Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Katika sehemu ya kwanza ya Katiba ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kifungu cha cha tatu, hitimisho la Azimio la kuunganisha TANU na ASP linasema hivi:
Kisha katiba ya CCM inaendelea kwa kusema hili
Halafu katika kifungu cha nne kinachozungumzia Imani ya CCM, katiba ya CCM inasema
Kisha ukiendelea nakifungu cha tano kinachogusia malengo ya CCM utakuana na maneno mazito na yenye nguvu kama yafuatayo:
Ukimaliza malengo na imani ya chama, kinachofuatilia ni Uanachama na wajibu wa Mwanachama wa CCM
Mwishoni, Katba hii ya CCM toleo la mwaka 2007 linaweka Ahadi za Mwanachama wa CCM ambazo ni hizi
Sasa ukishaisoma katiba ya CCM kisha ukasoma sehemu kadhaa za Muongozo wa CCM wa Mwaka 1981 hasa kifungu cha 36
Vikao viwili vikubwa vya CCM vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ambavyo vilanzia kule Butiama na hiki kilichoisha majuzi hapa Dodoma, vinaashiria wazi ni jinsi gani CCM iliyoundwa mwaka 1978 na malengo yake ya kimapinduzi katika kulijenga Taifa la Kijamaa na Kujitegemea, imetekwa nyara na kutumiwa kunufaisha wajanja wachache ambao ni watwana wa Wakoloni na Mabeberu, ni waroho, wavivu, wazembe, wasiowajibika na wanaojinufaisha kutumia hatamu ambazo CCM imepewa na Watanzania kuliongoza Taifa la Tanzania kwa manufaa yao binafsi.
CCM ni chama cha Wakulima na Wafanyakazi, si cha Wanafiki, Mafisadi au Wazembe!
CCM ni chama ambacho kilijijenga kwa Watanzania kwa ahadi za kulijenga Taifa letu liwe huru na lenye kujitegemea, liwe mfano wa kuigwa, na si Taifa dhaifu ambalo halina utashi wa kujiimarisha kwa kutumia Juhudi na Maarifa kupiga vita Ujinga, Umasikini na Maradhi!
Wanaoongoza CCM ni dhaifu na ndio wanaokidhoofisha Chama na kukipa taswira mbaya ambayo inanuka kama kidonda kilichooza.
Waliopewa dhamana ya kuongoza CCM katika ngazi zote anzia Mtaa, Kata, Kijiji, Tarafa, Wilaya, Mkoa na Taifa hawafai tena kuendelea kukiongoza Chama cha Mapinduzi au kunufaika kwa matunda ya Uimara wa CCM.
Uimara wa CCM umebakia kuwa nadharia na maneno na si vitendo na ndio sababu kauli za kipuuzi na kijinga zilizosikika Butiama na juzi Dodoma, zinadhihirisha wazi kuwa maneno ya Marehemu Kolimba kuwa CCM imepoteza dira kuwa ni maneno sahihi na ni lazima yapatiwe ufumbuzi.
Mimi nina jibu moja tena rahisi sana, nalo ni kuleta Mapinduzi ndani ya CCM kwa wale wote ambao wanasimama upande wa misingi ya awali na ya kweli ya kuundwa kwa CCM na wanaofuatilia masharti, wajibu, majukumu na dhamana ya kuwa Wana CCM, basi wao ndio walio warithi na wamiliki halisi wa CCM na si hawa wengine ambao wamegeuka na kuwa ndumilakuwili na kufikiria nafsi zao kwanza.
Walioko madarakani CCM wanatia AIBU!
Nasema tena kuwa CCM imetekwa nyara na mahaini na wahujumu ambao wanatumia kila nyenzo na nguvu za dola kujiimarisha kwa kutumia rushwa, wizi, uhujumu na kuvunja kabisa miiko ya uanachama na kupuuzia maagizo yote ya Chama ambayo bado hayajabadilika hata pamoja na kuwa tumeingia katika mfumo wa Vyama vingi na mfumo wa kiuchumi wa soko huria.
Hivyo basi, kauli ya Mchungaji kwa WanaCCM imara ni simameni kidete na msione haya Ufisadi ulioko ndani ya Chama! Msionee haya viongozi wabuvu na wazembe ambao wameendelea kushindwa kuleta maendeleo ya kweli kwa Tanzania!
Wapiganaji wa CCM, simameni imara msiyumbishwe na vitisho au mizenge. CCM ina wenyewe, na wenyewe ni Wakulima na Wafanyakazi na si Mafisadi na virabaka na makuwadi wao!
Asiwatishe mtu kwa kutumia kikao chochote kile cha Chama au hata vitisho vya kuvuliwa uanachama. Hakuna haja ya Walio CCM wa kweli ambao ni watiifu na waaminifu kwa Katiba na Miongozo ya CCM kuwa leo waondoke wakaunde Chama kingine cha Kisiasa au kuhamia chama kingine.
Jiungeni, mshikamane na mlete Mapinduzi ndani ya Chama, kwa maana wote hawa wanaotetea na kulinda ufisadi, wanaogopa kuondolewa madarakani na kuvuliwa uanachama, na hivyo wanaanza kuwatuhumu wale walio watiifu kwa Katiba ya CCM kuwa hawafuati maadili ya Chama na hawalindi maslahi ya Chama.
Maslahi ya CCM ni kuongoza Tanzania na kujenga Taifa imara linalotumia rasilimali zake kwa manufaa ya Wananchi wake.
Maslahi ya CCM ni kujenga Uongozi na kuwa na Siasa Safi ambazo lengo ni kumkomboa Mtanzania kutoka Unyonge wa kuwa Masikini, Mggonjwa na Mjinga.
Maslahi ya CCM ni kuhakikisha kuwa Tanzania inajitegemea na kujitosheleza.
Maslahi ya CCM ni kuhamasisha Uzalishaji mali, Utiifu wa Sheria, Haki, Utu na Uwajibikaji.
Haya ndio maslahi ya CCM ya kweli ya Wakulima na Wafanyakazi walioko pande zote za Muungano toka Wete, Vikokotoni, Malagarasi, Songea na Manyara.
Enyi mafisadi na vibaraka wenu, kiacheni CCM chama cha Wakulima na Wafanyakazi. Ondokeni mkaanzishe chama chenu kisicho na nidhamu wala dira!
Tumeamua kwa pamoja kuunda Chama kipya cha kuendeleza Mapinduzi ya Kijamaa nchini Tanzania na Mapambano ya Ukombozi wa Afrika juu ya misingi iliyojengwa na TANU na ASP.
Kisha katiba ya CCM inaendelea kwa kusema hili
Chama tunachokiunda tunataka kiwe chombo madhubuti katika muundo wake na hasa katika fikra zake na vitendo vyake vya kimapinduzi vya kufutilia mbali aina zote za unyonyaji nchini, na kupambana na jaribio lolote lile la mtu kumuonea mtu au shirika au chombo c a nchi kuonea na kudhalilisha wananchi, kudhoofisha uchumi au kuzorotesha maendeleo ya Taifa; Chama tunachokiunda tunataka kishike barabara
hatamu za uongozi wa shughuli zote za umma kwa maslahi ya wafanyakazi na wakulima wa Taifa letu; Chama tunachokiunda tunataka kiwe kiungo kati ya
wanamapinduzi wa Tanzania na wanamapinduzi wenzetu kokote waliko.
Halafu katika kifungu cha nne kinachozungumzia Imani ya CCM, katiba ya CCM inasema
4. Chama Cha Mapinduzi kinaamini kwamba:
(1) Binadamu wote ni sawa.
(2) Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake.
(3) Ujamaa na Kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na
huru.
Kisha ukiendelea nakifungu cha tano kinachogusia malengo ya CCM utakuana na maneno mazito na yenye nguvu kama yafuatayo:
(2) Kulinda na kudumisha Uhuru wa Nchi yetu na raia wake.
(3) Kuhimiza ujenzi wa Ujamaa na Kujitegemea kwa mujibu wa Azimio la
Arusha.
(5) Kuona kwamba kila mtu anayo haki ya kupata kutoka katika Jamii hifadhi ya
maisha yake na mali yake kwa mujibu wa sheria.
(6) Kuona kwamba katika Nchi yetu kila mtu aliye na uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi; na kazi maana yake ni shughuli yoyote halali inayompatia mtu riziki yake.
(7) Kusimamia haki na maendeleo ya Wakulima, Wafanyakazi na Wananchi
wengine wenye shughuli halali za kujitegemea; na hasa kuona kwamba kila
mtu ana haki ya kupata malipo yanayostahili kutokana na kazi yake.
(12) Kuona kwamba Dola inakuwa Mhimili wa Uchumi wa Taifa.
(13) Kuona kwamba Serikali na Vyombo vyote vya Umma vinasaidia kwa vitendo kuanzishwa na kuendeleza shughuli za Ushirika na za Ujamaa, na shughuli nyinginezo halali za wananchi za kujitegemea.
(14) Kuona kwamba matumizi ya utajiri wa Taifa yanatilia mkazo maendeleo ya Wananchi na hasa jitihada za kuondosha Umasikini, Ujinga na Maradhi.
(16) Kuona kwamba katika nchi yetu hakuna aina yoyote ya dhuluma, vitisho, ubaguzi, rushwa, uonevu na/au upendeleo.
(17) Kuendelea kupiga vita Ukoloni Mamboleo,ubeberu na ubaguzi wa aina yoyote.
Ukimaliza malengo na imani ya chama, kinachofuatilia ni Uanachama na wajibu wa Mwanachama wa CCM
(3) Kuwa mtu mwenye kuamini kuwa kazi ni kipimo cha Utu, na kuitekeleza imani hiyo kwa vitendo.
6) Kuwa wakati wote ni mfano wa tabia nzuri kwa vitendo vyake na kauli yake, kuwa mwaminifu na kutokuwa mlevi au mzururaji.
(7) Kuwa ama Mkulima, Mfanyakazi, au mwenye shughuli nyingine yoyote halali ya kujitegemea.
(2) Kutumikia nchi yake na watu wake wote kwa kutekeleza wajibu wake bila hofu, chuki wala upendeleo wa nafsi yake, rafiki au jamaa.
(3) Kujitolea nafsi yake kuondosha Umasikini, Ujinga, Maradhi na Dhuluma, na kwa jumla kushirikiana na wenzake wote katika kujenga Nchi yetu.
(4) Kuwa wakati wote mkweli, mwaminifu na raia mwema wa Tanzania.
(7) Kuwa tayari kujikosoa na kukosolewa ili kuweza kuwa na msimamo sahihi wa siasa ya CCM.
Mwishoni, Katba hii ya CCM toleo la mwaka 2007 linaweka Ahadi za Mwanachama wa CCM ambazo ni hizi
AHADI ZA WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI
(1) Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja
(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote.
(3) Nitajitolea nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.
(7) Nitashirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.
( Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.
Sasa ukishaisoma katiba ya CCM kisha ukasoma sehemu kadhaa za Muongozo wa CCM wa Mwaka 1981 hasa kifungu cha 36
utabaini kuwa Chama cha Mapinduzi kama Chama cha Kisiasa, kwa Miongozo yake na Katiba zake, si chama kibovu, bali hali halisi ya sasa hivi ni kuwa kuna genge ama kundi la watu fulani ambao wamejiingiza ndani ya Chama na kushikilia madaraka na mamlaka ndani ya Chama na Serikali ambao ndio wanaokiharibia sifa CCM, ndio wanaolihujumu Taifa letu na kutumia kisingizi kuwa anayepiga vita Ufisadi na Uhujumu ni mhaini!36. Aidha, kuna matatizo ya kijamii kama vile kuongezeka kwa rushwa, hujuma za
kiuchumi, wizi, ujambazi na uharibifu wa mali ya umma, mambo ambayo
yanatupunguzia nguvu zetu za kiuchumi na kudhoofisha dhamira ya umma ya
kujenga ujamaa. Haya yote yamo katika uwezo wa Chama, Serikali na wananchi
kuyapiga vita na kuyashinda.
Vikao viwili vikubwa vya CCM vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ambavyo vilanzia kule Butiama na hiki kilichoisha majuzi hapa Dodoma, vinaashiria wazi ni jinsi gani CCM iliyoundwa mwaka 1978 na malengo yake ya kimapinduzi katika kulijenga Taifa la Kijamaa na Kujitegemea, imetekwa nyara na kutumiwa kunufaisha wajanja wachache ambao ni watwana wa Wakoloni na Mabeberu, ni waroho, wavivu, wazembe, wasiowajibika na wanaojinufaisha kutumia hatamu ambazo CCM imepewa na Watanzania kuliongoza Taifa la Tanzania kwa manufaa yao binafsi.
CCM ni chama cha Wakulima na Wafanyakazi, si cha Wanafiki, Mafisadi au Wazembe!
CCM ni chama ambacho kilijijenga kwa Watanzania kwa ahadi za kulijenga Taifa letu liwe huru na lenye kujitegemea, liwe mfano wa kuigwa, na si Taifa dhaifu ambalo halina utashi wa kujiimarisha kwa kutumia Juhudi na Maarifa kupiga vita Ujinga, Umasikini na Maradhi!
Wanaoongoza CCM ni dhaifu na ndio wanaokidhoofisha Chama na kukipa taswira mbaya ambayo inanuka kama kidonda kilichooza.
Waliopewa dhamana ya kuongoza CCM katika ngazi zote anzia Mtaa, Kata, Kijiji, Tarafa, Wilaya, Mkoa na Taifa hawafai tena kuendelea kukiongoza Chama cha Mapinduzi au kunufaika kwa matunda ya Uimara wa CCM.
Uimara wa CCM umebakia kuwa nadharia na maneno na si vitendo na ndio sababu kauli za kipuuzi na kijinga zilizosikika Butiama na juzi Dodoma, zinadhihirisha wazi kuwa maneno ya Marehemu Kolimba kuwa CCM imepoteza dira kuwa ni maneno sahihi na ni lazima yapatiwe ufumbuzi.
Mimi nina jibu moja tena rahisi sana, nalo ni kuleta Mapinduzi ndani ya CCM kwa wale wote ambao wanasimama upande wa misingi ya awali na ya kweli ya kuundwa kwa CCM na wanaofuatilia masharti, wajibu, majukumu na dhamana ya kuwa Wana CCM, basi wao ndio walio warithi na wamiliki halisi wa CCM na si hawa wengine ambao wamegeuka na kuwa ndumilakuwili na kufikiria nafsi zao kwanza.
Walioko madarakani CCM wanatia AIBU!
Nasema tena kuwa CCM imetekwa nyara na mahaini na wahujumu ambao wanatumia kila nyenzo na nguvu za dola kujiimarisha kwa kutumia rushwa, wizi, uhujumu na kuvunja kabisa miiko ya uanachama na kupuuzia maagizo yote ya Chama ambayo bado hayajabadilika hata pamoja na kuwa tumeingia katika mfumo wa Vyama vingi na mfumo wa kiuchumi wa soko huria.
Hivyo basi, kauli ya Mchungaji kwa WanaCCM imara ni simameni kidete na msione haya Ufisadi ulioko ndani ya Chama! Msionee haya viongozi wabuvu na wazembe ambao wameendelea kushindwa kuleta maendeleo ya kweli kwa Tanzania!
Wapiganaji wa CCM, simameni imara msiyumbishwe na vitisho au mizenge. CCM ina wenyewe, na wenyewe ni Wakulima na Wafanyakazi na si Mafisadi na virabaka na makuwadi wao!
Asiwatishe mtu kwa kutumia kikao chochote kile cha Chama au hata vitisho vya kuvuliwa uanachama. Hakuna haja ya Walio CCM wa kweli ambao ni watiifu na waaminifu kwa Katiba na Miongozo ya CCM kuwa leo waondoke wakaunde Chama kingine cha Kisiasa au kuhamia chama kingine.
Jiungeni, mshikamane na mlete Mapinduzi ndani ya Chama, kwa maana wote hawa wanaotetea na kulinda ufisadi, wanaogopa kuondolewa madarakani na kuvuliwa uanachama, na hivyo wanaanza kuwatuhumu wale walio watiifu kwa Katiba ya CCM kuwa hawafuati maadili ya Chama na hawalindi maslahi ya Chama.
Maslahi ya CCM ni kuongoza Tanzania na kujenga Taifa imara linalotumia rasilimali zake kwa manufaa ya Wananchi wake.
Maslahi ya CCM ni kujenga Uongozi na kuwa na Siasa Safi ambazo lengo ni kumkomboa Mtanzania kutoka Unyonge wa kuwa Masikini, Mggonjwa na Mjinga.
Maslahi ya CCM ni kuhakikisha kuwa Tanzania inajitegemea na kujitosheleza.
Maslahi ya CCM ni kuhamasisha Uzalishaji mali, Utiifu wa Sheria, Haki, Utu na Uwajibikaji.
Haya ndio maslahi ya CCM ya kweli ya Wakulima na Wafanyakazi walioko pande zote za Muungano toka Wete, Vikokotoni, Malagarasi, Songea na Manyara.
Enyi mafisadi na vibaraka wenu, kiacheni CCM chama cha Wakulima na Wafanyakazi. Ondokeni mkaanzishe chama chenu kisicho na nidhamu wala dira!