,
Pole sana Kafumu!
Pole sana mwana mawasiliano mwenzatu.
Kwa jeuri na ulevi wa madaraka,
Wasiostahili, wamekusababishia usichostahili.
Hukumu imeshatoka,
Taji la ubunge umevuliwa,
Mjengoni hawatakuona,
Pumzika, anza upya.
Ole wako CCM,
Ole kwa jeuri ya waliomo ndani yako,
Wakitumia rasilimali za umma,
Wanakiuka yaliyo ya umma.
Wanajivisha jeuri ya kutoguswa,
Wafanye wanalolitaka,
Watishie pasipo soni,
Wakiuke kwa matarajio,
Kwamba watadumu siku zote.
Amka enyi mlio wa CCM,
Mapinduzi ya haki myaibue,
Hasira zenu ziwaondoe wasioistahili jamii.
Watoke, watoke kabla hamjatoka.
Msibwete enyi wana wa CCM,
Mkayaona mabaya na kuyaacha,
Kwa vile yanatendwa na wenye majina,
Mkashindwa kuwakemea, kuwatimua.
Mtayaonja mauti ya kisiasa,
Kwa uzembe wa wasio haki,
Wakitisha na kukiuka,
Ubunge wenu mkavuliwa.
Kazi kwenu.