Ccm inalaumiwa bure haihusiki na umasikini wetu

Sangarara

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
13,100
5,649
Kuna uwezekano mkubwa kwamba katika jitihada zetu za kujikwamua kutoka kwenye umasikini tulio nao, watanzania tunatumia nguvu nyingi sana kukisakama chama cha mapinduzi kimakosa kwa sababu hakina ushawishi mkubwa kama tunavyofikiria kwenye mchakato mzima wa kuongoza serikali yetu zaidi ya kwamba viongozi wengi wa serikali ambao wameteuliwa kwa msingi wa kisiasa wanatoka chama hicho.

Moja ya Fact ni kwamba, sio Chama cha Mapinduzi, kwa maana ya kwamba hakuna organ yoyote ndani ya chama cha mapinduzi ambayo hukaa na kutoa maoni, au kupitia maoni au kuteua kiongozi yoyote katika serikali yetu. Kwa haraka haraka tunakilaumu chama cha mapinduzi kwa sababu viongozi wa serikali wanatokea huko kama mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na kwa muda mrefu wabunge karibia wote na madiwani kwenye halmashauri zetu wamekuwa wakitokea chama hicho, lakini UKWELI ni kwamba hawa wote wamekuwa wakipatikana kutokana na mchakato wa uchaguzi wa kitaifa na sio wa kichama.

KIUKWELI KABISA, hata viongozi wa Chama cha Mapinduzi wanapodai kwamba ndio wanaoongoza serikali inatokana na uroho wa kuonekana kwamba wao ndio wenye madaraka, na labda kwa sababu wamekuwa wabunifu wa kujinufaisha na hisia za wao kuongoza serikai eti kwa sababu tu viongozi karibia wote wa serikali wana kadi au wanajitambulisha kama wa CCM.

Chukulia mfano Mbichi, Mwiguru nchemba anajitanua kwamba yeye yuko jikoni na kupigana kuitetea bajeti iliyowasilishwa bungeni, huu ni ujuha na utoto, sababu hakuna wakati wowote katika process ya kuandaa bajeti hiyo chama cha mapinduzi kinashirikishwa including mwigulu mwenyewe hata kwa nafasi yake ya uweka hazina wa chama,anachokifanya ni kuchukuliwa na hisia za utawala na kuanza kupayuka kama vile mtu amepandwa na pepo mchafu bila kujua anachokifanya ni nini, ndio maana katikati ya mjadala wa muhimu kabisa kwa watanzania watu wanaanza kubehave kama waganga wa kienyeji.

Bajeti hii wenyeviti wa kata, mashina,tarafa, vijiji,wilaya mikoa wala viongozi wa mabaraza yoyote yale ya chama cha mapinduzi hawajashiriki kuiandaa kama vile ambavyo hawatashiriki kwenye mchakato wowote ule wa utekelezaji wa bajeti hii, kama ambavyo haijawahi kutokea huko nyuma pia.

Wito wangu kwa watanzania, Hii ni serikali yetu na tusiwaachie mafisi wakaiharibu wakati sisi tunakimbiza kivuli.
 
Ngoja tuwalaumu wala ubwabwa na wapokea khanga kwa kuwapa ridhaa ccm kutawala
 
Anayestahili kurespond vizuri ktk hii thread yako ni mweka zinaa wa sisiem. Anao ufahamu mzuri zaidi tena ni mchumi wa darja la kwanza.
 
Anayestahili kurespond vizuri ktk hii thread yako ni mweka zinaa wa sisiem. Anao ufahamu mzuri zaidi tena ni mchumi wa darja la kwanza.

Kwani katiba ya nchi inatoa maelekezo gani juu ya usimamizi wa serikali unaofanywa na chama tawala
 
Kuna haja kubwa sana ya kubadili mfumo wa elimu wa nchi hii, vinginevyo tutakuwa tunazalisha watu waliopitia shule na kupata vyeti. Kwa hati ya mwandishi wa mada hii lazima atakuwa kafika walau kidato cha nne, lakini inashangaza sana asivyoweza kuhusianisha mgawanyo wa madaraka, wajibu na majukumu.
 
Tumlaumu Nyerere na kiherehere chake cha kuchukuwa nchi wakati kuendesha hajaweza bado , hapo ndio chimbuko la umaskini lilianza, naongea sio kwa chuki, umataka tuchangie naomba tusibezane. Tufikirie umasikini ulianza wapi !

Baada ya kuchukuwa nchi sera za ujamaa na kujitegema , azimio la arusha zilikuwa si nzuri hizi ndio zilifanya nchi ikawa masikini wa kutupwa, alipoona nchi imekufa kabisa babu akamuachia mwinyi, ubepari ukaingia vitu vilikuwa vingi lakini mara wanyonyaji wakaingia rushwa ikaanza kuchomoza, alipoondoka mwinyi akaingia mkapa mtoto mwaminifu wa Nyerere akataifisha kila kitu watu wakaanza kujilimbikia mali rushwa ikaota kizizi akaja ndugu yangu wa Bwagamoyo huyu aliingia na nia nzuri tu ya kukwamua nchi bahati mbaya sana maswahiba wake wamamponza na wamechukulia upole wake kutenda wayatakayo. matokeo yake sasa hivi nchi inakwenda mrama mrama tu.

Rushwa imekithiri, watu wanawaza kuanzisha mikutano na vikao wale posho utendaji serikalini umekuwa mbovu mbovu pesa badala ya kwenda kwenye maendeleo yote inaliwa na watendaji serikalini saa ngapi wananchi wake watapata maendnelo. TRA wamejaa wenzetu wa kaskazi , misamaha ya kodi isiyo na tija , watu wanapokea rushwa ili mradi kuwawezesha watu wasilipe kodi pesa itapatikana vipi ya maendeleo. Serikali ina matumizi yasiyo na tija washauri hawamshauri rais. ni kaaazi kweli kweli.

Na wakija chadema ndio tumeisha kabisa... ni bora mbu alie ndani ya neti amekula ameshiba kuliko kumruhusu mbu alie nje anataka kuingia ndani ya neti atakumaliza kabisa! sidhani kama kutakuwa na jipya kwa story tunazozisikia za kina mbowe na unafiki mtu anasema hataki posho ilhali huku anapokea , hata gari huku analichukuwa kimya kimya hawa hawatufai bora CCM ila vitu vidogo vidogo virekebishwe nawasilisha ...
 
ubinafsi ndio chanzo cha umaskini , na ubinafsi hauna chama mfano Mh Mbowe anatembelea gari la kifahari .
 
Back
Top Bottom