CCM: Kamati Kuu Kulikoni Tena?

Dear brothers and sisters, I urge you not to use your precious time to react on a foolish comments, it will tend to demoralize your enthusiasms and motivation to fight against corruption and enemies of our good country. Try to be patient, kuna watu wengine hapa JF kwa makusudi kabisa wanataka kuturudisha nyuma, lakini naomba wajue hivi maji yameishamwagika, kuzoleka tena, ni mpaka yafuate water cycle system..... which means, there are a number of reactions should take place to get the poured water again with a function of time. CCM wamejimwagwa wenyewe as a result they have to face reactions. How? Kwa kuwadhurumu watanzania kwa muda mrefu, maumivu ya watanzania na mateso yao makuu na mizigo mizito tunayotwishwa sisi wananchi huku nchi yetu ikiwa na utajiri mwingi,,,,,,,,,wa kulaumiwa ni viongozi wa CCM.
 
Hawa wabunge wapiganaji wanatakiwa kuwa makini sana na statements za JK, kitu kilichowazi ni kwamba JK ni bingwa wa kuuma na kupuliza. Kwanini kwenye kikao NEC na CC hakuonyesha msimamo wake? Kwanini amesubiri kwanza kupima joto la wananchi kuhusu maamuzi ya NEC?

Alichofanya JK hivi majuzi alipokuwa anajibu maswali ya wananchi ilikuwa ni kujisafisha yeye binafsi, kitu ambacho bado ninakiona kwamba sio sahihi. Kitendo cha kusema CCM haina makundi ila ni wabunge wanachukiana wao kwa wao, hajiulizi kwamba kiini cha wao kwa wao kuchukiana ni nini? Bado kwenye kikao cha NEC kuna terminology zilizokuwa zikitumika kuainisha kundi la First 11 vs mafisadi, bado anasema ni chuki binafsi za wabunge? Zingekuwa ni chuki binafsi sidhani kama kungekuwa na alliance ya makundi, sana sana ingekuwa ni labda wabunge 2 au 3 vs wabunge wengine 2 au 3.

Kama watu walisikiliza vyema majibu ya Rais juzi, alisema wazi kwamba hawa wabunge wapambanaji wakumbuke kwamba serikali iliyo madarakani ni ya chama chao na wamechaguliwa kupitia CCM. Kauli hiyo ni nzito sana, ukiichambua kwa undani sana utakuta kwamba inawaonya wapunguze kasi ya kurusha makombora ama wakiyarusha wahakikishe hawaachi damage kwenye chama chao. Huo ni msimamo wa serikali na inaonyesha wazi kwamba serikali haiko tayari kusulubiwa kwa sababu za vita ya ufisadi ambayo imeonekana kuwa ni mwiba kwa kuwa inawagusa walio serikalini ama waliosaidia serikali iliyo madarakani ishinde kwenye uchaguzi wa 2005.

Swali la Richmond, alitumia muda mwingi kuji-distance yeye mwenyewe na pia kuonyesha namna alivyozuwia hazina isitoe udhamini kwa kampuni hiyo. Halafu anasema kwamba alizuwia udhamini wa hazina kwa kuwa alihisi inaweza kuwa "ghost company", hivi hapo haoni kama anaivua nguo Idara ya Usalama wa Taifa. Rais mzima unahisi kampuni ni ya mfukoni and yet unakaa kimya bila kuchukua hatua yoyote? Kuwa na mashaka pekee ilikuwa ni mojawapo ya sababu za kusimamisha kila kitu ili uchunguzi zaidi ufanyike. Kwanini hakutumia watu wa Usalama wa Taifa? Magazeti yaliandika sana kuhusu Richmond na mashaka waliyokuwa nayo kwamba hiyo ni kampuni fake, leo Rais anakuja kutoa cheap response kwamba alihisi ni ghost company, kwanini hakufanyia kazi hizo hisia zake mpaka asubiri mambo yaharibike? Kweli wanaosema kwamba swala la Richmond kaliweka sawa, mimi sijaona alipoweka sawa zaidi ya yeye mwenyewe kujitumbukiza kwenye tope na kuonyesha kwamba alihusika ama alikuwa na info za kutosha kuhusu hiyo kampuni na aliamua kukaa kimya.
 
Last edited:
- Okay wakuu kumekucha na tuko on tayari tunai-monitor situation ya hiki kikao muhimu sana kueleka uchaguzi on yanayojiri huko ndani, na as soon as tukizipata tu tutaziweka hapa ingawa niwe mkweli itakuwa a very long day.

- Lakini tunaendelea ku-touch base!

Respect.

FMEs!
 
FMES,mungu wangu azidi kukupigania upate zote zinazoendelea humo ndani ili tuwe wa mwanzo kuzipata na kujua muelekeo wa Taifa katika wakati huu kuelekea uchaguzi wa 2010.

Hisia zangu naona kama moja ya ajenda inaweza kuwa hili la ziara ya wapiganaji Mkoani Tabora? nasubiri kuconfirm maono yangu.
 
- Huko ni kukurupuka kwako mkuu, nenda kwenye original story utakuta hiyo mistari, huo muda sina mkuu, maana nimeanza kwenda majuu nikiwa na miaka kama mitatu, na robo tatu ya maisha yangu nimeishi majuu, si kuenda majuu nikiwa mtumzima kwamba sasa ninalimbuka na kuanza kupigia mistari majuu, au sikutokea mikoani na kupita tu Dar nikielekea Airport kwenda majuu.


FMEs!

JF great thinkers wanaona ni sifa eti kwenda majuu wakiwa na miaka mitatu?

Ndio maana wote wanatuacha walalahoi huku wilayani na kukimbilia kuficha pesa au kukinga mabakuli huko majuu.

Mbona wote mliokaa majuu ndio munaongoza kwa kuchemsha hapa nyumbani?

Kipimo ni hao akina Masha ambao sio tu wameenda majuu mapema lakini pia wamesoma huko tokea chekechea na bado wanachemsha ile tupa. Sitashangaa nikiona watu kama hao unawasifia au kuwaita marafiki.

Pia usinihusishe mimi muda wote na mambo ya Mwakalinga. Ninajitegemea na natoa hoja zangu. Hakuna anayeweza kuninyamazisha kama vile ambavyo hakuna anayeweza kukunyamazisha wewe usigeuke Yahaya Hussein au usilete matangazo yale ya kazi ambayo kila mtu anajua ni wizi mtupu.

Vinginevyo endelea kufurahisha genge hapa maana kwa wengine tunaangalia Ze Comedy!
 
- Respect wakuu kikao kimeisha tayari, agenda zilikuwa mbili tu according to the dataz, nazo ni kusimamishwa kwa zoezi la utamaduni wa wajumbe wa CC kutembelea majimbo na maeneo ya uchaguzi nationally ambayo huwa tabled as kuhamasisha wananchi kwa ajili ya uchaguzi, na pili Kikao kilitakiwa kutoa baraka zake kwa mfumo mpya utakaotumiwa na CCM kupitia mtandao, yaani online au internet.

- Briefly, the dataz za kikao ni kwamba:-

1. Rais amesitisha zoezi la wajumbe wa kamati hiyo kusafiri mikoani kuhamasisha wananchi kuelekea uchaguzi mbali mbali unaokuja, tabia ambayo imekua ni utamaduni wa CCM kwa miaka mingi.

- Sababu iliyotolewa ni kwamba chama hakina pesa kwa sasa, lakini wajumbe wengi wa kikao hicho wametoka huko ndani wakiwa na hisia mbali mbali kuhusiana na uamuzi huo wa mkulu. Kuna hisia moja nzito ambayo haijathibitishwa kwamba mafisadi wameamua kukichezea chama ili kikwame kipesa, ikiwa ni kwa kuwashawishi wafadhili wake wakubwa kutokipa pesa as usual.

2. CC ilitakiwa kutoa baraka kwa zoezi jipya la kuanza kutumia mtandao kama nyenzo muhimu ya kuwasiliana na wananchi na wanachama wake katika kutekeleza ilani za chama hasa za uchaguzi na utawala. Kikao hicho kwa kauli moja kilitoa baraka hizo ambazo ni kufuatia matayarisho makubwa ambayo yamekua yakifanywa kwa muda mrefu sana sasa, kuelekea kwenye kuhamishia shughuli nzito za chama yaani CCM, kwenye mtandao,

- Pia itakumbukwa kwamba ni majuzi tu Chadema walikuwa wa kwanza kuanzisha rasmi njia hii ya siasa kwenye mtandao.

- Hakukuwa na hoja ya ufisadi period, wala kizaa zaa cha NEC iliyopita.

Respect Wakuu.

Field Marshall Es!
 
JF great thinkers wanaona ni sifa eti kwenda majuu wakiwa na miaka mitatu?

Ndio maana wote wanatuacha walalahoi huku wilayani na kukimbilia kuficha pesa au kukinga mabakuli huko majuu.

Mbona wote mliokaa majuu ndio munaongoza kwa kuchemsha hapa nyumbani?

Kipimo ni hao akina Masha ambao sio tu wameenda majuu mapema lakini pia wamesoma huko tokea chekechea na bado wanachemsha ile tupa. Sitashangaa nikiona watu kama hao unawasifia au kuwaita marafiki.

Pia usinihusishe mimi muda wote na mambo ya Mwakalinga. Ninajitegemea na natoa hoja zangu. Hakuna anayeweza kuninyamazisha kama vile ambavyo hakuna anayeweza kukunyamazisha wewe usigeuke Yahaya Hussein au usilete matangazo yale ya kazi ambayo kila mtu anajua ni wizi mtupu.

Vinginevyo endelea kufurahisha genge hapa maana kwa wengine tunaangalia Ze Comedy!

Mbona unamtapikia hivyo FMS? Kulikoni?? au zile milioni 400??
 
Engineer: JF great thinkers wanaona ni sifa eti kwenda majuu wakiwa na miaka mitatu? Ndio maana wote wanatuacha walalahoi huku wilayani na kukimbilia kuficha pesa au kukinga mabakuli huko majuu. Mbona wote mliokaa majuu ndio munaongoza kwa kuchemsha hapa nyumbani?

- Engineer, tulikuwa tunaweka record straight kwamba hatulimbuki na majuu maana tulianza kwenda tukwia wadogo sana, as opposed na mtu kama wewe ambaye unaonekana umeanza kwenda majuu ukiwa mtumzima ndio maana kila mwenye connection na majuu kwako ni mwizi na anakinga bakuli na kuficha pesa,

- Na kama ninavyosema sana inaonekana unaongozwa na viongozi wezi na waficha hela za mabakuli, sio wote tuna hiyo tabia mkuu, huko wilayani umejiacha hoi mwenyewe kwa sababu ya uvivu wako, maana kuna watu wako huko huko uliko na wana maisha mazuri na mapesa pia ambayo wameyapata bila ya kwenda majuu, bali kwa kufanya kazi kwa bidi fanya kazi mkuu na wewe utafanikiwa ili uache hiyo hasira ya bila facts wala dataz against wa majuu,

- Pi amgombea wako kuwa majuu haina maana na yeye ni mwizi na mkinga mabakuli kama unavyodai!

Kipimo ni hao akina Masha ambao sio tu wameenda majuu mapema lakini pia wamesoma huko tokea chekechea na bado wanachemsha ile tupa. Sitashangaa nikiona watu kama hao unawasifia au kuwaita marafiki.

- Mgombea wako vipi kwani naye amechesha kwa sababu anaishi majuu au? Ya kuchemsha kiuongozi ni matatizo ya mtu, they have nothing to do na location, kwani Makamba naye amesoma chekechea majuu?

Pia usinihusishe mimi muda wote na mambo ya Mwakalinga. Ninajitegemea na natoa hoja zangu. Hakuna anayeweza kuninyamazisha kama vile ambavyo hakuna anayeweza kukunyamazisha wewe usigeuke Yahaya Hussein au usilete matangazo yale ya kazi ambayo kila mtu anajua ni wizi mtupu. Vinginevyo endelea kufurahisha genge hapa maana kwa wengine tunaangalia Ze Comedy

- Ya Mwakalinga na wewe, nenda kwenye ile thread ya mkutano wa Mwakyembe, wewe mwenyewe umesema kwamba Mwakalinga aliwaomba wewe na wenzako mtulie, sasa leo tena unamkana vipi tena Great Thinker?

- Ya kazi za majuu yana thread yake, ukinitaka kule anytime nitakuja na kukusaidia, hapa ni CC, wapiganaji na siasa ya masilahi ya taifa, kama umeishiwa hoja kaa pemebeni mkuu usichanganye ishus, ya ukaribu na Mwakalinga umeyasema mwenyewe, unaona wapambe njaa ukibanwa kidogo tu tayari umeshageuka, simama mwanaume wewe uhesabiwe, ni matumaini yangu kwamba Mwakalinga atajitokeza karibuni na kuku-denounce to this public kwamba hana anything to do na wewe, maana unamharibia sana mkuu,

- Siasa sio ya kila mtu, msiwe mnakurupuka tu na kujifanya mnajua siasa huwa ni kipaji, kampeni ya siasa haifanywi kwa kutumia nguvu kama ambazo umekua ukijaribu sana kuzitumia humu na ishu ya Mwakalinga na Kyela, weka hoja hapa za makosa ya mbunge wa sasa, na kwa nini Mwakalinga ndiye anyefaa kumrithi, lakini usitishe watu hapa na hoja za nguvu maana unazidi kumharibia unayemtetea, sasa quit now mkuu hizo kampeni!

Respect.

FMEs!
 
FMEs, naomba ufafanuzi au unisaidie kidogo, hivi Rostam Azizi aliondolewa lini kwenye uweka hazina wa CCM?
 
1. Rais amesitisha zoezi la wajumbe wa kamati hiyo kusafiri mikoani kuhamasisha wananchi kuelekea uchaguzi mbali mbali unaokuja, tabia ambayo imekua ni utamaduni wa CCM kwa miaka mingi.

- Sababu iliyotolewa ni kwamba chama hakina pesa kwa sasa, lakini wajumbe wengi wa kikao hicho wametoka huko ndani wakiwa na hisia mbali mbali kuhusiana na uamuzi huo wa mkulu. Kuna hisia moja nzito ambayo haijathibitishwa kwamba mafisadi wameamua kukichezea chama ili kikwame kipesa, ikiwa ni kwa kuwashawishi wafadhili wake wakubwa kutokipa pesa as usual.

Asante FMES kwa dataz, hili swala la ukata lina sura nyingi kama vile
1. Mafisadi (mfano RA, Somaiya, Manji nk) wameacha kutoa ufadhili.
2. Mafisadi wamewashawishi wafadhili wa nje (hasa Iran) kusitisha ufadhili
3. Mianya ya wizi/ufisadi kama ule wa Kagoda imezibwa (thanks Dr. Slaa na wenzako).
 
Rev.Kishoka,

..hizi kelele za wana CCM dhidi ya mafisadi ni jitihada za kutafuta madaraka tu.

..inashangaza kwamba wananchi wamesahau jinsi wanamtandao wa CCM walivyokuwa wakimwandama Frederick Sumaye kwamba ni fisadi, na kwamba tukiwachagua wao ufisadi utakwisha.


..hata Mkapa naye aliingia kwa gia ya kupigana na ufisadi uliokuwa umekithiri wakati wa awamu ya Mzee Mwinyi ambaye naye aliingia na makelele ya fagio la chuma.

..sielewi sababu za kuendelea kuichagua CCM kwa mategemeo ya kuutokomeza ufisadi, wakati imeishatoa maraisi watatu sasa walioshindwa ktk vita hiyo?

..inawezekana wana JF wengi "hawajala chumvi" vya kutosha, lakini kwa baadhi yetu ahadi ya vita dhidi ya ufisadi tulipewa kwa mara ya kwanza na Raisi Alli Hassan Mwinyi. kwa maoni yangu serikali za CCM kimelishughulikia suala hili kwa miaka takriban 24, au awamu 5 za uongozi, na hali inazidi kuwa mbaya.

NB:

..lakini hata ukiuweka ufisadi kando na kuangalia utendaji na rekodi ya serikali za CCM sidhani kama unaweza kuridhika hata kidogo.

..tuangalie sekta za kilimo, afya, elimu, uvuvi, biashara, viwanda, umeme, nishati, madini, usafirishaji etc. Hivi kweli wananchi mmeridhika?

..ukitaka kujua kwamba nchi imewashinda CCM angalieni jinsi vijana toka vijijini wanavyomiminika mijini bila ujuzi wowote na bila shughuli ya maana ya kufanya.

The Serpent Generale,

HIzi tunazoziaona ni vurugu za makusudi ndani ya CCM ili kuhakikisha kuwa Uchaguzi TAMISEMI mwaka huu na Uchaguzi Mkuu 2010, CCM inajizolea kura bwelele na kuuacha upinzani hoi.

Jiulizeni kwa nini Upinzani na kelele zote za Ufisadi, wameangushwa katika chaguzi zote ndogo tangu 2006 kasoro Tarime? Kama vita vya Ufisadi vingekuwa vinalipa na vina matokeo chanya, Watanzania wangewasikia Upinzani walivyokwenda Kiteto, Busanda, Mbeya Vijijini na kwingineko na kuiangusha CCM.

Ni ujuha wa hali ya juu kuamini kuwa Upiganaji ndani ya CCM ni kwa manufaa ya Tanzania.

Mnakumbuka Busanda, wakati kina Zitto walipopita na Operesheni Sangara na kuhubiri Ufisadi kuwa ni chupi ya CCM, je CCM waliwapeleka kina nani kuihakikishia Ushindi?

Tayari CCM wanatulaghai kuwa wana mvutano wa kiitikadi, CCM Mafisadi na CCM Wapiganaji, kisha Rais kacheza Ze-Comedy ya maswali na majibu ambayo imefanya watu wadinde kwa furaha eti sasa kuna tumaini na tunaelekea kwenye neema!

Leo hii kuna ripoti imeandikwa na Gazeti la Citizen kuwa Tanzania imepoteza sifa ya kupewa mikopo nafuu (soft loans), na tumepigwa kibano cha miaka mitatu mpaka tutakapotimiza masharti na kuonyesha rekodi ya ufanisi, uwajibikaji. Ripoti hii ni ya Benki ya Dunia katika ule mpango wao wa kusaidia nchi masikini.

http://web.worldbank.org/WBSITE/EXT...:51236175~piPK:437394~theSitePK:73154,00.html

http://siteresources.worldbank.org/IDA/Resources/73153-1181752621336/CPIA2008questionnaire.pdf

Kwa kushindwa kutimiza masharti haya, Tanzania itakosa mikopo nafuu na kuishia kupwe mikopo yenye Riba kubwa na masharti magumu.

Je CC, NEC na Bunge watakaa chini kumhoji aliyevurunda na kulitia Taifa letu gharama za ziada? Ni nani aliyeshindwa kazi yake kuhakikisha kuwa tunajizatiti na kufanikisha malengo ya sisi kupewa mikopo na misaada ambayo haina gharama kubwa?

Waache wakutane Ikulu, wapange mikakati mipya ya kuwalaghai Watanzania ili CCM iendelee na Utawala wake katika himaya ya Wadanganyika!
 
Rais Kikwete awakuna
wapambanaji wa ufisadi


*Kilango:Ametupa faraja kupambana zaidi
*Shellukindo:Ameweka sawa ya Richmond


WAANDISHI WETU
Dar es Salaam

SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kuhutubia Taifa na kufafanua juu ya masuala mbalimbali mazito ya kisiasa na kitaifa hususan vita vya ufisadi nchini, wabunge mbalimbali wa CCM hasa walio mstari wa mbele kupambana na ufisadi, wameipokea hotuba hiyo kuwa ni dira mpya.

Mbunge wa Same Mashariki-CCM, Anne Kilango Malecela, amelazimika kuzungumza akiwa ughaibuni kusisitiza kuwa msimamo wa Rais Jakaya Kikwete, kuhusiana na mapambano dhidi ya ufisadi hasa ahadi yake ya kuruhusu Serikali kukosolewa kwa nia ya kusahihisha makosa, umewapa faraja wabunge wanaopambana katika vita hivyo.

Akizungumza kwa simu kutoka Iowa, Marekani aliko kikazi, Kilango ambaye ni mmoja wa wabunge wachache ndani ya CCM wenye msimamo usioyumba, alisema Rais Kikwete ameonyesha ujasiri na kwamba wabunge makini wako nyuma yake.

“Kwa kweli tunampongeza sana Rais Kikwete kwa msimamo wake kuhusiana na ufisadi. Nimepata taarifa kupitia kwenye mtandao na kuwasiliana na wenzangu Tanzania, kwa kweli tumefarijika sana na msimamo wake ambao tunaufahamu siku zote,” alisema. Kilango alisema vita dhidi ya ufisadi ni vita vyenye changamoto nyingi ambazo wamekuwa wakipambana nazo na kwamba hata Rais Kikwete naye amekuwa akikumbana na changamoto nyingi, lakini ameonyesha ujasiri wa hali ya juu kubaki na msimamo wa kutounga mkono uhujumu wa fedha za wananchi.

“Tuko nyuma yake kwa moyo mmoja. Hatutapunguza kasi katika kutafuta mabadiliko ya dhati na yenye nia ya kukiimarisha chama chetu cha CCM (Chama Cha Mapinduzi) na Rais wetu asikate tamaa, tuko pamoja naye,” alisema. Alisema kutokana na furaha aliyoipata kutokana na kauli ya Rais Kikwete, Kilango anasema kwamba kwa sasa bado yuko katika maombolezo ya msiba wa ndugu yake lakini amelazimika kuzungumza hadharani kuonyesha furaha aliyoipata kutokana na msimamo wa Rais.

Alisema amekuwa kimya kwa muda mrefu, lakini Watanzania watarajie kishindo kikubwa mara atapoamua kuzungumza tena hadharani kutokana na kujiandaa kikamilifu kuitetea nchi yake. “Wasione nimekaa kimya, mimi nitajitokeza na kuibua mambo mazito kama Tsunami na watu najua mtatikisika na waandishi mtapata mambo ya kuzungumza,” aliahidi.

Kilango ambaye alitunukiwa tuzo ya mwanamke jasiri kutokana na kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya rushwa, alisema Rais Kikwete amekipa uhai mpya Chama Cha Mapinduzi na kwamba sasa chama kinazidi kuwa na nguvu kubwa. “Kwa kuimarisha chama, tunamhakikishia Rais Kikwete kwamba tutamsaidia kwa nguvu zetu zote bila kuchoka wala kuogopa misukosuko. Amegusa nyoyo zetu,” alisema.

Katika mazungumzo yake ya juzi usiku, Rais Kikwete alibainisha wazi kwamba katika mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi na aina zote za uhalifu hana mchezo. Hata alipoulizwa swali kwamba kuna watu wanalindwa kwa kuwa amekuwa na mahusiano nao, Rais alionekana kuwa jasiri kwa kusema wazi kwamba katika ufisadi hana rafiki wala ndugu na kwamba wahusika wanalifahamu hilo.

Mbunge wa Bumbuli-CCM, William Shellukindo yeye aliguswa na ahadi ya Kikwete kulimaliza suala la Richmond.

“Nampongeza sana Rais kwanza ametuthibitishia kwamba anafahamu kuwa Serikali inalazimika kuleta majibu kuhusu maazimio ya Bunge mwezi Novemba. “Na serikali ikituletea majibu ya kuridhisha sisi tutafurahi sana maana suala hilo litakuwa limefikia mwisho ili tuweze kuendelea na mambo mengine....Sisi katika kamati yetu (Nishati na Madini) tuliazimia na tumesema tutaendelea kusimamia haki hadi mwisho.”

Akizungumzia suala la wabunge wa CCM kutoelewana, Shellukindo alisema hilo ni suala la afya kwa chama tofauti na watu wanavyoona ni tatizo.

“Hiyo ni afya ya kisiasa maana katika wabunge zaidi ya 200 wa CCM huwezi kuwa na wabunge wote wenye mawazo yanayofanana. Sasa hili la kuwepo kwa msigano ni tatizo la baadhi ya wabunge wasiofahamu kutofautisha hoja na mahusiano. Mbunge anaweza kuwa na hoja na sisi mara zote hatuzungumzii mtu binafsi tunazungumzia hoja.

“Kwa mfano kama suala la Richmond lilikuwa ni azimio la bunge na wote wa CCM na wapinzani tulikubaliana katika hilo. Sasa lazima tujue kwamba wale waliochukuliwa hatua wana wabunge marafiki zao na wao wanaweza kuwa na hoja tofauti na mtazamo tofauti. Hili ni suala la kawaida na siyo tatizo wala mgawanyiko hasa kwa wale tunaoelewa.

Mbunge wa Mbozi Mashariki, CCM, Godfrey Zambi, mmoja wa walioshikia bango sakata la Ticts, alisema hotuba ya Kikwete imewaweka sawa:

“Labda niseme kwamba siku zote sisi wabunge tumechaguliwa ili kutetea maslahi ya umma. Kazi hii haiwezi kuwa ya wapinzani peke yao ni kazi ya wabunge wote. “Kama mimi ningekuwa mroho wa madaraka ningekwenda upinzani tangu mwaka 2000, lakini niliamini kwamba ni vyema kuikosoa serikali nikiwa ndani ya chama changu CCM. Lazima katika hili tuelewane na ninashukuru kwamba Rais ameliweka vizuri.

Mmoja wa wabunge vinara wa sakata la Richmond, Lucas Selelii-CCM Nzega, alimsifu Kikwete kwa kutangaza msimamo wa kutowaonea haya mafisadi. “Tunamshukuru sana Rais ameutangazia umma wa Watanzania msimamo wake na wa serikali yake. Lazima kama viongozi wa CCM na viongozi wa wananchi tujifunze kusoma ishara za nyakati. Naamini Rais hilo analijua na ndiyo maana kauli yake mmeisikia naamini ametuwekea njia na mwelekeo wa tunakokwenda,” alisema.

Source: Kulikoni 12/9/2009.


It is all about saving CCM face and nothing about Tanzania!

Wameridhika na kukongwa nyoyo kutokana na kauli za Rais ambaye ni Mwenyekiti wao. Lakini mbona kauli hizi Kikwete amekuwa akizitoa tangu aingie madarakani na vitendo ni haba?

Vita vya Ufisadi si kumkomboa Mtanzania kutoka Umasikini, Unyonge, Ujinga au Maradhi au hata kuleta mfumo wa Uongozi Bora wenye Siasa Safi, bali ni kufukuzana ndani ya Chama kwa manufaa ya Chama na si Tanzania!
 
It is all about saving CCM face and nothing about Tanzania!

Wameridhika na kukongwa nyoyo kutokana na kauli za Rais ambaye ni Mwenyekiti wao. Lakini mbona kauli hizi Kikwete amekuwa akizitoa tangu aingie madarakani na vitendo ni haba?

Vita vya Ufisadi si kumkomboa Mtanzania kutoka Umasikini, Unyonge, Ujinga au Maradhi au hata kuleta mfumo wa Uongozi Bora wenye Siasa Safi, bali ni kufukuzana ndani ya Chama kwa manufaa ya Chama na si Tanzania!


Mchungaji hapa ni kama Unampigia Mbuzi Gitaa ayarudi, hilo halipo mkuu, Tatizo letu sisi watanzania tunapenda sana KUKUNWA
 
It is all about saving CCM face and nothing about Tanzania!

Wameridhika na kukongwa nyoyo kutokana na kauli za Rais ambaye ni Mwenyekiti wao. Lakini mbona kauli hizi Kikwete amekuwa akizitoa tangu aingie madarakani na vitendo ni haba?

Vita vya Ufisadi si kumkomboa Mtanzania kutoka Umasikini, Unyonge, Ujinga au Maradhi au hata kuleta mfumo wa Uongozi Bora wenye Siasa Safi, bali ni kufukuzana ndani ya Chama kwa manufaa ya Chama na si Tanzania!

Mkuu Rev,

Mpaka hapo Katiba itakaporuhusu wagombea binafsi hakuna mwanasiasa Tanzania atakayedhubutu kukikosea chama chake, hata iwe kwa maslahi ya Taifa.
 
The Serpent Generale,

HIzi tunazoziaona ni vurugu za makusudi ndani ya CCM ili kuhakikisha kuwa Uchaguzi TAMISEMI mwaka huu na Uchaguzi Mkuu 2010, CCM inajizolea kura bwelele na kuuacha upinzani hoi.

Jiulizeni kwa nini Upinzani na kelele zote za Ufisadi, wameangushwa katika chaguzi zote ndogo tangu 2006 kasoro Tarime? Kama vita vya Ufisadi vingekuwa vinalipa na vina matokeo chanya, Watanzania wangewasikia Upinzani walivyokwenda Kiteto, Busanda, Mbeya Vijijini na kwingineko na kuiangusha CCM.

!

- Mchungaji heshima yako mkuu, hivi siku za karibuni umekutwa na nini mkuu?, I mean kelele za Upinzani kupinga ufisadi na kushindwa uchaguzi anyways unasema ni makosa ya CCM na wapiganaji?

- Is there something I am missing or what? kwa sababu so far I do not see the link? Hivi kweli unategemea wananchi ni wajinga sana kwamba wanaweza kuwasikiliza Zitto na Chadema kuhusu kupinga ufisadi wakati wamesikia kwa siku nyingi sana kuhusu ufisadi ndani ya chama chao ambao majuzi umekua displayed to the public big time? na kuwathibitishia kwamba zile suspicions walizokuwa nazo na hicho chama ni justified!

- Yaani hizi siku zote hizi Mchungaji, hujagundua kua wananchi hawawaamini mashetani wapya, kwa hiyo waliamua kuishi na mashetani wanaowajua vizuri CCM, ambayo ni simple political theory inayotumika sehemu nyingi sana duniani! Kama chadema hawachaguliwi pamoja na kelele zote za ufisadi maana yake ni moja tu kwamba hawaaminiki sasa watafute njia za kuaminika na wananchi, kuliko kuwalaumu CCM!

Mchungaji hapa unalalamikia strategies technicalities za chama katika uchaguzi, haliwezi kuwa kosa la CCM kwamba wanajua what wananchi wanataka kusikia wakati wa kampeni.

Respect.

FMEs!
 
Ni ujuha wa hali ya juu kuamini kuwa Upiganaji ndani ya CCM ni kwa manufaa ya Tanzania.

Mnakumbuka Busanda, wakati kina Zitto walipopita na Operesheni Sangara na kuhubiri Ufisadi kuwa ni chupi ya CCM, je CCM waliwapeleka kina nani kuihakikishia Ushindi?

!

- Mkuu Mchungaji, again ndani ya chama chochote cha siasa duniani lazima kuwe na makundi yenye itikadi tofauti, Zitto aliposimamishwa ubunge, kuna wabunge wapiganaji waliokataa kushiriki kumuhukumu Zitto na kukemewa sana na Waziri Mkuu, lakini waligoma kata kata sasa unasema kwamba wapiganaji walifanya vile kwa manufaa ya nani?

- Sasa wapiganaji wanaoandamwa na mafisadi kila siku ya Mungu, mpaka kutaka kufukuzwa NEC unasema wanapigania mafisadi, halafu mafisadi hao hao wanataka kuwafukuza kina Sitta kwenye CCM, labda kuna sehemu sikuelewi maana it does not make a sense kwa any Great listener, acha tu a Great Thinker!

Mkuu punguza hasira na jazba na wapiganaji, unless una ushahidi wa ufisadi wao kwa taifa uweke hapa tuuchambue! Otherwise, mafisadi hawawezi kulala macho kumtoa Sitta fisadi mwenzao, as of your claim!

Respect.

FMEs!
 
... unalalamikia strategies technicalities za chama katika uchaguzi, haliwezi kuwa kosa la CCM ....

FMEs!

Wakati wa ile saga ya wapiganaji na nec, ulituletea waraka ambao walidai kuwa waungwana ndio waliokutumia kukutisha nyau, je kijana waliyekuwa wamesema watamtuma kukuhakikishia kuwa wanakujua in/out alikuja?

Ama kweli ni bora ubaki na shetani umjuaye! Hii imani kali kweli kweli.
 
Back
Top Bottom