Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Nilianza kusikia kwamba 'kujivua gamba' kwa ccm, ni kuwaengua viongozi watatu wa ngazi za juu za chama hicho (majina yalitajwa), na walipewa muda wa siku 90 kufanya hivyo. Baadae nikawa nasoma humu jamvini kuwa, tafsiri hiyo ya awali ilibadilishwa, na sivyo hivyo. Baada ya hapo sikuwa na uhakika 'kujivua gamba' ni nini hasa tena, mpaka jioni hii nilimpomwona kijana Nnape akihutubia wana ccm, na kutoa tafsiri ya 'kujivua gamba'.
Kutokana na Nnape, ccm ni chama kilichotawala takriban miaka 50, kwa hivyo kwa muda wote huo kimekuwa kizee, hivyo kinahitaji 'kujivua gamba'.
Alisema, "Kujivua gamba ni kuongeza uwezo wa ccm kuwa karibu na wanachama wake". Baada ya kusema hivyo alipigiwa vigelegele na kina mama.
Nilijiuliza hivi ni kwa nini hao kina mama wanapiga vigelegele? Je wanafahamu kuwa hiyo ni version nyingine ya kujivua gamba tofauti na ile iliyotolewa na Nnape mwenyewe na katibu wa ccm?
Itakuwa ni vizuri kama chama tawala kitakuwa karibu na wananchi. Hata hivyo ni vizuri zaidi kuthibiti watu na vitendo ambavyo vinaweka chama tawala mbali na wananchi. Hapa ina maana kwamba, ili 'kujivua gamba' iwe ya kweli, na sio tu hotuba za majukwaani, version zote mbili hazina budi kutekelezwa.
Kutokana na Nnape, ccm ni chama kilichotawala takriban miaka 50, kwa hivyo kwa muda wote huo kimekuwa kizee, hivyo kinahitaji 'kujivua gamba'.
Alisema, "Kujivua gamba ni kuongeza uwezo wa ccm kuwa karibu na wanachama wake". Baada ya kusema hivyo alipigiwa vigelegele na kina mama.
Nilijiuliza hivi ni kwa nini hao kina mama wanapiga vigelegele? Je wanafahamu kuwa hiyo ni version nyingine ya kujivua gamba tofauti na ile iliyotolewa na Nnape mwenyewe na katibu wa ccm?
Itakuwa ni vizuri kama chama tawala kitakuwa karibu na wananchi. Hata hivyo ni vizuri zaidi kuthibiti watu na vitendo ambavyo vinaweka chama tawala mbali na wananchi. Hapa ina maana kwamba, ili 'kujivua gamba' iwe ya kweli, na sio tu hotuba za majukwaani, version zote mbili hazina budi kutekelezwa.